The Finest
JF-Expert Member
- Jul 14, 2010
- 21,605
- 6,080
Kiongozi wa hazina ya mkopo wa dhamana katika mataifa ya Ulaya yanayotumia sarafu ya Euro Klaus Regling amewasili mjini Beijing,Uchina katika harakati za kuishawishi Uchina kuwekeza fedha katika hazina hiyo.
Fedha hizo zitatumika kuzisaidia nchi wanachama wanaokabiliwa na tatizo la madeni.
China huenda ikaridhia ombi hili na kuwekeza dola bilioni mia moja katika hazina hiyo. Hata hivyo China imesisitiza kwamba lazima ihakikishiwe kuwa fedha hizi zitalindwa kabisa.
Viongozi wa mataifa hayo ya Ulaya tayari wameafikiana kuongeza hazina hiyo kwa dola trilioni moja nukta nne.
Fedha hizo zitatumika kuzisaidia nchi wanachama wanaokabiliwa na tatizo la madeni.
China huenda ikaridhia ombi hili na kuwekeza dola bilioni mia moja katika hazina hiyo. Hata hivyo China imesisitiza kwamba lazima ihakikishiwe kuwa fedha hizi zitalindwa kabisa.
Viongozi wa mataifa hayo ya Ulaya tayari wameafikiana kuongeza hazina hiyo kwa dola trilioni moja nukta nne.