Ultimatum: Serikali ina siku 14 kutangaza mahakama ya Kadhi! - Wahadhiri

Status
Not open for further replies.
.Hivyo kama wewe unaamini muundo wa canon law ktk Ukatoliki sioni sababu ya wewe kutaka kuniuzia mimi ambaye nimeukataa na kutokuwa Mkristu wa kanisa hilo la Katoliki..

Sijajaribu kukuuzia; nilikuwa naonesha ulinganifu na tofauti ya sheria za kanisa na sheria nchi kwamba siyo moja na hazihusiani.

Kisha basi, malelezo yako yote hapo juu unazungumzia Canon law ktk kanisa la Kikatoliki wakati hizi sheria zimeanza toka wakati wa Costantine akitawala Roma.

Hapana muundo wa sheria za Kirumi unatangulia Utawala wa Constantine wa Roma. Na Kanon Law siyo sawa na sheria za Kirumi.
Mkusanyiko wa sheria na kuachagua kile kinachkubalika ktk dhehebu moja sio Canon Law ya Ukristu ila ni ya dhehebu unalozungumzia.

Kuna Canon Law ya Kanisa Katoliki tu.

Labda kwa kukusahihisha vizuri ni kwamba Canon Law zimetumika kuunda mfumo, utaratibu na sheria za nchi nyingi za Magharibi na sisi kama tuloifga na kuchukua mengi toka kwa Watawala wetu (Muingereza) basi bila shaka sheria nyingi zimetokana na Canon law.

Kuna ukweli humo kama vile mfumo wa falsafa za Kirumi na kigiriki zina mchango wa wana Falsafa wa Kiarabu na mafundisho ya Kifalsafa ya mtu kama Mt. Thomas yana msingi mkubwa katika wanazuonni wa Kiislamu ambao walijifunza Aristotle. Sasa hilo siyo jambo geni, jamii mbalimbali duniani zimechangiana katika kuchangia ujuzi wa dunia. Hivyo, katika mifumo yetu sisi leo hii tuna michango ya elimu ya Kiislamu, Kikristu, Kigiriki n.k


Kwa hiyo unaposema sisi wakatoliki tunafanbya hivi na vile ni tafsiri ya Canon law according to Romans Catholic ambayo sii lazima ikubalike kwa Anglican..

Kuna Canon Law moja nayo ni Kanisa Katoliki. Makanisa mengine yanasheria na taratibu zao. Kumbuka kuwa makanisa mengine yote mengi yamekuja baada ya 1600 (kabla ya hapo kulikuwa na Kanisa Moja tu upande wa Magharibi)) na upande wa Mashariki kulikuwa na Kanisa moja la Orthodox (baada ya utengano wa 1054). Kabla ya hapo kulikuwa na kanisa moja tu.

Na madhehebu hayo mengine ya Kikristu yana taratibu zao za kuendesha makanisa yao na haviitwi Canon Law.

na haikuwekwa muhuri kufanyiwa marekebisho na madhebeu mengineyo ambayo yalijitenga na kanisa hilo.

Ndiyo maana zinaitwa Kanuni za Kanisa Katoliki.. siyo Kanuni za Ukristu.
Ni hizi taratibu za uongozi, sheria na tafsiri ya mambo mengi ndizo zimetugawanya katika dini na madhehebu mbalimbali..

Tofauti zetu zinaletwa na mambo mengi zaidi kuliko Sheria za Kanisa.
Hivyo kuwepo kwa mahakama ya kanisa Katoliki na nguvu alopewa Padre au Vatica huwezi kuijengea hema ikawa mfano bora kwa madhehebu mengine ya Kikristu au hata Waislaam,.

Kwanini isiwe wakati Ukatoliki nao ni dini, na mambo yanayohusu mahakama hizo yanayuhusu Ibada, ndoa na mambo ya utawala wa Kanisa hilo?

.kwani waislaam hata yule sheikh Mkubwa wa msikiti wa Mecca bado ni binadamu ambaye hana madaraka makubwa kwa Waislaam wote duniani, hata yeyey anafuata kitabu hicho hicho nachokifuata mimi na anafuata sheria sawa na mimi Mkandara ambaye hata kusalisha watu wawili ni jambo kubwa kwangu.

Na hapo ndipo matatizo yalipo; na ndio sababu wanahitaji serikali kuingilia kati kwani hakuna chombo cha juu cha kusimamia maslahi yote.

Na nazidi kusema ndio maana sote hapa tunaamini dini tofauti kutokana na mifumo kama hii laa sivyo sisi sote tunaamini Mungu mmoja, tungekuwa dini..

labda.
Halafu tazama basi unavyozi8di kujipiteza kwa madai kwamba kama Bakwata sio chombo cha Waislaam je chombo chao ni kipi?..

Siyo madai yangu hayo, hayo ni madai ya baadhi ya Waislamu ambao wameikataa Bakwata kuwa si chombo chao.


Mkuu huwezi kuelewa kwa sababu wewe sii Muislaam. Huwezi kupima uzito wa wa kitu kwa ujazo wa hekima ndani ya Uislaam.. Kifupi Waislaama hawana chombo isipokuwa wanaweza kuunda chombo kinachowakilisha waislaam ktk maswala ya uatwala nma sii dini kama unavyoijua KKK au chombo cha Kikristu..

Sasa huoni hapo ndio tatizo? Kwamba, kama hakuna chombo cha kusimamia maslahi yenu ni vigumu kuweza kujadili na kuwa na msimamo mmoja. Hapa ndipo haja ya serikali inaingia. Lakini sasa ni nani atakayezungumza na serikali kwa niaba ya Waislamu?

Bakwata sii chombo cha Waislaam ila ni chombo kilichoundwa na serikali kwa waislaam..

Je ipo haja ya kuwa na chombo cha Waislamu na nani akiunde?

Ni imani yangu kwamba bakwata iliundwa kwa mpango wa Kisiasa zaidi kukidhi mahitaji ya waislaam kisiasa hasa baada ya kuona nguvu ya KKK ktk Utawala ikabidi wawape Waislaam nao chombo chao ngoma ionekane draw

Na hao Waislamu wanajua hili tangu 1969?, miaka 40 iliyopita? Sasa wafanye nini ili kuondokana na Bakwata?
Bakwata wapo kama NGO zinazoundwa inayojidhughulisha zaidi na Uislaam ktk misaada, kukitangaza chama na kadhalika.. Kesho Bakwata inaweza kunyimwa kibali na ikafa lakini Uislaam hautaondoka kutokana na kufa kwa Bakwata.

Hilo ni kweli, na nisawa na TEC na CCT zinaweza kufutwa lakini Ukristu utaendelea kuwepo. ama?

Huwezi kulinganisha wala kufananisha Bakwata na KKK au chombo kinginecho cha kidini..

Naamini inawezekana tu.
 
Hivi hii Hoja sio Janja ya CCM kuwahamisha wananchi kutoka kwenye mada kuu ya UFISADI wakati w akipindi hiki cha kuelekea uchaguzi? Nahisi kama kwa vile issue za Meremeta, EPA, TANGOLD, Mwananchi, Richmond, TPL, TRL, TTCL, etc ni ngumu kutolea majibu, na kwa vile kuna uwezekano mkubwa kuwa hoja ya hizo pesa zilizopatikana kwenye huo ufisadi zilihusika kwenye kampeni za 05 na kwa vile wataka ukweli uwe wazi na wataka mabadiriko walikuwa wana nafasu nzuri ya kuifumbua macho jamii ya kitanzania, Je Haiwezekani kuwa hii ni strategic plan ya kuwaanyamazisha watu na kuwagawa ili kuunda fraction mbili, wanaotaka mahakam ya kadhi na wasiotaka, na baadaye enemy of the people atashinda tena>
 
Last edited:
Am a Christian but if this is true it is BAD! We are dividing Tanzanians into first and second class citizens; those financially supported by the government and those left to fend for themselves; those whose problems are readily dealt with and those whose problem solutions take eternity!!! -This is I repeat very, very bad.

