17th June 2010
Kambi ya Upinzani Bungeni imeitaka serikali kuacha visingizio kuhusu hali ya maisha inayozidi kuwa mbaya miongoni mwa wananchi wa kawaida kila kukicha, badala yake itafute mbinu ya kupunguza makali ya maisha "kwani hali ni ngumu kwa sasa kuliko wakati wowote".
Akichangia hotuba ya Bajeti ya Waziri Mkuu na ile ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Msemaji Mkuu wa upinzani katika eneo hilo, Dk. Willibrod Slaa, alisema uchunguzi wa kambi hiyo unaonyesha kwamba bei ya karibu kila kitu imepanda maradufu lakini kipato cha Mtanzania kimebaki pale pale, huku nguvu ya mwananchi kununua bidhaa hizo ikishuka kwa kasi kutokana na kuporomoka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania.
"Mathalan wananchi wengi wameacha kunywa chai kwa vile sukari sasa imekuwa bidhaa ya anasa, wastani wa Sh. 1,200 hadi 1,800 wakati mwaka 2005 ilikuwa Sh. 500-600, mikate iliyokuwa kimbilio la walalahoi hasa mijini imekuwa haishikiki tena kwa vile bei inakimbilia Sh. 1,500 – 2,000.
Nyama inazidi kuwa hadithi ya kusadikika kwani inakimbilia kati ya Sh. 4,500 na Sh. 5,000 kwa kilo katika maeneo mengi," alisema. Alisema mchele ambao ukiacha mahindi unakuwa chakula cha Watanzania wengi unakimbilia sh. 5,000 kwa kilo huku hata kitoweo cha maharage kilichokuwa mkombozi wa familia nyingi nacho hakishikiki kwani kilo katika maeneo mengi ni zaidi ya sh. 1,000.
"Ndiyo maana kuna msemo ‘all politics is local' (siasa zote zilenge watu wa kawaida). Visingizio vya hali ya uchumi wa dunia hauwahusu wananchi kwani waliiweka/ajiri serikali kwa lengo pekee la kushughulikia masuala hayo," alisema na kuongeza kwamba serikali inaposhindwa kutimiza hayo ndiyo inaitwa; "Serikali iliyoshindwa maslahi ya ndani ya wananchi wake."
Alisema hali hiyo inafanya taarifa ya serikali kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania kwa mwaka 2008 ni sh. 682,737 inapoteza maana kwani watu wenye kipato hicho wasingeshindwa kununua angalau sukari na mchele.
Alisema wananchi wanataka kula vizuri, kulala vizuri, mishahara inayokidhi haja na siyo takwimu zinazoonyesha kukua kwa uchumi.
"Wananchi hawali takwimu za vitabuni. Wanahitaji mahitaji yao muhumu kwa maisha ya kila siku," alisema.
Hata hivyo, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani inapotoa tathmini kuhusu hali ya sasa ya wananchi si kwamba haioni kama kuna mambo mazuri yaliyofanywa na serikali kuanzia zama za chama cha Tanu hadi CCM.
"Tunachosema ni kuwa kwa raslimali tulizonazo tungeweza kufanya vizuri zaidi…Tungelizielekeza kwenye maeneo muhimu yanayomnufaisha mwananchi," alisema.
Dk. Salaa ambaye wakati akirusha ‘madongo' mitambo ya televisheni ya taifa ilizima na kuwashwa akiwa kamaliza kuongea, alisema kambi ya upinzani haiwezi kupoteza muda kuzungumzia vitu ambavyo vimefanywa, bali kila wanapochambua mambo wanagundua kwamba vipaumbele vingi vya serikali vina kasoro na kwamba hata pale pesa zinapoonekana kama zimetengwa kwa ajili ya kurekebisha mambo, mara nyingi huwa si kweli ama hazisimamiwi vizuri.
Alisema serikali isiyoweka vipaumbele kwa wananchi wake ni serikali pia isiyojali wananchi.
