Ujenzi wa Morogoro Road kuanzia Ubungo kwenda Kimara

Strabag ambae ndio anaejenga hiyo barabara sio aliedesign hiyo barabara, yeye anapewa michoro ambayo inaonyesha nini anatakiwa afanye kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Alidesign hiyo barabara ni SMEC International, hawa ni kutoka Australia, na ndio wanaoisimamia hiyo barabara. Swala la mitaro ya ubungo design ya mwanzo haikuwa sahihi, kwanza ilikua ni hatar kwa usalama wa watumia barabara watembea kwa miguu na hata waendesha vyombo vya moto,maana ilikua ni mikubwa sana na iko wazi. Pili hakuku na haja ya kujenga mtaro mkubwa vile kufuata barabara toka mbali wakati karibu tu kuna ule mto ambao unaweza punguza maji. Tatu, hakukua na haja ya mtaro mkubwa vile maana hakuna catchment area ya ukubwa ule, maji yanagawanywa vizur na mtaro mdogo tu wa sasa unatosha!

Chifu, hakika wewe ndiyo mhandisi.
Ile mitaro ya awali ni kweli ilikuwa ni hatari kwa usalama wa waendesha magari na watembea kwa miguu.

Halafu pia inapokuwa wazi ni rahisi kwa waswahili kuigeuza mitaro kama madampo ya takataka, hivyo inaponyesha mvua, taka hizo ndizo uziba mitaro hiyo.

Kwa upande mwingine, ujenzi wa sasa (wa kuifunika mitaro) ndiyo utaratibu wa kimataifa. Hivi Ulaya unaweza kukuta mitaro kama hiyo ya Morogoro road? Ha wapi!! Mitaro yote kama sehemu ya sewage systems za kubeba flash and storm waters, uwa imefunikwa.

Hivyo hawa STRABAG wako sawa kwa kile wanachofanya.
 
Chifu, hakika wewe ndiyo mhandisi.
Ile mitaro ya awali ni kweli ilikuwa ni hatari kwa usalama wa waendesha magari na watembea kwa miguu.

Halafu pia inapokuwa wazi ni rahisi kwa waswahili kuigeuza mitaro kama madampo ya takataka, hivyo inaponyesha mvua, taka hizo ndizo uziba mitaro hiyo.

Kwa upande mwingine, ujenzi wa sasa (wa kuifunika mitaro) ndiyo utaratibu wa kimataifa. Hivi Ulaya unaweza kukuta mitaro kama hiyo ya Morogoro road? Ha wapi!! Mitaro yote kama sehemu ya sewage systems za kubeba flash and storm waters, uwa imefunikwa.

Hivyo hawa STRABAG wako sawa kwa kile wanachofanya.

Wabongo kila kitu tunafikiria kinyume na watu wengine Duniani sijui tatizo liko wapi, na cha ajabu hao wanaojiita wahandishi ndio wako tofauti na Dunia nzima, Mtu anajiita Muhandisi halafu kutwa nzima yuko hapa kulalamikia ujenzi wa strabag wakati ni kitu rahisi tu anaweza kupita kwa hao jamaa muda wowote wana makontena yao kama ofisi akaongea nao wakampa jibu kwa nini wanafanya hivyo, badala ya kukimbilia JF na kuanza kulalama!
 
nimepita hapo wikiendi iliyopita na kuzibwa kwa ile mitalo ni kitu kinachosikitisha kweli, nimehisi yafuatayo;- yule mkandarasi

anajenga ile barabara katika mazingira magumu sana , hana sehemu ya kujenga "diversion roads" ili kurahisisha ujenzi wa

huo mrad, pili, serikali haijafidia watu wenye nyumba zao zilizopo kando kando ya barabara ili waweze kupisha ujenzi wa

barabara mpya hata serikali yenyew imeshnwa kuondoa majengo yake yakiwemo ya tanesco ubungo na wizara ya maji!

kilichofanyika nikuziba ile mitaro kwa juu ili magari yaweze kupita kwa juu na hiyo sehem itumike km diversion road .....
 
Kusahihisha kidogo ili kuweka records vizuri, ni kwamba section hii ya Ubungo-Kimara-Mlandizi ilijengwa na kampuni inaitwa SKAMPHIL COLAS ya Denmark na nakumbuka supervisor alikuwa COWI consult ya Denmark, hii ilikuwa moja ya barabara viwango. Unajuwa hawa jamaa wa Denmark hawajihusishi na rushwa hata angalia section ya barabara ya Iringa ilivyo kazi nzuri.
 
Ndugu wadau leo nimepita kuanzia ubungo mataa kwenda kimara nikakuta ile mifereji mikubwa ya maji imefunikwa na mkandarasi anayejenga hii barabara kwa kuweka mitaro ya chini kwa chini na ni midogo kulinganishwa na ya zamani na ukiingalia kwa kina itakapoziba uwenda ikasababisha mafuriko makubwa.

Swali: Je, TANROADS wanaliona hilo? Je hawa maengineer wa manispaa na TANROADS wamewashauri kweli hawa jamaa?

Kama mnavyoelewa hiyo mitaro inashusha maji mengi sana wakati wa mvua na mnavyoelewa maji ya mvua huchanganyika na udongo & matakataka na ni rahisi kuziba kwa mitaro hii na kusababisha adha kubwa kwa jamii.

Naomba kuwasilisha.
Wenu raia mwema
View attachment 85249

Hawa wajenzi hawako makini kabisa, na TANROADS wana waachia tu.
Nani asiyejua kwamba wakisha kabidhi(na pengine hata kabla) hizi chuma za barabarani zitakuwa zimeshauzwa kama chuma chakavu!!
Hapa ni Morogoro Road katikati ya jiji.
 
Back
Top Bottom