Esther Kimario
Member
- Nov 17, 2011
- 62
- 13
Ni kweli wengi tunatafuta kazi, lakini ni muhimu kujua kama kweli tunazihitaji kazi hizo, vinginevyo kazi hizo zitageuka KUWA LAANA kwetu! Nina ndugu yangu ambaye alikaa muda mrefu bila kazi, mwisho alichakachua cheti cha form four na kupata kazi ya jeshi. Cha kushangaza alipopata tuu akatafuta cheti kingine cha kufoji kinachoonesha ni mgonjwa! Kwa miaka zaidi ya mitano anakwenda kuripoti tuu kazini na kurudi nyumbani!! Na anajisifia sana kwa hili... Mimi nasema HII NI LAANA na mtu kama huyu hapaswi kuwa na kazi!!!!! KABISA!! Najisikia vibaya kuwa mimi nakatwa hela mwisho wa mwezi (PAYE na makato mengine kibao) kumlipa mshahara mzembe kama huyu!!!!!
Serikali nayo iamke bana!! utamlipaje mtu kwa miaka mitano mshahara kwa yeye kufika na kuripoti kazini na kurudi??:argue:
Jamani naombeni tukipata kazi tuwatendee haki wenzetu na tuitendee haki nchi yetu!!!!!
Serikali nayo iamke bana!! utamlipaje mtu kwa miaka mitano mshahara kwa yeye kufika na kuripoti kazini na kurudi??:argue:
Jamani naombeni tukipata kazi tuwatendee haki wenzetu na tuitendee haki nchi yetu!!!!!