Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Tangu Raisi kikwete alipokuwa katika harakati zake za kugombea uraisi kulikuwa na matukio ya hapa na pale kuhusiana na ulinzi wake kwa ujumla. Wengi tunakumbuka tukio la kikwete kuvamiwa jukwaani kule Mwanza, jaribio la msafara wake kurushiwa mawe kule mbeya, na juzi hapa Dar msafara wake kukumbwa na matukio ya gari kuharibika mara mbili kwa mtazamo wangu naona ni hatari....Najiuliza je, ni kuwa walinzi wa raisi hawajui wanachofanya? au kuna uzembe ndani ya idara ya usalama katika kumlinda raisi? Sitashangaa hali hii siku moja ikasababisha maafa kwani udhaifu tunaouona si jambo jema kabisa.....:fencing: