Uingereza imepigwa mkwara na kutikiswa, Tanzania itaweza?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Wakati nchi za dunia ya kwanza/zilizoendelea zikipigana vikumbo kuhusu masuala ya kutawala kiuchumi, nchi za dunia ya tatu/zinazoendelea zinasubiri matokeo hayo ili kujua ukubwa wa athari kiuchumi katika nchi hizo.

Kinachoendelea katika nchi za Amerika ya Kaskazini kuhusu makubaliano ya NAFTA (The North American Free Trade Agreement) kinagusa kwa karibu uchumi wa nchi za Amerika ya Kusini ambao umejumuisha nchi nyingi za dunia ya tatu/zinazoendelea.

Vile vile kinachoendelea katika nchi za Ulaya kuhusu BREXIT (British exit) kinagusa kwa karibu uchumi wa nchi za Afrika ambao umejumuisha nchi nyingi za dunia ya tatu/zinazoendelea.

Kuna methali inayosema, ''wapiganapo tembo nyasi huumia. Hii ina maana kuwa zipiganapo nchi zinazoongoza kiuchumi, nchi masikini kiuchumi huumia.

Mkwara wa Marekani kwa Mexico ambayo nchi nyingi za Amerika ya Kusini zilikuwa zinaitegemea katika mapambano na Marekani kuhusu NAFTA kulifanya nchi hiyo kukubali masharti ya Marekani ambayo yanaziumiza kiuchumi nchi za Amerika kusini. Kwa maana nyingine, nchi za Amerika ya Kusini zilidhani Mexico ina nguvu mbele ya Marekani wakati kiuhalisia hakuwa nazo.

Yanayoendelea kwenye suala la BREXIT huko Ulaya ambapo Uingereza inapambana katika meza ya makubaliano ya kiuchumi, kisiasa na kijamii na Nchi zingine za Umoja wa Ulaya kinaonyesha kuwa ile nguvu ambayo nchi nyingi za Afrika zilidhani Uingereza inazo kumbe haina.

Tanzania tumekataa kuingia Mkataba wa EPA (Economic Partnership Agreements) na Nchi za Umoja wa Ulaya kwa kuitegemea Uingereza tukidhani ina nguvu za kiuchumi na kiushawishi lakini kinachoendelea kinaonyesha Uingereza haina nguvu ya kiushawishi, kiuchumi na kijamii mbele ya Nchi zingine za Umoja wa Ulaya.

Nchi za Umoja wa Ulaya kwa sasa zinaipiga mkwara Uingereza kama ilivyofanya Marekani kwa Mexico ili kuilazimisha Uingereza kuingia makubaliano ambayo kwa kiwango kikubwa yananufaisha nchi zitakazobaki kwenye Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU). Waingereza kwa sasa hasa wananchi wa kawaida wanajuta kwa nini waliamua kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya baada ya kugundua nchi yao haina uwezo wa ushawishi na nguvu nje ya Umoja wa Ulaya. wanawalaumu wanasiasa wao kwa kuwadanganya kuhusu nguvu na uwezo wa Uingereza kwenye Umoja wa Ulaya. Kuna kampeni inaendelea ili kumshinikiza Waziri Mkuu ajiuzulu.

Baada ya kumalizana na Uingereza, nchi za Umoja wa Ulaya zitaigeukia Tanzania kwenye suala la EPA kwa sababu Tanzania ndio kizingiti kikuu kwenye haya makubaliano kwa nchi za Afrika Mashariki.

Yanayoendelea kwa sasa kati ya Tanzania na Jumuiya ya Ulaya ni mvua za rasharasha tu, bado mvua za masika kuanza kunyesha.
Kama Uingereza imeweza kupigwa mkwara na kuanza kulia kulia, Tanzania ambayo iliitegemea Uingereza kuwa kama ngao yake itaweza vipi kupambana na Umoja wa Ulaya?

Je, tunakoelekea kuhusu suala la EPA, viongozi wetu wakuu pamoja na bunge watageuka jiwe kama ule mfano wa ruthu kwenye Maandiko ya Biblia ili wakiepuke kikombe cha ghadhabu za Umoja wa Ulaya?

Kwa wasiojua kuhusu EPA gonga hii LINK>>>Tanzania Yachomoa Kusaini Mkataba wa EPA - JamiiForums

Nakumbuka Mwl Nyerere alipokataa kugeuka jiwe baada ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na pia Benki ya Dunia (WB) kumtaka kushusha thamani ya Shilingi pamoja na kufanya marekebisho kwenye mashirika mengi ya umma, ambayo yalionekana yakijiendesha vibaya tulijikuta kama taifa kwenye hali mbaya sana kiuchumi kiasi kwamba alilazimika ‘’kung’atuka’’ ili kutunza heshima yake!
 
acheni kuleta visingizio vya kizushi, dunia inatutenga kwa sababu ya ubabe wa magufuli na kutokuzingatia utawala bora. mwambieni azingatie katiba na aheshimu haki za raia wake harafu aone kama hao wazungu watambugudhi.
 
