unahitaji wazo la biashara ? soma hapa.

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
wadau napenda kuliona hili jukwaa la watu wanaopeana mbinu za kutatua matatizo na sio walalamishi, hivyo basi kama unawazo jipya la biashara liweke hapa au modify waliyoweka wengine.
Naanza mimi: ningekuwa na mtaji au kwa watu wenye mtaji naona kujenga vyoo kwenye barabara kuu sehemu ambazo watu huwa wanachimba dawa unaweza kuwa mradi mzuri, ni kwamba kila abiria kwenye gari analipia kama tsh mia mbili hivi kwa magari ya abiria na watu binafsi. Nahisi ni biashara ya uhakika sababu watu hawapendi kujisaidia wazi kama wanyama pia ni aibu wageni kutoka nje kuondoka na picha eti watanzania wanajisaidia hovyo. mwana jamii irekebishe hii au to wazo lako jipya hasa lisilo hitaji mtaji mkubwa.
 
wadau napenda kuliona hili jukwaa la watu wanaopeana mbinu za kutatua matatizo na sio walalamishi, hivyo basi kama unawazo jipya la biashara liweke hapa au modify waliyoweka wengine.
Naanza mimi: ningekuwa na mtaji au kwa watu wenye mtaji naona kujenga vyoo kwenye barabara kuu sehemu ambazo watu huwa wanachimba dawa unaweza kuwa mradi mzuri, ni kwamba kila abiria kwenye gari analipia kama tsh mia mbili hivi kwa magari ya abiria na watu binafsi. Nahisi ni biashara ya uhakika sababu watu hawapendi kujisaidia wazi kama wanyama pia ni aibu wageni kutoka nje kuondoka na picha eti watanzania wanajisaidia hovyo. mwana jamii irekebishe hii au to wazo lako jipya hasa lisilo hitaji mtaji mkubwa.

Mkuu RG, yaan hili bado ni wazo! Au umeshaanza kulifanyia kazi? Hapo kwenye red sio tatizo sana, kwani mtaji mkubwa zaidi ni kichwa chako. Kwan utahitaji kiasi gani kuongea na serikali ya kijiji ili wa kupatie eneo kwenye hayo maeneo watu wanayochimba dawa?

Kumbuka unaweza ukaanza kujenga choo kwa rasilimali zinazopatikana pale pale. Kikubwa zaidi ni usafi. Kitu kingine cha msingi, ni by laws (ambazo ni lazima zitungwe na serikali ya kijiji) ili kuwadhibiti watu watakaokuwa wanachafua mazingira baada ya uwepo wa hizo huduma za choo.

Ukitaka utekelezaji uwe mzuri na rahisi, ifanye iwe SOCIAL ENTERPRISE, na ushirikiane na kijiji husika. Kwa kufanya hivi ardi utapata bure (kama machango wa kijiji). Ukiweza kutengeneza proposal nzuri, unaweza ukapata wadhamini, kwani mradi huu ni suala mtambuka na taasisi nyingi zina interest huko kwenye mambo ya sanitation

All the best
 
hilo bado ni wazo sijatake even a single step, halafu kuifanya social interprise ni wazo ambalo nililifikiria pia, maeneo yale watu huwa wanauza na snacks kwa hiyo mnakuwa mnawezeshana kwa kuboresha mazingira ya biashara, hivi NEMC hawawezi kuhusika hapo?
 
hilo bado ni wazo sijatake even a single step, halafu kuifanya social interprise ni wazo ambalo nililifikiria pia, maeneo yale watu huwa wanauza na snacks kwa hiyo mnakuwa mnawezeshana kwa kuboresha mazingira ya biashara, hivi NEMC hawawezi kuhusika hapo?

NEMC hawawezi kuwa kikwazo kwenye mradi mdogo kama huu. Go for it, mkuu
Anza kwa kuainisha maeneo husika watu wanayopenda kuchimba dawa kienyeji? Kisha fanya utafiti kuhusu suala la umiliki na uangalie ni eneo lipi litakuwa muafaka kwako kwa kuanzia
 
Mie napenda sana kuwa na biashara yangu.
Tatizo nahisi kuwa nakuwa na vibes za negativity wakati wote.
naona vikwazo kuliko opportinities.
Mfano tu kwa mradi huu hapa naona kama itakuwa capital kubwa sana kusafiri hadi sehemu utakayoweka ofisi mara kwa mara kuisimamia. Ukijua kuwa Tanzania hii, biashara bila kuisimamia mwenyewe, ni kumuanzishia huyo mfanyakazi.
Naombeni msaada nitoke huku gizani
 
ukiona mawazo hasi yanakuja anza kufikiria njia anazoweza kuepuka au kusolve hizo challenges usiache vikwazo ndio viwe mwisho wako. mfano kuhusu kusafiri unaweza kupanga labda mara moja kwa mwezi labda iwe imejensi halafu biashara yenyewe sidhani kama inataka uangalizi mwingi, kama unaogopa kuibiwa mwanzoni unafanya research ujue kwa siku unaweza kuingiza tsh ngapi halafu unamwambia mfanyakazi upate daily report ya mapato na matumizi hapo huwezi ibiwa.
jamani wenye mawazo huko lets share!
 