MoU ya Serikali ya JMT
na
THE CHRISTIAN COUNCIL OF TANZANIA &
TANZANIA EPISCOPAL CONFERENCES

Versus

MAHAKAMA YA KADHI

TATHMINI KWA MAKINI tu unafiki na undumilakuwili wa wabunge na mawaziri
wetu kuhusu uamuzi waliochukua kwa
kuwakatia wakiristo sekta ya elimu na afya (jambo la kijamii na kiuchumi)
na kunyimwa haki ya Waislamu haki ya kuwa na Mahakama ya Kadhi (jambo la ibada na imani):

1. Haki ya Elimu na Afya ni kwa kila Mtanzania na sio jambo la dini
moja ila kama tunataka kuigawa nchi na jamii husika. Serikali yetu imeingia katika MoU inayopendelea upande
mmoja kwa hasara ya upande mwingine katika jamii inayostahili kuwa kitu kimoja,
****** ****** ******

2. Mahakama ya Kadhi sio mahakama ya kiserikali bali ni suala la ibada na
imani kwa Waislamu sio Tanzania tu bali dunia nzima, na haiwezekani kuwaachia watu wa dini nyingine kuja kusimamia masuala yetu ya ibada labda kama sote tunataka kwenda motoni,

****** ****** ******
3. MoU hiyo ina mtazamo kama vile Tanzania ni ya Wakiristo tu na Waislamu
hawakuwepo,hawapo na hawatakuwepo ili hali kila mmoja wetu anajua nani alipigania uhuru na ni nani alikaa pembeni au kumuunga mkono mkoloni wakati ule,

****** ****** ******
4. Waislamu wengi wanaamini katika hili kuwa nchi sasa inaongozwa na
Wakatoliki wakisindikizwa na
manasara wenzao na serikali tunayoichagua ni kofia tu,
****** ****** ******
4. Eti wanaoweza kuokoa masuala ya elimu, afya na tiba nchini ni
Wakatoliki na wenzao (of kozi kwa misaada
toka Ujerumani) lakini Waislamu hawawezi kwa kuwa haohao Wakatoliki na
Wamarekani wamewafungia Waislamu fursa ya kupata fedha toka nchi za Kiislamu kwa kisingizio cha ugaidi na
udobi wa fedha haramu. Je, Mahakama ya
Kadhi isingelichangia nayo kuinua sekta ya elimu na afya kwa kuwadhibiti
viongozi wabovu na mafisadi miongoni mwa Waislamu ? Vijana wa Kiislamu watakuwa na adabu, nidhamu na tabia njema bila kulelewa katika maadili na sheria za Kiislamu ? Au serikali na Wakatoliki wana njama za kutaka kuona ni vijana wa Kiislamu ndio wanaostahili kujaza magereza na kuwa mateja barabarani ?
****** ****** ******

5. MoU hiyo inaelekea imetungwa na kufikishwa serikalini bila serikali
kushirikishwa na litakuwa jambo la
kushangaza kama imekubalika na kusainiwa kama ilivyoandikwa na maaskofu
hao.
Je, ili haki hapa itendeke si na Waislamu nao chini ya mwamvuli mmoja
wangeliandika MoU yao kwa serikali juu ya Mahakama ya Kadhi na OIC na kuipeleka isaniwe na sio kuzungumzwa na
yeyote yule sembuse wasiohusika na imani
na ibada za Kiislamu na madhehebu yake,

****** ****** ******
6. Je, serikali inayopigiwa kura na watu wote hivi kweli inaweza kukubali
kutengwa kwa sababu yoyote ile
iwayo zaidi ya nusu ya wapiga kura wake kwa sababu yoyote ile ?
****** ****** ******

7. Serikali inafanya maamuzi kama vile haijui na haielewi jinsi suala la
elimu na afya lilivyo zito na linalogusa
maisha ya kila mtu na kwamba likichiwa na watu wenye tabia kama zile za
Wahutu wa Rwanda linaweza kuipeleka nchi pabaya. Au kama sivyo basi inaamini kwamba Waislamu wamechoka mno kiasi
ambacho wanahitajiwa kusaidiwa na
watu wenye imani tofauti na yao na wao watakubali na wataliona hili ni
sawa tu kwao ?
****** ****** ******
8. Waislamu walitaka Mahakama ya Kadhi na kwa kuwa hukumu za kesi
ambazo awali zingelipelekwa
kuhukumiwa kwenye mahakama isiyo na dini basi gharama zake huko zipewe
Waislamu kwa kuendesha mahakama
yao ya kiimani na kiibada bila utata wowote. Hili likakataliwa. Je,
inakuwaje sasa serikali hiyo hiyo kuwapa FEDHA
KWA MLANGO WA NYUMA wale ambao watazitumia fedha hizo ili kuchagua
madiwani wao, wabunge wao,
watumishi wao, wakuu wa wilaya wao, wakuu wa mikoa wao, mawaziri wao,
waziri mkuu wao na rais wao maana
hakuna tena chaguo la Mungu leo!!! Au serikali katika MoU hii ilichanganywa, kuchanganyikiwa au kujichanganya ?
****** ****** ******
9. Ni serikali gani yenye kujali haki na usawa inayoruhusu wakiristo
wapewe fedha na Ujerumani, Marekani,
Wakorea na Wazungu wengine halafu jamaa hao waziharamishe fedha
wanazopewa Waislamu na waislamu wenzao
kutoka sehemu nyingine duniani na hivyo kung'oa kabisa mizizi ya kuota na
kuendelea kwa Uislamu sehemu nyingi
hapa Tanzania ambazo zina watu wengi ambao wangelipenda kuwa Waislamu? Kwa uono wake serikali inadhani jambo hili linajenga udugu na umoja au linavibomoa ?
****** ****** ******
10. Je, haitatokea kuwa hadithi ya ngamia na Mwarabu jangwani kwa masuala
ya Wakiristo kuwa na Bodi za
Elimu na Afya?
****** ****** ******
11. Je, Tanzania inataka kuwa kama Belgium na magomvi yasiyokwisha kwa
kujenga tabaka mbili za jamii, yaani, jamii ya Wakiristo walionacho, na jamii ya Waislamu wasio nacho? Na hao
maaskofu wetu ndicho hicho
wanachokitaka kweli na masheikh nao wanalikubali hili ? Ni nini itakuwa
ya hatima ya msimamo na mtazamo kama huu
kwa muktadha wetu wa umoja na mshikamano wa kitaifa?
****** ****** ******
12. Nini kitatokea wakati Wakiristo ndio watakaokuwa wakimiliki viwanda
vyote vya uchapishaji vitabu na vifaa vya elimu hapa nchini na Waislamu hawana lao ? Au serikali haijui hii ndiyo nia ya wachapishaji vitabu wa Ujerumani na Marekani ili kukuza soko lao kupitia dini fulani ?
****** ****** ******
13. Nini kitatokea wakati Wakiristo watamiliki njia zote za usafiri (kama
ilivyoua biashara ya Muislamu wa
Scandinavia ili wakiristo watambe katika biashara hiyo hapa Tanzania)
achilia uwezo waliopewa TRA kuziadhibu
biashara za Waislamu na kuzipa ahueni biashara za Wakiristo ni nani
asiyejua hili.
Na juu ya hapo waweze kudhibiti kampuni za intaneti, simu za kawaida na
simu za mikononi huku Waislamu kama
wale wa Zantel wakiwekewa ngumu kila hatua ?
****** ****** ******
14. Nini kitakachotokea katika nchi endapo kama shule na vyuo vitakuwa
katika mpangilio huu:

