Unazikumbuka enzi za Barua!

Leo kuna njia mbalimbali za kuwasiliana ila kile kipindi tunaandikiana mabarua ",....kwako wewe uliyembali sijui na upeo wangu..,,.....," dhumuni la barua hii......"jamani barua (sio kadi) zimepoteza mvuto??? au ndo kwenda na wakati!

Maneno haya ilikuwa ni lazima yawepo: '... mpenzi ninakupenda sana, kula sili, kulala silali. Tafadhali naomba majibu mapema baada na hata kabla ya kupata barua hii ...' Lo, kilikuwa kipindi kizuri sana ambacho kizazi cha leo wanakosa mengi.
 
Barua za mapenzi zilikuwa nzuri na za kusisimua zaidi kuliko meseji za simu, kwa sababu.
  1. Mtu alikuwa anaandika kitu alichokibuni kutoka moyoni
  2. Barua ilikuwa na michoro ya kusisimua yenye ishara za mapenzi
  3. Barua ilikuwa ndefu haaishi hamu
  4. Wakati mwingine ilikuwa na nyongeza ya mashairi au nyimbo za wakati ule ambazo zilikuwa zinasisimua sana sio hizi za sasa eti demu wangu, demu wangu sijui kachakachuliwa aaah!
SIMU HAZINA UTAMU
  1. Mapenzi yake ni ya kompyuta yaani mtandao unatengeneza meseji za mapenzi wewe unatuma tu.
  2. Ujumbe wake ni mfupi sana na hauingii moyoni
  3. Ubunifu wa maneno matamu ya mapenzi unakuwa mdogo kwa sababu yanakuwa mafupi mno.
  4. Watu hawabuni kutoka moyoni ndio maana meseji ya aina moja unaweza kutumiwa na watu kumi tofauti Natamani zama za barua zirudi tena.
  5. Halafu unajua tu kuwa hizi ni kamba za mtandao

sasa kaka kwa ushauri wangu unaonaje tulejee enzi zetu maana vijana wanatupoteza bwana, sisi tuanze wataiga tu na kurudisha heshima ya barua
 
Niliacha kusoma na kuandika barua nilipoandikiwa mwishoni mwa barua ' usipopata hii barua nijulishe'

Niliishiwa nguvu kabisa
 
Maneno haya ilikuwa ni lazima yawepo: '... mpenzi ninakupenda sana, kula sili, kulala silali. Tafadhali naomba majibu mapema baada na hata kabla ya kupata barua hii ...' Lo, kilikuwa kipindi kizuri sana ambacho kizazi cha leo wanakosa mengi.

Hahahahahaaaa!...............umenivunja mbavu mdau sasa atjibuje wakati barua hata haijamfikia. so msomaji aliportray hamu yake ya kupata majibu. duh ilikuwa bomba na ukisoma lazima kesho utie ndani ya mfuko wa shule ukawaonyeshe ma-best kuwa unapendwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom