Mada inahusika,
Ujumbe huu unawahusu wana mageuzi wa Kweli wa CHADEMA na GT pekee na sio wafia chama na wapiga debe.
Kuifahamu historia ya mapambano ya Zanzibar walau kuanzia 1995 hadi sasa
Vyovyote iwavyo huwezi kuacha mchango wa Maalim Seif na wanamageuzi wenzake. Tafakarini nguvu ya Upinzani Zanzibar licha ya uchache wa watu wa huko lakini wamejitofautisha kwa mbali na watu wa huku Bara. Kikubwa ni uaminifu, umadhubuti na kujielewa. Hiyo inachagizwa na AJENDA ya Zanzibar.
Chama chochote kile kikikubalika Zanzibar na Yumkini wafuasi wa Maalim Seif hicho chama kinakuwa na nguvu kwa siasa za Zanzibar. Ilikuwa CUF na sasa ni ACT. Kwanza kubalini kuwa ACT kwa sasa Zanzibar ndio inakubalika na imebebeshwa Ajenda ya Zanzibar kupitia Maalim Seif.
Kumbukeni kuwa Wazanzibari wamepitia mateso mengi, maudhi, kebehi, mauaji na kila aina ya uovu wa kisiasa kuliko jamii nyengine yoyote hapa Tanzania baada ya kuja vyama vingi. Kumbukeni hawa wanajuwa wanachokifanya na kamwe hawahitaji mwalimu wa kudadavuwa kutoka kwengine.
Kitendo cha Kupendwa ACT-Wazalendo ni baada ya wasaliti ndani ya CUF kutaka kuipoteza Ajenda ya Zanzibar. Wazanzibari wanahitaji viongozi wakweli na wanaotambua shida zao ndani ya Muungano. Kiongozi yoyote wa chama chochote kile hawezi kuuungwa mkono Zanzibar bila kukubaliana na usalama wa ajenda zao.
Kama mnakumbuka migomo ya 1995 hadi wanafunzi kufukuzwa mashule, wafanyakazi wapinzani kufukuzwa makazini, watu kuuwawa yalitokea Zanzibar pekee hadi ikafanyika miafaka ya awali zaidi ya miwili na bado hakukuwa na mafanikio. Wakati Wazanzibari wanafanya haya na hadi kuilazimisha CCM kuuwa na kuzalisha wakimbizi mwaka 2001 Wazanzibari walikuwa Peke yao wakati ule na CUF yao.
Wakati wanagoma, kunyanyaswa na kudhulumiwa hivyo vyama vyengine vilikuwa havionekani kukerwa na kilichowapata Wazanzibari. Hatukuona wengine wakiandamana na kupaza sauti za wazi. Watu walifikiri yale yaliwahusu wazanzibari sasa jitihada hizo za kujitolea hadi kufanikiwa Zanzibar kuwa na GNU kulihitaji Sacrifice na Risk za roho za watu. Hatua hiyo hata kama haijafanikisha malengo kwa asilimia mia lakini walau kuna kauchochoro fulani ambacho kwa Upande wa Bara hata robo ya siasa za Zanzibar hazijafikia.
Maana yangu wasitokee wana Mageuzi hasa CHADEMA tunayoiamini, ikawa wepesi wa kusahau historia na kushindwa kuitazama Zanzibar kwa jicho la pekee. Hii inaitwa Zanzibar Chapter, siasa za kule zisichukuliwe kirahisi kihivyo.
Hebu jiulizeni kwa nini mara baada ya Maalim Seif kufanikiwa yeye na Mh Mstaafu Karume kupata GNU wahafidhina wa CCM walichukia kweli kweli?
Jiulizeni Miaka 5 ya GNU ya 2010 - 2015, wahafidhina walivyopata tabu ndani ya serikali na sasa kutamani kuivunja GNU?
