Ufafanuzi: Zitto Hajakimbia Mjadala wa Tuongee Asubuhi leo (LIVE ON Star TV)

Yahya Mohamed

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
270
317
Salaam wakuu,

Heri ya Mwaka Mpya

Kama ilivyokuwa maazimio katika mjadala wa Jumapili ya wiki iliyopita tulijiwekea malengo ya kuwa na Mjadala wa muendelezo ili kuwawezesha wazungumzaji kuzijibu issues specific ambazo zilijotokeza katika mjadala huo.

Na kama mtakumbuka mpaka mara ya mwisho tunakaribia kumaliza mjadala siku ya Jumapili, tulilazimika kumruhusu Mh. Zitto katikati ya mjadala aweze kuwahi ndege kwa safari yake ya kwenda Ruaha.

Pamoja na kutingwa na safari hiyo hakuweza kuacha kuja hasa akijua inawezekana kabisa msigano wa vyama ukaibuka katika mjadala huo. Na aliendelea kuwepo mpaka dakika za karibu na mwisho ambapo isingeweza kuvumilka tena.

Mpaka jana nafanya mawasiliano ya Mwisho kuthibitisha uwepo wa wageni katika kipindi Mh. Zitto alikuwa bado safarini, kwa hiyo hatukuweza kumjumuisha katika Kipindi.

Kwa kuwa tulishaundaa Mjadala hatukuwa na maarifa ya kubadili na lengo halikuwa msigano wa vyama zaidi ya kujibu specific issues kwa kila chama kama ilivyojitokeza katika mjadala uliopita.

Kutokana na Afya yangu kuendelea kutatizwa na kutoyamudu kwa haraka mazingira ya Dar Es Salaam niliomba usaidizi wa kuendesha kipindi hicho kwa matayarishaji mwenza.

Nichukue fursa hii kuweka sawa dhana hii ambayo inalenga kumchonganisha Mh. Zito na chama chake cha CHADEMA, Si haki na sawa kuhisi kama aliukimbia mjadala.

Bado tuna nafasi za mijadala hii mingi tutawaalika tena viongozi hawa kuendelea kujenga hoja za kusaidia kuwa na siasa za kistaarabu na zenye tija kwa mtanzania.

Niombe radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa Mh. Zito kutokana na mkanganyiko huo, na pia wafuatiliaji wa mijadala hii Star TV na nikiri kuwa tungeweza bado kuuahirisha mjadala huu ili kuepusha manung'uniko haya hasa baada ya kuthibitisha Mh. Zitto hatokuwepo, kutofanyika kwa hilo ni makosa na mtuwie radhi; umakini utazidishwa katika usimamizi huo.

ANGALIZO: Maelezo haya si kauli ya Kituo (Star TV) wala utawala wa Kituo hicho bali ni ufafanuzi wa mtayarishaji wa kipindi kama mmoja wa wanaforum


Nawasilisha
 
Ahsante Mkuu kwa Jitihada zako za kuondoa wingu hilo jeusi kwa Mh.Zito Kabwe...
The rest tuachie sisi tuelewe tunavyoona wenyewe..
Heri ya Mwaka Mpya.
 
Unachonikera Bwana Yahya unapendelea sana CCM kwenye uchambuzi wako na kuwaponda sana wapinzani , sijui kwa nini unakuwa na upofu na utakwisha lini . Upendeleo wa wazi unaoneshwa kwa sasa na wewe na Star Tv hauwezi kuleta tija kwa maendeleo ya nchi. Nashauri uweke msimamo wa kiuandishi na uchambuzi wa kweli bila kupendelea
 
Ndugu Yahya,

Last time wakati wa kipindi na hawa wanasiasa 3 (Zitto, Mwigulu na Mtatiro) wadau wengi walitoa maoni na maswali ambayo wangeta kupata ufafanuzi toka kwa hao wanasiasa.

Naomba niseme hivi, nilitegemea majadala wa leo ungejikita kupata ufafanuzi kwa mambo ambayo hayakujadiliwa last time. Kwa masikito, Star Tv mmejibebesha dhamana ya kuwa dawati la 'Jeshi la polisi'. Ni mtindo huu ndio unafanya watu wadharau mainstream media maana mnashindwa kabisa kujua wananchi wanataka nini?

