Ujumbe wangu kwa wale wafugaji wa kuku wa kienyeji

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
1230077_511303425617632_1208004700_n.jpg


NI VIZURI KUJUA VITU FLANI, USUSANI KATIKA UJASIRIAMALI

Ulishaji: Kuku wa kienyeji wanaweza kulishwa

kwa kumia mahindi, mchele, na mabaki ya
ugali. Vyakula hivi ni lazima vikaushwe vizuri na
kusagwa vizuri. Ulishaji ni lazima ufanyike katika
sehemu safi au kwa kutumia vyombo
vilivyotengenezwa maalumu kwa ajilii ya kulishia
kuku.
Banda: Kuku wawe wa kienyeji au wa kisasa,
wanahitaji kuwa na banda zuri kwa ajili ya
malazi na kuwalinda. Wanahitaji chumba chenye
nafasi ya kutosha na kinachopitisha hewa ya
kutosha. Ni lazima kuwawekea fito kwa kuwa
ndege hupenda kupumzika juu ya fito. Ni lazima
banda la kuku lifungwe vizuri nyakati za usiku ili
kuzuia wanyama wanaoweza kuwadhuru kuku.
Ni lazima liwe safi wakati wote ili kuzuia
magonjwa kama vile mdondo na mengineyo.
Usitumie pumba za mbao au nguo kuukuu
kwenye viota vya kutagia kwani huchochea
kuwepo utitiri na funza wa kuku. Inashauriwa
kutumia mchanga laini.
Maji ya kunywa: Kuku wapatiwe maji safi. Ni
lazima kuangalia mara kwa mara na
kuyabadilisha maji. Kamwe usiwape kuku maji
machafu.
Chanjo: Chanjo kwa mifugo ni lazima ili kuzuia
mashambulizi ya magonjwa. Magonjwa
yaliyozoeleka ni kama vile Mdondo, Kideri, Ndui
ya kuku, na homa ya matumbo (typhoid).
Chanjo kwa kawaida hutolewa mara moja kwa
kila baada ya miezi miwili.
Uwekaji wa kumbukumbu: Kumbukumbu
zijumuishe aina ya ulishaji, namba ya uzalishaji,
muda wa mwisho wa matumizi, kiasi cha
malisho kwa kila siku, idadi ya vifo, na idadi ya
mayai yaliyozalishwa.
Mwanzoni unahitaji nini?
Wafugaji walio wengi wanauliza wanahitaji nini
katika hatua za awali ili kuweza kuanzisha mradi
wa ufugaji wa kuku. Hii itategemea aina ya kuku
uliochagua kufuga.
Ni busara kuwa na vifaa muhimu vinavyohitajika
na viwe katika hali ya usafi kabla ya kuweka
kuku bandani mwako. Kama unaanza na
vifaranga, vifuatavyo ni vifaa muhimu
vinavyohitajika kwa ajili ya vifaranga 200.
• Tenga na utengeneze banda zuri lenye joto na
hewa ya kutosha wakati wote.
• Vyombo vinne (4) vya kunyweshea maji, hii ni
katika wiki 2 za mwanzo na uongeze vyombo
taratibu kulingana na kuku wanavyokua.
• Vyombo vinne (4) vya kulishia chakula, na
viongezeke kulingana na kuku wanavyokua.
• Matandazo makavu na safi, inaweza kuwa
maranda au mabua ya ngano.
• Pakiti moja au mbili za dawa ya Coccid (hii
inapatikana katika maduka yote ya kilimo). Hata
hivyo, utaratibu wa chanjo ni lazima
ukamilishwe.
• Chakula kwa ajili ya vifaranga ambacho
kimezalishwa na watengenezaji wanaoaminika.

chanzo:MziziMkavu

Kazi kwenu Wafugaji wa kuku wa Kienyeji.
 
Asante sana mkuu, mi nauliza ni chakula gani niitawapa kuku wa kienyeji ili wawe wanataga sana, mana kwa sasa ninatumia pumba na mashudu ya alizeti.
 
Asante sana mkuu, mi nauliza ni chakula gani niitawapa kuku wa kienyeji ili wawe wanataga sana, mana kwa sasa ninatumia pumba na mashudu ya alizeti.