SHULE NA VYUO BORA KABISA- ZOTE ZA WAKIRISTO

SHULE NA VYUO WASTANI-
ZOTE ZA SERIKALI

SHULE NA VYUO DUNI KABISA- ZOTE ZA WAISLAMU
****** ****** ******
15. Nini kitakachotokea dini mojawapo nchini itakapopora kazi ya 'Human
Resource Development' ambalo ni
jukumu la serikali na linalostahili kuwa katika sera mama ya chama chochote tawala kinachojua wajibu wake katika uongozi wa nchi na sio mtu mwingine ? Hatujui maana ya hili kama vile
hatukwenda shule jamani?
****** ****** ******
16. Inavyoelekea ni kwamba serikali imeshindwa kubainisha na kuonesha
waziwazi MIPAKA KATI YA
SHUGHULI ZA SERIKALI NA ZILE ZA MASHIRIKA YA KIDINI na hili sasa
linaifanya kufanya kazi kwa namna
ambayo inatia mashaka na tuhuma kubwa-ndani na nje ya nchi! Na MoU ya kiranja Wakatoliki ni tusi kwa serikali. MoU hiyo inawaambia viongozi kwamba wao maaskofu wana akili, uwezo, rasilimali, visheni, kompetensii na kapasitee kubwa zaidi ya kuongoza nchi kuliko wao na kuwa wamewaachia tu kwa sababu Katiba nawafungafunga lakini wanaamini wanaweza kuwapika watu wao, wao wenyewe, nao wakawa na uwezo mkubwa kuliko madiwani, wabunge, mawaziri, waziri mkuu na rais waliopo madarakani sasa,
****** ****** ******
17. Hivi kuna shirika la kidini litakalotamalaki katika kuwa na shule,
vyuo na hospitali litakaloajiri kwa urahisi
watu wa dini nyingine. Na hata likiwaajiri, je, litawathamini kama watu
wa dini yao ?
****** ****** ******
18. Je, ni busara na hekima kutoa ruzuku kwa SHULE, VYUO NA HOSPITALI za
WATU BINAFSI AMBAZO
HAZINA UDINI au kutoa hilohilo kwa MASHIRIKA YA KIDINI YENYE UDINI WA
KUPINDUKIA ?
****** ****** ******
19. Je, kwanini tunavumilia nchi kama UJERUMANI na zingine
zinazotanguliza UDINI kwanza wakati zikisaidia
nchi yetu. Je, nchi kama hii ina nia njema na hatima yetu ?
****** ****** ******
20. Je, SHIRIKA LA KIDINI KAMA WAKATOLIKI ambao wameanza kuonesha roho
mbaya kwa WAISLAMU
wakiachiwa kuagiza madawa ya binadamu na mifugo Waislamu watakuwa na
uhakika na usalama wa afya na maisha
yao? Na hasa katika miaka hii ambayo wenzetu wanatengeneza sio binadamu
tu bali hata manii kwenye maabara
achilia mbali 'genes' ambazo zinaamua mtu awe mbwia unga, ****** au
kafiri au mwenye kuabudu Mungu mmoja!! Na vijana wa Kiislamu wanaosoma shule za Kikatoliki watakuwa salama kweli au watafanyiwa yale Wajerumani hao hao ambao ndio marafiki zao leo waliyowafanyia watoto na vijana wa Kiyahudi kwenye miaka ya 1930 hadi 1945 ?
****** ****** ******
21. Huduma ya bima ya taifa ni kwa Waislamu tu kiasi cha Wakatoliki
kushadidia kuwa na Bima ya Afya ya
Kikatoliki? {Wengine kwangu ni mabogi tu na itafika mahala jamaa
watayaacha mabogi hayo bila wasiwasi!}. Huduma hii inaanzishwa kwa ajili ya mapadri au wafuasi wao au Watanzania wote ? Sheria ya nchi inasemaje kuhusu mifuko ya akiba ya uzeeni na afya na tiba ?
****** ****** ******
22. Kwanini serikali isitoe nafasi za masomo ya Ualimu kwa walimu wa
shule na vyuo vya dini zote na sio kwa
shule na vyuo vya Kikiristo tu ? Mbona viongozi wa zamani wa makanisa hayo waliweza kufanya mambo mengi bila msaada wa serikali. Hela siku hizi zinakwenda wapi ? Vatican au kuna ukata huo kiasi cha kulilia kugawana hela serikali inayofadhiliwa na wazungu ?
****** ****** ******
23. Serikali ikianza kugawa mapato yake kwa Wakatoliki basi kiuadilifu na
kwa haki na usawa isiache kufanya
vivyo hivyo kwa dini nyinginezo na hata kwa wale wasiokuwa na dini pia !
****** ****** ******
24. Je, serikali iliyoko madarakani inajua UZITO WA DHAMBI YA UJIVUNI NA
UBAGUZI WA KIDINI katika jamii yoyote na madhara yake kwa jamii inayojisahau na kujikuta katika
dhambi hiyo?
****** ****** ******
25. Je, wanasheria Waislamu wanaweza kutueleza ni kwa kiasi gani katiba, sheria na sera za CCM zimefuatwa au kuvunjwa katika masuala ya Mahakama ya Kadhi ulinganisha na Bodi ya Elimu ya Wakiristo na Bodi ya Afya ya Wakiristo ?
****** ****** ******
26. Wakoloni wa Kijerumani na Kiingereza hawakuupenda kabisa Uislamu lakini wao waliiachia Mahakama ya Kadhi kuendelea kuwepo kwa kutambua kwamba wanaweza kuitumia kama 'an arm of administrative law yao,' sasa angalia wenzetu wa CCM na serikali yao walivyo na akili. Pamoja na kushindwa kuwatekelezea wananchi wao mambo mengi na wengine huko Zanzibar kuanza ujuha wa kugombania shilingi milioni moja ya mafuta watakayoikota kesho, tena bila inshallah, wameshindwa kutambua fursa ambayo Mahakama ya Kadhi imewaachia nje nje, nayo sio nyingine, ila kupunguza mzigo wao ambao kama sio kwa udhaifu na kushindwa kuungana kwa vyama vya upinzani njoo 2010 chama hicho kingelikuwa almanusra kubakia madarakani.
****** ****** ******
27. Hawa jamaa sio kwamba wanaendelea kuwepo madarakani kwa sababu ya 'ujinga' wa wananchi vijijini ni kina nani wanaoweza kujitolea kubadili hali ilivyo na kuwafungua macho wananchi vijijini kwamba Chama kimoja kuwa na viti vingi bungeni ndiko kunakochangia rushwa, ufisadi, wizi wa kura, njaa, kukosa maji vijijini, shule duni, kipato duni, barabara duni na yote yanayowakabili sasa. Na kwamba kwa Waislamu vijijini kukosa Mahakama ya Kadhi watakuja ishia wote kuritadishwa wao na watoto wao watakaokujakusomeshwa na manasara ? Na katu umasikini wao hautaondoka bila Mahakama ya Kadhi kusimama kidete kwenye masuala ya ZAKAT inayotkiwa iwaondoe wao kutoka kwenye umasikini. Watambue hakuna nasara atakayewatajirisha bali ni Zakat kutoka Bait ul Mali itakayosimamiwa na Mahakama ya Kadhi kwa haki, bila rushwa na bila ufisadi na longolongo nyingi.
****** ****** ******
28. Zaidi ya asilimia 68 ya viongozi serikalini ni Wakiristo, wengi wao wakiwa Wakatoliki je wanaharibu mipango na mikakati ya kuendeleza shule, vyuo, hospitali na taasisi nyingine kama hizo ili serikali ionekane kushindwa na kuwa ni kanisa tu ndilo linaloweza kufanikisha masuala ya elimu, afya na tiba nchini ?
****** ****** ******
29. Tabia ya viongozi wetu wa juu kutaka kuendelea kuwa karibu na nchi za Kikiristo kama vile Ujerumani, Uingereza, Marekani na nyingine kama hizo halionekani kama ndio chanzo cha matatizo mengi ya kidini hapa nchini. Maana hawa ndio wanaowapa vichwa viongozi wa makanisa. KWANINI TUSIKURUBIANE KABISA NA NCHI KAMA CHINA, JAPANI, KOREA, VIETNAM NA INDIA ili kuondokana na tatizo hili la kuwa na WAFADHILI WANAOTAKA KUIFANYA NCHI YETU YOTE IWE YA KIKIRISTO ?????
****** ****** ******
30. Vinginevyo kwa kila shilingi 1 inayotolewa kwa madhehebu za KIkiristo toka nchi za Wakiristo na Waislamu nao waruhusiwe kuchukua shilingi 1 toka nchi za Kiislamu. Nchi hizo zina nia, sababu na uwezo wa kuwasadia Waislamu lakinti tatizo ni serikali na CHAMA CHA MAPINDUZI!!!!!!!!

