Ufisadi waivuruga ngome ya Dk. Slaa

singidadodoma

JF-Expert Member
Nov 11, 2013
4,394
1,531
KINYUME cha taswira ya miaka mingi kwamba Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia viongozi wake wakuu, hasa Katibu Mkuu, Dk. Wilbroad Slaa, ni chama kinachopinga ufisadi, mambo yameripotiwa kugeuka katika baadhi ya ngome za chama hicho nchini.

Kwa muda mrefu sasa, Dk. Slaa amekuwa akijipambanua kuwa kinara wa kupinga ufisadi na akiwa Mbunge wa Karatu hadi kufikia mwaka 2010, amekwishafanya kazi ya kufichua uozo mkubwa uliopata kufanywa na watendaji wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM), lakini sasa Halmashauri ya Karatu inayoongozwa na chama hicho imekubwa na kashfa za ufisadi.

Hali hiyo ilibainishwa bungeni mjini Dodoma jana na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mary Chatanda, ambaye aliweka bayana kwamba si tu Halmashauri ya Karatu ambayo ni ngome ya kisiasa ya Dk. Slaa, imeoza kwa ufisadi bali hali pia hali ni hiyo hiyo kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, akisema mbunge huyo ‘ametafuna' kifisadi fedha za maendeleo ya mfuko wa jimbo.

Akichangia mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) jana bungeni mjini Dodoma, Chatanda alidai hakuna mbunge fisadi kama Lissu katika kutafuna fedha za mfuko wa jimbo.

"Nawashangaa hawa wapinzani wanapiga kelele hapa kuhusu ufisadi wakati ndio wanaoongoza kwa ufisadi. Hakuna mbunge ambaye anatafuna fedha za mfuko wa jimbo kama Lissu, tunaomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), akamfanyie ukaguzi maalumu,"alisema Chatanda

Alisema wapinzani wamekuwa wakipiga kelele kukemea mafisadi na kudai kwamba CCM ndio wanaofanya ufisadi wakati Halmashauri ya Karatu inayoongoza na Chadema ndiyo kinara katika kuendeshwa kwa ufisadi uliopindukia.

"Halmashauri ya Karatu ambayo ni ya Chadema ndiyo fisadi kuliko, kuna mbunge wa upinzani, Cecilia Pareso, nilimuuliza kuhusu yule fisadi ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ya Karatu, kwamba amechukuliwa hatua gani akanijibu…yule hatagombea tena au hatapita,"

"Kwa hiyo wao wanapiga kelele za nini hapa ndani (bungeni) wakati maeneo machache tu wanayoongoza wananuka ufisadi? Wakipewa nchi itakuwaje?," alihoji Chatanda ambaye amewahi kuwa Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha na kwa sasa ni Katibu wa CCM, mkoani Singida.

Akizungumzia kauli iliyotolewa na baadhi ya wabunge wa Chadema kwamba Mbunge wa Viti Maalumu wa Chama hicho, Rose Kamili, alipigwa na kusababishiwa ulemavu na baadhi ya wanaCCM alisema huo ni uongo uliokithiri, akisistiza kwamba mbunge huyo alipata ajali kabla ya kwenda kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga.

"Wapinzani mkiwa hamna hoja ni vyema mkanyamaza kuliko kuongea uongo, Kamili ni rafiki yangu siku nyingi lile tatizo la mkono alilonalo hakusababishiwa na CCM bali alipata ajali na hata kipindi akiwa anataka kwenda kwenye kampeni nilimuuliza kuhusu mkono wake uliokuwa umepachikwa chuma, akajibu kwamba hawezi kuacha kwenda kwenye kampeni chama chake kitamuelewa vibaya,"


"Yaliyotokea Kalenga kipindi kile siyo yaliyomfanya Kamili kuumia mkono bali alikuwa tayari ana chuma kwenye bega hivyo alitoneshwa kidonda, acheni kuudanganya umma kwamba CCM imeumiza mtu. Hakuna kitu kama hicho," alisema Chatanda.

Hata hivyo kauli hiyo ilimfanya Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, kuomba kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Bunge hilo, Mussa Azzan Zungu, ambapo alisema wakati tukio hilo likitokea katika uchaguzi huo mdogo wa Kalenga alikuwapo na alishuhudia mbunge huyo akipigwa na kuumizwa na CCM.

Chanzo
: Raia Tanzania
 
Hakuna kitu hapa CHADEMA ndo chama tunachokiamini mno.
Tatizo Dr. Slaa na Lissu wamewashika pabaya maccm
Ufisadi kila kona maccm rudisheni hela zetu mlizoficha Uswiss we need our money
October patachimbika
 
Hapo bado hujaongelea watu kudai wamekopesha chama bila ushahidi wowote na baada ya hapo kudai marejesho yenye riba ya 100%. Lack of transparency and democracy inanipa mashaka sana kuwa Chadema itakuwa tofauti na CCM
 
"Yaliyotokea Kalenga kipindi kile siyo yaliyomfanya Kamili kuumia mkono bali alikuwa tayari ana chuma kwenye bega hivyo alitoneshwa kidonda, acheni kuudanganya umma kwamba CCM imeumiza mtu. Hakuna kitu kama hicho," alisema Chatanda.

kwa tafsiri ya Ma CCM kutonesha sio kuumiza...na kutonesha ni sawa kabisa..hakuna kosa lolote
 
Aliweka nyaraka kuthibitisha tuhuma zake kama wanavyofanya wanaoituhumu serikali sikivu ya CCM? Au maneno yake matupu yatosha?
 
hakuna kitu hapa chadema ndo chama tunachokiamini mno.
Tatizo dr. Slaa na lissu wamewashika pabaya maccm
ufisadi kila kona maccm rudisheni hela zetu mlizoficha uswiss we need our money
october patachimbika

saccos kufilisika muda si mrefu
 
Riwaya hizi hazina msaada kwa ccm.