Tukubali tu chama chochote kitakachokubali kubeba ajenda ya Zanzibar bila watu wengine na wafuasi wa vyama vyengine kuielewa siasa ya Zanzibar wanaweza kuwahukumu tofauti viongozi wa vyama kama inavyoonekana leo ACT. Hiki ni chama ambacho kama vilivyo vyama vyengine lazima vitangulize maslahi ya wanachama wao na hapa muhimu ni ile dhana ya Zanzibar Chapter. Huwezi kuendesha siasa za Zanzibar kwa mtazamo wa Tanzania nzima. Kama kuna Viongozi ndani ya CHADEMA au kwengineko wanashindwa kuliona hili ndio huibuka zile dhana za Ukoloni wenyewe.
Hivi unadhani mtu kama Maalim Seif aweze kuwasaliti Wazanzibari kweli kama inavyotaka kuaminishwa leo eti kufuata vyeo ? wamesahau kwamba hakuna sacrifice ambayo hajaifanya ikiwemo hiyo ya kukubali kupoteza vyeo kwa maslahi ya wazanzibari?
Mtu ambaye ni mastermind anayejua wapi pa kugoma, wapi pa kususa, wapi pa kuridhiana wapi pa kusamehe, wapi pa kukemea, wapi pa kushupaa na wapi pa kulainika ili kufikia malengo eti watokee watu waanze kutumia scenario moja tu ya 2020 kuhukumu haya bila kujua kituo kiko wapi cha Maslahi ya Wazanzibari?
Hivi mnadhani ACT walikuwa wajinga kwenda kuchukuwa maoni ya wanachama wao Zanzibar yote? Hivi mnadhani siasa za Zanzibar zinahitaji direct method tu ? huko ni kutozijua siasa za Zanzibar.
Lau mngejua kwamba Dr Mwinyi anapata tabu ya Wahafidhina wa CCM leo na vile wahafidhina wanavyolaani ACT kukubali kuingia GNU basi baadhi ya wafuasi wenzetu wa Chadema wasingethubutu kupaza maneno ya kuudhi hadharani. Ni kukosa kujua kinachoendela Zanzibar.
Unaopaswa kuwa Mwelekeo Sahihi
Chukueni mwelekeo wa baadhi ya viongozi weledi ndani ya CHADEMA ambao hadi sasa wameamua kunyamaza kimya. Wekeni hakiba ya maneno kuhusu ACT na waachiieni ili mprove wrong ili mje muwasute baadae.
Tambuweni strategies za siasa na mikakati inatofautiana na wakati, mahitaji na maeneo. Eneo la Zanzibar ni very Perculiar, linahitaji lipewe nafasi yake na sio kuanza kuparamia Viongozi wa chama kinachokubalika huko bila kuzingatia hayo.
Tambueni kuwa Siasa za Zanzibar zinajitosheleza kwa sababu ya uwepo wa Muungano, ukishalijua hilo utajuwa Mbinu za mapambano ya Zanzibar sio lazima ziwe za Tanzania nzima.
Hakuna haja ya kutoa kebehi na matusi naamini iko siku kupitia haya maamuzi ya ACT wanamageuzi wanaweza kuja kuwapongeza hawa hawa ACT.
Chukueni dhana ya Maridhiano japo feki ikibidi iwasaidie kusogeza mbele dhana ya mageuzi na mapambano na jitahidini kusoma njiambali mbali za mapambano duniani.
MWISHO
Nachukuwa nafasi hii kuawapongeza ACT kwa kujali hisia za wengi za wanachama wao hasa wa Zanzibar na kuwatilia maanani kama supporters wao kindaki ndaki kwa sasa lakini na kwa pekee kuibeba ajenda ya Zanzibar kwa vitendo kwa kutambua siasa za Zanzibar zina kona nyingi. Natambua mchango wa manahodha Hodari waliopo ACT. Kudos.
Nashauri vyama vyengine viwape muda ACT na mambo ya ndani ya Upinzani yasianikwe hadharani kwa maslahi mapana ya Upinzani. Bora kuweka hakiba ya maneno. Kubwa zaidi watu watambuwe Zanzibar inahitaji kutazamwa kama Ajenda Maalumu kwenye siasa za Upinzani za Tanzania. Hawa walishatangulia katika mapambano ya siasa. Tukubali hilo na tuwe nao ili dhana ya mabadilo isonge mbele.
Nadhani nimeeleweka na wahuisika tu.
