Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,033
- 9,923
MAPICHA YANGU...
THE RAP MONSTER, LYATUU
Ee bwana weee! Huyu niliye naye pichani alikuwa bonge la mtu kwenye rap na mwonekano wake.
Picha linaanza, jamaa ni mtu wa chuga, rudi nyuma mpaka kwa Fido kwenye SISI HAPA, anakwambia, "SISI HAPA ND'O HIP HOP CITY" Yes, kuna time nilitamani na mimi ningekuwa mzawa wa Chugastan hivi.
Turudi kwa mwamba, tumeingia kidato cha tano na kukuta jamaa ndiye KIONGOZI wa burudani maana skuli yetu iligawanya idara; idara ya michezo ilikuwa na KIONGOZI wake na idara ya burudani, maafa na starehe ilikuwa kimpango wake.
Mwamba alikuwa ananyuka buti kubwa, tisheti kubwa, makapelo miksa na ule mwili jumba wake, yaani ilikuwa HIP HOP ILIYOJIONGELEA, HAKUHITAJI UTAMBULISHO MREFU.
Mara tukatangaziwa kwamba tungefanyiwa welcome form five. Watu tukajiandaa ileile unaambiwa. Kulikuwa na mashindano ya misosi, Miss na Mr shule, vichekesho na makorokoro kibao lakini akili yangu yote ilikuwa kwenye rap tu.
Nikaenda kwenye rehearsal na kupiga ngoma yangu ambayo siikumbuki jina (ila ninayo kwenye daftari langu la mistari mpaka leo). Ngoma ile ilikuwa inapendwa sana na mwanangu, BOY SEARCHER kwa sababu ilikuwa ya Kiingereza, sikukaza uandishi Kama ngoma zangu nyingine lakini pia niliandika juu ya beat ya KITU GANI ya D KNOB FT Q JAY.
Watu walipagawa sana, nakumbuka manzi moja nilikuwa nayo class ikanifuata miksa kunipa pole kwa yaliyonikuta wakati ulikuwa utunzi tu, stori ya wimbo haikunihusu. Ila kisela nikasema hii manzi imeona Kuna kitu ninacho inataka iishi kwa msela hii. Nikaikataa.
Siku ya talent show imefika, jina langu halipo, kisa nilimtukana WINSTONE Mogha (Sasa hivi ni Kiongozi ACT-Wazalendo) (jamaa alikuja skuli na laptop miksa kujidai yeye ndio MC kwenye rehearsal. Alipotaka nichane acapella kama wengine nikamtolea uvivu. Wakanipunyua bila kujua. WISTONE alikuwa **** sana ila kwa sasa ni mheshimiwa fulani huko Kigoma kwenye chama kikubwa cha siasa.
Show ikapigwa mchana, nikasema famililai kwani nini! Wana wote walichana mchana. Nikawa na mchecheto wa kumsikia LYATUU lakini hakuchana. Na waliochana niliona famba tu. Nilifurahia battle ya Mchawi na Liffo kwenye msosi na vichekesho vya KAIDUDU.
ASEEE! Kipunga kikapigwa na jioni wana tukahamia bwaloni kuruka debe! Oyaaa, moja flani hivi jioni nikasikia sauti flani hivi bila kuona mtu
"MAJUKUMU YANABANAAAAA" Form six wakaitikia
"YANABANAAAAA"
Akarudia, "MAJUKUMU YANABANAAAAA"
Wakaitikia "YANABANAAAAAA"
MAJUKUMU
YYEEEEEAAAAH
MAJUKUMU
WOOAAAAAAAH
Yes alikuwa LYATUU bwana! Jeans kali, mpya na mtisheti wa Unyamwezini huko, alipiga show kubwa sana yule mjomba.
Goma likaisha, nikasikia makofi, sielewi nini kinaendelea, nakuta CHARITY anaingia STEJINI taratibu, watu wanazidi kupiga makofi
Charity akapewa microphone, kilichofuata sikuambii!!!
"NINACHOTAKA DUNIA IJUEEEEE"
"ACROSS THE WORLD, ACROSS THE WORLD, WHAT"
"NINACHOTAKA, WATU WATAMBUEEE"
Ule mdude, jamaa alirekodia juu ya beat ya TI halafu Bwana mdogo Pascal Francis akawa anasema Lyatuu aliharibu beat ya TI. Mchawi mpaka leo huyu mtoto.
Lyatuu ALIINGIA zake chuoni IFM na baada ya hapo sina taarifa zake na sijui kama bado anafanya game au laa!
Hats off Lyatuu! Alikuwa na ngoma mbili alizorekodi wakati mimi nilikuwa najirekodi kwenye visimu vya Kichina, Mchawi memory card enzi hizo, japo kuna mwana alitaka nimuuzie ngoma yangu niliyojirekodi kwa simu.
NDIYO, NILIOMBA KUPIGA PICHA NA STAA
Kama ulisoma Mwakaleli mwaka 2009 hadi 2012 possibly ulipata kumjua.
