Ukosefu wa ajira kwa Vijana: Lowassa atabiri vita Tanzania...

tumaini makene hatukushangai manake tuna uzoefu na watoto wengi wa nje ya ndoa huwa wanavichwa vigumu sikuzote,naww ni kati ya wachumia tumbo

Matusi yanatoka wapi bro? Kwani ndoa ni chupa, kwamba wanandoa ndo wanakaa humo? Hebu jielekeze kwenye ufafanuzi yakinifu alioutoa Makene, tena ametupatia mpaka sehemu ya maoni ya KUB Mbowe... Vijana wa Lumumba badiliken, mnakera sana.
 
Yaani ukweli imeshangaza sana wale watu siku ile kama wanatazama mechi ya simba na yanga ukweli hili taifa linapoelekea pabaya its the shame all media around the world show that victory
 
Una ushahidi wa ufisadi wa Lowassa? au na wewe unaishi kwa porojo!

Ukitoka Msalani ushahidi utaukuta mezani, maliza kwanza! Ngoja Katiba mpya yenye maoni ya wananchi ipite uone kama hatahamia Papua New Guinea.
 
Tumaini makene nyie wale wale kasoro tar
hakunaga hata siku moja wewe umeamin habar yeyote
nadhan hata yule baba yako wa kambo huamini kama ni baba yako,ila subir muda utasema

Una jina la kikaguru, lakin sijakuelewa haya matusi na chuki za kimipasho ya kiintarahamwe umeyatoa wapi
 
Una jina la kikaguru, lakin sijakuelewa haya matusi na chuki za kimipasho ya kiintarahamwe umeyatoa wapi

We ndio makene?au ndio mmeanza kuchanganya id!manake vijana wa ufipa mnaongoza
jitahid uwe utumia akili yako usipende kushikiwa akili
 
Matusi yanatoka wapi bro? Kwani ndoa ni chupa, kwamba wanandoa ndo wanakaa humo? Hebu jielekeze kwenye ufafanuzi yakinifu alioutoa Makene, tena ametupatia mpaka sehemu ya maoni ya KUB Mbowe... Vijana wa Lumumba badiliken, mnakera sana.

Nahisi nawew jiwe limekukupata!
 
Lowasa hawezi kusafiria nyota ya rais kivuli wa kudumu ambae ana kipaji cha kuunda baraza la mawaziri vivuli wa kudumu. Hao vivuli ndio wanaosafiria nyota za CCM maana CCM ni serikali hai na bila CCM hakuna kivuli (CDM & others)
Hahahah naona leo
CCM mmeamua Lowassa asafirie nyota ya Mwenyekiti wa Chadema Freeman
Mbowe. Kwel mnadhihirisha Lowassa amechoka.

Anyway... Hakuna mahali ambapo Mwenyekiti Mbowe alitaja jina la Lowassa
katika mchango wake. Hiyo ni tafsiri ya gazeti moja leo.

Tena kwenye mchango wake Mwenyekiti Mbowe aliposema kuwa ajira kwa sasa
tayari ni janga la taifa akitumia mfano wa ile interview ya Uhamiaji,
alikwenda mbali na kuonesha namna ambavyo Serikali ya CCM haiwezi
kutatua tatizo la ajira, ijiandae kuondoka madarakani mwaka kesho ione
wapinzani wa leo wakikamata nchi mwaka kesho watakavyoweza kuibadili
nchi.

Akaongeza kuwa upinzani wanayo mawazo mbadala ambayo wamekuwa wakiyatoa
kila siku, lakini kwa sababu Serikali ya CCM imechoka, imekuwa haiwezi
kupokea Mawazo mapya tena.

Kama haitoshi akasema madam upinzani hawajaingia serikalini wataendelea
kutoa maoni yao kwa ajili ya manufaa ya nchi na Watanzania wote, hivyo
ni jukumu la walioko madarakani kupokea au kuacha.

Akaonesha uongozi zaidi kwa kuonesha njia mbadala ya namna ambavyo
halmashauri nchini zinaweza kuzalisha ajira kati ya 5,000 hadi 10,000
kila mwaka badala ya kutegemea Central Govt ifanye kazi hiyo kwa kila
kijana wa Kitanzania kutoka kila kona ya nchi nzima. Central govt ambayo
tayari ndiyo imetufikisha hapa na imechoka.

