UHAKIKI WA VIONGOZI....JAJI (MSTAAFU) SALOME kAGANDA AMENIKERA KWELI!!!!

Malyenge

JF-Expert Member
Jan 16, 2012
6,658
3,646
Wakuu nilikuwa naagalia taarifa ya habari ya TBC1. Ikaja taarifa inayohusu uhakiki wa mali ya watumishi wa umma. Majina 10 yakatajwa wanaofuata kuhakikiwa, yakijumuishwa na majina 71 yaliyohakikiwa mwezi Feabruari 2012. Ikaja zamu ya kumwonesha jaji Kaganda akizungumzia zoezi hilo la uhakiki. Akasema watumishi hao wa umma wasidhani ya kuwa wanahisiwa kuwa wamejilimbikizia mali bali eti yeye anatekeleza sheria....... Hapo ndipo nimekereka kweli. Kwani hiyo sheria ya utumishi wa umma anayoitekeleza inaruhusu kujilimbikizia mali?? Kwani sheria inasemaje ikiwa mtumishi atakutwa amejilimbikizia mali? Huu ni udhaifu wa kitaaluma!!! Yeye hakupaswa kukikosha kwa wahusika anaowahakiki bali labda kama alitaka kuzungumza basi angetoa ratiba ya namna zoezi hilo litakavyofanyika na si kujipendekeza kwa stail ya kujidhalilisha.
Lo, Tanzania hatuna watu wanaojiamini kabisa. Poor professionalism!!!
 
Kaka jiulize post hiyo aliomba au kateuliwa ?
Kama kateuliwa lazima aangalie asiharibu maelekezo ya aliyemteua

we need people who are commited hata kama wameteuliwa waweze kusimama kwa msimamo yao
watu ni waoga kutenda haki na kuonyesha misimamo yao,
Fear of God(Hofu ya Mungu) ndio inakupa ujasiri wa kuwa na msimamo nothing else
 
Kaka jiulize post hiyo aliomba au kateuliwa ?
Kama kateuliwa lazima aangalie asiharibu maelekezo ya aliyemteua

we need people who are commited hata kama wameteuliwa waweze kusimama kwa msimamo yao
watu ni waoga kutenda haki na kuonyesha misimamo yao,
Fear of God(Hofu ya Mungu) ndio inakupa ujasiri wa kuwa na msimamo nothing else

hapa umenena kwa kuongezea hapo ni kwamba hiki kitengo hakina tija kabisa je baba riz akijirimbikizia mali itakuwaje nani atamusimamia weakness ya kwanza hiyo
harafu huwa nakiona ni kitengo cha kuongeza ajira tanzania lakini je wazee tanzania ndo unemployment? Na hapo nashindwa kuelewa
hiki kitengo hakina tija kwa taifa hili kwa sababu nyingi tu moja ikiwa hii ya lowasa na marafiki zake kumwaga pesa mitaani bila kuulizwa wamezitoa wapi
 
Sasa kakukera nini? kusema kweli ndio ukereke? yeye anasema hivyo ili waelewe kuwa kuhakiki ni random na sio kuwa suspected, ni sheria inataka wahakikiwe na hakuna uwezo wa kuhakiki watumishi wote wa Serikali kwa mara moja ndio maana wanawachukuwa randomly, unless kuwe kuna shutuma zimepelekwa kuwa fulani ana mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali hapo ndio anahakikiwa uhalali wa hizo mali as a suspect nje ya hapo anahakikiwa kama sheria inavyotaka lakini haimaanishi kuwa anaehakikiwa ni suspect.

Mfano wake ni kama traffic police anavyokusimamisha njiani, yeye hajui kama atakukuta unakosa lakini ana sheria inayomruhusu kuhakiki kama huna makosa.
 
Kama kiongozi ataonekana hajajilimbikizia mali hupigiwa simu na kupongezwa akiitwa Mzee wewe ni kama Sokoine kabisa.
 
Sasa kakukera nini? kusema kweli ndio ukereke? yeye anasema hivyo ili waelewe kuwa kuhakiki ni random na sio kuwa suspected, ni sheria inataka wahakikiwe na hakuna uwezo wa kuhakiki watumishi wote wa Serikali kwa mara moja ndio maana wanawachukuwa randomly, unless kuwe kuna shutuma zimepelekwa kuwa fulani ana mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali hapo ndio anahakikiwa uhalali wa hizo mali as a suspect nje ya hapo anahakikiwa kama sheria inavyotaka lakini haimaanishi kuwa anaehakikiwa ni suspect.

Mfano wake ni kama traffic police anavyokusimamisha njiani, yeye hajui kama atakukuta unakosa lakini ana sheria inayomruhusu kuhakiki kama huna makosa.


Du! Huo mfano wa traffic nimeupenda. Lakini mbona sijawahi kuona traffic amesimamisha gari kisha akaanza kumweleza dereva "usidhani najua kama una kosa la bali natimiza sheria ya usalama barabarani?"
 
Back
Top Bottom