****** ****** ******
ian_jua
 
swali: Kama bakwata ni chombo kama chombo kingine cha waislamu na hivyo hakiwezi kuzungumza kwa niaba ya waislamu wote je jumuiya ya wahadhiri inazungumza kwa niaba ya waislamu wote au nayo ni chombo kingine cha waislamu na hivyo hakiwezi kuzungumza kama sauti moja ya waislamu?

A. Kama jwk (jumuiya wahadhiri wa kiislamu) siyo chombo cha waislamu wote basi hakina uwezo wa kuipa serikali siku 14 kwa niaba ya waislamu wote

b. Kama jwk ni chombo cha kuwawakilisha waislamu wote basi bakwata iseme kama inaunga mkono mkwara huo. Kama walioko bakwata hawaungu mkono basi jwk haiwakilishi waislamu wote.

C. Kama (a) na (b) ni kweli, basi ultimatum ya siku 14 haina msingi katika waislamu na haiwezi kuilazimisha serikali kufanya jambo lolote.

D. Kama (a) ni kweli, na (b) ni kweli na (c) ni kweli; basi waislamu wakae chini na kuunda chombo kimoja ambacho kitazungumza kwa sauti moja ya waislamu. Chombo hicho kinaweza kuwa muamvuli wa vyombo vingine vya waislamu. Chombo hicho kitakachoundwa ndicho kitatakiwa kiwakilishe misimamo rasmi ya waislamu kama kundi. Hii itafanana na tec ambayo inazungumza kwa niaba ya wakatoliki wote (siyo wakristu wote); tcc inayozungumza kwa niaba ya makanisa ya kiprotestant na tpc inayozungumza kwa niaba ya makanisa ya kipentekoste.

Hii ina maana hata kama haiwezekani kuunganisha waislamu wote basi wanaweza kujipanga kwa kufuata madhehebu yao. Kuwe na chombo cha kuwakilisha sunni, shia na ahmaddiya n.k pasipo waislamu kuunda umoja wa aina hiyo watajikuta mara nyingi wanagawanyika katika misimamo yao.

Kwa sababu hata mahakama ya kadhi ikiundwa haina maana itakuwa imewaunganisha waislamu kwani katika applications za sheria hizo itabidi bado wataalamu/wanazuoni wa ilimu mbalimbali kutoka madhehebu mbalimbali kuweza kukubaliana katika masuala kadha wa kadha.

satisfactory!
 
Jamani,

Mimi sielewi kitu kimoja; naomba msaada - mahakama ya kadhi itakuwa ya waislamu, na siyo ya serikali; sasa ni kwa nini waislamu wanataka serikali ndiyo iwaanzishie hiyo mahakama? Kwa nini wasianzishe wao wenyewe huko misikitini or wherever?



Waislamu hawawezi kuunda mahakama yao kwa kuwa kisheria haitakuwa a statutory body yaani hakitakuwa chombo cha kisheria,hivyo ni lazima ipitishwe bungeni na hiyo ndio sababu ya msingi inayowafanya waislamu kuitaka serikali kuunda mahakama ya kadhi.Bahati mbaya serikali haina dini na hilo ni jambo ambalo limetamkwa kwenye katiba yetu,pamoja na waislamu kufahamu hilo lakini bado wanalazimisha katiba ibadilishwe kwa ajili ya kufanikisha uundwaji mahakama ya kadhi kwani bila kufanya hivyo mahakama ya kuanzishwa na wao wenyewe bila kuwa sheria ya nchi haitakuwa na nguvu. Mfano huwezi kumsummon mtu mbele ya mahakama ambayo atakuwa na option ama kukubari au kukataa kufika mahakamani hapo,kwa hiyo ili mtu huyo alazimike kufika mahakamani ni lazima sheria imlazimishe. Mimi nasema ni bahati mbaya sana kwa dini ya kiislamu kuwa na utaratibu wa mahakama ambayo ni chombo cha serikali,upande wa wakristo wana mahakama zao lakini bahati nzuri kutokana na usomi zimebaki kuwa za wakristu wenyewe na serikali haiusiki,utaratibu huu uliwekwa toka mwanzo na wasomi wao baada ya kubaini kuwa dini ni imani kwa hiyo mambo ya serikali yatabaki kushughulikiwa na serikali na ya dini yatashughulikiwa na dini husika,hoja kwamba serikali iunde tu mahakama ya kadhi lakini mambo mengine yatafanywa na waislamu wenyewe bado haina msingi kwani maana bado itabaki palepale kuwa ni chombo cha serikali mfano itapitishwa bungeni,itasainiwa na rais wa nchi(bahati nzuri walipoona ni muislamu mwenzao wanalazimisha) lakini pia kama kuna mabadiliko aidha ya kuongeza jambo au kufuta jambo kwenye sheria iliyounda mahakama ya kadhi ni lazima lipelekwe bungeni kwa ajili ya kupitishwa kuwa sheria hivyo kutumia kodi za wananchi je hapo mtu atasema ni waislamu pekee wataendesha mahakama hiyo? Waislamu wametengeneza a time bom hivyo for god's sake serikali inalazimika kuunda mahakama ya kadhi,mimi siiungi mkono lakini nasema kutoundwa mahakama hiyo kutakuwa ni chanzo cha mapigano kati ya waislamu na wakristo kwa kuwa muislamu siku zote umsingizia mkristu ndiye anayekwamisha mambo yake na kwa hili hali itakuwa hivyohivyo,kwa hiyo wataona solution ni kupigana,wapo watakaobisha jambo hili lakini msimamo wa dini ya kiislamu ni kulipiza kisasi,ni kupigana ili kupata haki ingawa wakristu pia wanapigania haki za dini yao lakini si kwa mapanga,mabomu n.k bali ni kwa neno pekee,kwenye uislamu hiyo haipo kwenye uislamu kuna jino kwa jino,ndio maana wanazungumzia kuinyima ccm kura kwenye uchaguzi ujao badala ya kuzungumzia haki ya kuchagua kiongozi unayemtaka kama wakristu(wakatoliki)walivyotoa walaka wao wa kisomi. Mwisho sitaki kuonekana natangaza dini fulani,lakini nimelazimika kusema hayo yote kwa kuwa ndio ukweli ulivyo,anayebisha ni sawa kwa kuwa yatakuwa ni maoni yake bali nilichozungumza mimi ni fact.
 
