Uchaguzi Serikali za Mitaa 2014: Matokeo kutoka nchi nzima (TZ Bara)

acha uongo mabomu yapo tabata kimanga jr

sio kimanga ni tembomgwaza pembeni nyumba yangu, barabara nyuma ya nyumba ndio mpaka wa kimanga na tembomgwaza, huko kimanga mnasikia sauti tu mchezo upo huku kisukuru (tembomgwaza)
 
Nipo hapa jirani na ukumbi wa CCM 77 Morogoro jirani na Vijana Social Hall, miCCM inashangilia ushindi kwa kupiga taarabu na kufungua Champaigne....waliowengi ni wanawake na watu wazima fulani hivi. Vijana ni wachache sana.
Hivi kweli mpaka leo kuna watu hawaoni uozo wa hiki chama? Ama kweli ndiyo maana mkoa wa Morogoro ni Maskini sana na upo nyuma kimaendeleo.
morogo naijua hiyo ilishajifia kwenye kijani taabani!!! hata hivyo nasikia kidooogo huko khonda angalau chadm wanajitikisa
 
Mwakyembe atajuta kuwabeza wanakyela, tunachukua wilaya yetu kwa bei ya jumla, lete matokeo mengine kamanda.:cheer2:

By Malafyale:
Wilaya ya Kyela
KITONGOJI CHAMA KILICHOSHINDA
Butiama- CHADEMA
Kyela kati -CHADEMA
Roma -CHADEMA
Mikoroshoni -CCM
Mbugani -CHADEMA
Nazareti -CHADEMA
Unyakyusa -CCM
Kapwil- CCM
Itunge mashariki -CCM
KEIFO -CCM
OROFEA -CHADEMA
SAMA B -CCM
Mikumi -CHADEMA
Mwaikambo -CHADEMA
Kilasil- CCM
Mkombozi -CHADEMA
Bondeni A-CCM
Bondeni B-CHADEMA
Itunge-Mundekesye CHADEMA
NB Uchaguzi uliopita WAPINZANI HAWAKUPATA
viti zaidi ya 5 Kyela lkn uchaguzi huu watapata
viti vingi mno,hii ni dalili mbaya sana kwa CCM
uchaguzi mkuu mwakani

mwakyembe na ccm wanapumulia mashine kyela
 
Mawakala wa CCM wa mtaa wa Gulka
Kwalala anakotoka meya wa Ilala
wamekimbia vituoni. Kura zinaendelea
kuhesabiwa kama kawaida.
Kwa Jimbo la UKONGA Mitaa ya Taliano,
Kichangani, Mwanagati, Mzinga, Kivule,
imeshatiwa kibindoni na Chadema. Mtaa
wa Mwongo la Ndege kibindoni kwa CUF.
Updates zinakuja
.............................................
.............
Mitaa ya Ulongoni A, Ulongoni B, Gongo la
mboto Kata ya Gongolamboto imeahirisha
uchaguzi mpaka Jumapili ijayo
 
sio kimanga ni tembomgwaza pembeni nyumba yangu, barabara nyuma ya nyumba ndio mpaka wa kimanga na tembomgwaza, huko kimanga mnasikia sauti tu mchezo upo huku kisukuru (tembomgwaza)

Chanzo nn mkuu?! uchaguzi km mdau mmoja alivyokwisha sema ama kuna mengine!
 
Back
Top Bottom