CHANZO: NIPASHE
Kambi ya Upinzani Bungeni imeitaka serikali kuacha visingizio kuhusu hali ya maisha inayozidi kuwa mbaya miongoni mwa wananchi wa kawaida kila kukicha, badala yake itafute mbinu ya kupunguza makali ya maisha "kwani hali ni ngumu kwa sasa kuliko wakati wowote".
Akichangia hotuba ya Bajeti ya Waziri Mkuu na ile ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Msemaji Mkuu wa upinzani katika eneo hilo, Dk. Willibrod Slaa, alisema uchunguzi wa kambi hiyo unaonyesha kwamba bei ya karibu kila kitu imepanda maradufu lakini kipato cha Mtanzania kimebaki pale pale, huku nguvu ya mwananchi kununua bidhaa hizo ikishuka kwa kasi kutokana na kuporomoka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania.
"Mathalan wananchi wengi wameacha kunywa chai kwa vile sukari sasa imekuwa bidhaa ya anasa, wastani wa Sh. 1,200 hadi 1,800 wakati mwaka 2005 ilikuwa Sh. 500-600, mikate iliyokuwa kimbilio la walalahoi hasa mijini imekuwa haishikiki tena kwa vile bei inakimbilia Sh. 1,500 – 2,000.
Nyama inazidi kuwa hadithi ya kusadikika kwani inakimbilia kati ya Sh. 4,500 na Sh. 5,000 kwa kilo katika maeneo mengi," alisema. Alisema mchele ambao ukiacha mahindi unakuwa chakula cha Watanzania wengi unakimbilia sh. 5,000 kwa kilo huku hata kitoweo cha maharage kilichokuwa mkombozi wa familia nyingi nacho hakishikiki kwani kilo katika maeneo mengi ni zaidi ya sh. 1,000.
"Ndiyo maana kuna msemo ‘all politics is local' (siasa zote zilenge watu wa kawaida). Visingizio vya hali ya uchumi wa dunia hauwahusu wananchi kwani waliiweka/ajiri serikali kwa lengo pekee la kushughulikia masuala hayo," alisema na kuongeza kwamba serikali inaposhindwa kutimiza hayo ndiyo inaitwa; "Serikali iliyoshindwa maslahi ya ndani ya wananchi wake."
Alisema hali hiyo inafanya taarifa ya serikali kuwa wastani wa kipato cha Mtanzania kwa mwaka 2008 ni sh. 682,737 inapoteza maana kwani watu wenye kipato hicho wasingeshindwa kununua angalau sukari na mchele.
Alisema wananchi wanataka kula vizuri, kulala vizuri, mishahara inayokidhi haja na siyo takwimu zinazoonyesha kukua kwa uchumi.
"Wananchi hawali takwimu za vitabuni. Wanahitaji mahitaji yao muhumu kwa maisha ya kila siku," alisema.
Hata hivyo, Dk. Slaa alisema kambi ya upinzani inapotoa tathmini kuhusu hali ya sasa ya wananchi si kwamba haioni kama kuna mambo mazuri yaliyofanywa na serikali kuanzia zama za chama cha Tanu hadi CCM.
"Tunachosema ni kuwa kwa raslimali tulizonazo tungeweza kufanya vizuri zaidi…Tungelizielekeza kwenye maeneo muhimu yanayomnufaisha mwananchi," alisema.
Dk. Salaa ambaye wakati akirusha ‘madongo' mitambo ya televisheni ya taifa ilizima na kuwashwa akiwa kamaliza kuongea, alisema kambi ya upinzani haiwezi kupoteza muda kuzungumzia vitu ambavyo vimefanywa, bali kila wanapochambua mambo wanagundua kwamba vipaumbele vingi vya serikali vina kasoro na kwamba hata pale pesa zinapoonekana kama zimetengwa kwa ajili ya kurekebisha mambo, mara nyingi huwa si kweli ama hazisimamiwi vizuri.
Alisema serikali isiyoweka vipaumbele kwa wananchi wake ni serikali pia isiyojali wananchi.
CHANZO: NIPASHE