Hivi kitabu kwanini kinachukuliwa kama ndio msahafu wa mahusiano ya Kanisa, Waislamu na Serikali? Hivi kuna mtu amewahi kukaa chini na kukiangalia kifasihi au kile sentensi humo imechukuliwa kuwa ni ukweli, ukweli mtupu, na si kingine bali ukweli!?



Maandishi ya mtu mmoja yanapochukuliwa kama maandishi rasmi ya Kanisa au vyombbo vya kanisa si sahihi. Ukikisoma vizuri kitabu hicho utaona jinsi gani kimejaa maoni ya mwandishi na tasfiri yake kuhusu facts mbalimbali.



Haya ni maneno ya kujikatisha tamaa. Kama Bakwata siyo chombo cha Waislamu ni chombo gani basi ni cha waislamu? Shura ya Maimamu ni chombo cha Waislamu wote wa Tanzania? Jumuiya ya Wahadhiri wa Kiislamu ni chombo cha Waislamu wote?


Mtu anayeona anadhulumiwa au ananyimwa haki kamwe huwezi kumuita mtu wa fujo. Sijui ni watu gani "wengi" wenye mtazamo huo. Kwa sisi ambao tumekulia na kuishi miongoni mwa Waislamu, kusoma nao, kwenda nao jeshini, kucheza pamoja n.k kufikiria kuwa waislamu ni watu wa fujo ni kuwazia kitu kisichokuwepo.





Nimetoa mfano hapo juu kuwa Kanisa Katoliki lina mahakama zake na zinafanya kazi na zinahusu mambo hayo hayo ya ibada, ndoa n.k sasa
Tatizo ambalo watu hawataki kuliangalia ni kuwa katika Tanzania hakuna chombo kimoja chenye kuzungumza kwa niaba ya Waislamu. Chombo ambacho kinaonekana kinaweza kufanya hivyo ni serikali. Hii ndiyo sababu pekee na ya msingi ya kwanini Mahakama za Kadhi Tanzania haziwezi kuanzishwa bila ya serikali, kwa sababu Waislamu wa Tanzania tayari wamegawanyika na hawajafanya juhudi yoyote ya kuunda umoja ambaoa utakuwa ni sauti yao.

kila kitu ni political kuanzishwa kwa jumuiya nyingine sio rahisi kiasi hicho, pana jumuiya moja ilikuwa inakuja juu kwenye masuala ya elimu, watuwa serikali walianza kuifuatilia kila kona kujua inapata wapi funds nk, wakagundua ni nguvu za waislam wameiacha na inaendelea, inasambaa mikoani with time litafanikiwa, na pia nguvu ya kuifanya BAKWATA kuwa kitu moja inaendelea waislam sio wajinga na mambo haya hayahitaji kutangazwa

Badala ya kuibadilisha Bakwata ili kiwe chombo chao wengine wanafanya kila juhudi ya kuidhoofisha bila kujaribu kuleta kitu kingine matokeo yake, boti ambayo japo inavuja wanazidi kuijaza maji bila kutafuta mtumbwi mwingine wa kuwapeleka ng'ambo!




Hii ni kejeli! Kwani hao walioko Bakwata siyo Waislamu? Uislamu ni nini na Muislamu ni nani? Je Muislamu hawezi kuwa mwanachama wa Bakwata au hadi awe nje ya Bakwata ndiyo anakuwa Muislamu mzuri.

La maana ni kwa watu walioko Bakwata au nje kuamua kuyaboresha mashule hayo badala ya kukaa pembeni. Mbona shule za Wazazi wakati ule zilikuwa ni shule mbayambaya lakini baadhi yake siku hizi zimeboreshwa sana? Lakini haikusemwa kuwa hazikuwa ni za CCM?



Sasa hizo taasisi zinawakilisha Waislamu wote? Jamani hata Wakatoliki wana taasisi mbalinmbali na wakati mwingine hata hazihusiani. Kwa mfano ukisikia shule za St. Mary (Bagamoyo au Mbeya) haina maana ni shule moja ile ile. Seminari za Kikatoliki zote haziko kwenye jimbo moja au hazimilikiwa na jimbo moja, na nyingine haziongozwi hata na majimbo zinafanya mambo yake kivyake vyake.


ndio tunafanyavyo kwani sasa kuna shule ngapi zimeanzishwa hazipo chini ya bakwata?

Lakini taasisi zote za Kikatoliki (zenye kutumia jina hilo la "kikatoliki") ziko chini ya Askofu wa Jimbo husika na mambo yake na maslahi yake yanawakilishwa kwenye Baraza la Maaskofu Katoliki na zinaongozwa na kanuni au katiba za mashirika ya kiroho au Kanuni ya Kanisa (Canon Law). Hili ni kweli kwa shule yoyote ya Kikatoliki duniani na hata pale ambapo baadhi zinakuwa huru lakini bado zinahusiana kwa karibu na uongozi wa Jimbo Katoliki.

Mfano huu ungeigwa na Waislamu. Badala ya kushindanisha Bakwata na taasisi nyingine za Kiislamu na kuanza kuitana kuwa "hawa ni waislamu, au hawa si waislamu" au kusema " hii si ya waislamu na ile ni ya waislamu" ni vizuri kama watu wangekaa chini na kusema katika tofauti zetu tunaweza vipi kuunda umoja".

Hivyo kwa mfano Bakwata inabadilishwa na kurudishwa kuwa "Tanzania Muslim Council" au kitu kama Shirikisho la Taasisi za Waislamu Tanzania (SHITAWATA) basi chini yake kunakuwa na taasisi mbalimbali zinazojitegemea. Kila taasisi inaongozwa kwa taratibu zake na sheria yake lakini zote zinakuwa chini ya uvuli wa BMC.

Kwa kufanya hivyo, chombo kimoja na chenye nguvu chenye watu wenye tofauti, wenye kushikilia mafundisho tofauti ya kidini (theological schools of thoughts) na madhehebu mbalimbali wanaounganishwa kwa msingi uliokubaliwa na kanuni za msingi.

Nitatumia mfano wa Makanisa ya Kipentekoste. Japo kuna makanisa mengi ya Kipentekoste si yote yanayoamini kile wengine wanaamini. Hata hivyo, ili Kanisa la Kipentekoste likubaliwe kuwa ni la Kipentekoste kuna kitu kinaitwa "IMANI ZA MSINGI" au kile wenyewe wanakiita "Tunachoamini".

Sasa mtu anaweza kuanzisha kanisa lake akaliita "Kijijini Pentekostal Church of Last Believers" na akajipachika Uchungaji na Uaskofu na akawa na waamini wa kwanza wapatao wanne tu (mkewe na watoto wake) basi kanisa lake hilo ili lijiunge na makanisa mengine ya Kipentekoste litatakiwa lioneshe mambo yake linayoamini na yakiwa sawa na yale ya PCT basi linaunganishwa huko.

