Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,899
Viongozi wakuu wa Chadema hawapo ila Mbowe peke anaonekana kubanana na Lowasa
Wimbi la kuanzishwa chama cha ACT kulikuwa na mengi yaliuyoongelewa kuhusu udikteta ndani ya Chadema unaofanywa na Mbowe, pia kwamba kuna msuguano kati ya Mbowe na Slaa, ingawa ilikanushwa lakini ufa huo unaonekana kujitokeza sasa.
Kilichoendelea ni CHADEMA kuonekana kumwandaa Slaa kuwa mgombea wa Urais. Pia Slaa kuonekana kukubalika kimataifa hata kualikwa na mataifa makubwa au jumuia za kimataifa duniani kama Marekani, Ujerumani na Umoja wa nchi za Ulaya.
UKAWA ilionekana NCCR wako radhi Dr Slaa awe mgombea, ila upade wa CUF Lipumba hakuridhika na alitaka yeye agombee. Mbowe alipoonekana kumilikiwa na kisha kummiliki Lowassa kuwa mgombea, Lipumba akapoa kwa vile wote yeye na Slaa wamekosa, huko alikokuwa mafichoni akajifichua na kuanza kuonekana katika vikao vya UKAWA.
Mgawanyiko Kamati Kuu CHADEMA kutokana na Lowassa
Katibu Mkuu Slaa, makamu wake bara John Mnyika na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu hawakushiriki mapokezi ya Lowassa wakati walionekana wako na moyo kwa mapokezi ya Lembeli na wengineo. Dalili kwamba Lowassa ni chaguo la Mbowe na kushinikiza kamati kuu waridhie matakwa yake.
Mbowe amkumbatia Lowasa anayewawakilisha Rostam na Chenge
CHADEMA ilijipambanua na kueleweka kwa umma kwamba wako kinyume kabisa na ufisadi na katu hawatakaa sahani moja na mafisadi, lakini leo Freeman Mbowe anakula sahani moja na fisadi Lowasa anayewakilisha mafisadi wenzake akina Rostam Aziz na Chenge.
LOWASA AKWEPA MASWALI YA WAANDISHI KUHUSU KUWAKUMBATIA MAFISADI WENZAKE
Katika tukio la kukabidhiwa kadi za Chadema, Lowasa alipoulizwa na waandishi kuhusu yasemwayo na watu kwamba akiwa Rais atawakaribisha mafisadi wenzake Chenge na Rostam, hakujibu akakwepa na kusema tu anachukia ufukara na anataka watanzania wengi wawe matajiri. Hapo kuna jambo ambalo dhahiri analikwepa kuliweka wazi kuhusu uhusika wake kugombea urais nyuma yake wakiwamo mafisadi Chenge na Rostam. Akishakalia kiti cha magogoni ni mfalme nani wa kumnyoshea kidole?
Lowasa kukaribishwa CHADEMA na UKAWA badala ya uongozi CHADEMA
Lowasa akaribishwa na kukabidhiwa kadi ya Chadema na UKAWA badala ya safu ya uongozi wa Chadema. Jambo la kufikirisha na kuonyesha dhahiri kuna msuguano fulani na kwa vyo vyote jibu litapasuka maana uvundo huu hauwezi kuendelea muda mrefu.
Zengwe la kuteua mgombea urais CHADMA
Imedhihirika Mbowe ana kauli ya mwisho nani achukue fomu ya kugombea urais na bila yeye kuidhinisha haitafanyika na ndivyo ilivyotokea, wakati huo huo yeye Mbowe alishakuwa na mgombea wake fisadi Lowasa.
Wakati watanzania wakiwa na kiu ya kutangaziwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema mazingira tatanishi yameendelea kwa kuchelewesha kwa makusudi hadi Lowasa alipokatwa CCM Mbowe akamkumbatia.