mkuu

wazo zuri, siku hizi kuna style nyingi za ku-manage biashara ambapo lazima uwe na controlling tools za uhakika,

ningekushauri ufanye built and outsource operations, jenga vyoo, weka standards zako za usafi na ada ya matumizi, tafuta mtu au kikundi cha watu mbalimbali, wape waendeshe hivyo vyoo kwa kuwapangia hesabu ya siku baada ya kuwa umeshaestablish kiasi cha mapato kwa siku kwa kufanya pilot study ya collections, hata wafanya usafi outsource, pesa yako iingie kwenye m-pesa kila siku, kama utakuwa na vituo katika njia za kaskazini, kati na kusini unaweza ukafanikiwa vizuri

assume njia ya kaskazini ina mabasi zaidi ya 40 yanayofanya safari kila siku

assume watakao tumia huduma hiyo ni 70% ya basi lenye abiria 60 - 42 passengers per day

42 x TZS 300 per person = 12,600

12,600 x 40 buses = 504,000

ukiwa na vituo 5 vyenye choo njia zote kubwa - 504,000 x 5 = 2,520,000 per day

weka mabasi madogo na magari madogo mengine katika vituo hivyo vyote yaingize 300,000 per day

total = TZS 2,820,000

chukua 40% ya kipato chote = TZS 1,128,000 per day

oooppppps, too good to be true

hebu na wadau wengine watoe mawazo yao

have a good day
 
mkuu

wazo zuri, siku hizi kuna style nyingi za ku-manage biashara ambapo lazima uwe na controlling tools za uhakika,

ningekushauri ufanye built and outsource operations,
hili wazo la kufanya outsourcing nimelipenda linaweza pia kupunguza worries tha Haika
 
Mie napenda sana kuwa na biashara yangu.
Tatizo nahisi kuwa nakuwa na vibes za negativity wakati wote.
naona vikwazo kuliko opportinities.
Mfano tu kwa mradi huu hapa naona kama itakuwa capital kubwa sana kusafiri hadi sehemu utakayoweka ofisi mara kwa mara kuisimamia. Ukijua kuwa Tanzania hii, biashara bila kuisimamia mwenyewe, ni kumuanzishia huyo mfanyakazi.
Naombeni msaada nitoke huku gizani

Mkuu, kuwa na biashara, haimaanishi ni lazima uisimamie mwenyewe (yaan uwe owner manager). Pitia huo ushauri wa LAT hapo juu uongeze uelewa kwenye masuala ya outsourcing. Au labda jiulize halmashauri nyingi zinaendesha vipi vitegauchumi vyake? (Swali hili "Mbona kiasi cha mapato wanachokubaliana na hao waendeshaji kwa mwezi ni kidogo?" linahitaji mjadala mwingine)

Na hapo kwenye RED, usijishangae sana kwani haupo peke yako, huu ni ugonjwa mkubwa kwenye sehemu pana ya Jamii zetu. I bet it has something to do with Emotional Intelligence (chanzo chake ni nini? huu ni mjadala mwingine) lakin tiba yake ya kwanza (kwa mujibu wa mimi) ni kutafuta ukombozi wa kifikra kwa kujisomea vitabu (inspirational novels) tofauti tofauti (lakin hasa vinavyohusiana na mambo ya ujasiriamali na biashara)

Unaweza ukaanza na hiki ingawa hakihusiani na ujasiriamali, "HOW TO CONQUER NEGATIVE EMOTIONS" by Roy Masters
 
mkuu

wazo zuri, siku hizi kuna style nyingi za ku-manage biashara ambapo lazima uwe na controlling tools za uhakika,

ningekushauri ufanye built and outsource operations, jenga vyoo, weka standards zako za usafi na ada ya matumizi, tafuta mtu au kikundi cha watu mbalimbali, wape waendeshe hivyo vyoo kwa kuwapangia hesabu ya siku baada ya kuwa umeshaestablish kiasi cha mapato kwa siku kwa kufanya pilot study ya collections, hata wafanya usafi outsource, pesa yako iingie kwenye m-pesa kila siku, kama utakuwa na vituo katika njia za kaskazini, kati na kusini unaweza ukafanikiwa vizuri

assume njia ya kaskazini ina mabasi zaidi ya 40 yanayofanya safari kila siku

assume watakao tumia huduma hiyo ni 70% ya basi lenye abiria 60 - 42 passengers per day

42 x TZS 300 per person = 12,600

12,600 x 40 buses = 504,000

ukiwa na vituo 5 vyenye choo njia zote kubwa - 504,000 x 5 = 2,520,000 per day

weka mabasi madogo na magari madogo mengine katika vituo hivyo vyote yaingize 300,000 per day

total = TZS 2,820,000

chukua 40% ya kipato chote = TZS 1,128,000 per day

oooppppps, too good to be true

hebu na wadau wengine watoe mawazo yao

have a good day

Mkuu, namna ulivyo break down hii kitu, mpaka inavutia, (lakini ungemalizia na ceteris peribus ingekaa vizuri zaidi). Sasa kazi ipo kwa RG. Inaonekana hata payback period ya huu mradi haiwezi kuwa ni zaidi ya miaka miwili

1,128,000 x 30
= ?
Ooh my God, are we talking about 33,840,000/= Tsh? (40% of Monthly income)
Wako wapi wataalamu wa ujenzi, waje watupe BOQ?
 
