Ubalozi wa Tanzania UK Wamwita Kikwete Uingereza

Mbona GT unaruka Kimasai maana si Kimanga tena .



Tanzania Association in UK

soma hii thread:
Jumuiya Ya Watanzania Uingereza Yadaiwa Kuwa Kigenge Cha Maslahi Binafsi
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8907

halafu inakuwa tamu zaidi hapa:


Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Watanzania Uingereza, Abubakar Faraji amelaumiwa kwa kutumia jumuiya hiyo kwa maslahi yake binafsi. Hayo yameelezwa na viongozi wenzake ndani ya Jumuiya waliodai wamemvumilia vya kutosha lakini kwa sasa wanahisi kwa maslahi ya wengi ni vyema akajiuzulu kwa faida ya watanzania waishio nchini hapa.

''Kwa kweli huyu bwana tangu ameingia imekuwa ni kutumia jumuiya hii kujinufaisha binafsi, tunashindwa kumuelewa hasa ni lini ataweka mbele maslahi ya watanzania'' alisema kiongozi mwandamizi wa Jumuiya hiyo ambae hata hivyo aliomba jina lisitajwe kwa sasa.

Abu Faraji ambae aliingia madarakani mnamo mwezi wa tatu baada ya kushinda uchaguzi inadaiwa kutumia madaraka, anajishughulisha zaidi na biashara ya kutuma mizigo nchini Tanzania ingawa tangu kuingia madarakani amekuwa na biashara nyingine kadhaa ambazo zinahusiana moja kwa moja na jumuiya ya watanzania waishio Uingereza.

Imedaiwa kuwa Abu Faraji kwa kutumia mwamvuli wa wadhifa wake amekuwa wakala wa taasisi ya kutuma fedha, Western Union ambayo humlipa kiasi kikubwa cha fedha ili waweze kuwafikia watanzania. ''Sasa badala ya kuingiza fedha hizi katika mfuko wa watanzania zitumike kwa maendeleo, Bwana Faraji amekuwa akidai kuwaleta Western Union kufadhili shughuli za Jumuiya ni mkataba wake binafsi na hivyo fedha hizo ni za kwake!'' alilalamika kiongozi huyo.

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni, Abu Faraji aliwaburuza wajumbe wenzie wakubali yeye na aliekuwa Mwenyekiti Mwanzilishi Bi Norah Sumari wawe ndio waidhinishaji wakuu wa matumizi ya fedha za Jumuiya kwa kuwa ndio wadhamini wa akaunti ya Jumuiya, ''Kipindi kile hatukujua lengo lao kumbe walikuwa na njama maalum kwa vile sasa wawili hao wamesajili kampuni ABN REALESTATES wakishirikiana na Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania Johnson Lukaza ambae ni mmoja wa waliotajwa kuhusika na kashfa ya BOT iliyopelekea kufukuzwa kwa Bwana Daudi Balali kama gavana wa Benki Kuu'' alisema.

Aidha kiongozi huyo alidai kuwa kwa kuwa Abu Faraji na Bi Norah Sumari ndio wadhamini wakuu wa akaunti ya Jumuiya kitendo chao cha kufungua biashara pamoja kinakwenda kinyume na maadili mema ya biashara kwa vile kuna uwezekano mkubwa wa fedha za jumuiya kutumiwa kwa miradi yao kwa vile ni wao pekee wenye mamlaka ya kuziidhinisha.

''Hivi sasa tunaandaa mkutano mkubwa kwa ajili ya kuhimiza uwekezaji nyumbani Tanzania na tunatarajia Rais Kikwete kuwa ndio mgeni rasmi, Abu na Norah wamejipa uratibu mkuu wa shughuli hiyo na hakika inahitaji fedha nyingi kutoka kwa wafadhili, sisi wajumbe tuna wasi wasi na matumizi ya mapato toka kwa wafadhili kwa vile ni wao tu ndio wanaojua nini kinaendelea na sisi tumewekwa kando, muda kama huu ilitakiwa tushirikishwe kuandaa mkutano huu lakini ni Abu peke yake na Norah ndio wanaouandaa sisi hata tukiulizwa tunaambiwa subirini mkutano muone vitu vyetu!'' alizungumza kwa masikitiko kiongozi huyo.

