Uchambuzi: Undani wa Wabunge wa CCM kuikataa Bajeti 2009/2010

MwanaHaki

R I P
Oct 17, 2006
2,401
705
Waungwana,

Leo ninakuja kwenu (iwapo nitakuwa nimekosea mnikosoe), kwa mara ya kwanza kabisa, nikichambua undani wa Wabunge wa CCM kuikataa bajeti ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwaka wa Fedha 2009-2010, kama ifuatavyo.


  1. Nyote mnaelewa jinsi CCM ilivyogubikwa na kashfa nyingi, kuanzia Richmond, Meremeta Gold, Tangold, Kagoda, na EPA. Washauri/wabunifu/spin doctors wa CCM wakafanya tathmini na kubaini madhara ya muda mrefu na muda mfupi wa kashfa hizi zote, wakaona, bora waonekane kwamba "wanawajibika" kuliko kukaa kimya kabisa na kuyaacha mambo yaende kama yalivyo kwa sasa.
  2. Kuwajibika huku kulianza kwa Wabunge "machachari" kuanza kutoa taarifa mapema kwenye vyombo vya habari, siku chache kabla ya Mkutano wa Bunge kuanza, wakidai kwamba Bajeti hii imejaa "upendeleo". Hata kama madai hayo yalikuwa kweli, je, haupo uwezekano kwamba bajeti "ilipangwa vibaya" kwa makusudi, ili umma uone kwamba Wabunge wa CCM wanapigania maslahi ya umma, na si maslahi yao na ya chama chao?
  3. Kwa hiyo basi, kinachoendelea sasa ni kwamba, kwanza, leo mchana, majira ya saa saba, kulikuwa na Kikao Maalum cha Wabunge wa CCM, kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa, Jijini Dodoma. Tetesi za Dodoma zinasema kwamba "Wabunge wa CCM wamewekwa sawa" kwamba waikatae bajeti, ili Bunge livunjwe, wao wakiwa wamepata "ushujaa" wa "kuwatetea" wananchi, kwa "kuwajibika".
  4. Kesho jioni, Bunge likivunjwa, Uchaguzi Mkuu utaitishwa mapema zaidi kuliko ilivyo kawaida, CCM ikiwa inaonekana kupata ushindi wa kishindo, kwa kutumia "gia" ya "uwajibikaji kwa wananchi", hivyo kupata nafasi ya kukubalika, huku nyuma, kashfa zote za ufisadi zikiwa zimewekwa kando.
Sasa tujiulize maswali haya yafuatayo:


  1. Je, Wananchi wa Tanzania ni wasahaulifu kiasi hicho kwamba wataweza kuzisahau kashfa za Richmond, Meremeta Gold, Tangold, Dowans, EPA na nyinginezo (hata DECI....), kiasi cha kuwakubali Wabunge wa CCM ambao wanaonekana dhahiri kwamba "watacheza kiinimacho" ifikapo Alhamis, Juni 18, 2009?
  2. Je, kwa kuvunja Bunge kwa sababu ya "kuikataa bajeti", Wabunge watakuwa "wamewajibika" kweli kwa Wananchi, ama ndio "si hasa" yenyewe? Ni lini Wabunge "waliwajibika" kiasi hiki, mpaka kufikia "kuikataa bajeti"?
Ama kweli "mfa maji heshi kutapatapa"!

Sasa kama yatatokea haya kesho, msiulize nimeyajuaje. Hakuna aliyeniambia. Ni tafakuri jadidi yangu ndio imenifikisha kufikia "uchambuzi" huu. Kama kuna mwenye maoni tofauti, naye anaombwa kuchangia.

Naomba Kuwasilisha!

Ahsanteni!

./Mwana wa Haki
 
Mkuu na mimi haya ni maoni yangu tu.
Siamini kuwa (serikali au CCM) inaweza kuwaweka sawa wabunge ili waikatae bajeti ili bunge livunjwe.
Kuna mistari imeschorwa katika uongozi na utawala siku hizi. Wapo ambao walishajipambanua kuwa wapo upande gani. Wapo ambao walichelewa kufanya hivyo na wanaamua kutangaza sasa kwua wapo upande gani. haya ni mapambano baina ya kambi mbli ndani ya chama kimoja na serikali moja.
Wakatiw aenda haraka na wale ambaon walikwua hawajafanya maamuzi wapo upande gani wanalazimika kupiga kelele sana ili kujionyesha wazi wazi wapo upande gani. Wanafahamu fika kuwa wanatakiwa wachague hivi sasa watakayemtumikia kuelekea saa ile
 
If that's the case, here is my take:

Kama bunge litavunjwa, ina maana hakuna bajeti kwa mwaka ujao wa fedha. Serikali itajiendeshaje? Maamuzi yote yatatoka kwa mtu mmoja, MKULU.

What next?
Utakuwa ni wizi wa hali ya juu ambao Tanzania haijawahi kuiona. There will be no checks and balance until the new legislative body is in place.

They can not fool us any longer. We are behind each and every corner they turn.
 
Huyo mbunge wa CCM atakayepiga kura dhidi ya serikali ya CCM hajazaliwa bado. CCM ni wamoja kwa matendo na tabia - nje ya hapo ni usanii tu.
Birds of a feather fly together.
 
mambo makubwa kama haya (kuvunja bunge) hayawezi kutokea bongo! Serikali imekaliwa na watu waoga, wasioweza kuthubutu hata katika mambo madogo kama Kiwira Coal Mine. So, hakuna kitu hapo, bajeti itapita, uchaguzi wa Serikali za Mitaa watapeta (japo si kwa sana) na mwakani wataiba uchaguzi (siyo kura) staili ya Mugabe (kutishia wapiga kura wa mashambani na kurubuni wa mijini). Ngoma inakwenda, labda tufikirie 2015 ndo tunaweza kupata nafuu.
 
je, haupo uwezekano kwamba bajeti "ilipangwa vibaya" kwa makusudi, ili umma uone kwamba Wabunge wa CCM wanapigania maslahi ya umma, na si maslahi yao na ya chama chao?

Mwanahaki,

Hapo itakuwa sawa na kupeleka gari shimoni ukifiri kuwa kwa sababu utakuwemo ndani ya gari huko shimoni basi utaweka gear gari ipae utoke shimoni. haiendi hivyo na kwa hali ya ccm ilivyo makundi kwa sasa ni vigumu kufanikisha mipango ya namna ya "Tufe wote, ili tufufuke pamoja"

Tegemea moja tu, Bunge kuvunjwa! Kuna watu hawana la kupoteza ndani ya ccm ambao kurudi kwao 2010 hakutegemei chama maana tayari kimeonyesha kuwapa kisogo, wengine wametishwa na kutii. Bali wale wanaoheshimu misingi ya ridhaa ya uongozi kutoka kwa wananchi, na wamebanwa sana kuwatekelezea wananchi ahadi zao kupitia bajeti hii watalipuka kesho na kuandika historia. Lakini chini ya ardhi na mbingu ya Danganyika yote yanawezekana, kutokea au kutotokea. Ukisikia JK katembelea UDOM kukagua maendeleo ya ujenzi kesho, elewa tutakuwa tunaelekea pahala fulani pazuri.
 
Well, wameamua vingine! Tehe tehe tehe! Au waliogopa? Kibarua kingeota MBAWA mapema!
 
Back
Top Bottom