Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Taarifa kutoka ndani ya chama makao makuu zina sema kuwa kumejitokeza mgogoro wa kiuongozi ndani ya chadema kufuatia tofauti za maamuzi katika masuala kadhaa ya kitaifa.kumekuwa na kuvumiliana kwa kiasi kikubwa lakini wadau wanaeleza kuwa sasa hali imekuwa tete na haivumiliki tena.moja ya masuala ambayo yamekigawa chama ni pamoja na uamuzi wa chama kutuma ujumbe kwenda ikulu kuonana na rais.wapo waliopinga na wengine waliafiki lakini sasa walipinga wanahoji nini faida yake kwa chama kufuatia hatua ya rais kuusaini tofauti na msimamo wa cdm ambayo ilipinga.suala lingine linalokitafuna chama ni mgogoro wa madiwani arusha kufuatia uamuzi wa chama kuwafukuza uanachama madiwani wake watano.katika ngazi ya taifa wapo wanaopinga hatua hiyo kwa maelezo kwamba uamuzi huo umekiumiza chama.suala lingine ni posho kwa wabunge ambapo wapo wanaopinga na wengine wanaunga mkono......jambo lingine kubwa ni harakati za kuelekea uchaguzi mkuu ndani ya chama mwaka 2014 ambapo nafasi inayoleta vuta nikuvute ni ya uenyekiti.wapo wanaopenda mwenyekiti aliyepo madarakani agombee tena wengine wanasema angeondoka hata leo...aachie vijana waonyeshe vipaji...
my take;nawashari viongozi wangu watulie na kuwa wamoja katika masuala haya ili chama kiendelee kukua..kuteleza si kuanguka..
my take;nawashari viongozi wangu watulie na kuwa wamoja katika masuala haya ili chama kiendelee kukua..kuteleza si kuanguka..