Jitihada za mwandishi wa habari hizi ziligonga mwamba kumpata Bwana Faraji kujibu tuhuma hizo za kumfanya Bi Norah kuwa mwenza wake kibiashara ingawa imebainika kuwa Bi Norah licha ya kuwa mjumbe wa kawaida kwenye jumuiya hiyo ana nguvu kubwa kutokana na ''kukumbatiwa'' na Mwenyekiti Faraji ambae humuweka mbele katika kila jukumu lenye fursa au mikutano na viongozi wakubwa wa nchi wakipita London kiasi cha kusababisha mgawanyiko baina ya Bwana Faraji na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Bwana John Lusingu.

''Norah ukumbuke mdogo wake ndio alikuwa mmoja wa wahusika wa lile sakata la upimaji wa magari MOT na ndio maana kulikuwa na jitihada za jumuiya kuiunga mkono kampuni ya WTM Utility Services mpaka watu wa nje walipoingilia ndio Mwenyekiti akashtuka.

Jumuiya ya Watanzania waishio Uingereza ilianzishwa kutokana na jitihada kubwa ya Balozi Mwanaidi Maajar lakini hadi hivi sasa bado haijaonekana kufanya lolote kubwa katika kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania licha ya viongozi wake kuingia madarakani na ahadi kede kede ikiwemo ya kukusanya paundi 80,000 ndani ya miezi mitatu iliyotolewa na Mwenyekiti Abu Faraji wakati wa kuomba kura. ''Hata asilimia moja ya fedha hizo haipo kwenye akaunti, ni vichekesho kwa kweli, alifanya watu wajinga'' alisema kiongozi huyo ambae amedai kuwa amelazimika kuzungumza na Mwandishi wa habari hizi baada ya jitihada zake za kumtaka Mwenyekiti kuitisha kikao kujadili hayo kushindikana.

Hivi sasa ofisi za Jumuiya hiyo ndio pia makao makuu ya biashara za Bwana Abu Faraji na Bi Norah Sumari ambao kampuni yao ya ABNREALESTATES inashirikiana na Mfanyabiashara Johnson Lukaza ambae ametajwa kama mmoja wa wamiliki wa kampuni zilizojinufaisha katika utaratibu wa EPA sakata iliyosababisha aliekuwa gavana wa benki hiyo kujiuzulu.

Mwenyekiti Abu Faraji ambae hadi hivi karibuni alikuwa na heshima kubwa miongoni mwa Watanzania ameelezwa kuwa karibu mno na Balozi Mwanaidi Maajar ambae inadaiwa ndio hasa aliemshawishi Bwana Faraji agombee kwa vile anafahamiana na familia ya Bwana Faraji.

Mama yake Bwana Abu Faraji ni afisa mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini ambae ana ukaribu mkubwa na Balozi Maajar tangu wakiwa shuleni pamoja.


Time For Abu Faraji To Go
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=3091
 
Tanzania Association in UK

soma hii thread:
Jumuiya Ya Watanzania Uingereza Yadaiwa Kuwa Kigenge Cha Maslahi Binafsi
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8907

halafu inakuwa tamu zaidi hapa:


Time For Abu Faraji To Go
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=3091

Watanzania bwana .Hakuna aliye na uongozi safi ? Nimeyasikia madai haya muda sasa toka UK nikawa nadhani ni utani . Lakini je watu wa usama ambao walimpiga Yakubu kuuchukua Uenyekiti wanayaona haya na wanamweleza Rais ambaye anaingizwa kwenye mtego ?
 
Kikwete usiogope njoo hapa Marekani kwani kuna Wasomi wengi hapa kulipo Europe yote combined. Kuna Watanzania wengi sana wenye nafasi nzuri mfano kuna mtanzania mwenye asili ya kiasia ni vice president wa Microsoft huko Washington States, wengine ni na vice president wa universities. Hapa ndiyo deal lakini siyo vibaya kuanza na wanasiasa wako wa uingereza hapa ni business tu.
 
Kamundu,
hawezi kuja Marekani kirahisi kwanza fungueni tawi la CCM ndipo anakuja na bakhshishi kama za UK. Unajua tena wenzenu wamejitengeneza kisawasawa ndani ya mwavuli wa Chama..Haa haa haaa!
refuse to kneel before the sights you choose to see - Under my Umbrela, ela ela he hehe hey!
 
Kamundu,
hawezi kuja Marekani kirahisi kwanza fungueni tawi la CCM ndipo anakuja na bakhshishi kama za UK. Unajua tena wenzenu wamejitengeneza kisawasawa ndani ya mwavuli wa Chama..Haa haa haaa!
refuse to kneel before the sights you choose to see - Under my Umbrela, ela ela he hehe hey!

Mkandara JK ni mpenda sifa na Blah blah hawezi kukutana na watu serious bali wale wapiga soga wenzake na wanao imba wimbo wake .
 
Kamundu,
hawezi kuja Marekani kirahisi kwanza fungueni tawi la CCM ndipo anakuja na bakhshishi kama za UK. Unajua tena wenzenu wamejitengeneza kisawasawa ndani ya mwavuli wa Chama..Haa haa haaa!
refuse to kneel before the sights you choose to see - Under my Umbrela, ela ela he hehe hey!
halafu msisahau kuwa London ni kama USWAHILINI vile sasa muungwana naye kwa kuwa ni mswahili he feels more at home na waswahili wenzie London kuliko huko USA watu kutwa nzima mnaongea kidhungu tuuuu

boriiiiing

hata ningekuwa mimi ningewaavoid sana nyie watu wa USA
 
SIJAONA WATANZANIA WALIOPO NJE WAKAFANYA YA MAANA kwa WABONGO wenzao(wakiwepo basi tujulisheni)....watu wataishia ktk matumbo yao, Familia zao na wale mmhh....

UBINAFSI, UKABILA, MAJUNGU, FITNA, UZEMBE, BAADHI HAWATAKI KUSOMA, WAMETOSHEKA AU KURIDHIKA KUBEBA MABOX, NA KULETA MAFRIJI NA MAGARI MABOVU...NA MAFISADI WA WABONGO kwakuwa WANAONA MNAPATA WANAWAWEKEENI MOT...ETI INSPECTION...MWAMVULI wa INSPECTION....
 
Nzokankulu,
UK poa kabisa mkuu wangu yaani hakuna watu wanaofanya kwa vitendo kama UK hilo wazi. Bila shaka mmeonyesha uzalendo wa hali ya juu kuvaa uniform za CCM jambo ambalo hakuna nchi yeyote wameweza kulifanya labda China enzi za Mao tse Tung!... na ndio hao hao wavaa jezi waliokwenda Marekani wakaiba technologia na leo hii ni matajiri wawekeshaji wakubwa China na Marekani yenyewe. Ni mabo madogo madogo kama haya huleta tofauti zinazojiweza wekwa ktk kipimo.

Kusema kweli hatua ya JK ni nzuri sana na nitapendekeza kama ataifanya hata Marekani kwa ajili ya North Amerika yote na Japan au China kwa Asia nzima. Trust me ni hatua moja nzuri sana na nina hakika hii hoja imetoka kwa Membe kwani niliwahi zungumza naye miaka hiyooo.

Good move nampa sifa JK ila sije kuwa tu ni kwa raia wa Tanzania (wenye card ya CCM).
 
SIJAONA WATANZANIA WALIOPO NJE WAKAFANYA YA MAANA kwa WABONGO wenzao(wakiwepo basi tujulisheni)....watu wataishia ktk matumbo yao, Familia zao na wale mmhh....

UBINAFSI, UKABILA, MAJUNGU, FITNA, UZEMBE, BAADHI HAWATAKI KUSOMA, WAMETOSHEKA AU KURIDHIKA KUBEBA MABOX, NA KULETA MAFRIJI NA MAGARI MABOVU...NA MAFISADI WA WABONGO kwakuwa WANAONA MNAPATA WANAWAWEKEENI MOT...ETI INSPECTION...MWAMVULI wa INSPECTION....
RANT la nini sasa. Kwenye vitabu vitakatifu wanasema ukitoa sadaka kwa mkono wa kulia basi akikisha mkono wa kushoto hauoni. Walio nje wanasaidia sana lakini mkono wa kushoto hautakiwi kujua.
 
halafu msisahau kuwa London ni kama USWAHILINI vile sasa muungwana naye kwa kuwa ni mswahili he feels more at home na waswahili wenzie London kuliko huko USA watu kutwa nzima mnaongea kidhungu tuuuu

boriiiiing

hata ningekuwa mimi ningewaavoid sana nyie watu wa USA
Labda Mwanakijiji anakusimulia vizuri. Uhuru wa Tanzania ulianzia uswahilini, lakini Nyerere na usomi wake alikubali kwenda uswahilini na kuchangia mawazo yake hukihuko uswahilini.

Kama wewe ni msomi na una nia ya kubadilisha nchi yako nenda huko na toa points. Hizo points zako zinaweza kuwafanya watu wawe serious.
 
...waswahili ndio wapiga kura,wa US mtampa nini? watu hupendelea viwanja vya nyumbani,ila hii imekaa kama kupoteza pesa za walipa kodi tuu!
 
Abu Faraji, Juma Pinto, Maina Owino and the whole bunch wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuiaminisha serikali yetu na hayo mawazo yao yaliyotawaliwa zaidi na ufisadi wa kuwawezesha kuishi hapa kwa fedha za walipa kodi wa TZ.Siwalaumu, coz unapomwambia mtu akupe milioni moja uiweke chini ya mto kisha zitazaa milioni kumi, akikupa basi wewe sio wa kulaumiwa bali ujinga wa huyo aliyekupa. Wamekuja na project ya kutangaza TZ kwenye mabasi, wamedakishwa mshiko wa nguvu... lakini huwezi kuwalaumu coz inafahamika kuwa watalii wanaovutiwa na matangazo hayo wataenda kujaza pounds kwenye akaunti za akina Severe et al.

Wameshajua kinachomleta Muungwana UK frequently, na sio Kiingredha kama anavyodai Brazameni, au Uswahili as somebody claimed, ni mambo ya kiutu uzima.

Nadhani Muungwana atapomaliza muda wake anaweza kuweka rekodi ya kuwa kiongozi aliyetembelea UK mara nyingi kuliko wote duniani. Nani mwenye akili timamu atavutiwa na mikutano ya kizushi kama hiyo ilhali mafisadi wanaendelea kuinyonya nchi yetu? Yaani ajira milioni kadhaa zilizoahidiwa 2005 zimeshapata watu huko home hadi kuja kuwasaka wengine huku?
 
SIJAONA WATANZANIA WALIOPO NJE WAKAFANYA YA MAANA kwa WABONGO wenzao(wakiwepo basi tujulisheni)....watu wataishia ktk matumbo yao, Familia zao na wale mmhh....

UBINAFSI, UKABILA, MAJUNGU, FITNA, UZEMBE, BAADHI HAWATAKI KUSOMA, WAMETOSHEKA AU KURIDHIKA KUBEBA MABOX, NA KULETA MAFRIJI NA MAGARI MABOVU...NA MAFISADI WA WABONGO kwakuwa WANAONA MNAPATA WANAWAWEKEENI MOT...ETI INSPECTION...MWAMVULI wa INSPECTION....

Chuma,

Kufanya ya maana mpaka wakusaidie na wewe? Mtu hata akisaidia ndugu zake, tayari amesaidia Bongo.

Wala hata sio lazima watu watangaze au wajitangaze ili kuona wanasaidia nyumbani. Hata wakiwafungulia ndugu zao viduka vidogo vidogo bado ni kwa faida ya TZ, maana hao ndugu wanalipa kodi pamoja na kulisha familia (Watanzania wenzetu).

Rais JK, kafurahi mpaka jino la pembeni kuonekana shauri ya hizo 600M za USA. Je umefanya uchunguzi kidogo kujua Watanzania walioko nje wanaingiza pesa kiasi gani TZ?

Kazi ni kazi, hata kama mtu anabeba box, bado ni bora mno kuliko kuwa fisadi. Acheni kudharau kazi. Watu wanabeba box kwasababu na wala sio kwa kutaka kubeba box.
 
Hili soga la forum lishawai kuja US, I believe last time Jakaya alipokuja US kuna baadhi ya watanzania walikwenda kuongea nae concern that nonsense.

I know a couple of Tanzania here in US hold big positions in multbillion corporations, the problem wapi JK ataanzia. I know VP of Huliburton in global market ambae ni Mtanzania,Merrill Lynch VP wa research and acqusition ni Mtanzania na hawa wote wana dream na bongo lakini wote wana conclude kwamba Bongo ni kichwa cha mwenda wazimu.

Educated people need to ask WHY, and demand for reasons. Hawa kina Faraji walishajaribu hapa US kuleta hizo habari za CCM, then nikauliza simple question "Why CCM", "why do i need to Join CCM", majibu yalikuwa yale yale ooohh ukirudi Tanzania, ooooh ukitokea umekwenda Tanzania, nikasema same sh**** different smell.
 
Okay, hebu lets be serious kidogo about this. Mkandara mimi napenda rangi ya kijani, ila njano hapana, kwahiyo sio wote tuko kwenye mwamvuli wa CCM. The idea for the forum is fine and good start. Sasa je, vitu vichache ambavyo naona wakae wakifikiria kati ya sasa na mkutano huo. This is meant to be a challenge and not a hindrance. We want this to be a successful forum for all of us;

1) Will BoT be represented? – maana huwezi ukaongelea uwekezaji nchini kwetu wakati uchuro unaotokea nchini kwetu kila mtu anaona. Huwezi ukaongelea investments ya pesa zetu za kubeba maboksi wakati institution yetu kubwa inasumbuliwa na matatizo ya EPA na wanaongea na ku-deal na hii ishu ki-udikteta. That is just disrespectful to the diaspora intelligence, if they can get away with it in TZ, all good.

2) In 2006 according to the World Bank, Remittances to Tanzania were US Dollars 100 Million. That is 17% of what the USA has ‘donated’ to Tanzania. I bet you our $100 million has more impact that that $600 million. Can we get a better deal than the USA in terms of Tanzanian resources if we pass the money the way they want us to? Can we have a voice? Nasisi tunaweza kupata ka-contract ka-kujikaramagi ili tuwe na mining concessions dizaini hivi. We need something interesting, sio wanaokatiwa madili wawe waCanada tu na waMarekani etc. Sisi tutafanya kwa upendo wa nchi yetu. I think as peoples, we need to think in terms of investing in our resources rather than sending money to our uchwara Banks and their systems.

3) ‘The event is aimed at galvanising the Tanzanian Diaspora of all generations in harnessing their skills, knowledge and investment in the continued economic development of Tanzania.’ – What skills are they serious about? Ninachoelewa, vijana wengi wanaorudi nyumbani ni aidha kwenye mambo ya HR, na sana sana Banking systems nyumbani. Hata Engineers wanaenda kufanya benki, coca cola, makampuni ya simu….vitu havihusiani na masomo yao na experience zao (ili mradi wamerudi nyumbani na kupata kazi). Nothing wrong with that, but why don’t we think of creating other industries?? What is the government doing about it? And for that matter how do they want our contribution? Skills pool ipo hadi watu wazima/wazee, je, ili warudi, wameonyesha misingi gani ya kupambana na rushwa kuwapa imani kwamba Tanzania ni nchi ya vitendo (sio kuongea). Hawa watu wana-security gani na kazi zao. Are those industries sustainable…….i.e do we have the foundations to hold these industries?

Investment Climate for the Diaspora focusing on:
 Dar es Salaam Stock Exchange - Role of the Stock Exchange and opportunities for Diaspora investors
 Tanzania Investment Centre
 National Housing Tanzania
 Setting up and running a business – practicalities and opportunities
o Presentations will cover the performance of the stock exchange and then provide clear examples of opportunities in how to invest and the sectors, which have real growth opportunities
o The specific steps that are required to establish a business in Tanzania will follow information on the issues and opportunities in the housing sector
o National Housing will offer opportunity for plots and construction on a loan basis of residential houses for the Diaspora.


I love the idea of investing in property at home. In reality, for this I believe the greatest wealth is in the Tanzanian people (at home) themselves. What the Tanzania government needs to do is facilitate a way of putting a valuing scale to people’s wealth, especially land. As we have decided to embrace capitalism, then we need to start at the grassroots. They need to value the people of Tanzania first, before they look at our pounds and dollars.

Industry Opportunities and Challenges for Diaspora Skills Engagement
 Radar Recruitment
 Zantel Telecom Ltd
 Stanbic Bank Tanzania
 Deloitte and Touché Tanzania
o Delegates will receive information on opportunities for employment in Tanzania. This will cover areas where there are skill shortages, employment constraints and specific requirements. Organisations that are seeking to provide employment opportunities for Tanzanians in the Diaspora will also present.


For this, I would like to see numbers what they have achieved, the potential markets, sustainability and competitiveness in the market. How they got those numbers and how they project their future figures. We don’t want fudged numbers without concrete foundations.
For mobile companies, how they justify their costs of service (being higher than Europe at times) in comparison to the standard of life and little economic clout.

Kulikuwa na mapungufu mengi katika vi-presentation vya mwaka jana, they need to step-up big time. Lasivyo tutabaki kuambiana ooh waswahili tu blah blah. At the same time we need to give em benefit of doubt na kutoa mawazo ili wote tufaidi. Lakini lazima waelewe kwamba Economy inaendana na Political movement...and at the moment zina contradict zana Tanzania kuleta imani (atleast kwangu).
 