Serikali hiyo iliyochoka ndiyo ambayo Lowassa amekuwa sehemu yake na
hakuwahi kutoa alternatives ya kutatua tatizo hilo ambalo amekuwa sehemu
ya kulikuza na kuliatamia.

Mbowe alionesha kwa facts namna ambavyo muundo huu wa utawala tukionao
ambao Lowassa amekuwa sehemu yake na anausapoti kwa matamanio yake ya
kutawala (si kuongoza) hauwezi kumaliza tatizo la ajira bali utaendelea
kulikuza tu kwa sababu hakuna mkakati wowote ambao unawekwa kushughulika
na tatizo hili ambalo alisema tayari ni janga la taifa kwa kutumia
mfano huo wa interview ya uhamiaji ambayo ni dalili ya tatizo kubwa kati
ya mengi ambayo yameshawazidi uwezo CCM.
 
Ni habari ya miaka mitatu iliyopita ila ina ukweli ndani yake. Vijana hawana kazi wanajiunga na Al Shabab, mbwa mwitu, panya road na wengine. Na polisi waliwashindwa. Kwani vita inaanzaje mpaka ishike kasi? Mwanzo wa makubwa ni madogo.
 
EL amesema hayo mwanza alipokua mgeni rasmi kuchangia kanisa katoliki, kukosekana kwa ajira kwa vijana ni bomu linalotarajia kulipuka wakati wowote hivyo kusababisha vita nchini.

Kuna vijana 2.5m wasio na ajira!

==========
UPDATED:

Na mwandishi wa FikraPevu.com

Kuna vijana 2.5m wasio na ajira!

==========
UPDATED:

Na mwandishi wa FikraPevu.com[/QUOTE]

UPDATED:

Na mwandishi wa FikraPevu.com


Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (MB), amesema kwamba, amani iliyopo hapa nchini ipo mashakani kutoweka, kutokana na wimbi kubwa la vijana kutokuwa na ajira maalumu, hivyo Serikali inapaswa kuweka mikakati madhubuti ya kuzalisha ajira nyingi kwa vijana.

Amesema, kati ya nguvu kazi ya taifa inayokadiriwa kufikia milioni 25 kwa sasa, kati yake milioni 17.5 ni vijana ambao kimsingi wanakabiliwa na
ukosefu wa ajira maalumu, jambo ambalo Serikali inapaswa kulipatia ufumbuzi haraka sana ili kulinda amani ya nchi isiyumbe au kutoweka kabisa.

Lowassa, aliyasema hayo leo Jijini Mwanza, wakati alipokuwa akizungumza kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa Katoliki, Parokia ya Nyakato Jimbo Kuu la Mwanza.

Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa alisema, hali hiyo inachangiwa na uchumi duni wa nchi ikiwa ni pamoja na sera mbovu za elimu zisizozingatia uhitaji wa
soko la ajira na vijana wengi kutotaka kuchukuwa masomo ya sayansi na hisabati ambayo yana fursa kubwa ya kupata ajira.

Kiongozi huyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyokusanya sh. milioni 200 na kuvuka lengo la sh. milioni 120, alisema kwa sasa tatizo la ukosefu wa
ajira kwa vijana hapa Tanzania limefikia zaidi ya asilimia 30, ikilinganishwa na wastani wa asilimia 21 wa tatizo hilo linalozikumba nchi zote za Bara la Afrika.

"Siku zote nimekuwa nikisema nchi yetu inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa
ajira kwa vijana. Hali hii isipopatiwa ufumbuzi na Serikali, amani ya nchi yetu inaweza kuyumba.

"Kati ya vijana 850,000 wanaoingia kwenye soko la
ajira baada ya kumaliza masomo yao ya msingi, sekondari na vyuo, ni asilimia tano tu ndiyo wanapata ajira katika sekta rasmi isiyo ya kilimo. Na hii ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa letu", alisema Lowassa ambaye alichangia sh. milioni 11 katika harambee hiyo.

