Nape Nnauye
MP Mtama
- Dec 26, 2012
- 99
- 408
Naandika hili kwa masikitiko makubwa maana watani zangu CHADEMA siku zao zinahesabika kwa kasi inayonitisha sana. Mimi ni muumini wa uimara wa CCM kutegemea sana uimara na umakini wa upinzani nchini! Kwahiyo anguko la upinzani nchini si jambo zuri kwa CCM, nchi na demokrasia yetu, CHADEMA kikiwa moja ya taasisi muhimu kwenye ukiaji wa demokrasia hiyo.
Kilichonistua ni degree ya unafiki inayojidhihirisha kila kukicha ya viongozi wengi wa CHADEMA. Kupinga ufisadi kwa mdomo mpana halafu unaendesha Chama kwa pesa hizohizo huu ni unafiki wa ajabu! Tunajifunza nini kwa kiongozi wa Chama anayesema pesa ni pesa tu inategemea unaitumiaje!!? Ha! Kwahiyo unaweza kuuza nchi ilimradi unapewa pesa.
Niliwahi kutoa mfano mkubwa wa unafiki wa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa (sikuhizi nasikia vijana wanamwita Mzee wa Gongo) akihubiri watu waichukie CCM.
Na wakati mwingine alihamasisha wachane na hata kuchoma kadi za CCM wakati yeye kabanisha yake tena kwa matunzo makubwa! Huu ni unafiki mkubwa! Vijana tunajifunza nini kwa unafiki huu.
Lakini niliwahi kusema Chadema kinaendeshwa kwa pesa kutoka nje, wakabwata wakinipa siku saba kukanusha, kabla mate hayajakauka, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Ndg. Zitto anakiri hadharani kuwa gazeti leo, ambacho ni chombo kikuu cha propaganda limeanzishwa kwa pesa kutoka nje!! Huwezi kujenga Chama kwa msingi wa uongo kuliko wa shetani halafu ukadhani chama kitadumu.
Utaratibu wa vyama kufukuza wanasiasa vijana kwenye vyama hivyo ni wa hovyo na unapaswa kukemewa! Vijana wasipokosea mnataka wakafanyie wapi makosa?? Vyama lazima vitumike kulea na kuwafumdisha vijana badala ya kuwafukuza. Toka watani zangu waanze kufukuza wamekuwa wakifukuza vijana tu hasa wanaohoji. Kuhoji ndani ya CHADEMA ni mwiko! Mtakumbuka ya Kafulila na vijana wengine wengi tu. Mtauliza we Nape!! Ndio mimi chama changu kilinisikiliza na ndio maana nipo sikufukuzwa! Ukomavu ni pamoja na kuwa tayari kusikiliza maoni tofauti na uliyonayo.
Ushauri wa bure: Watani anzeni upya! Msione aibu fumua anza upya tutawasubiri mkomae msihofu kuachwa sana! Mmekutana na ajali ya kisiasa kutafuta mchawi sio dawa, tafuteni mmejikwaa wapi.
Kilichonistua ni degree ya unafiki inayojidhihirisha kila kukicha ya viongozi wengi wa CHADEMA. Kupinga ufisadi kwa mdomo mpana halafu unaendesha Chama kwa pesa hizohizo huu ni unafiki wa ajabu! Tunajifunza nini kwa kiongozi wa Chama anayesema pesa ni pesa tu inategemea unaitumiaje!!? Ha! Kwahiyo unaweza kuuza nchi ilimradi unapewa pesa.
Niliwahi kutoa mfano mkubwa wa unafiki wa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa (sikuhizi nasikia vijana wanamwita Mzee wa Gongo) akihubiri watu waichukie CCM.
Na wakati mwingine alihamasisha wachane na hata kuchoma kadi za CCM wakati yeye kabanisha yake tena kwa matunzo makubwa! Huu ni unafiki mkubwa! Vijana tunajifunza nini kwa unafiki huu.
Lakini niliwahi kusema Chadema kinaendeshwa kwa pesa kutoka nje, wakabwata wakinipa siku saba kukanusha, kabla mate hayajakauka, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Ndg. Zitto anakiri hadharani kuwa gazeti leo, ambacho ni chombo kikuu cha propaganda limeanzishwa kwa pesa kutoka nje!! Huwezi kujenga Chama kwa msingi wa uongo kuliko wa shetani halafu ukadhani chama kitadumu.
Utaratibu wa vyama kufukuza wanasiasa vijana kwenye vyama hivyo ni wa hovyo na unapaswa kukemewa! Vijana wasipokosea mnataka wakafanyie wapi makosa?? Vyama lazima vitumike kulea na kuwafumdisha vijana badala ya kuwafukuza. Toka watani zangu waanze kufukuza wamekuwa wakifukuza vijana tu hasa wanaohoji. Kuhoji ndani ya CHADEMA ni mwiko! Mtakumbuka ya Kafulila na vijana wengine wengi tu. Mtauliza we Nape!! Ndio mimi chama changu kilinisikiliza na ndio maana nipo sikufukuzwa! Ukomavu ni pamoja na kuwa tayari kusikiliza maoni tofauti na uliyonayo.
Ushauri wa bure: Watani anzeni upya! Msione aibu fumua anza upya tutawasubiri mkomae msihofu kuachwa sana! Mmekutana na ajali ya kisiasa kutafuta mchawi sio dawa, tafuteni mmejikwaa wapi.