Una uhakika huo mchanganyiko unawapa kuku mahitaji yote wanayohitaji?
 
Niwape dawa gani kuku wangu iwapo nimewanunua sehemu tofauti tofauti ukizingatia ni wa kienyeji ili kuepuka mlipuko wa magonjwa.
 
Asante sana Dr. MziziMkavu, my multi-purpose Doctor. Shida kubwa iko pale kuku wa kienyeji wanataga na umeshawawekea kila mmoja kiota ila sasa wanapigania sehemu moja kutaga na kuatamia. Daktari nisaidie kwa hili maana mayai huharibika sana.
 
Asante sana Dr. MziziMkavu, my multi-purpose Doctor. Shida kubwa iko pale kuku wa kienyeji wanataga na umeshawawekea kila mmoja kiota ila sasa wanapigania sehemu moja kutaga na kuatamia. Daktari nisaidie kwa hili maana mayai huharibika sana.

Kwa hili jipange utafute incubator ndio itakuwa suluhisho sahihi...
 
Kwa hili jipange utafute incubator ndio itakuwa suluhisho sahihi...

Asante sana mkuu, hakika hili ni suluhishi, kuna moja niliiona inatumia bothe kerosene and electricity ila mtengenezaji yuko Arusha. Nitajitahidi niipate maana siku hizi ni bora ujiandalie mwenyewe nyama maana kuku wa kisasa na nyama nyekundu ni majanga. Bora ule wako wa kienyeji na mayai yake kwa afywa.
 
naomba unsaidie kuniambia mchanganyko mwingine utakao tosha vru2bsho vyote

Pumba za mahindi, mashudu ya alizeti/pamba, soya cake, dagaa waliosagwa, chokaa na chumvi..........jaribu kutengeneza chakula cha kilo 50 kwa mchanganyiko ufuatao....
Pumba ya mahindi........................kilo 25
soya cake..................................kilo 5
mashudu ya alizeti au pamba..........kilo 15
dagaa waliosagwa........................kilo 2.5
chokaa.......................................kilo 1
chumvi.......................................kilo 0.5
 
aise mkuu mimi natafuta mayai ya broilers au layers anayeweza kunipatia tafadhali nahitaji mengi sana kila baada ya wiki moja nataka mayai elfu moja wakuu
 
Pumba za mahindi, mashudu ya alizeti/pamba, soya cake, dagaa waliosagwa, chokaa na chumvi..........jaribu kutengeneza chakula cha kilo 50 kwa mchanganyiko ufuatao....
Pumba ya mahindi........................kilo 25
soya cake..................................kilo 5
mashudu ya alizeti au pamba..........kilo 15
dagaa waliosagwa........................kilo 2.5
chokaa.......................................kilo 1
chumvi.......................................kilo 0.5

Asante kwauo mchanganyiko k2 gan naweza ku2mia badala ya chokaa?
 
Asante kwauo mchanganyiko k2 gan naweza ku2mia badala ya chokaa?

Chokaa ni ya muhimu kwa sababu inawapatia madini ya Calcium ili mayai yawe na ubora,,,,,sijajua kama kuna mbadala.
 
Asante sana mkuu, mi nauliza ni chakula gani niitawapa kuku wa kienyeji ili wawe wanataga sana, mana kwa sasa ninatumia pumba na mashudu ya alizeti.

Ingia Jukwaa La Ujasiliamali Kuna Maelezo Mengi Sana
 
Nahitaj KUKU wa kienyej koo 45 na dume 15 ili nianze Kufuga ,je Niko sahihi kuanza na kuku hawa ? Nitawapataje ?
 
Nahitaj KUKU wa kienyej koo 45 na dume 15 ili nianze Kufuga ,je Niko sahihi kuanza na kuku hawa ? Nitawapataje ?

ok jaribu kuwasiliana na wataalamu lakin kuhusu wapi pa kuwapata kuku nitafute mm ninakuuzia kuku kutoka malawi ni kuku wenye umbo kubwa na wanataga vizuri ,tuwasiliane karibu tufanye biashara mim nipo mbeya,piga0764786277
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom