Mazindu Msambule
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 7,509
- 6,863
BAdo naendelea tu na utafiti wangu, Wanaume wenye makalio makubwa akili zao mara nyingi hua chache na ni wepesi sana wa kusahau! Naendelea kulifanyia utafiti hilo kwanza.
"NIMEPATA BAHATI YA KUZINGUKA PAMOJA NA KATIBU MKUU NDUGU ABDULRAHMAN KINANA NCHI NZIMA, NIMESHUHUDIA KWA MACHO YANGU KUWA UPINZANI UNAKUFA KILA KONA YA TANZANIA" - NAPE MOSES NNAUYE, uwanja wa Barafu, Dodoma.
Maneno hayo ni nukuu ya katibu wa halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi wa Chama bora Tanzania CCM alipokuwa akizungumza na maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana katika Viwanja vya barafu vilivyopo Dodoma mjini, pembezoni mwa uwanja wa mpira wa Jamhuri.
Nape ametoa ushuhuda huo akiwaasa baadhi ya vijana na wananchi wa Dodoma ambao bado wanadanganyika na maneno ya uzushi na uongo wa upinzani ambao wanautunga kila asubuhi, Nape amesema kutunga uongo dhidi ya CCM na Serikali yake ni kutapatapa kwa upinzani ukiwa unakata roho.
Nae Katibu Mkuu katika Mkutano huo wa hadhara, amesema wajibu wa CCM ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maisha bora, asema miaka ya hivi karibuni watanzania wameshuhudia maendeleo makubwa na kupiga hatua kubwa katika elimu, miundombinu ya barabara, madaraja, teknolojia na nishati.
Kinana amesema ni kazi ngumu kutenda rahisi kubeza, kazi ya CCM kutenda kazi ya upinzani ni kusema. Asema tumefanikiwa katika shule za UPE ambazo zimetoa mabalozi, mawaziri na wakurugenzi wakubwa ingawa wakati zinaanzishwa zilibezwa kama zinavyobezwa shule za Kata lakini zinatoa vijana wanaojiunga na vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini na tutapata wataalamu na wazalendo wa kweli kutoka shule za kata ingawa wapinzani wanazibeza.
....ungekuwa na cheti cha "VETA" ungeukwaa Ukuu wa Wilaya hujachelewa nenda CHINA
Prettyspicey Benazir,
Si vizuri kujifanya umepoteza kumbukumbu kwa kile unachokifahamu vizuri
Tangu asubuhi kazi yako ni kunizushia na obsession zako tu.What's wrong with you?
I have courage,patience and determination to see it through.
..but one thing for sure as long as people read and not only entertained but touched ,I 'll keep writing,I'll keep the fight on...
Good evening!
Ben Saanane ulipiga hii mashine??Niliwahi kuwakuta vijana wa bavicha siku moja wakijadili jambo kuhusu wewe, na baadhi yao wakasema kuwa wewe ni jembe lao katika kujenga hoja jf na hivyo unafaa kuwa kiongozi wao mkubwa ndani ya bavicha..
Samahani kidogo ndugu yangu..,hizo hapo juu ndio hoja zenyewe ambazo ndizo zilikuwa mtaji wako wa kisiasa wakati wa uchaguzi...??
"NIMEPATA BAHATI YA KUZINGUKA PAMOJA NA KATIBU MKUU NDUGU ABDULRAHMAN KINANA NCHI NZIMA, NIMESHUHUDIA KWA MACHO YANGU KUWA UPINZANI UNAKUFA KILA KONA YA TANZANIA" - NAPE MOSES NNAUYE, uwanja wa Barafu, Dodoma.
Nape na Kinana siku hizi wanatembea na fisi angalau kuwavutia watoto waende kwenye vikao vilivyosusiwa na watanzania waliojitambua
Hivi nyie watu ubongo wenu umemwagiwa gundi au! Mbona mko sloo sana kufikiri na kusoma alama za nyakati??. Takwimu za hapo juu nina mashaka nazo, ila ngoja nizitumie kukuelewesha, maana yaonekana ni mgumu sana kuelewa!
Kama chaguzi za 2009 mlishinda zaidi ya 90%, leo imeshuka mpaka 85%, unasemaje hapo kuwa upinzani unakufa????
Una maembe mia, ktk tembea tembea yako unadondosha maembe mazima 20, mwenzako aliye nyuma anayaokota na kuondoka nayo, alafu wewe unakuja sema bado haujapoteza maembe mengi wakati kama ukoo wako una watu 25 na kila mmoja alikuwa anakula maembe 4 ili ashibe sasa inabidi baadhi ya wanaukoo wale maembe machache sababu ya maembe uliodondosha, huoni kuna hitilafu hapo?
Jipangeni, acheni kujipa moyo pasipo na ukweli.
If wishes were horses.....
Leo nimepata taarifa kuwa jimboni kwa Lusinde CCM imeshinda kwa asilimia 98...sasa hapa kuna ubishi gani kuwa Upinzani unakufa..!!