Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
Inasemekana kwamba Mafuta yamegundulika ndani ya Tanzania.
Kama hii ni kweli, basi naomba nianze kwa kusema kwamba Mungu ashukuriwe maana ame tubariki kuliko tunavyostahili, na ame tubaliki kuliko viwango vya akili zetu.
Mwaka 1965, serikali ya Tanzania iliamua kuanzisha kampuni ya TIPER (Tanzanian and Italian Petroleum Refining Company Ltd).
Kazi ya hii kampuni ilikua ni kupokea mafuta machafu, Crude Oil, kuyasafisha, na kisha kuhifadhi kwa muda kabla ya kuya peleka kwa wauzaji kama vile BP, Shell nk.
Katika kusafishia mafuta hapa hapa nchini, tulikuwa tunaweza kunufaika kwa mambo yafuatayo:
1. Tulipata Bitumen, ambayo ni residue ambazo zina tengezea lami, kwa ajili ya ujenzi wa barabara, na vifaa vya kuezekea nyumba kama mabati, vigae etc
2. Fuel Oil, ambayo ni mafuta mazito, hutumika kwenye meli, na hata kwenye furnace kwa ajili ya joto kali sana hasa kuyeyushia vyuma nk.
3. Mafuta ya kulainishia vyuma, kama vile grease ambazo unapaka kwenye minyororo, geti, nk.
4. Diesel, kwa ajili ya magari makubwa.
5. Gasoline, kwa ajili ya magari madogo, piki piki etc.
6. LPG,...ambayo ni gesi tunayotumia kwa kupikia majumbani, wengine wanatumia kwenye gari siku hizi badala ya gasoline.
7. Na mengineyo mengi.
Hizi zote ni faida kubwa sana, ambazo tulikua tuna zipata kwa kununua mafuta machafu na kuyasafishia hapa hapa nchini.
Lakini mwaka 1999, kwa akili za ajabu kabisa, serikali ikasimamisha kampuni hii. Naomba niuite uhujumu uchumi labda mkubwa kuliko maelezo ulio wahi kutokea Tanzania kwa sababu kufungia TIPER kuliua viwanda vingine vingi vidogo vidogo.
Mwaka 2001, wakaamua waifufue TIPER (Tanzania Internationa Petroleum Reserve),...lakini sasa hivi, kama jina lilivo, ikiwa sio kwa ajili ya kwa ajili ya refining, ila kwa ajili ya kutunza mafuta yaliyoagizwa toka nje.
Sasa najiuliza:
1. Hivi kweli tumewahi ongozwa na rais mzalendo? Ni nani aliyeua TIPER ya zamani na kuleta TIPER ambayo sasa ni kama "godauni" tu?
2. Kulikuwa na ulazima wa kuagiza lami nje ya nchi wakati tulikuwa tunaweza wenyewe kutengeneza hapa hapa nchini? Hizi gharama za kuagiza lami kama product ya crude oil peke yake ni kubwa kuliko zile za kutengeneza mitambo ya refining inayooza pale tuanze kurekebisha makosa yetu?
3. Crude oil ndani yake unapata materials kwa ajili ya kutengeneza matairi ya magari (refer to General Tyres Tanzania),...serikali inawaza nini kukifufua kiwanda hiki?
Uganda wamegundua mafuta kwao, Museveni amekataa kuchimba hadi wasomeshe vijana wao kwanza watakaosimamia shughuli hiyo wenyewe, wakati huohuo wakijenga mitambo madhubuti kwa ajili ya kazi hiyo.
Huku kwetu tunaendelea kulialia mafuta yawe ya muungano au sio, sasa tukianza kuchimba tutasafirisha crude oil kwenda Uganda kusafisha au?
Hizo gharama zitakuwa ndogo kuliko kufufua TIPER ambayo pia ni itachukua watu wengi sana kwa kuwaajili?
Mungu sasa inatosha, ILAANI kidogo Tanzania.