Kwa mujibu wa Lowassa ambaye alionekana kushangiliwa kila wakati pale jina lake linapotajwa, vitendo vya rushwa vinavyoonekana kuota mizizi katika sehemu za utoaji
ajira rasmi Serikalini na kwenye taasisi za umma, ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo kama hayo.

Sababu nyingine alizozitaja Lowassa zinazochangia kukosekana kwa
ajira kwa vijana nchini ni pamoja na sera mbovu za ajira na mitaala ya elimu isiyokidhi mahitaji ya soko la ajira Bara la Afrika na duniani kwa ujumla.

"Kutozingatia mabadiliko ya kiuchumi, kibiashjara, kisiasa, kijamii na kiteknolojia nchini, Afrika Mashariki, Afrika na dunia nzima ndiyo inayozalisha yote haya mabaya", alisema Lowassa ambaye alionekana kuwa kivutio kikubwa kwenye harambee hiyo.

Awali, Makamu Baba Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Mwanza, Askofu Richard Makungu aliwaonya watu wanaowanyooshea vidole wenzao, na kusema vitendo hivyo si vizuri hata kidogo, kwani watu hao wakichunguzwa nao wana mabaya yao, na wala hata choo majumbani mwao hawana kabisa.

Askofu Makungu alisema, vitendo vya kulalamika lalamika ama kwa kuilalamikia Serikali, ofisa, kiongozi au mtu fulani huo ni sawa na ufedhuli mtupu, na kwamba Watanzania waache kusonta vidole watu, ili taifa liweze kupata taranta kutoka kwa Mungu.

Hata hivyo, alisema ujio wa Lowassa katika harambee hiyo ni mzuri sana, na alisema kwa vile kanisa hiolo limejengwa kwa tofali moja moja, basi na waumini wa kanisa hilo watakuwa tofali moja moja kwa Lowassa.






ITS A TIME OPPORTUNITIES AND NOT A TIME BOMB!

Tukiamua VITA HII ITAKUWA KWA MEMA NA SI MABAYA, HUU NI MLIPUKO WA FURSA, KUNDI HILI NI JESHI KUBWA SANA LIKIPATA MUUNGANISHAJI NA KUELEKEZA NGUVU YOTE HII KWENYE MBADALA WA AJIRA RASMI NA KUJENGA UCHUMI.

Maandiko yanasema yamtokayo mtu ndiyo yaujazayo, pia wanafalsafa wanasema ukiweza kubadili mawazo na maneno yako unaweza kubadili maisha yako, matarajio ya wengi kwa Kiongozi awaye yote ni uwezo wake wa kuwa mbunifu wa kutafuta milango mingine badala ya kunganania mlango uliofungwa.

Tukibadili mawazo na maneno yetu tutabadili si tu maisha yetu bali taifa na dunia kwa ujumla.

"the words you believe in will create the world you will live"

"You cannot arrest what you cant address"

"There is no such a thing as possession without confession, for our confession gives us possession"

"words can injure your ego or inflame your ego"

"Words not only create emotions, they create actions"


Ubunifu ni kuanza na picha ya mwisho mwanzoni, tujiulize mwisho wa siku tunataka nini, iwe ni katika ajira rasmi, zisizo rasmi, ujasiriamali au kilimo, nini tunataka mwisho wa siku, kisha tutafute njia mbadala ya kupata tutakacho.

Laiti angewekeza kutafuta njia mbadala toka muda maneno haya yamesemwa hivi leo nina uhakika angekuwa ameshawatoa zaidi ya asilimia 50 kwenye mtanziko huu, for THIS IS NOT A TIME BOMB in my opinion ITS TIME OPPORTUNITIES all we need is someone who can connect this workforce to do miracles.



AJIRA, yes kama yapatikana na kila mtu awe nayo. lakini kama hakuna na ni ukweli hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kutengeneza ajira kwa wahitimu wote wanaozalishwa kila mwaka, kuendelea kufikilia kuwa njia pekee ni kupoteza muda, tufikiri njia mbadala, ziko nyingi sana.

Kulalamika, kulaumu kulia kama alivyosema Baba Askofu (ni kama amjibu kiongozi) hakutatusaidia kama taifa. tunahitaji viongozi wabunifu, na si lazima uwe rais ndo uwe mbunifu, kuwa mbunifu sasa utupe sababu ya kukuweka magogoni.
 