Tegemea lolote this time we are "economically novice and inexperienced" kuhusu uchumi wa Dunia.......kwangu raisi ambaye angetufikisha katika viwango wa uchumi wa dunia baada ya Nyerere's "economic experiment" angekua Benjamin Mkapa alikua na exposure na uelewa mkubwa wa uchumi wa dunia ila wa Tanzania hawakumpa ushirikiano.
 
Tumeshaonekana hatuna msimamo na maamuzi yetu mengi ni ya kukurupuka!
Uzi wako nauona zaidi kama wakutuandaa kisaikolojia pale tutakapokubali kuingia EPA!
Fedha za WB zitatoka pale tu ambapo masharti na vigezo wavitakavyo vitakapotazamwa!
Unaposema tulionekana hatuna msimamo una kuwa na maana gani? Msimamo kwa mujibu wa nani na msimamo wa nini?

Kuhusu EPA, mimi sio mwandaaji wa masuala ya EPA bali ninajaribu kuuliza maswali yatokanayo na hali inavyokwenda.

Kumbuka siasa zinakwenda na wakati na hakuna msimamo wa milele kwa binadamu hasa kwenye masuala ya kisiasa.
 
Uingereza kuamua kujitoa EU, kunasababisha euro kudrop in value as compared to USD, Ila kwa kushuka thamani huku kunaashiria pengine Uingereza INA nguvu kubwa, maana inachangia kiasi kikubwa pia
Suala la kushuka kwa thamani ya Euro ni suala la muda tu kwa sababu mpaka sasa haijajulikana makubaliano rasmi pamoja na kwamba draft imeishafahamika.
 
acheni kuleta visingizio vya kizushi, dunia inatutenga kwa sababu ya ubabe wa magufuli na kutokuzingatia utawala bora. mwambieni azingatie katiba na aheshimu haki za raia wake harafu aone kama hao wazungu watambugudhi.
Ni wapi Tanzania imetengwa? Nchi gani kwa sasa imeitenga Tanzania?

Nielimishe!
 
Unaposema tulionekana hatuna msimamo una kuwa na maana gani? Msimamo kwa mujibu wa nani na msimamo wa nini?

Kuhusu EPA, mimi sio mwandaaji wa masuala ya EPA bali ninajaribu kuuliza maswali yatokanayo na hali inavyokwenda.

Kumbuka siasa zinakwenda na wakati na hakuna msimamo wa milele kwa binadamu hasa kwenye masuala ya kisiasa.
Tutegemee flow inayopungua ya Grants, Aids, for govt and non govt institutions from the EU member countries, pengine loans zitaongezeka, maana kwao ni assets
 
Sikubaliani na ushoga ila kwa karnee hii ya sodoma part two ambapo wazungu washaathirika na huo mchezo, tunatakiwa tuapambane na ushoga kwa akili sana bila kutumia mabavu ili tusishtukiwe, tunatakiwa tudhibiti ushoga kwa kutoa elimu kwa vijana wetu na kila mzazi amchunge mwanae kwani ushoga unaanzaga mapema sana kwa watoto

North korea na jeuri yake yote juzi kaomba poo sembuse tanzania, kila kitu kuomba omba tu, Arv madawa ya tb, misaada ya ujenzi kila kitu unamtegemea mzungu alafu unakuja kichwa kichwa na matamko ya ajabu ajabu
 
Unaposema tulionekana hatuna msimamo una kuwa na maana gani? Msimamo kwa mujibu wa nani na msimamo wa nini?

Kuhusu EPA, mimi sio mwandaaji wa masuala ya EPA bali ninajaribu kuuliza maswali yatokanayo na hali inavyokwenda.

Kumbuka siasa zinakwenda na wakati na hakuna msimamo wa milele kwa binadamu hasa kwenye masuala ya kisiasa.
Nikuulize swali moja kabla hatujaendelea kujadili,unaunga mkono TZ kujiunga na EPA?
 
Tegemea lolote this time we are "economically novice and inexperienced" kuhusu uchumi wa Dunia.......kwangu raisi ambaye angetufikisha katika viwango wa uchumi wa dunia baada ya Nyerere's "economic experiment" angekua Benjamin Mkapa alikua na exposure na uelewa mkubwa wa uchumi wa dunia ila wa Tanzania hawakumpa ushirikiano.
Ninakubaliana kwa kiwango kikubwa na hoja yako kuhusu Benjamin Mkapa kuwa alikua na exposure na uelewa mkubwa wa uchumi wa dunia.