Umeniibia wazo langu wewe,nimewaza hchi kitu miaka lakini huwa nasema watajenga 2 siku moja especially kutoka moshi kwenda dar,
 
Umeniibia wazo langu wewe,nimewaza hchi kitu miaka lakini huwa nasema watajenga 2 siku moja especially kutoka moshi kwenda dar,

Haa haa haa, unapaswa kujisifia kwa kutambua OPPORTUNITY (kwan kwa wengine ni kazi sana). Halafu kufanana mawazo si tatizo, tatizo liko hapo kwenye namna ya kuyaweka haya mawazo kwenye vitendo (UNIQUENESS). By the way mbona wewe hukulitekeleza hili kwa kipindi chote hicho? Au changamoto ndio ile ile anayosema RG? (Capital)

Hivi Mamzalendo kwenye hii Barabara (Dar- Arusha), ni sehemu gani watu wanapochimba Dawa kienyeji? Mbona Pale Msata (kwenye mizani) nimeona hii huduma? Halafu barabara hii inahoteli nyingi sana njiani, hivyo ni rahisi kupata hizi huduma (mfano Highway Hotel)
 
Haa haa haa, unapaswa kujisifia kwa kutambua OPPORTUNITY (kwan kwa wengine ni kazi sana). Halafu kufanana mawazo si tatizo, tatizo liko hapo kwenye namna ya kuyaweka haya mawazo kwenye vitendo (UNIQUENESS). By the way mbona wewe hukulitekeleza hili kwa kipindi chote hicho? Au changamoto ndio ile ile anayosema RG? (Capital)

Hivi Mamzalendo kwenye hii Barabara (Dar- Arusha), ni sehemu gani watu wanapochimba Dawa kienyeji? Mbona Pale Msata (kwenye mizani) nimeona hii huduma? Halafu barabara hii inahoteli nyingi sana njiani, hivyo ni rahisi kupata hizi huduma (mfano Highway Hotel)

my friend suala ni capital lakini pia hiyo ardhi,nilianza kuwaza jambo hili kuna siku nilimeza dawa jamani nilitamani kuwamaliza wa2 wa kmanjaro bus ni siku hyo oh hatusimami hadi highway,majina sitaweza kujua kwa usahihi mpendwa ila kwa kweli ukitoka moshi hadi highway halafu highway dar haifai,hotel zipo lakini hawasimami mkuu,labda vikijengwa hivi vitu itakuwa sio ombi tena kusimama na viwe katika umbali maalumu,
 
ma mzalendo ukiona inafaa changamkia faster kaongee na wadau,siku tukitaka kujiingiza tunakukukuta umejaa full tutatafuta kitu kingine na hili linchi tutakuwa tunalisogeza mdogomdogo. vipi haukuwa na wazo lingine?
 
Umeniibia wazo langu wewe,nimewaza hchi kitu miaka lakini huwa nasema watajenga 2 siku moja especially kutoka moshi kwenda dar,

hujaibiwa wazo lako,business ideas ni zile zile ambazo huwa tunaweza kila siku gap ipo kwenye implementation hapo huwa tunatofautiana.
 
Wazo zuri sana RG. Nafikiri inabidi ulifanyie kazi hata kama huna mtaji kwa sasa hivi. Unaweza kuanza kuandika Master Plan ya business nzima wakati huu. Survey maeneo ambayo unaweza weka biashara katika route tofauti, jinsi ambavyo biashara itaendesheshwa, n.k. Kuhusu wafanyakazi, unaweza ukatafuta mtu mwenye kiwanja karibu na barabara mkakubaliana profit sharing kwa yeye kukupa kiwanja ujenge halafu yeye awe msimamizi.

Still there's so many way this can be done. Keep up!
 
Wazo zuri, weka katika vitendo niliona Namibia njia ya Windhoek - Wavis Bay, halikuhusisha huduma ya Msalani tu, bali hata uchafu mwingine.
 
Chalenji ya biashara hii ni maji. Ili kumaintain usafi na ubora, lazima kuwe na maji ya kutosha. Solution yaweza kuwa kuchimba kisima kirefu, kuweka pump, tank na generators.
 
Wananchi nemefurahishwa sana na hili group.

ila kwasasa naomba mnisaidie wazo la biashara ambalo litakidhi vigezo vifuatavyo.

1. Kutunza mazingira.
2. Kutoa ajira kwa wanawake.
3. Kuingiza kipato.

Nimeumiza sana kichwa nimekosa kabisa nisaidieni wakuu.
 
Back
Top Bottom