Kwanini kutupa mafuta ilihali tu MAJUHA?
Kama hii ni kweli, basi naomba nianze kwa kusema kwamba Mungu ashukuriwe maana ame tubariki kuliko tunavyostahili, na ame tubaliki kuliko viwango vya akili zetu.
Mwaka 1965, serikali ya Tanzania iliamua kuanzisha kampuni ya TIPER (Tanzanian and Italian Petroleum Refining Company Ltd).
Kazi ya hii kampuni ilikua ni kupokea mafuta machafu, Crude Oil, kuyasafisha, na kisha kuhifadhi kwa muda kabla ya kuya peleka kwa wauzaji kama vile BP, Shell nk.
Katika kusafishia mafuta hapa hapa nchini, tulikuwa tunaweza kunufaika kwa mambo yafuatayo:
1. Tulipata Bitumen, ambayo ni residue ambazo zina tengezea lami, kwa ajili ya ujenzi wa barabara, na vifaa vya kuezekea nyumba kama mabati, vigae etc
2. Fuel Oil, ambayo ni mafuta mazito, hutumika kwenye meli, na hata kwenye furnace kwa ajili ya joto kali sana hasa kuyeyushia vyuma nk.
3. Mafuta ya kulainishia vyuma, kama vile grease ambazo unapaka kwenye minyororo, geti, nk.
4. Diesel, kwa ajili ya magari makubwa.
5. Gasoline, kwa ajili ya magari madogo, piki piki etc.
6. LPG,...ambayo ni gesi tunayotumia kwa kupikia majumbani, wengine wanatumia kwenye gari siku hizi badala ya gasoline.
7. Na mengineyo mengi.
Hizi zote ni faida kubwa sana, ambazo tulikua tuna zipata kwa kununua mafuta machafu na kuyasafishia hapa hapa nchini.
Lakini mwaka 1999, kwa akili za ajabu kabisa, serikali ikasimamisha kampuni hii. Naomba niuite uhujumu uchumi labda mkubwa kuliko maelezo ulio wahi kutokea Tanzania kwa sababu kufungia TIPER kuliua viwanda vingine vingi vidogo vidogo.
Mwaka 2001, wakaamua waifufue TIPER (Tanzania Internationa Petroleum Reserve),...lakini sasa hivi, kama jina lilivo, ikiwa sio kwa ajili ya kwa ajili ya refining, ila kwa ajili ya kutunza mafuta yaliyoagizwa toka nje.
Sasa najiuliza:
1. Hivi kweli tumewahi ongozwa na rais mzalendo? Ni nani aliyeua TIPER ya zamani na kuleta TIPER ambayo sasa ni kama "godauni" tu?
2. Kulikuwa na ulazima wa kuagiza lami nje ya nchi wakati tulikuwa tunaweza wenyewe kutengeneza hapa hapa nchini? Hizi gharama za kuagiza lami kama product ya crude oil peke yake ni kubwa kuliko zile za kutengeneza mitambo ya refining inayooza pale tuanze kurekebisha makosa yetu?
3. Crude oil ndani yake unapata materials kwa ajili ya kutengeneza matairi ya magari (refer to General Tyres Tanzania),...serikali inawaza nini kukifufua kiwanda hiki?
Uganda wamegundua mafuta kwao, Museveni amekataa kuchimba hadi wasomeshe vijana wao kwanza watakaosimamia shughuli hiyo wenyewe, wakati huohuo wakijenga mitambo madhubuti kwa ajili ya kazi hiyo.
Huku kwetu tunaendelea kulialia mafuta yawe ya muungano au sio, sasa tukianza kuchimba tutasafirisha crude oil kwenda Uganda kusafisha au?
Hizo gharama zitakuwa ndogo kuliko kufufua TIPER ambayo pia ni itachukua watu wengi sana kwa kuwaajili?
Mungu sasa inatosha, ILAANI kidogo Tanzania.
Kwanini kutupa mafuta ilihali tu MAJUHA?