Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,646
Wakuu nilikuwa naagalia taarifa ya habari ya TBC1. Ikaja taarifa inayohusu uhakiki wa mali ya watumishi wa umma. Majina 10 yakatajwa wanaofuata kuhakikiwa, yakijumuishwa na majina 71 yaliyohakikiwa mwezi Feabruari 2012. Ikaja zamu ya kumwonesha jaji Kaganda akizungumzia zoezi hilo la uhakiki. Akasema watumishi hao wa umma wasidhani ya kuwa wanahisiwa kuwa wamejilimbikizia mali bali eti yeye anatekeleza sheria....... Hapo ndipo nimekereka kweli. Kwani hiyo sheria ya utumishi wa umma anayoitekeleza inaruhusu kujilimbikizia mali?? Kwani sheria inasemaje ikiwa mtumishi atakutwa amejilimbikizia mali? Huu ni udhaifu wa kitaaluma!!! Yeye hakupaswa kukikosha kwa wahusika anaowahakiki bali labda kama alitaka kuzungumza basi angetoa ratiba ya namna zoezi hilo litakavyofanyika na si kujipendekeza kwa stail ya kujidhalilisha.
Lo, Tanzania hatuna watu wanaojiamini kabisa. Poor professionalism!!!
Lo, Tanzania hatuna watu wanaojiamini kabisa. Poor professionalism!!!