OMBUDSMAN mtoto
Member
- Sep 28, 2012
- 87
- 32
Hata angesema atakuwa hana moral authority. Mimi Ombudsman nasema chunguza uchukuwe hatua!
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.
Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.
Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.
Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?
Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,
Nawasilisha.
"(EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba," Atazungumziaje, wakati mwenye umekiri kwamba anautaka kwa udi na uvumba?
Uwanja ni wa CCM kama kuingia ikulu ni kwa manemane, udi na uvumba.
........... Hakuna cha ajabu kujipanga ni kujipanga tu.... Mh. EL anajipanga kama kuna anayeweza ajaribu kupangua..... si muda bado upo!
last week kwenye kipindi cha hamza kasongo hrs alikuwepo mkama moja ya maneno aliosema ni hatari sana kujionesha mapema kwamba unataka kugombea nafasi kubwa kwani unawapa maadui nafasi kubwa ya kukupinga
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.
Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.
Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.
Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?kama ni simple jibumwenyewe sisi tunajibu maswali magumu na kufanya maamuzi magumu.
Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,
Nawasilisha.
Umeuliza swali ambalo jibu lake linafahamika directly! EL ana ukwasi mkubwa sana! ni Expert wa mbinu chafu hasa rushwa! ndiye aliyemuweka JK madarakani.
Tatizo la wana JF wengi ni kuandika mambo mengi kwa kuongozwa na hisia, chuki binafsi na unafiki badala ya kufanya utafiti na kuwa na ushahidi hasa linapokuja suala linalomhusu Lowassa. Hivi kama mna ushahidi na tuhuma za Lowassa kuwa ni fisadi na mtoa rushwa mkubwa je ni kipi hasa kilichosababisha msiupeleke huo ushahidi wenu mahakamani?. Je hakuna vyombo vya kupambana na rushwa na ufisadi nchini vya kumkamata na kumhoji?. Kama hayo yote hayawezekani basi Lowassa ni "mtakatifu" na anastahili kuingia ikulu 2015. No research no right to speak.
Lowassa aongee nini wakati karibu rushwa yote inatoka kwake? Ulitegemea kweli nguruwe ausifie uturi wakati yake kinyaa? Lowassa haoni kama kilichofanyika ni jinai na rushwa kwa vile yeye na genge lake ndiyo wanufaika. Ahongea hao CCM wenzake lakini hatahonga watanzania wote. Hata akifanya hivyo akiingia kwenye kinyang'anyiro kama mgombea wa CCM nitapenda sana.Hii itakukwa ni fursa ya aina yake kwa upinzani kuchukua nchi kirahisi ingawa nasikia wana mpango wa kumuengua kwa kuchagua mwanamke. Tuombe Lowassa aendelee kampeni zake ili tummwange mambo kwenye uchaguzi.
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.
Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.
Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.
Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?
Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,
Nawasilisha.