Sasa ni kwanini jumuiya mbalimbali za Waislamu wa Tanzania zimeshindwa kuundana na kuunda mwamvuli mmojja wa jumuiya itakayosimamia maslahi, mashule, mahospitali ya Waislamu. Jumuiya ambayo inaweza kabisa kuwa sauti ya Waislamu wote licha ya tofauti ya madhehebu, uwezo, malengo n.k?

Ni katika kufanya hivyo, basi Waislamu wa Tanzania wanaondoa ule unyonge ambao wanaudhihirisha wa kuilalamikia Bakwata bila kujaribu kuibadilisha, kulalamikia shule zao badala ya kuziboresha, kuilalamikia serikali badala ya kuisahihisha na hata kusabaisha isichaguliwe tena, kulalamikia makanisa badala ya kutafuta namna ya kushirikiana.

Ni lazima waislamu wa Tanzania watambue kuwa ni katika kuunganisha nguvu tu ndipo nguvu yao itaonekana.

Taasisi za Kiislamu/Waislamu:(Nyingine unaweza kuongeza)
- BAKWATA
- BALUKTA
-JWI -
- SHURA YA MAIMAMU
- BARAZA LA KUGOMBOA MALI ZA WAISLAMU
-MSAUD (Wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar)
- Warsha ya Waandishi wa Kiislamu (Warsha)
- DUMT (Dar-es-Salaam University Muslim Trusteetship)
- BARAZA KUU LA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAMU (Ndiyo ilikusudiwa kuipiku Bakwata)
-

kila mtu anapolisimamia jambo lake ananukuu kile anaona kinamtetea kwa upande wake, kwa mtizamo wangu muandishi yupo sahihi na nakubaliana naye na ndio maana namtumia kama ngao ya kutetea hoja yangu, sitarajii mkuu nawe uelewe hivyo wewe utatumia nukuu yako unayoiona inafaa kuwaelimisha watu ila mie nasimamia hapo pamona, kufahamu zaidi tatizo la waislam na serikali unaweza ukaangalia:
Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania


Kama Waislamu hawaridhiki na BAKWATA kwanini wasiivunje isipokuwa kwa sababu kuna Waislamu ambao wanaikubali BAKWATA?
,
mzee hili halina mjadala wala huna sababu ya kuliweka nyuma ni suala la wazi na linafahamika, sio tu kuivunja na kuanzisha nyingine bali tu kuweka viongozi ambao watakuwepo kwa maslahi ya waislam na hii ndio jitihada inayofanyika kwa uwezo wa allah ipo siku litafanikiwa, Mheshimiwa Rais kikwete alijaribu, na palifanyika mabadiliko kipindi fulani lakini hayakufanikiwa moja kwa moja ila kwa jinsi tuendavyo tutafika tutakapo, hakuna lisilowezekana kwa juhudi na kwakumpa mungu nafasi yake.
Mtu wa fujo ni mhalifu yeyote na mtu yeyote ambaye anaamua kutenda mambo nje ya sheria na ambaye kama sheria haipendi hajafanya juhudi za kuibadilisha sheria hiyo, na kama ni uongozi hajajihusisha kuubadilisha uongozi huo.

well mzee umesema nimekuelewa if that is what you mean!

Hili mbona halina mjadala; Wasomi wa Kiislamu na Wasomi Waislamu wapo tangu kabla ya Uhuru. Hata leo serikali yetu imejaa wasomi wa kila fani ambao ni Waislamu. Na suala la uwezo wa kuongoza ndio wapo wenye uwezo huo na wapo ambao hawawezi kuongoza. Mfano mzuri ni jinsi suala hili la Mahakama ya Kadhi linavyoshughulikiwa; hakuna chembe ya usomi inayooneshwa na watu wengi tu miongoni mwao ni "wasomi wakristu na wasomi waislamu"!

nadhani suala hili tatizo lake ni media na haswa redio mbao, uhuru wa maoni na utandawazi unaathari zake katiak sensitive issue na hili ni moja miongoni mwa athari hizo, unaweza kuona tu hapa JF kwa uchache jinsi linavyoshabikiwa na kuandikwa katika mtizamo tofauti, lakini nina imani zipo harakati za kisheria zinafanyika kupitia wanasheria wa kiislam, nadhani linahitaji muda na nafasi kwa waislam kulimaliza na serikali bila influence ya vyombo au vikundi ambavyo haliwahusu katika uundaji wake,


Kwanini Waislamu wasiamue tu kuanzisha mahakama zao wao wenyewe na tuone kama serikali itaingilia kati .

Kanisa katoliki lilipewa nguvu na serikali toak enzi hizo, linafanya kazi kama serikali sioni ajabu kuwa na mahakama, hata kama aitakuwa inagharamiwa na serikali, kuanzishwa kwa mahakama hiyo kwa waislam sio suala jepesi ndio maana hadi leo bado serikali inashindwa kutolea maamuzi, kwani kama serikali inafahamu kuwa katoliki ina mahakama ya aina hiyo kwa nini ichukue muda wote kutoa maamuzi, na hapo waislam wameomba idhini ka serikali je wangeanzisha tu si ingekuwa MWEMBECHAI NYINGINE; MUNGU ATUNUSURU NA KUTUEPUSHA NA KADHIA HIZO! hatutaki litokee ndio maana hamna namna inabidi kuipa serikali nafasi ya kutoa maamuzi

Nimetoa mfano hapo juu kuwa Kanisa Katoliki lina mahakama zake na zinafanya kazi na zinahusu mambo hayo hayo ya ibada, ndoa n.k sasa
Tatizo ambalo watu hawataki kuliangalia ni kuwa katika Tanzania hakuna chombo kimoja chenye kuzungumza kwa niaba ya Waislamu. Chombo ambacho kinaonekana kinaweza kufanya hivyo ni serikali. Hii ndiyo sababu pekee na ya msingi ya kwanini Mahakama za Kadhi Tanzania haziwezi kuanzishwa bila ya serikali, kwa sababu Waislamu wa Tanzania tayari wamegawanyika na hawajafanya juhudi yoyote ya kuunda umoja ambaoa utakuwa ni sauti yao.

kila kitu ni political kuanzishwa kwa jumuiya nyingine sio rahisi kiasi hicho, pana jumuiya moja ilikuwa inakuja juu kwenye masuala ya elimu, watuwa serikali walianza kuifuatilia kila kona kujua inapata wapi funds nk, wakagundua ni nguvu za waislam wameiacha na inaendelea, inasambaa mikoani with time litafanikiwa, na pia nguvu ya kuifanya BAKWATA kuwa kitu moja inaendelea waislam sio wajinga na mambo haya hayahitaji kutangazwa
Sasa hizo taasisi zinawakilisha Waislamu wote? Jamani hata Wakatoliki wana taasisi mbalinmbali na wakati mwingine hata hazihusiani. Kwa mfano ukisikia shule za St. Mary (Bagamoyo au Mbeya) haina maana ni shule moja ile ile. Seminari za Kikatoliki zote haziko kwenye jimbo moja au hazimilikiwa na jimbo moja, na nyingine haziongozwi hata na majimbo zinafanya mambo yake kivyake vyake.


ndio tunafanyavyo kwani sasa kuna shule ngapi zimeanzishwa hazipo chini ya bakwata?


kuhusu taasisi:
umezitaja ya kutosha na nyingine kadha wa kadha, miongoni mwa hizo nyingi hapo zinafanya kazi pamoja na hazipingani katika mamuzi yake, hizo ni juhudi za kutafuta njia ya kuwafikia waislam popote kwa wakati tofauti, lengo ni moja,


all in all nadhani suala la kadhi na mahakama ni la waislam, nao wamelifikisha kwa serikali sioni tatizo la waislam, serikali na waislam ni baba na mwana, kama ilivyo kwa wakristo na dini nyingine, kwa serikali kama tutachukulia katika mtizamo mmoja,

sioni tatizo kwa mwana kutaka ushauri kwa mlezi wake, hivyo basi nafasi ya kuamua nini kifanyike ni kwa serikali na waislam ndani ya makubaliano yao, sioni sababu ya watu kupiga kelele juu ya suala hili kuzungumzwa na serikali! so far ni suala linalowahusu waislam wa tanzania na si wa uarabuni!