Ni kitu gani kiliwashinda kuongoza kipindi na kupata majibu kwa maswali mliyokuwa mnauliza? Kwanini mnawapotezea muda watazamaji kwa mambo ambayo hayawahusu? Ni lini Star Tv wataendesha mijadala inayolenga kupata majibu kwa mambo ya msingi?
 
Unachonikera Bwana Yahya unapendelea sana ccm kwenye uchambuzi wako na kuwaponda sana wapinzani , sijui kwa nini unakuwa na upofu na utakwisha lini . Upendeleo wa wazi unaoneshwa kwa sasa na wewe na Star Tv hauwezi kuleta tija kwa maendeleo ya nchi. Nashauri uweke msimamo wa kiuandishi na uchambuzi wa kweli bila kupendelea


Huwa najenga Hoja kutetea chama chochote? Sina hakika sana na hili
 
Shukrani kwa ujumbe.

Ila nina swali ndg...kwanini kila siku ZZK tuu hata anapokuwa safari na sio siku nyingine, Mnyika,Lissu, Lema...ni swali tuu lkn.

Heri ya mwaka mpya.
 
Ndugu Yahya,

Last time wakati wa kipindi na hawa wanasiasa 3 (Zitto, Mwigulu na Mtatiro) wadau wengi walitoa maoni na maswali ambayo wangeta kupata ufafanuzi toka kwa hao wanasiasa.

Naomba niseme hivi, nilitegemea majadala wa leo ungejikita kupata ufafanuzi kwa mambo ambayo hayakujadiliwa last time. Kwa masikito, Star Tv mmejibebesha dhamana ya kuwa dawati la 'Jeshi la polisi'. Ni mtindo huu ndio unafanya watu wadharau mainstream media maana mnashindwa kabisa kujua wananchi wanataka nini?

Ni kitu gani kiliwashinda kuongoza kipindi na kupata majibu kwa maswali mliyokuwa mnauliza? Kwanini mnawapotezea muda watazamaji kwa mambo ambayo hayawahusu? Ni lini Star Tv wataendesha mijadala inayolenga kupata majibu kwa mambo ya msingi?

Bahati mbaya sana sikukiona kipindi naomba nisi-comment chochote katika hilo unless swali hili linahusu mjadala uliopita ambao nilishiriki
 
Yahya Mohamed

moderation ya hichi kipindi imekuwa very poor, indeed biasing

inapeleke watazamaji wa starTv kukata tamaa nq kipindi hichi, wakati mwingine inaleta hisia kwamba kipindi kama hichi kilichomshirikisha mwigulu nchemba kuna conspiracy undernearth na maudhui yake ni ku-propel failed politics and propaganda za huyu kada wa ccm kutoa shtuma za kuchafua chama kingine cha siasa ..... mualikwa anashindwa kuthibitiwa na moderator, mwigulu anatoka nje ya mada bado moderator anamuachia airtime awajaze watu ujinga

tahadhari, starTv itapoteza umakinibna kuaminika kwa mtindo huu

jirekebisheni
 
Last edited by a moderator:
Shukrani kwa ujumbe.

Ila nina swali ndg...kwanini kila siku ZZK tuu hata anapokuwa safari na sio siku nyingine, Mnyika,Lissu, Lema...ni swali tuu lkn.

Heri ya mwaka mpya.

Ulikuwa ni mjadala wa Viongozi wa rank moja (Manaibu Katibu Wakuu), Viongozi wengine pia mtawaona kwa kadiri siku zinavyozidi kusonga. Lengo ni kuwakutanisha Viongozi wenu nanyi katika mijadala ya TV
 
Yahya Mohamed

moderation ya hichi kipindi imekuwa very poor, indeed biasing

inapeleke watazamaji wa starTv kukata tamaa nq kipindi hichi, wakati mwingine inaleta hisia kwamba kipindi kama hichi kilichomshirikisha mwigulu nchemba kuna conspiracy undernearth na maudhui yake ni ku-propel failed politics and propaganda za huyu kada wa ccm kutoa shtuma za kuchafua chama kingine cha siasa ..... mualikwa anashindwa kuthibitiwa na moderator, mwigulu anatoka nje ya mada bado moderator anamuachia airtime awajaze watu ujinga

tahadhari, starTv itapoteza umakinibna kuaminika kwa mtindo huu

jirekebisheni

Tulipokamua kushirikiana na wanaforum ni kwa lengo la kupata postive critism rejea thread yangu ya kwanza kabisa hapa JF. Dosari mnazozibaini tunazifanyia kazi.

