Uliza jambo lolote kuhusu Bahari na safari na vimbwanga vya Baharini

Lakini kiongozi,,,Mimi ni BAHARIA,,, na sio mvuvi ,,samahani kwa swali langu,,tunaposoma somo la PERSONAL SURVIVE TECHNIQUES... wanasema inapotokea ajali,,haswa mkiwa na life jackets,,mnapaswa kukaa eneo la ajali ili muweze kupatiwa msaada,,,tena muwe kikundi.,,kuliko kuogelea na kutoka eneo la ajali.....sasa naomba kukuuliza,,hao waliokufa umesema walijitakia,,je kwanini iwe walijitakia?
kuhusu wale jamaa wa boti waliopotea nakuzama na kufanikiwa kupona mtu mmoja wale jamaa kile kifo cha kujitakia sababu yule aliepona ndio aliwaambia baada ya kuzama wakati wanazama walibahatika kuvaa life jacket ile boti ikaenda chini sasa wao wakabaki wanaelea ndipo yule nahodha akawaambia itabidi tuogelee huku tukifata maji muelekeo wake wale jamaa wengine walikataa ikabidi kila mtu aogelee kivyake isipokuwa yule nahodha aliogelea kwa kufuata maji ndio pona yake yeye aliokotwa kisiwa cha koma akiwa mzima maana aliogelea mpaka ufukweni alipofika kalala hapo hapo mpaka maji yalipokuwa yanajaa ndo yakamuamsha ndo akapandisha juu ndio akapewa huduma ya kwanza nayo ni uji ila wale wengine wenziwe alozama nao hakuna alopona akiwemo mzungu ndio mwenye safari
 
Lakini kiongozi,,,Mimi ni BAHARIA,,, na sio mvuvi ,,samahani kwa swali langu,,tunaposoma somo la PERSONAL SURVIVE TECHNIQUES... wanasema inapotokea ajali,,haswa mkiwa na life jackets,,mnapaswa kukaa eneo la ajali ili muweze kupatiwa msaada,,,tena muwe kikundi.,,kuliko kuogelea na kutoka eneo la ajali.....sasa naomba kukuuliza,,hao waliokufa umesema walijitakia,,je kwanini iwe walijitakia?
Umemuuliza swali zuri sana, ngoja arudi kutupa majibu ya kauli hii.
 
Kwann yale maji ya bahari ni blue?
Kwanza kabisa Maji hayana Rangi,,
Kinachofanya uone yana Rangi ni kutokana na eneo yalipo yaani Mazingira ya eneo husika na usafi wa eneo hilo.

Mfano yakiwa pwani mwa bahari yanakuwa na weusi fulani hii ni kutokana na mito inayoingiza maji hayo kuwa na tope au uchafu.
Ila kadri Yanavyotulia kukaa bahari yale Matope yanaenda chini na maji huzidi kung'aa zaidi..

Kwa upeo wa macho yetu tuona Ubluu wa kawaida yaani umbali wa kuanzia 100M ila ukiangalia zaidia ya 3Km Utaona Ubluu Umezidi.

Hii nimejibu Kwa Uzoefu wangu Siyo kwa Phd.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Ebwana eh ambari vp ushawahi kuigumia
Mm nli bahatika kukutana nayo kilwa ila jamaa walishindwa iuza hapa wa kaenda iuza mombasa
Hebu wape elimu wadau humu kuhusu hiyo kitu

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
Halafu Mkuu nasikia kuna samaki anaitwa Chongoe ni mkubwa kama nyumba ni kweli?
ni kweli tena ntaleta kisa chake hapa kuna siku wakati tunatega samaki kwa bahati mbaya mtoto wa chongoe alinasa balaa alivyokuja mama yake sitasahau maishani
 
kuhusu mtu ambae hajui kuogelea alafu amevaa life jacket huyo mtu lazima atachukuliwa na maji tu life jacket husaidia sana ukiwa unaweza kuogelea sababu utakuwa unaweza kujidhibiti hata akizama akiwa kavaa life jacket huwezi mpa wakusubiri aokolewe hasa ikiwa maji ya usiku ndo kabisa alafa tambua hata ajali hupangwa na watu tena hizo ndio nyingi
 
chongoe hicho kisa cha chongoe mwana na mama yake nakisubiri. Lakini pia, maajabu ya baharini japo kisa kimoja. Nasikia pia wamiliki wa boti mara nyingi huhusika na ajali kwa ajili ya kurogana ili kurudishana nyuma. Pia kukumbushia swali la mdau mmoja namna tasi anavyovuliwa maana mm hupenda tasi ss kusikia huvulia kwa kondo la nyuma la mama au maiti naanza kujifikiria mara mbili.
 
Wale jamaa waliozama na kuto patikana sehem waliozama maji yalikuwa yana muelekeo wa kwenda namaanisha visiwa vya koma mapanya mpaka nje ya buyuni kabisa na ndio maana wale watafutaji walikuwa na vifaa tu ila ujuzi wa utafutaji hawawana
 
chongoe hicho kisa cha chongoe mwana na mama yake nakisubiri. Lakini pia, maajabu ya baharini japo kisa kimoja. Nasikia pia wamiliki wa boti mara nyingi huhusika na ajali kwa ajili ya kurogana ili kurudishana nyuma. Pia kukumbushia swali la mdau mmoja namna tasi anavyovuliwa maana mm hupenda tasi ss kusikia huvulia kwa kondo la nyuma la mama au maiti naanza kujifikiria mara mbili.
nikweli la kurogana la kawaida sana lipo tasi huvuliwa kama samaji wengine wanavyovuliwa kuhusu kondo la nyuma sina hakika ila nia za ushirikina watu hutumia katika uvuvi wengine huua hata mvuvi mwenzao ili wapate samaki (wakojani)
 
Wale jamaa waliozama na kuto patikana sehem waliozama maji yalikuwa yana muelekeo wa kwenda namaanisha visiwa vya koma mapanya mpaka nje ya buyuni kabisa na ndio maana wale watafutaji walikuwa na vifaa tu ila ujuzi wa utafutaji hawawana

Nimewahi sikia mtu akizama,badae akifa maji maiti anakuja juu ya maji na hazami tena hivyo ni rahisi kumpata maiti. Hii unasemaje mkuu?
 
Habari zenu waungwana,

Leo nipo hapa kwa ajili ya maswali ambayo yanahusu mambo ya bahari tu. Mimi ni nahodha wa majahazi ya mizigo Mafia, Kisiju, Kilwa, Nyamisati na Koma.

Uliza swali linalohusu maeneo hayo pia kuhusu safari na vimbwanga vya baharini.

Karibuni.


Mkuu, ulishawahi kukutana na majini ukiwa safarini, yaani kupakia abiria kumbe ni jini kufika katikati ya bahari anazama baharini.
 
Back
Top Bottom