 
Waislamu wanadai uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, je, ilikuwa ni ahadi, pendekezo au kitu gani?
Tujikumbushe juu ya sehemu ya Ilani hiyo:
Sekta ya Sheria
[FONT=AHIFFO+Tahoma,Tahoma]108. CCM itazitaka Serikali ziendelee na hatua zilizoanza kuchukuliwa ili kuiboresha Sekta ya Sheria kusudi nayo itoe huduma bora zaidi kwa jamii. Yatakayosisitizwa katika kipindi hiki ni pamoja na yafuatayo:-
(a) Kuzifanyia marekebisho sheria za mirathi na zile zinazoonekana kuwakandamiza wanawake.
(b) Kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara.
(c) Kuanzisha na kutekeleza mpango maalumu wa kuanzisha Ofisi za Mahakama Kuu katika kila Mkoa.
(d) Kukamilisha mchakato wa kutenganisha shughuli za upelelezi na uendeshaji mashitaka.
(e) Kuziimarisha na kuzioanisha sheria zinazohusiana na mapambano dhidi ya rushwa.
(f) Kutekeleza Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Sheria hususani ujenzi wa majengo ya mahakama ya ngazi zote na kuajiri majaji na mahakimu wa kutosha.
(i) Kuweka mfumo wa kuwasaidia wananchi wasiojiweza kupata msaada wa kisheria. (j) Kuweka mfumo utakaowezesha kutumika kwa wanasheria wa awali (para-legals) katika mahakama za mwanzo.
[/FONT]
 
HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya CCM [NEC] imewataka waislamu kama wako sahihi katika kuanzisha Mahakama hiyo ili haki zitendeke kwa waislamu watapewa uhuru wa kuanzisha mahakama hiyo kwa masharti ili kuepuka migongano ya kidini nchini. Hayo yalisemwa jana na Katibu wa NEC Taifa Bw. Chiligati katika kikao kikuu kilichowakutanisha wajumbe wa Halmashauri hiyo mjini Dodoma.

Chiligati alisema kuwa kama waislamu wanaona mahakama hiyo itawasaidia kuleta haki zao wanazodai basi waislamu waanzishe Mahakama hiyo lakini Serikali haitajihusisha na maamuzi ya Mahakama hiyo.

Alisema kuwa mahakama hiyo itakayoanzishwa Serikali itajitoa juu ya maamuzi na sheria ya Mahakama hiyo kwa kuwa serikali ya Tanzania haina dini.

Alisema na kama mahakama hiyo itaanzishwa nchini basi isijihusishe na makosa ya jinai wala makosa ya madai ili kuleta usawa na amani nchini.

Hivyo amesema serikali ipo kwenye michakato ya kukutana na viongozi wa ngazi za juu za dini zote nchini ili kuleta ruhusa ya kuanzisha mahakama hiyo inayoleta migongano kwa viongozi nchini.

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2853442&&Cat=1
 
We welcome the news. However, Waislamu hizo ni kampeni za CCM kwa ajili ya uchaguzi 2010.
 
Hapo bado hakijaeleweka, wanasema isijihusishe na makosa ya madai wakati mahakama ya Kadhi inahitajika ili ishughulikie hayo makosa ya madai ambayo waislam wenyewe wanahitaji yashughulikiwe kwa upande wao.
 
We welcome the news. However, Waislamu hizo ni kampeni za CCM kwa ajili ya uchaguzi 2010.

Haki!

Usitake niamini kwamba Waislamu ni wajinga! Katiba ya nchi si imeandikwa kwa kiswahili?Hii thread spendi kuchangia lakini kuweka rekodi sawa ni kwamba matakwa ya kuwa na mahkama ya kadhi ni kuvunja katiba kwa sababu judiciary is a state function na wakati serikali haina dini. Huwezi kuanzisha mahakama kama NGO na kama haihusiki na jinai wala madai then sio mahakama but could be some sort of a Kangaroo court.

Kwa kweli nawaheshimu waislamu na I don't want to cause trouble ila kwa hilo la mahakama ya kadhi I beg to differ period. Nimefanya a simple research hata kule Sudan na majimbo ya kaskazini mwa Nigeria kwenye sharia law hizo mahakama aren't operating. Kwa sababu hakuna exclusion zones only for muslims vinginevyo ni ubaguzi per se!!

Muslim scholars come straight and let us put this Kadhi thing behind hawa akina Chilighati John ni wasanii na wahuni tu wanaogopa mtawatosa kwenye uchaguzi lakini take it from me hakuna jimbo la uchaguzi la waislam peke yao hapa Bara vinginevyo JMK ambaye ni mwislam anaunga hoja hii mkono ndio maana ameweka plaster kwenye mdomo ni jukumu la rais aliyeko madarakani kuweka msimamo wa serikali yake bayana huo woga na kigugumizi kinatoka wapi? Tujadili but no fighting najua mtanishukia kama kunguru wa Zanzibar wanavyoshukia vifaranga lakini kwa vile leo ni Jumapili na wapenda dezo hawana mtandao nitawangojea kesho!!!!
 
Hicho ni kizungumkuti kwa CCM , nazidi kujiuliza kwanini waliweka hoja hii katika ILANI YAO YA UCHAGUZI 2005.

Itakuwa ngumu kuifanya hivyo wanavyotaka iwe kwani itakuwa sio effective kwa jamii ya waislamu.

Ok, Tusubiri tuone
 
HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya CCM [NEC] imewataka waislamu kama wako sahihi katika kuanzisha Mahakama hiyo ili haki zitendeke kwa waislamu watapewa uhuru wa kuanzisha mahakama hiyo kwa masharti ili kuepuka migongano ya kidini nchini. Hayo yalisemwa jana na Katibu wa NEC Taifa Bw. Chiligati katika kikao kikuu kilichowakutanisha wajumbe wa Halmashauri hiyo mjini Dodoma.

Chiligati alisema kuwa kama waislamu wanaona mahakama hiyo itawasaidia kuleta haki zao wanazodai basi waislamu waanzishe Mahakama hiyo lakini Serikali haitajihusisha na maamuzi ya Mahakama hiyo.

Alisema kuwa mahakama hiyo itakayoanzishwa Serikali itajitoa juu ya maamuzi na sheria ya Mahakama hiyo kwa kuwa serikali ya Tanzania haina dini.

Alisema na kama mahakama hiyo itaanzishwa nchini basi isijihusishe na makosa ya jinai wala makosa ya madai ili kuleta usawa na amani nchini.

Hivyo amesema serikali ipo kwenye michakato ya kukutana na viongozi wa ngazi za juu za dini zote nchini ili kuleta ruhusa ya kuanzisha mahakama hiyo inayoleta migongano kwa viongozi nchini.