NAkumbuka mh Edward Lowassa alisema sana kuwa vijana wasio na ajira ni sawa na BOMU linalosubiri kulipuka. Wengi walimbeza sana pengine kwa kutomuelewa au kwa ishabiki tu hasa kutokana na msukumo wa kisiasa ulivyokuwa.

Hivi leo huu ni mwaka wa pili tunaelekea vijana waliohitimu vyuo mbalimbali wamezagaa mitaani hawajui hatma yao.

Nguvu ya kuwa watulivu ilichagizwa pengine na zoezi la uhakiki wa watumishi hewa ikiwemo walioghushi vyeti isipokuwa Bashite.

Kila mhusika leo hana ujasiri wa kulisemea hili na vijana wameanza kuzoea maumivu ya kukaa bila ajira ya uhakika pamoja na kuwa na elimu.

Mkuu wa Mkoa wa Dar aliwahi kutangaza operesheni ya kukamata vijana na wale wote wasio na ajira jijini, japo hakuweka wazi akishawakamata atawapeleka wapi? Lakini baadhi ya watu walihisi hiyo inaweza kuwa namna ya kusaidia kuonesha ukubwa wa tatizo la ukosefu wa ajira. Mpaka leo zoezi kimyaaaaaa.

Nihitimishe kwa kusema tu kuwa hili Bomu bado halijateguliwa na lingalipo, hivyo ni wajibu wa wahusika kuwajibika kutegua Bomu hili.
 
subirini bado tuna hakiki wenye vyeti feki, hamuoni hata bashite bado hajafikiwa.

mkishaona bashite kahakikiwa vyeti vyake ndio muanze kulalamika suala la ajira, kwa sasa muwe wapole kwanza
 
Serikali tunajua haiwez kuajir wahitim wote lkn inauwezo wa kuajir baadh yao ingefanya hvyo ili kupunguza msongamano wa hawa watu kwny vifursa vichache huku mtaani sasa kila mtu anakuwa mjasiriamali kaz za kitaaluma atafanya nan??? Nina rafik yng ni registered doctor MD kabisa lkn ni dereva wa daladala kule moshi mwaka unakatika sasa tangu aingie huko inamaana tanzania tuna madaktar wng kias hicho???
 
Mambo muhimu yameingiliwa na siasa, tusitegemee awamu hii ya ubaguz itatenda haki, itafka muda vjana CV zao zioneshe na chama, ukiwa ACT tu sio kipaumbele maana siku hiz kuna makundi ya wanufaika wa nchi,
 
Huyo fisadi anatafuta attention kwa gharama zozote.Alipokua waziri mkuu alifanya nini zaidi ya kuzidisha tatizo la ajira kwa kuingiza nchi gizani kupitia Dili lake la RUCHMOND na uzalishaji kupungua huku vijana wengi wakiachishwa kazi viwandani ili viwanda visipate hasara? Leo hii watoto 16,500 wameshindwa kujiunga kidato cha tano.Mradi wake wa shule za kata ulioendeshwa bila kuwa na mtaaala wa elimu hakuona kuwa nao ni tatizo?

Hebu huyu mzee aache unafiki yeye na chama chake aseme wahusika wa RICHMOND ni akina nani kwanza

Ndugu yangu sasa hivi wenzako wanampigia magoti wanamsujudia wanamuabudu
 
Lowassa anaweza kuinunua hata JF impigie kampeni. Pesa ni kitu kingine kabisa.

Utabiri wako ulikuwa kweli mkuu...sasa si kashakinunua kile chama cha kubadilishia gear angani na sasa Manyumbu yakoje busy kumsafisha kweli mkuu ulionaga mbali
 
ZD,

Udhaifu wa JK unasababisha hata wale walioonekana ni wabaya waonekane Malaika. And they know how to play this game, I'm speechless!

Tusaidie JK, ng'atuka mkuu... Tunaelekea kubaya kama taifa, unaweza usielewe nini kinaendelea au unaambiwa unapuuza lkn dalili si nzuri kwako!
Tumemmis
 
Back
Top Bottom