CHADEMA IMEPASUA UFA MKUBWA MUHIMU KUZIBA HARAKA
Siyo siri na wengi wamebaki kunyamaza kuangalia movie inayoendelea huku Mbowe akijipongeza kumpata fisadi Lowasa huku wengi wa wanakamati kuonekana kutomwunga mkono na mgomo baridi ni pale waliposusia tukio la kumsafisha Lowasa Buguruni ofisi za CUF kisha kufuatiwa na tukio la Lowasa kukabidhiwa kadi za Chadema Bahari Beach Hotel. Huko kote aliyekuwa kifua mbele toka Chadema alikuwa Mbowe wakati watendaji wakuu wengine wa chama wakisusia.
Mbowe na Lowassa watafanya nini mkutano mkuu wa CHADEMA ukimkata Lowassa?
Mkutano Mkuu wa Chadema una nafasi ya kumchagua mgombea kiti cha Urais kwa kura na si kwa shinikizo la mwenyekiti. Iwapo Dr Slaa ataamua kuchukua form za Kugombea Urais kadiri ya msukumo wa wanachama wengi wa Chadema na watanzania, kisha mkutano mkuu ikatokea kumkata Lowasa chaguo la Mbowe nini hatima ya Lowasa na Mbowe atajisikiaje ndani ya Chama?
MBOWE KAIDHALILISHA CHADEMA/TANZANIA NA KUKIPASUA VIPANDE VIWILI
Mbowe amekidhalilisha chama chake kwa kumkumbatia Lowasa kinyume cha maadili ya chama chake na bila ridhaa ya chama chake chenye haiba ya kupinga kwa nguvu zote ufisadi nchini. Asipokatwa Lowasa mpasuko huu umeshajidhihirisha kutoka ndani ya Kamati kuu, hakuna hasara ya kumtosa Lowasa kwa vile Chama kilikuwa na mshikamano kabla ya Lowasa. Kimsingi ujio wa Lowasa umesababisha mpasuko mkubwa wa wanachadema na watanzania wapenda mageuzi nchini.
CCM IMEWEZA KUWADHIBITI MAFISADI HAWA CHADEMA IMETEKWA NA MAFISADI
CCM waliweza kulithibiti hili kundi la mafisadi wanaotaka kumpitisha mmoja wao kuwa Rais wa nchi, lakini Mbowe kaingia kichawakichwa na hatimaye umakini usipokuwepo kumkata Lowasa utawala wake utakuwa wa maumivu kuliko tunachoshuhudia sasa hivi utawala wa Kikwete.
Lowasa ni mfalme si mtu wa kukaa kujadili na watu nini kifanyike ila anaonekana ni wa mfumo wa kifalme kutoa amri.
Akiwa rais atawaingiza na kuwapatia nafasi nyeti mafisadi wenzake, nani wa kumnyoshea kidole wakati katiba inamlinda?
Dr.W.Slaa
Today 06:20
#1 JF Senior Expert MemberArray
Join Date : 1st July 2008
Posts : 681
Rep Power : 0
Likes Received1359
Likes Given282
[h=2]Re: Dr. Slaa kuwasilisha leo mpango mkakati wa ushindi mbele ya Sekretarieti[/h]Yericko,
Siasa ya unafiki sipendi. Nimenyamaza lakini naona mnazidi kunichokoza. Ni afadhali mngelikaa kimya kama nilivyonyamaza mimi. Uwongo wowote na upotoshwaji wowote sitauvumilia. Nitaukanusha hapo hapo. Hata kama una lengo lako ambalo silifahamu naomba sana usitumie jina langu. Nimefundishwa uwongo ni dhambi siko tayari kushiriki dhambi hiyo.
sina kikao chochote cha Secretariat sina mpango wowote ninaopanga kuwasilisha popote. Naomba watanzania wapuuze propaganda zote zinazofanyika kwa jina langu.
Ningehitaji kutuma taarifa yoyote kwa umma ningeliita Press Conference Mwenyewe au ningelitumia utaratibu wowote uliouliozoeleka.
Naomba kutoa onyo kwa mtu yeyote awaye, matumizi ya jina la Dr Slaa yakome.