Mongoiwe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 524
- 263
SAKATA la Jossephini na Dk. Slaa, leo jioni limemfanya Makamu Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Benno Malisa kuzomewa hapa Geita wakati akimnadi ubunge wa CCM jimbo la Geita Donard Max.
Kilishomponza Malisa ni kuwaambia wananchi wa Geita kuwa Dk. Slaa ni Paroko aliyeshindwa kuongoza kanisa sasa anataka kuongoza nchi, na kueleza MAANA YA NENO FISADI kwamba Kenya wanatambua kuwa Fisadi ni MTU ANAYETEMBEA NA WAKE ZA WATU, Hivyo kumtaja Dk. Slaa ni Fisadi namba moja kwa vile ndiye aliyepora mke wa mtu.
Baada ya kutamka maneno hayo umati wa wananchi uliokuwa umejaa katika kiwanja cha Kalangalala mjini Geita ulianza kumzomea na na kuonyesha alama ya vidole viwili (Vyema).
Kilishomponza Malisa ni kuwaambia wananchi wa Geita kuwa Dk. Slaa ni Paroko aliyeshindwa kuongoza kanisa sasa anataka kuongoza nchi, na kueleza MAANA YA NENO FISADI kwamba Kenya wanatambua kuwa Fisadi ni MTU ANAYETEMBEA NA WAKE ZA WATU, Hivyo kumtaja Dk. Slaa ni Fisadi namba moja kwa vile ndiye aliyepora mke wa mtu.
Baada ya kutamka maneno hayo umati wa wananchi uliokuwa umejaa katika kiwanja cha Kalangalala mjini Geita ulianza kumzomea na na kuonyesha alama ya vidole viwili (Vyema).