Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 13,226
- 26,048
Nawasalimu kwa Jina la JMT
Leo napenda kutoa uchambuzi wangu kidogo juu ya Mabadiliko ya Baraza la Mawaziri
Kwa Mawaziri
Kwanza napenda kusema Mama hajafanya vibaya! Mawaziri ni wasimamizi wa Sera ana haki ya kuweka yeyote amtakaye.
Malalamiko kadhaa yamesikika juu ya watu hawa
1. Mchengerwa kutolewa utumishi
Hapa inaonekana watumishi wengi walimpenda na kumkubali sana mchengerwa. Mimi sio mtumishi wa umma ila kiukweli hata mimi niliona jamaa ametosha pale. Sijui nini kimemfanya Rais amtoe Ila naamini kama Samia ameona reaction ya watumishi atafikiri upya Kama hakukuwa na ulazima wa kumtoa pale
2. Kuondolewa Lukuvi
Kusema kweli Mimi sijawai kuwa mfuasi wa Lukuvi na ukiniuliza Kwa nini nitakwambia kwa miaka yote aliyokaa Lukuvi ardhi nilichokuwa nakuona ni ongezeko la makazi holela kila siku. Bora uholela ungekuwepo kwenye makazi ya zamani na sio maeneo mapya ila mfano kwa Dar tu, Hadi maeneo mapya ya chanika, goba, madale, kibamba uholela unazidi kukua kila siku wakati Wizara ipo na wanaweza kutumia hata wanafunzi wa vyuo vya ardhi katika kupima na kupanga makazi ila kwake huo ubunifu sikuwai uona. Mikoa yote Tanzania ni uholela tu wa makazi! Nilimuona kwenye vyombo vya Habari tu akitoa matamko na si lolote lingine. Kwenye hili nasema Mama yuko sahihi.
3. Jaffo kuendelea kuwa Waziri
kama ilivyo Kwa Lukuvi, nimeona Jaffo nae bado yupo kwenye baraza. Kwangu Mimi Jaffo alifeli kwenye mazingira. Mwaka 2019 tulipitisha Sheria kuzuia mifuko ya plastiki ila kwenye hili Jaffo amefeli big time. Kuna uzi niliandika humu kumshauri Makamu wa Rais kuzunguka kwenye vibanda vya chips Dar na Dodoma aone kwa Jinsi gani mifuko ya plastiki imerudi kwenye hadi kufungia chips. Jaffo alifeli kwenye Mazingira hivyo hakustahili kurudi. Naamini Mama Samia ataendelea kuliangalia hili
4. Kabudi na Kitila
Najua Rais ana utashi wake Ila Kwa kumuondoa Prof Kitila naweza kusema kuwa hajakosea! Sikuona ubunifu wowote kwa kitila kwa alivyokuwa Biashara na hata Uwekezaji. Ni mtu wa maneno mengi tu
Kwa Kabudi nikiri huyu mzee uwezo anao Ila naona kama alikata tamaa kufanya kazi baada ya kifo cha JPM. Naona pia mama yuko sahihi. Naamini anaweza kunfikiria badae
5. Ridhiwani na Nape
Kwa hawa wote maneno yamesemwa kumgusa JK kuwa ndo sababu ya wao kuteuliwa. Kwa hawa naweza kusema sioni Tatizo kwao. Nape ni mtendaji mzuri sana. Alionekana alivyokuwa Wizara ya habari Mara ya mwisho. Ridhiwani watu wanakosea kumjudge mapema. Ni mpya kabisa kwenye Baraza. Sioni Tatizo kwake zaidi ya maneno ya kutunga ya watanzania yanayoongozwa na chuki tu. Huyu awe judged Kwa utendaji wake atakaouonesha pale Ardhi.
Mwisho kwenye Baraza la Mawaziri napenda kukiri kusikitika kutokuwepo kwa Charles Kimei- Sijui Mama anamuwazia nini Ila Kwa mafanikio ya huyu mtu akiwa crdb ninaona ni mtu muhimu sana kuwepo kwenye wa shauri wa Mama Samia kwenye cabinet
Dr Charles Kimei namfanisha na watu wenye weredi na u smart wa kupekee kama Prof Luoga, Nehemia Mchechu, Prof Chamuliro, Prof Mchome, Kanali Simbakalia ambao wana uwezo mkubwa sana wa kiakili hivyo hawana budi kuwa washauri wa Karibu wa Mamlaka.
Nataka na napenda sana Mama Samia afanikiwe. Ameanza vizuri na anakwenda vizuri. Napenda sana azidi kufanikiwa zaidi. Natumai Kwa sehemu chache nilizoshauri atazingatia humu.
Leo napenda kutoa uchambuzi wangu kidogo juu ya Mabadiliko ya Baraza la Mawaziri
Kwa Mawaziri
Kwanza napenda kusema Mama hajafanya vibaya! Mawaziri ni wasimamizi wa Sera ana haki ya kuweka yeyote amtakaye.
Malalamiko kadhaa yamesikika juu ya watu hawa
1. Mchengerwa kutolewa utumishi
Hapa inaonekana watumishi wengi walimpenda na kumkubali sana mchengerwa. Mimi sio mtumishi wa umma ila kiukweli hata mimi niliona jamaa ametosha pale. Sijui nini kimemfanya Rais amtoe Ila naamini kama Samia ameona reaction ya watumishi atafikiri upya Kama hakukuwa na ulazima wa kumtoa pale
2. Kuondolewa Lukuvi
Kusema kweli Mimi sijawai kuwa mfuasi wa Lukuvi na ukiniuliza Kwa nini nitakwambia kwa miaka yote aliyokaa Lukuvi ardhi nilichokuwa nakuona ni ongezeko la makazi holela kila siku. Bora uholela ungekuwepo kwenye makazi ya zamani na sio maeneo mapya ila mfano kwa Dar tu, Hadi maeneo mapya ya chanika, goba, madale, kibamba uholela unazidi kukua kila siku wakati Wizara ipo na wanaweza kutumia hata wanafunzi wa vyuo vya ardhi katika kupima na kupanga makazi ila kwake huo ubunifu sikuwai uona. Mikoa yote Tanzania ni uholela tu wa makazi! Nilimuona kwenye vyombo vya Habari tu akitoa matamko na si lolote lingine. Kwenye hili nasema Mama yuko sahihi.
3. Jaffo kuendelea kuwa Waziri
kama ilivyo Kwa Lukuvi, nimeona Jaffo nae bado yupo kwenye baraza. Kwangu Mimi Jaffo alifeli kwenye mazingira. Mwaka 2019 tulipitisha Sheria kuzuia mifuko ya plastiki ila kwenye hili Jaffo amefeli big time. Kuna uzi niliandika humu kumshauri Makamu wa Rais kuzunguka kwenye vibanda vya chips Dar na Dodoma aone kwa Jinsi gani mifuko ya plastiki imerudi kwenye hadi kufungia chips. Jaffo alifeli kwenye Mazingira hivyo hakustahili kurudi. Naamini Mama Samia ataendelea kuliangalia hili
4. Kabudi na Kitila
Najua Rais ana utashi wake Ila Kwa kumuondoa Prof Kitila naweza kusema kuwa hajakosea! Sikuona ubunifu wowote kwa kitila kwa alivyokuwa Biashara na hata Uwekezaji. Ni mtu wa maneno mengi tu
Kwa Kabudi nikiri huyu mzee uwezo anao Ila naona kama alikata tamaa kufanya kazi baada ya kifo cha JPM. Naona pia mama yuko sahihi. Naamini anaweza kunfikiria badae
5. Ridhiwani na Nape
Kwa hawa wote maneno yamesemwa kumgusa JK kuwa ndo sababu ya wao kuteuliwa. Kwa hawa naweza kusema sioni Tatizo kwao. Nape ni mtendaji mzuri sana. Alionekana alivyokuwa Wizara ya habari Mara ya mwisho. Ridhiwani watu wanakosea kumjudge mapema. Ni mpya kabisa kwenye Baraza. Sioni Tatizo kwake zaidi ya maneno ya kutunga ya watanzania yanayoongozwa na chuki tu. Huyu awe judged Kwa utendaji wake atakaouonesha pale Ardhi.
Mwisho kwenye Baraza la Mawaziri napenda kukiri kusikitika kutokuwepo kwa Charles Kimei- Sijui Mama anamuwazia nini Ila Kwa mafanikio ya huyu mtu akiwa crdb ninaona ni mtu muhimu sana kuwepo kwenye wa shauri wa Mama Samia kwenye cabinet
Dr Charles Kimei namfanisha na watu wenye weredi na u smart wa kupekee kama Prof Luoga, Nehemia Mchechu, Prof Chamuliro, Prof Mchome, Kanali Simbakalia ambao wana uwezo mkubwa sana wa kiakili hivyo hawana budi kuwa washauri wa Karibu wa Mamlaka.
Nataka na napenda sana Mama Samia afanikiwe. Ameanza vizuri na anakwenda vizuri. Napenda sana azidi kufanikiwa zaidi. Natumai Kwa sehemu chache nilizoshauri atazingatia humu.