Uchaguzi Mdogo
Member
- Dec 9, 2014
- 12
- 14
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mhe. Diwani mmoja wa CCM hapa wilayani Mwanga akiwa na Mpambe wake ambaye pia anagombea uenyekiti wa mtaa kupitia CCM, jana usiku walijikuta katika wakati mgumu baada ya kuvamiwa na wananchi wenye hasira pale walipokuwa wakijaribu kuwarubuni wagombea wa upinzani katika chaguzi zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni. Imefahamika kuwa Mhe, Diwani huyo alitumwa na KIGOGO mmoja katika chama hicho hapa wilayani Mwanga. Na hadi sasa inaaminika kuwa KIGOGO huyo amefanikiwa kuwanunua wagombea kadhaa wa kutoka upinzani na wamejitoa katika kinyangányiro hicho.
Hali ya mhe, Diwan huyo na mpambe wake inaendelea vizuri, kwani bado wamelazwa katika hospital ya wilaya kwa matibabu zaidi. Hata hivyo, wahanga hao walipofikishwa kituo cha polisi na bahadhi ya wapenzi wa Chadema katika majira ya saa nne usiku, na katika mahojiano kituoni hapo, walisema hawawatambui wananchi waliowavamia na kuwapiga.
My take: Wananchi wa sasa wameanza kujitambua, VIVA 4ever...!!! hakuna kulala
Hali ya mhe, Diwan huyo na mpambe wake inaendelea vizuri, kwani bado wamelazwa katika hospital ya wilaya kwa matibabu zaidi. Hata hivyo, wahanga hao walipofikishwa kituo cha polisi na bahadhi ya wapenzi wa Chadema katika majira ya saa nne usiku, na katika mahojiano kituoni hapo, walisema hawawatambui wananchi waliowavamia na kuwapiga.
My take: Wananchi wa sasa wameanza kujitambua, VIVA 4ever...!!! hakuna kulala