Kishada.
Ujumbe huu unawahusu wana mageuzi wa Kweli wa CHADEMA na GT pekee na sio wafia chama na wapiga debe.
Kuifahamu historia ya mapambano ya Zanzibar walau kuanzia 1995 hadi sasa
Vyovyote iwavyo huwezi kuacha mchango wa Maalim Seif na wanamageuzi wenzake. Tafakarini nguvu ya Upinzani Zanzibar licha ya uchache wa watu wa huko lakini wamejitofautisha kwa mbali na watu wa huku Bara. Kikubwa ni uaminifu, umadhubuti na kujielewa. Hiyo inachagizwa na AJENDA ya Zanzibar.
Chama chochote kile kikikubalika Zanzibar na Yumkini wafuasi wa Maalim Seif hicho chama kinakuwa na nguvu kwa siasa za Zanzibar. Ilikuwa CUF na sasa ni ACT. Kwanza kubalini kuwa ACT kwa sasa Zanzibar ndio inakubalika na imebebeshwa Ajenda ya Zanzibar kupitia Maalim Seif.
Kumbukeni kuwa Wazanzibari wamepitia mateso mengi, maudhi, kebehi, mauaji na kila aina ya uovu wa kisiasa kuliko jamii nyengine yoyote hapa Tanzania baada ya kuja vyama vingi. Kumbukeni hawa wanajuwa wanachokifanya na kamwe hawahitaji mwalimu wa kudadavuwa kutoka kwengine.
Kitendo cha Kupendwa ACT-Wazalendo ni baada ya wasaliti ndani ya CUF kutaka kuipoteza Ajenda ya Zanzibar. Wazanzibari wanahitaji viongozi wakweli na wanaotambua shida zao ndani ya Muungano. Kiongozi yoyote wa chama chochote kile hawezi kuuungwa mkono Zanzibar bila kukubaliana na usalama wa ajenda zao.
Kama mnakumbuka migomo ya 1995 hadi wanafunzi kufukuzwa mashule, wafanyakazi wapinzani kufukuzwa makazini, watu kuuwawa yalitokea Zanzibar pekee hadi ikafanyika miafaka ya awali zaidi ya miwili na bado hakukuwa na mafanikio. Wakati Wazanzibari wanafanya haya na hadi kuilazimisha CCM kuuwa na kuzalisha wakimbizi mwaka 2001 Wazanzibari walikuwa Peke yao wakati ule na CUF yao.
Wakati wanagoma, kunyanyaswa na kudhulumiwa hivyo vyama vyengine vilikuwa havionekani kukerwa na kilichowapata Wazanzibari. Hatukuona wengine wakiandamana na kupaza sauti za wazi. Watu walifikiri yale yaliwahusu wazanzibari sasa jitihada hizo za kujitolea hadi kufanikiwa Zanzibar kuwa na GNU kulihitaji Sacrifice na Risk za roho za watu. Hatua hiyo hata kama haijafanikisha malengo kwa asilimia mia lakini walau kuna kauchochoro fulani ambacho kwa Upande wa Bara hata robo ya siasa za Zanzibar hazijafikia.
Maana yangu wasitokee wana Mageuzi hasa CHADEMA tunayoiamini, ikawa wepesi wa kusahau historia na kushindwa kuitazama Zanzibar kwa jicho la pekee. Hii inaitwa Zanzibar Chapter, siasa za kule zisichukuliwe kirahisi kihivyo.
Hebu jiulizeni kwa nini mara baada ya Maalim Seif kufanikiwa yeye na Mh Mstaafu Karume kupata GNU wahafidhina wa CCM walichukia kweli kweli?
Jiulizeni Miaka 5 ya GNU ya 2010 - 2015, wahafidhina walivyopata tabu ndani ya serikali na sasa kutamani kuivunja GNU?
Tukubali tu chama chochote kitakachokubali kubeba ajenda ya Zanzibar bila watu wengine na wafuasi wa vyama vyengine kuielewa siasa ya Zanzibar wanaweza kuwahukumu tofauti viongozi wa vyama kama inavyoonekana leo ACT. Hiki ni chama ambacho kama vilivyo vyama vyengine lazima vitangulize maslahi ya wanachama wao na hapa muhimu ni ile dhana ya Zanzibar Chapter. Huwezi kuendesha siasa za Zanzibar kwa mtazamo wa Tanzania nzima. Kama kuna Viongozi ndani ya CHADEMA au kwengineko wanashindwa kuliona hili ndio huibuka zile dhana za Ukoloni wenyewe.
Hivi unadhani mtu kama Maalim Seif aweze kuwasaliti Wazanzibari kweli kama inavyotaka kuaminishwa leo eti kufuata vyeo ? wamesahau kwamba hakuna sacrifice ambayo hajaifanya ikiwemo hiyo ya kukubali kupoteza vyeo kwa maslahi ya wazanzibari?
Mtu ambaye ni mastermind anayejua wapi pa kugoma, wapi pa kususa, wapi pa kuridhiana wapi pa kusamehe, wapi pa kukemea, wapi pa kushupaa na wapi pa kulainika ili kufikia malengo eti watokee watu waanze kutumia scenario moja tu ya 2020 kuhukumu haya bila kujua kituo kiko wapi cha Maslahi ya Wazanzibari?
Hivi mnadhani ACT walikuwa wajinga kwenda kuchukuwa maoni ya wanachama wao Zanzibar yote? Hivi mnadhani siasa za Zanzibar zinahitaji direct method tu ? huko ni kutozijua siasa za Zanzibar.
Lau mngejua kwamba Dr Mwinyi anapata tabu ya Wahafidhina wa CCM leo na vile wahafidhina wanavyolaani ACT kukubali kuingia GNU basi baadhi ya wafuasi wenzetu wa Chadema wasingethubutu kupaza maneno ya kuudhi hadharani. Ni kukosa kujua kinachoendela Zanzibar.
Unaopaswa kuwa Mwelekeo Sahihi
Chukueni mwelekeo wa baadhi ya viongozi weledi ndani ya CHADEMA ambao hadi sasa wameamua kunyamaza kimya. Wekeni hakiba ya maneno kuhusu ACT na waachiieni ili mprove wrong ili mje muwasute baadae.
Tambuweni strategies za siasa na mikakati inatofautiana na wakati, mahitaji na maeneo. Eneo la Zanzibar ni very Perculiar, linahitaji lipewe nafasi yake na sio kuanza kuparamia Viongozi wa chama kinachokubalika huko bila kuzingatia hayo.
Tambueni kuwa Siasa za Zanzibar zinajitosheleza kwa sababu ya uwepo wa Muungano, ukishalijua hilo utajuwa Mbinu za mapambano ya Zanzibar sio lazima ziwe za Tanzania nzima.
Hakuna haja ya kutoa kebehi na matusi naamini iko siku kupitia haya maamuzi ya ACT wanamageuzi wanaweza kuja kuwapongeza hawa hawa ACT.
Chukueni dhana ya Maridhiano japo feki ikibidi iwasaidie kusogeza mbele dhana ya mageuzi na mapambano na jitahidini kusoma njiambali mbali za mapambano duniani.
MWISHO
Nachukuwa nafasi hii kuawapongeza ACT kwa kujali hisia za wengi za wanachama wao hasa wa Zanzibar na kuwatilia maanani kama supporters wao kindaki ndaki kwa sasa lakini na kwa pekee kuibeba ajenda ya Zanzibar kwa vitendo kwa kutambua siasa za Zanzibar zina kona nyingi. Natambua mchango wa manahodha Hodari waliopo ACT. Kudos.
Nashauri vyama vyengine viwape muda ACT na mambo ya ndani ya Upinzani yasianikwe hadharani kwa maslahi mapana ya Upinzani. Bora kuweka hakiba ya maneno. Kubwa zaidi watu watambuwe Zanzibar inahitaji kutazamwa kama Ajenda Maalumu kwenye siasa za Upinzani za Tanzania. Hawa walishatangulia katika mapambano ya siasa. Tukubali hilo na tuwe nao ili dhana ya mabadilo isonge mbele.
Nadhani nimeeleweka na wahuisika tu.
Kishada.