THE RAP MONSTER, LYATUU
Ee bwana weee! Huyu niliye naye pichani alikuwa bonge la mtu kwenye rap na mwonekano wake.
Picha linaanza, jamaa ni mtu wa chuga, rudi nyuma mpaka kwa Fido kwenye SISI HAPA, anakwambia, "SISI HAPA ND'O HIP HOP CITY" Yes, kuna time nilitamani na mimi ningekuwa mzawa wa Chugastan hivi.
Turudi kwa mwamba, tumeingia kidato cha tano na kukuta jamaa ndiye KIONGOZI wa burudani maana skuli yetu iligawanya idara; idara ya michezo ilikuwa na KIONGOZI wake na idara ya burudani, maafa na starehe ilikuwa kimpango wake.
Mwamba alikuwa ananyuka buti kubwa, tisheti kubwa, makapelo miksa na ule mwili jumba wake, yaani ilikuwa HIP HOP ILIYOJIONGELEA, HAKUHITAJI UTAMBULISHO MREFU.
Mara tukatangaziwa kwamba tungefanyiwa welcome form five. Watu tukajiandaa ileile unaambiwa. Kulikuwa na mashindano ya misosi, Miss na Mr shule, vichekesho na makorokoro kibao lakini akili yangu yote ilikuwa kwenye rap tu.
Nikaenda kwenye rehearsal na kupiga ngoma yangu ambayo siikumbuki jina (ila ninayo kwenye daftari langu la mistari mpaka leo). Ngoma ile ilikuwa inapendwa sana na mwanangu, BOY SEARCHER kwa sababu ilikuwa ya Kiingereza, sikukaza uandishi Kama ngoma zangu nyingine lakini pia niliandika juu ya beat ya KITU GANI ya D KNOB FT Q JAY.
Watu walipagawa sana, nakumbuka manzi moja nilikuwa nayo class ikanifuata miksa kunipa pole kwa yaliyonikuta wakati ulikuwa utunzi tu, stori ya wimbo haikunihusu. Ila kisela nikasema hii manzi imeona Kuna kitu ninacho inataka iishi kwa msela hii. Nikaikataa.
Siku ya talent show imefika, jina langu halipo, kisa nilimtukana WINSTONE Mogha (Sasa hivi ni Kiongozi ACT-Wazalendo) (jamaa alikuja skuli na laptop miksa kujidai yeye ndio MC kwenye rehearsal. Alipotaka nichane acapella kama wengine nikamtolea uvivu. Wakanipunyua bila kujua. WISTONE alikuwa **** sana ila kwa sasa ni mheshimiwa fulani huko Kigoma kwenye chama kikubwa cha siasa.
Show ikapigwa mchana, nikasema famililai kwani nini! Wana wote walichana mchana. Nikawa na mchecheto wa kumsikia LYATUU lakini hakuchana. Na waliochana niliona famba tu. Nilifurahia battle ya Mchawi na Liffo kwenye msosi na vichekesho vya KAIDUDU.
ASEEE! Kipunga kikapigwa na jioni wana tukahamia bwaloni kuruka debe! Oyaaa, moja flani hivi jioni nikasikia sauti flani hivi bila kuona mtu
"MAJUKUMU YANABANAAAAA" Form six wakaitikia
"YANABANAAAAA"
Akarudia, "MAJUKUMU YANABANAAAAA"
Wakaitikia "YANABANAAAAAA"
MAJUKUMU
YYEEEEEAAAAH
MAJUKUMU
WOOAAAAAAAH
Yes alikuwa LYATUU bwana! Jeans kali, mpya na mtisheti wa Unyamwezini huko, alipiga show kubwa sana yule mjomba.
Goma likaisha, nikasikia makofi, sielewi nini kinaendelea, nakuta CHARITY anaingia STEJINI taratibu, watu wanazidi kupiga makofi
Charity akapewa microphone, kilichofuata sikuambii!!!
"NINACHOTAKA DUNIA IJUEEEEE"
"ACROSS THE WORLD, ACROSS THE WORLD, WHAT"
"NINACHOTAKA, WATU WATAMBUEEE"
Ule mdude, jamaa alirekodia juu ya beat ya TI halafu Bwana mdogo Pascal Francis akawa anasema Lyatuu aliharibu beat ya TI. Mchawi mpaka leo huyu mtoto.
Lyatuu ALIINGIA zake chuoni IFM na baada ya hapo sina taarifa zake na sijui kama bado anafanya game au laa!
Hats off Lyatuu! Alikuwa na ngoma mbili alizorekodi wakati mimi nilikuwa najirekodi kwenye visimu vya Kichina, Mchawi memory card enzi hizo, japo kuna mwana alitaka nimuuzie ngoma yangu niliyojirekodi kwa simu.
NDIYO, NILIOMBA KUPIGA PICHA NA STAA
Kama ulisoma Mwakaleli mwaka 2009 hadi 2012 possibly ulipata kumjua.