Kuna kuteleza nasi si wakamilifu wala Malaika na hatufanyi kazi kwa masilahi ya yoyote zaidi ya misingi ya Taaluma.

Tunapojikwaa ni ubinadamu tu
 
Shukrani kwa ujumbe.

Ila nina swali ndg...kwanini kila siku ZZK tuu hata anapokuwa safari na sio siku nyingine, Mnyika,Lissu, Lema...ni swali tuu lkn.

Heri ya mwaka mpya.

N/katibu mkuu CCM/ CUF/ CHADEMA.o therwise labda uulize kwa mantiki kuwa je waliwasiliana na cCHADEMA kuona kama kuna uwezekano wa kupata kiongozi mwingine?
 
Tumekuelewa na pia wewe pale startv ndiyo unaipaisha sana JamiiForums endelea hvohvo mkuu.
 
Sijui kwa nini mnakosa wageni na badala yake mnaalika watu wanao onekana kichwani amnazo kbisa mfano Mwigulu Nchemba!

Na washauri kabla ya kuanza mijadala muwe mnaalika madaktari wa kufanyia uchunguzi wa kichwa watu wanao shiriki kwenye mijadala!
 
Last edited by a moderator:
Yahya irudishe objectivity na consistence mliyokuwa nayo kipindi cha nyuma.Naona kama inapotea kwenye hiko kipindi chenu.Ulipokuwa na yule jamaa aliyeenda BBC mlikuwa mnaperform vizuri.
 
Ulikuwa ni mjadala wa Viongozi wa rank moja (Manaibu Katibu Wakuu), Viongozi wengine pia mtawaona kwa kadiri siku zinavyozidi kusonga. Lengo ni kuwakutanisha Viongozi wenu nanyi katika mijadala ya TV

Nikushukuru kwa dhati kabisa Yahya mohamed kwa kujibu vzr swali langu. Pia nilikua naelewa kuwa hawa ni manaibu Katibu wakuu wa vyama vyao.

Nikiri pengine sikuliweka sawa swali langu, hoja kuu ya swali langu nikuwa mara nyingi mijadala yenu unaweza kuangalia kwa statistics kwenye ofisi yenu ZZK amealikwa au kufanyiwa mahojiano mara ngapi...ukilinganisha na viongozi wengine hasa vijana wa CHADEMA.

Lkn pia nishukuru kama umeshanijibu kuwa wengine tutawaona kadiri siku zinavyosonga...Angalizo sasa iwe hivyo isiwe ni jibu tu lkn kkwenye utekelezaji anapewa coverage kubwa sn mtu mmoja nielewe hapa yaani mawazo na mtazamo wa mtu mmoja unapewa coverage kubwa sn kuliko wengine kwenye chama kimoja ...the same kwa CCM.

Asante.
 
StarTV mnaheshimika sana, ombi langu kwenu ni KUDHIBITI waalikwa kujikita kwenye MADA halisi na MSIRUHUSU mtu atoke hapo. Mie nimeona kabisa huyo Mchemba hafai KABISA kwenye mijadala kwani anaumwa CHADEMAmania, tafuteni mtu mwngine ambaye atatueleza CCM iko vipi.
 
Ulikuwa ni mjadala wa Viongozi wa rank moja (Manaibu Katibu Wakuu), Viongozi wengine pia mtawaona kwa kadiri siku zinavyozidi kusonga. Lengo ni kuwakutanisha Viongozi wenu nanyi katika mijadala ya TV
bado tutataka mchemba au viongozi wa CCM mtakaowakaribisha,watueleze serikali yao iliyo madarakani wanamaana gani kuwaachia watu wenye kuuwa watu na kufanya mipango ya mauaji,ilihali wanaushahidi wa kutosha na video wanazo.vinginevyo tutaamini maneno ya vyama pinzani kwamba,serikali hii ni legelege hivyo haifai kuongoza.maana tutakuwa tunauwawa bila hatua kuchukuliwa bora tuwe hatuna serikali kila mtu ajue namna ya kujilinda.
 
Back
Top Bottom