Hata hivyo mazingira ya utawala wa Rais Mkapa huwezi kulinganisha na sasa kutokana na mabadiliko ya siasa na uchumi wa dunia.
 
ITs all about new world order.
Tanzania ya awamu hii inauwezo mkubwa sana ya kuiinua kiuchumi nchi yetu kuliko awamu zote zilizopita. kinachotakiwa ni Mh.Raisi kuendelea kuchutama ndani ya IKULU mpaka kieleweke. hii Nchi imebarikiwa sana na rasilimali na ndio sababu kila kukicha hawaishi kujileta kutaka kutukopesha pesa na mengineyo.
Nchi za west zina hofu kubwa sana na China
 
Ninakubaliana kwa kiwango kikubwa na hoja yako kuhusu Benjamin Mkapa kuwa alikua na exposure na uelewa mkubwa wa uchumi wa dunia.

Hata hivyo mazingira ya utawala wa Rais Mkapa huwezi kulinganisha na sasa kutokana na mabadiliko ya siasa na uchumi wa dunia.
Mkuu fafanua kidogo hayo mabadiliko ya uchumi wa Dunia kwa sasa, nakumbuka pia kulikuepo na changamoto za agoa, nk.
 
Tutegemee flow inayopungua ya Grants, Aids, for govt and non govt institutions from the EU member countries, pengine loans zitaongezeka, maana kwao ni assets
Ni kweli Grants and Aids zimeishapungua sana kwa sasa kutoka Umoja wa Ulaya, Data kuhusu hili zinapatikana Bank of Tanzania.

Nadhani Grants and Aids zitatolewa kwa wingi kama tutakubali kuingia mkataba wa EPA. Kinachofanyika kwa sasa ni delaying tactic kwa sababu tumetoa sababu ambazo zinahusiana na suala la BREXIT.

Kwenye suala la loan ninakubaliana na wewe hasa ikichukuliwa kuwa kuna China ambayo pia iko kwenye soko la kutoa loan kwa nchi za Afrika.
 
Mazingira yapi hayo yanayotengenezwa?

JPM amelegeza uzi gani kwa WB?
Sisi watuache tu tuendelee,

- Kupigana risasi hadharani

- Kudhulumiana

- Kupigana mabomu

- Kutungiana sheria kandamizi ambazo hata mkoloni hakuwahi kufikiria kuzitunga

- Kutukanana na kubaguana hadharani

- Kuishi kwa hofu na vitisho.

Hatutaki mtu atuingilie maana tunaowaumiza ni WATU WETU.
 
Sisi watuache tu tuendelee,

- Kupigana risasi hadharani

- Kudhulumiana

- Kupigana mabomu

- Kutungiana sheria kandamizi ambazo hata mkoloni hakuwahi kufikiria kuzitunga

- Kutukanana na kubaguana hadharani

- Kuishi kwa hofu na vitisho.

Hatutaki mtu atuingilie maana tunaowaumiza ni WATU WETU.
Mkuu, u sound tired of all bulshit stories of tz, so is everyone
 
Sikubaliani na ushoga ila kwa karnee hii ya sodoma part two ambapo wazungu washaathirika na huo mchezo, tunatakiwa tuapambane na ushoga kwa akili sana bila kutumia mabavu ili tusishtukiwe, tunatakiwa tudhibiti ushoga kwa kutoa elimu kwa vijana wetu na kila mzazi amchunge mwanae kwani ushoga unaanzaga mapema sana kwa watoto

North korea na jeuri yake yote juzi kaomba poo sembuse tanzania, kila kitu kuomba omba tu, Arv madawa ya tb, misaada ya ujenzi kila kitu unamtegemea mzungu alafu unakuja kichwa kichwa na matamko ya ajabu ajabu
Mkuu;
Mimi nadhani tatizo sio ushoga bali kuna sababu ambayo imebebwa ndani ya ushoga.

Ninakubaliana na wewe kuhusu viongozi wetu kuepuka kuingia kwenye mitego ambayo wanaweza kuepuka. Hakukuwa na sababu ya kutoa matamko ya kuanza kusaka mashoga kama wanavyofanya wawindaji wa wanyama. Kuna njia nyingi mbadala ya kupambana na ushoga kama ulivyoainisha.

Serikali lazima itambue kuwa imetengeneza maadui wa kiuchumi ambao wametega mtego utakaobeba sababu ya kutimiza malengo yao.
 
Back
Top Bottom