Kachocho T.K
Member
- Feb 1, 2011
- 25
- 3
siku chache zilizopita waziri mkuu alisikika akiongelea suala la kupanda bei kwa sukari na mazao mengine kama mchele, mahindi na maharage kuwa sababu kubwa ni biashara ya magendo inayofanywa na wafanya biashara haramu, wanavusha biashara hii nje ya nchi. Waziri aliagiza jeshi la polisi kuhakikisha watu hawa wanadhibitiwa na ikibidi jeshi la wananchi liingilie kati. Mnavyojua wanajeshi wetu walivyo sharp kutekeleza agizo la wakubwa. Mkoani kagera kagera belia zimezagaa kila mahali hata kwenye njia za ng'ombe, wakitekeleza agizo la mkubwa. haiingii akilini kuona raia wa ndani wanakosa bidhaa hizi kwani hata mfanya biashara anayenunua kilo 50 za sukari kutoka Bukoba mjini akapeleka katoma km5 ili aweke kwenye duka lake na wananchi wa katoma wapate sukari karibu, lkn mfanya biashara huyo ananyanganywa kilo 50 kwa madai alikuwa anavusha sukari, sijui kwenda wapi kwani katoma si Tanzania? na je hawaoni kuwa hali hii itasababisha baadhi ya maeneo kukosa sukari kabisa? kwani wenye maduka huko vijijini wanazuiwa belia kupitisha sukari. mwisho agizo la waziri mkuu ilikuwa ni kudhibiti usafirishaji ndani au nje ya nchi. Na kama ni hivyo kwa nini belia hizi zisiwe mipakani ambapo bidhaa hizi zinavushiwa kwenda nje?.