Mwenda_Pole
JF-Expert Member
- Jul 5, 2008
- 281
- 66
Nilikuwa nasikiliza Radio Maria jana usiku mida ya saa mbili hivi ya usiku,
kama kawaida leo kulikuwa na kisa kingine, acha bwana duniani kuna mambo.
Kisa chenyewe ni hichi,
Nilikutia kati lakini kwa haraka ni kuwa kuna Mwana Dada mmoja ameolewa na wanaishi pamoja na mume wake na walikuwa na msichana wa kazi (House Girl/ Maid), Huyo mdada alikuwa anafanyakazi lakini huyo mume alikuwa hafanyi kazi kwa wakati huo haya yakitokea na walikuwa hawajafanikiwa kupata mtoto.
Kutokana na kazi huyo Mdada huwa anaondoka nyumbani asubuhi na kurudi jioni karibu kila siku. Yule mdada alianza kusikia kwa majirani kuwa yule jamaa hana tabia nzuri, alikuwa "anatembea" na yule msichana wa kazi na pia alikuwa anatongoza tongoza wanawake wa hapo mtaani na amekwisha tembea na wasichana/wanawake kadhaa wa hapo mtaani.
Baada ya kusikia hivyo akatafuta jinsi ya kujua ukweli wa hili suala, kutokana na ratiba yake ya kazi akaona njia nzuri ni kuleta mdogo wake aje akae pale nyumbani ili awe kama mchunguzi wake japokuwa hakuwa amemwambia kuhusu huyo kazi kwani aliona ni wazi kama kuna vitu visivyo vizuri vinaendelea kwa mme wake ni wazi mdogo wake angemwambia tu.
Muda ukapita bila kusikia lolote kutoka kwa mdogo wake na zile story za mtaani zikiendelea. Baada ya muda hivi hali ya pale nyumbani ikaanza kibadilika. Yule msichana wa kazi akaanza kulalamika mara kwa mara kuwa anajikisika mgonjwa huku akitapika tapika, punde na yule msichana mwingine (mdogo wa yule mke) na yeyey akaanza hali kama ile ya yule house girl kuugua mara kwa mara pamoja na kutapika tapika.
Kuona hivyo yule mdada siku moja akaomba ruhusa kazini na kuwachukua wote wawili na kuwapeleka hospitali kwa ajili ya vipimo, walichekiwa na wote kuonekana wanafanana kwa kila kitu, wote wawili walikuwa na malaria na pia walikuwa wajawazito. Akarudi nao nyumbani akawaweka kitimoto mme wake nae akiwepo ili wataje ni wa kina nani walio wapa hizo mimba ili waone hatua cha kuchukua. Lakini wale wasichana hawakutaja mtu huku wakati wote wakiwa wanamuangalia yule jamaa. Baada ya kugoma kutaja akaachana nao siku hiyo na kama baada ya siku 2 akamhoji kila mmoja kivyake. Kutahamaki wote wakamtaja kuwa yule jamaa (Mume wa huyo Mdada) ndio aliowapa mimba.
Duh kusikia hivyo yule mdada akachanganyikiwa asijue nini cha kufanya,
baada ya mume wake kampa mimba msichana wa kazi pamoja na mdogo wake (mdogo wa huyo Mke wa jamaa).
Aliona uamuzi mzuri ni yeye kuondoka na kuwaachia nyumba hao wasichana wajawazito na mume. Kabla hajachukua uamuzi akapeleka radioni kupata ushauri wa nini cha kufanya.
Kuna watu walipiga simu na wengi waliangukia katika makundi haya 3 walisema aondoke kwani kilikuwa ni kitendo cha aibu sana, wengine wakasema aendelee kukaa na mume wake ila awafukuze wale wasichana na wengine wakasema waendelee kuishi tu kama sasa awaache wale wasichana wakae hapo wajifungue na wawatunze tu hao watoto.