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2853442&&Cat=1

Mkuu naona ni jambo ambalo haliwezekani kusema kuwa serikali haitaingilia maamuzi ya mahakama hiyo. Serikali ndio ina mamlaka ya juu kuhusu mambo yote yanayotokea Tanzania. Kama ikitokea mtu hatakubaliana na maauzi ya mahakama ya kadhi ni lazima atakwenda serikalini kuomba haki yake ipatikane. Naona mhe Chiligati anasema bila kuangalia mbali na kwa assumption kuwa mahakama ya kadhi itakuwa sahihi wakati wote.
 
Haki!

Usitake niamini kwamba Waislamu ni wajinga! Katiba ya nchi si imeandikwa kwa kiswahili?Hii thread spendi kuchangia lakini kuweka rekodi sawa ni kwamba matakwa ya kuwa na mahkama ya kadhi ni kuvunja katiba kwa sababu judiciary is a state function na wakati serikali haina dini. Huwezi kuanzisha mahakama kama NGO na kama haihusiki na jinai wala madai then sio mahakama but could be some sort of a Kangaroo court.

Kwa kweli nawaheshimu waislamu na I don't want to cause trouble ila kwa hilo la mahakama ya kadhi I beg to differ period. Nimefanya a simple research hata kule Sudan na majimbo ya kaskazini mwa Nigeria kwenye sharia law hizo mahakama aren't operating. Kwa sababu hakuna exclusion zones only for muslims vinginevyo ni ubaguzi per se!!

Muslim scholars come straight and let us put this Kadhi thing behind hawa akina Chilighati John ni wasanii na wahuni tu wanaogopa mtawatosa kwenye uchaguzi lakini take it from me hakuna jimbo la uchaguzi la waislam peke yao hapa Bara vinginevyo JMK ambaye ni mwislam anaunga hoja hii mkono ndio maana ameweka plaster kwenye mdomo ni jukumu la rais aliyeko madarakani kuweka msimamo wa serikali yake bayana huo woga na kigugumizi kinatoka wapi? Tujadili but no fighting najua mtanishukia kama kunguru wa Zanzibar wanavyoshukia vifaranga lakini kwa vile leo ni Jumapili na wapenda dezo hawana mtandao nitawangojea kesho!!!!


TUANZE kujadili kwa kukuliza ni ni msimamo wako kuhusu kuwepo kwa mahakama ya kazi ndani ya serikali?
Tafadhali usiniambie suala la Katiba au udini kwani Katiba ni suala la kufanyiwa marekebisho na kama Mahakama hiyo isiwepo eti kwa kuwa si nchi ya kidini, Tanzania hata wakati wa Ukoloni kama Tanganyika haijakuwa nchi ya kidini lakini Mahakama ya kadhi ilikuwepo.
Naomba hoja na sio jazba.
 
TUANZE kujadili kwa kukuliza ni ni msimamo wako kuhusu kuwepo kwa mahakama ya kazi ndani ya serikali?
Tafadhali usiniambie suala la Katiba au udini kwani Katiba ni suala la kufanyiwa marekebisho na kama Mahakama hiyo isiwepo eti kwa kuwa si nchi ya kidini, Tanzania hata wakati wa Ukoloni kama Tanganyika haijakuwa nchi ya kidini lakini Mahakama ya kadhi ilikuwepo.
Naomba hoja na sio jazba.
Ngekewa!

Unataka jibu? Hatuwezi kubadili katiba kwa jambo la kipuuzi. Nimesema narudia usitake kunifanya niamini kwamba waislamu ni wajinga. Nimeshafanya research wanachotaka waislamu wengi sio mahakama ya kazi bali ni kupata maendeleo. Nadhani kabla ya uhuru wewe bwana mdogo hukuwepo fine. Kama ulikuwepo mwaga data hapa ni mambo gani mazuri aliyofanya kadhi na kama mahakama ilioperate wapi na hao waislamu wanaopiga kifua kuidai walifaidi nini zaidi ya kutokwenda shule. Do you want to go back into barbarism watu kuchapana viboko au kupigana mawe mpaka wafe kama mtu akifanya ufuska tu. Narudia this kadhi issue won't take you anywhere. It is only the first step to sharia na matokeo yake yako wazi you don't need spectacles. Ona hapo Unguja ikifika Ramadhani kama sasa watu wanalazimishana kushinda na njaa mpaka watalii wanakimbia unataka hapa bara tuwe na upuuzi huo? Tatizo ni elimu very few of you have ever touched the quoran apart from kukariri mnayoambiwa!!

Serikali ya kikoloni never gave any leverage mkitaka tafuteni pori lenu mkaishi huko under sharia kwani hamkawii kujilipua. Nitajie taifa moja la kiislamu amabako kuna utengamano!!! Hey Ngekewa huna jipya. Just katafute futari mkeo akupikie kama unae!!!
 
Tatizo ni elimu very few of you have ever touched the quoran apart from kukariri mnayoambiwa!!

wasioruhusiwa ku toach Bible ni wakatoliki, wao wamepewa kitabu kidogo cha katekissm na chuo kidogo cha sala.

Anaye touch bible ni wale wasiokuwa na wake ila wanaweka vimada
 
Tatizo ni elimu very few of you have ever touched the quoran apart from kukariri mnayoambiwa!!

wasioruhusiwa ku toach Bible ni wakatoliki, wao wamepewa kitabu kidogo cha katekissm na chuo kidogo cha sala.

Anaye touch bible ni wale wasiokuwa na wake ila wanaweka vimada
 
kama ningekuwa Rais ningeruhusu hii mahakama ianze kazi mara moja, na ningewaomba hawa Islam wafuate kweli sharia inavyotaka, nadhani kinachofuatia ni baada ya wiki moja baada ya kuanzishwa wangeiomba serikali iifute. Kwa mfano mdogo:
1. Sharia inataka mtu akiiba akatwe mkono je ni muislam gani angekubali yeye au familia yake akumbane na adhabu hii wakati anajua akipelekwa mahakama za kawaida atafungwa miezi mitatu.

2. Ukikutwa na mke wa mtu au ukikutwa unazini nje ya ndoa au kabla ya ndoa upingwe mawe hai ufe, nalo sidhani kama lingekubalika.

sasa kwa mifano hii miwili ningeomba tu serikali isijiingize katika migogoro na waislam bila sababu, sijiingizi katika udini ila ni ukweli kuwa sisi vijana hasa wengi wa kiislam ndio ambao tunaongoza kwa matatizo ambayo kama maakama ya kadhi ingeruhusiwa tungekuwa waathirika wakubwa ha hiyo Sharia,

mungu ibariki tanzania na uwajaalie viongozi wetu wairuusu hii maakama haraka iwezekanavyo, ila pia ijiandae kuwa na walemavu wengi sana wa mikono
 
kama ningekuwa Rais ningeruhusu hii mahakama ianze kazi mara moja, na ningewaomba hawa Islam wafuate kweli sharia inavyotaka, nadhani kinachofuatia ni baada ya wiki moja baada ya kuanzishwa wangeiomba serikali iifute. Kwa mfano mdogo:
1. Sharia inataka mtu akiiba akatwe mkono je ni muislam gani angekubali yeye au familia yake akumbane na adhabu hii wakati anajua akipelekwa mahakama za kawaida atafungwa miezi mitatu.

2. Ukikutwa na mke wa mtu au ukikutwa unazini nje ya ndoa au kabla ya ndoa upingwe mawe hai ufe, nalo sidhani kama lingekubalika.
soma vizuri. mahakama ya kadhi itaanzishwa kwa ajili ya kesi za madai kama ndoa, talaka na mirathi.

na wala haitajihusisha na criminal issues.

Usikengeuke, soma vizuri nia na madhumuni ya mahakama hizo.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom