Mawaziri waliotemwa katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano Agosti 30, 2023 amefanya mabadiliko Baraza la Mawaziri ambapo Waziri mmoja na Manaibu wawili wameachwa na nafasi zao zimechukuliwa na wengine.

mabula.jpg

Aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula

Miongoni mwa walioachwa ni aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula ambaye nafasi yake imechukuliwa na Jerry Silaha Mbunge wa Ukonga.

masanja.jpg

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja

Pia, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja naye ameachwa huku nafasi hiyo ikichukuliwa na Dunstan Kitandula.

277927241_3599921363567692_6091062154660713807_n.jpg

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete

Mwingine aliyeachwa ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete ambapo kwa sasa wizara hiyo imegawanywa mara mbili; upande wa Ujenzi Rais Samia amemteua Godfrey Kasekenya kuwa Naibu Waziri na Uchukuzi amemteua David Kihenzile kuwa Naibu Waziri.

Mabadiliko haya yanatokea ikiwa ni siku 56 tangu afanye mabadiliko madogo katika baraza hilo kwa kuigawa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na kuunda Wizara tatu; Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara.

Ambapo alimteua Mbunge wa Ubungo Profesa Kitila Mkumbo kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji.

Pia alimteua aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Fedha.
 
Atupele Mwakibete halali yake kutemwa hajafanya chochote jimboni kwake

Barabara ya kutoka Katumba hadi mwakaleli taabu tupu wakati hiyo barabara ndiko kunatoka gesi na chai inayoingizia Chi pesa za kigeni kwa wingi

Yaani serikali inavuna pesa kule lakini kutengeneza barabara hawataki na Mwakibete wao
 
Miongoni mwa walioachwa ni aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Angeline Mabula ambaye nafasi yake imechukuliwa na Jerry Silaha Mbunge wa Ukonga.

Pia, aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja naye ameachwa huku nafasi hiyo ikichukuliwa na Dunstan Kitandula.
Hawa wote ni Wasukuma. Mama anaswagia Sukuma gang ziIzini kwa amri ya IGP
 
Atupele Mwakibete halali yake kutemwa hajafanya chochote jimboni kwake

Barabara ya kutoka Katumba hadi mwakaleli taabu tupu wakati hiyo barabara ndiko kunatoka gesi na chai inayoingizia Chi pesa za kigeni kwa wingi

Yaani serikali inavuna pesa kule lakini kutengeneza barabara hawataki na Mwakibete wao
Hata mimi mkulima wa Parachichi pale Suma Nditu nakubaliana na wewe. Ukitaka kwenda Lwangwa kwa njia hiyo ukiwa na gari ndogo ni almost haiwezekani
 
Hata mimi mkulima wa Parachichi pale Suma Nditu nakubaliana na wewe. Ukitaka kwenda Lwangwa kwa njia hiyo ukiwa na gari ndogo ni almost haiwezekani
Yaani kabisa kuna mandizi pia kibao yanaenda mikoa yote bado barabara serikali haitaki kutengeneza sehemu yenye uchumi mkubwa kama hiyo wanatengenezea barabara mitaani za wauza maandazi na vitumbua wa dar es salaam
 
Mabadiliko haya yanatokea ikiwa ni siku 56 tangu afanye mabadiliko madogo katika baraza hilo kwa kuigawa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na kuunda Wizara tatu; Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Mabadiliko kila baada ya siku 56. Ukiwa na bahati. Huu umeshakuwa mchezo.
 
Atupele Mwakibete halali yake kutemwa hajafanya chochote jimboni kwake

Barabara ya kutoka Katumba hadi mwakaleli taabu tupu wakati hiyo barabara ndiko kunatoka gesi na chai inayoingizia Chi pesa za kigeni kwa wingi

Yaani serikali inavuna pesa kule lakini kutengeneza barabara hawataki na Mwakibete wao
Lakini ubunge wake si unabaki kwa maana ya kwamba ataendelea kuwawakilisha? Au alivyotolewa uwaziri sasa barabara itajengwa kwa kiwango cha lami?
 
Katika Teuzi na haya mabadiliko yako uliyoyatangaza,Nafasi ziko 16,waislam ni wawili tuh na wakristo wako 14.

Nawahakikishia laiti hili lingekuwa vice versa hii nchi kila kona ungeskia kelele na kusingekalika.

1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

2. Amemteua January Makamba (MUISLAM) kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.

3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana (MKRISTO) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.

4. Amemhamisha Steven Byabato (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.

5. Amemteua Jerry Silaa (MKRISTO)kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.

6. Rais amemteua Anthony Mavunde(MKRISTO) kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.

7. Prof Makame Mbarawa (MUISLAM) aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.

8. Innocent Bashungwa (MRISTO)amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.

9. Godfrey Kasekenya (MKRISTO) aliyekuwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi

10. Alexander Mnyeti (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo

11. David Mwakiposa (MKRISTO)Kihenzile ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi. Ni mbunge wa Jimbo la Mufindi

12. Judith Kapinga (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa nishati, ni mbunge wa viti maalum Ruvuma.

13. Dunstan Kitandula (MKRISTO)ameteuliwa Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, ni mbunge wa Mkinga

14. Stergomena Tax (MKRISTO)amehamishwa wizara ya mambo ya Nje kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

15. Angellah Kairuki (MKRISTO)amehamishwa kutoka TAMISEMI na kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii

16. Dkt. Damas Ndumbaro (MKRISTO) amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba ba Sheria na kuwa Waziri wa Utamaduni

Hongera sana kwa kuwa na moyo wa ujasiri na uthubutu.
Daah
 
Katika Teuzi na haya mabadiliko yako uliyoyatangaza,Nafasi ziko 16,waislam ni wawili tuh na wakristo wako 14.

Nawahakikishia laiti hili lingekuwa vice versa hii nchi kila kona ungeskia kelele na kusingekalika.

1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

2. Amemteua January Makamba (MUISLAM) kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.

3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana (MKRISTO) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.

4. Amemhamisha Steven Byabato (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.

5. Amemteua Jerry Silaa (MKRISTO)kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.

6. Rais amemteua Anthony Mavunde(MKRISTO) kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.

7. Prof Makame Mbarawa (MUISLAM) aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.

8. Innocent Bashungwa (MRISTO)amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.

9. Godfrey Kasekenya (MKRISTO) aliyekuwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi

10. Alexander Mnyeti (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo

11. David Mwakiposa (MKRISTO)Kihenzile ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi. Ni mbunge wa Jimbo la Mufindi

12. Judith Kapinga (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa nishati, ni mbunge wa viti maalum Ruvuma.

13. Dunstan Kitandula (MKRISTO)ameteuliwa Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, ni mbunge wa Mkinga

14. Stergomena Tax (MKRISTO)amehamishwa wizara ya mambo ya Nje kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

15. Angellah Kairuki (MKRISTO)amehamishwa kutoka TAMISEMI na kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii

16. Dkt. Damas Ndumbaro (MKRISTO) amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba ba Sheria na kuwa Waziri wa Utamaduni

Hongera sana kwa kuwa na moyo wa ujasiri na uthubutu.
Ni mpishano tu kuna mkeka inakuwaga na muslim wengi kuzingi Wagalatia wenye nchi
 
Hata tupangue vipi hizi wizara, kama hatutoacha mfumo ufanye Kazi inavyotakiwa basi haya mabadiliko hayana maana.
Upanguaji kwa nafikiri unaangalia tu yupi anawafaa viongozi wa juu sio kule kwa wananchi kuwa kawasaidia nini au atawasaidia nini wananchi wa kawaida mfano ni hiyo barabara .Labda sasa kabaki.mbunge labda atapiga miyowe labda

Barabara ya kule jimbo la Mwakibete Katumba hadi Mwakaleli hovyo lakini akapewa cheo cha unaibu waziri
 
Upanguaji kwa nafikiri unaangalia tu yupi anawafaa viongozi wa juu sio kule kwa wananchi kuwa kawasaidia nini au atawasaidia nini wananchi wa kawaida mfano ni hiyo barabara .Labda sasa kabaki.mbunge labda atapiga miyowe labda

Barabara ya kule jimbo la Mwakibete Katumba hadi Mwakaleli hovyo lakini akapewa cheo cha unaibu waziri
Huyo nae mzembe kweli acha wamteme
 
Katika Teuzi na haya mabadiliko yako uliyoyatangaza,Nafasi ziko 16,waislam ni wawili tuh na wakristo wako 14.

Nawahakikishia laiti hili lingekuwa vice versa hii nchi kila kona ungeskia kelele na kusingekalika.

1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

2. Amemteua January Makamba (MUISLAM) kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.

3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana (MKRISTO) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.

4. Amemhamisha Steven Byabato (MKRISTO)kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.

5. Amemteua Jerry Silaa (MKRISTO)kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.

6. Rais amemteua Anthony Mavunde(MKRISTO) kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.

7. Prof Makame Mbarawa (MUISLAM) aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.

8. Innocent Bashungwa (MRISTO)amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.

9. Godfrey Kasekenya (MKRISTO) aliyekuwa Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Ujenzi

10. Alexander Mnyeti (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Kilimo

11. David Mwakiposa (MKRISTO)Kihenzile ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi. Ni mbunge wa Jimbo la Mufindi

12. Judith Kapinga (MKRISTO) ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa nishati, ni mbunge wa viti maalum Ruvuma.

13. Dunstan Kitandula (MKRISTO)ameteuliwa Naibu Waziri wa maliasili na Utalii, ni mbunge wa Mkinga

14. Stergomena Tax (MKRISTO)amehamishwa wizara ya mambo ya Nje kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

15. Angellah Kairuki (MKRISTO)amehamishwa kutoka TAMISEMI na kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii

16. Dkt. Damas Ndumbaro (MKRISTO) amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba ba Sheria na kuwa Waziri wa Utamaduni

Hongera sana kwa kuwa na moyo wa ujasiri na uthubutu.
Kuna kitu labda kashtuka
Kuwa kuna mahali watu wanamdanganya na kumpeleka kusiko na minong'ono yao ya kumnong'oneza ya uongo

Uongo na udanganyifu huwa una mwisho

Mtu hadanganyiki milele
 
Back
Top Bottom