Ungekuwa wewe ungefanyaje? ama unamshauri nini huyu dada?
N.B: Hiki ni kisha cha kweli
kama kawaida leo kulikuwa na kisa kingine, acha bwana duniani kuna mambo.
Kisa chenyewe ni hichi,
Nilikutia kati lakini kwa haraka ni kuwa kuna Mwana Dada mmoja ameolewa na wanaishi pamoja na mume wake na walikuwa na msichana wa kazi (House Girl/ Maid), Huyo mdada alikuwa anafanyakazi lakini huyo mume alikuwa hafanyi kazi kwa wakati huo haya yakitokea na walikuwa hawajafanikiwa kupata mtoto.
Kutokana na kazi huyo Mdada huwa anaondoka nyumbani asubuhi na kurudi jioni karibu kila siku. Yule mdada alianza kusikia kwa majirani kuwa yule jamaa hana tabia nzuri, alikuwa "anatembea" na yule msichana wa kazi na pia alikuwa anatongoza tongoza wanawake wa hapo mtaani na amekwisha tembea na wasichana/wanawake kadhaa wa hapo mtaani.
Baada ya kusikia hivyo akatafuta jinsi ya kujua ukweli wa hili suala, kutokana na ratiba yake ya kazi akaona njia nzuri ni kuleta mdogo wake aje akae pale nyumbani ili awe kama mchunguzi wake japokuwa hakuwa amemwambia kuhusu huyo kazi kwani aliona ni wazi kama kuna vitu visivyo vizuri vinaendelea kwa mme wake ni wazi mdogo wake angemwambia tu.
Muda ukapita bila kusikia lolote kutoka kwa mdogo wake na zile story za mtaani zikiendelea. Baada ya muda hivi hali ya pale nyumbani ikaanza kibadilika. Yule msichana wa kazi akaanza kulalamika mara kwa mara kuwa anajikisika mgonjwa huku akitapika tapika, punde na yule msichana mwingine (mdogo wa yule mke) na yeyey akaanza hali kama ile ya yule house girl kuugua mara kwa mara pamoja na kutapika tapika.
Kuona hivyo yule mdada siku moja akaomba ruhusa kazini na kuwachukua wote wawili na kuwapeleka hospitali kwa ajili ya vipimo, walichekiwa na wote kuonekana wanafanana kwa kila kitu, wote wawili walikuwa na malaria na pia walikuwa wajawazito. Akarudi nao nyumbani akawaweka kitimoto mme wake nae akiwepo ili wataje ni wa kina nani walio wapa hizo mimba ili waone hatua cha kuchukua. Lakini wale wasichana hawakutaja mtu huku wakati wote wakiwa wanamuangalia yule jamaa. Baada ya kugoma kutaja akaachana nao siku hiyo na kama baada ya siku 2 akamhoji kila mmoja kivyake. Kutahamaki wote wakamtaja kuwa yule jamaa (Mume wa huyo Mdada) ndio aliowapa mimba.
Duh kusikia hivyo yule mdada akachanganyikiwa asijue nini cha kufanya,
baada ya mume wake kampa mimba msichana wa kazi pamoja na mdogo wake (mdogo wa huyo Mke wa jamaa).
Aliona uamuzi mzuri ni yeye kuondoka na kuwaachia nyumba hao wasichana wajawazito na mume. Kabla hajachukua uamuzi akapeleka radioni kupata ushauri wa nini cha kufanya.
Kuna watu walipiga simu na wengi waliangukia katika makundi haya 3 walisema aondoke kwani kilikuwa ni kitendo cha aibu sana, wengine wakasema aendelee kukaa na mume wake ila awafukuze wale wasichana na wengine wakasema waendelee kuishi tu kama sasa awaache wale wasichana wakae hapo wajifungue na wawatunze tu hao watoto.
Ungekuwa wewe ungefanyaje? ama unamshauri nini huyu dada?
N.B: Hiki ni kisha cha kweli