Ccm imeshafanya madharau ya kutisha kwa wananchi wake kiasi kwamba imefika kipindi watu wameshatia nia kuifuta.

Story za kuokoteza namna hii haziwezi kuufuta ukweli kuwa ccm imeihujumu nchi hii kwa kiwango cha kutisha.

Mkiweza kueleza ATC ilipo na ina hali gani ukilinganisha na Rwandair achilia mbali KQ.

Mkiweza kuniambia tuna hifadhi ya dhahabu kiasi gani benki kuu kwa kuzingatia dhahabu inapatikana kila kona ya nchi yetu.

Mkiweza kuniambia kwanini TTCL shirika letu la umma linalojihusisha na huduma za simu na mtandao (mawasiliano) ambalo ni kongwe kuliko kampuni yoyote ya mawasiliano nchini

LIMEBEMENDWA kwa usimamizi mahsusi ulioratibiwa kwa ustadi mkubwa na serikali ya ccm!!!!! Iweje halifanyi kazi kukidhi matakwa ya kibiashara huku linapata ruzuku kila mwaka???

Mkiweza niambieni Uda yetu iko wapi???!!!!

Mkiweza niambieni mmekifanya nini kiwanda chetu cha magurudumu cha general tire mpaka hakitengenezi tena magurudumu hali ya kuwa soko la magurudumu linaendelea kukua usiku na mchana???

Halafu mnakuja na vistory vyenu vya kipumbavu hapa mnadhani watu wote humu ni wapumbavu!!!! Nnkdkrkrkrrrrr

MLICHIKOMAZA SEEEH!!!!
 
Kumbe umem-quote huyo chatanda,
Nisingetegemea aseme tofauti!
 
Usilo lijua ni kama usiku wa giza, kwa faida ya wale wasio jua, fedha za jimbo ni nini na zinatolewa kwa malengo gani. Hizi fedha zinatolewa ili kutatua changamoto ndogo ndogo ambazo mbunge husika anakutana nazo ili kuweza kufanikisha kuzitatua. Fedha hizi zinatolewa kwa kiwango tofauti tofauti kulingana na jimbo lenyewe lilivyo, bajeti ya mwaka ni chini ya million 100. Fedha zinapelekwa moja kwa moja kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya. Matumizi yake yanapangwa baada ya kamati maalum kukaa , ambayo katibu wake ni afisa mipango wa wilaya na mwenyekiti wake ni mbunge. Baada ya kukaa kamati hiyo upeleka mapendekezo kwenye baraza la madiwani ili kuweza kuridhiwa.

Napata shaka juu ya uelewa wa huyo Mary chatanda, amekuwaje mwakilishi wa wananchi kama utaratibu mwepesi namna hii haujui ? Ni jambo la aibu kama watanzania mpaka sasa tunashabikia post za ovyo kama hizi ,huku fika tukijua jinsi utaratibu wa fedha kupokelewa na kutolewa halmashauri kuwa mhusika mkuu wa kupitisha ni mweka hazina wa halmashauri pamoja na mkurugenzi. Tundu Lissu anaingiaje hapo ?
 
Mary chatanda ni mbunge wa singida .arusha au tanga? Anaongea uharo mtupu full mbululah
 
Stupid buger kama karatu kuna wizi ccm si ina serikali kwanin isitume police iwakamate watuhumiwa wakashtakiwe? Toka lini serikali inalalamika whats the point of controling state aparatus?
 
kweli hawa jamaa hawafai, wanayozungumza na kutenda tofauti kabisa, wakati huyu mama akiongea jana wabunge wa chadema viti vilikuwa havikaliki kila dakika wanaomba muungozo ili kumpotezea muda huyu mama, pongezi kwa mwenyekiti wa jana mhe. Zungu alikuwa stable, sasa naona umuhimu wa mzalendo Zitto katika siasa za upinzani bungeni.
 
kweli hawa jamaa hawafai, wanayozungumza na kutenda tofauti kabisa, wakati huyu mama akiongea jana wabunge wa chadema viti vilikuwa havikaliki kila dakika wanaomba muungozo ili kumpotezea muda huyu mama, pongezi kwa mwenyekiti wa jana mhe. Zungu alikuwa stable kabisa naanza kumkumbuka mzalendo Zitto sasa,

We kichwa kopo kwanin serikali isiwakamate wezi wa cdm? Jinai si state inashughulikia? Wakamatwe washtakiwe otherwise tutajua uzushi
 
Back
Top Bottom