Nzokankulu,
Mkuu maelezo yako ndio vichwa vinavyotakiwa Tz leo, kesho na kesho kutwa. Ni mawazo endelevu na yanayotafuta solution lakini kwa bahati mbaya ni kwamba utaonekana mchawi. Ethics za NDIVYO TULIVYO zinapingana na mawazo kama haya, mawazo yanayojipanga kuanza kazi ngumu ya kutafuta tiba ya umaskini wetu hali tunaweza endelea kuwa ombaomba na vikopo vyetu mitaani huku hesabu ndogo ikijengwa mamillionea 100 kabla ya 2010.

Shukran mawazo yako bomba kishenzi na sina la kuongeza isipokuwa ni kumwomba Mungu atokee mwenye kuyaona haya ndani ya Utawala wa Julius Caesar kisha kuyapatia majibu kulingana na mapendekezo yako!..sii rahisi.

Pili, kumbuka kwamba mtu yeyote anayekataa CCM na hasa wakimbizi toka Zanzibar huko UK wamepoteza na Uraia wao. Hivyo basi huwezi kusema unaipenda Tanzania bila kuwa mwanachama wa CCM... Ndivyo tulivyo na muhimu kufahamu hilo ikiwa unataka kuleta changes zozote ktk society inayokutambua wewe kwa rangi hizi mbili - Kijani na njano.

Mkuu mnaweza fikiria ni fanya joke lakini ndivyo ilivyo in reality.. Kama hamtakubali CCM basi serikali haiwezi kuwatambua iwe US ama Australia. Kwa hiyo ni muhimu kwenu ku give up something ili mpate something for you country. Kifupi, moja ya ilani za Ndivyo tulivyo ni kwamba - Wewe ndiye mwenye shida sio Tanzania. Tafsiri fupi inasema hivi:- Kama ni umasikini basi wewe ndiye maskini sio watu wote - watu (CCM) wanatesa.
 
Nzokankulu,
Mkuu maelezo yako ndio vichwa vinavyotakiwa Tz leo, kesho na kesho kutwa. Ni mawazo endelevu na yanayotafuta solution lakini kwa bahati mbaya ni kwamba utaonekana mchawi. Ethics za NDIVYO TULIVYO zinapingana na mawazo kama haya, mawazo yanayojipanga kuanza kazi ngumu ya kutafuta tiba ya umaskini wetu hali tunaweza endelea kuwa ombaomba na vikopo vyetu mitaani huku hesabu ndogo ikijengwa mamillionea 100 kabla ya 2010.
Shukran mawazo yako bomba kishenzi na sina la kuongeza isipokuwa ni kumwomba Mungu atokee mwenye kuyaona haya ndani ya Utawala wa Julius Caesar kisha kuyapatia majibu kulingana na mapendekezo yako!..sii rahisi.

Pili, kumbuka kwamba mtu yeyote anayekataa CCM na hasa wakimbizi toka Zanzibar huko UK wamepoteza na Uraia wao. Hivyo basi huwezi kusema unaipenda Tanzania bila kuwa mwanachama wa CCM... Ndivyo tulivyo na muhimu kufahamu hilo ikiwa unataka kuleta changes zozote ktk society inayokutambua wewe kwa rangi hizi mbili - Kijani na njano.

Mkuu mnaweza fikiria ni fanya joke lakini ndivyo ilivyo in reality.. Kama hamtakubali CCM basi serikali haiwezi kuwatambua iwe US ama Australia. Kwa hiyo ni muhimu kwenu ku give up something ili mpate something for you country. Kifupi, moja ya ilani za Ndivyo tulivyo ni kwamba - Wewe ndiye mwenye shida sio Tanzania. Tafsiri fupi inasema hivi:- Kama ni umasikini basi wewe ndiye maskini sio watu wote - watu (CCM) wanatesa.

Haya maneno yanavunja moyo na ni dalili ya kukata tamaa. Sijui kama leo tungewasikia akina Obama,Condoleeza, Collin Powel, etc kama civil rights acitivists huko US wangekuwa na fikra kama hizi. Since when two wrongs do make a right? Yaani kwa vile ufisadi unawaneemesha watu flani basi kila Mtanzania a-cherish ufisadi?

Unaweza kuwa sahihi kuwa mie ndio mwenye shida,for 4 electoral years...In the 5th,it's CCM itakayokuwa na shida na kura yangu. Ok, let's forget abt elections. Hivi kaka, mwanaume rijali mwenye shida aliye kwenye ndoa, akikumbwa na shida, then akamuomba rafiki msaada, lkn rafiki akampa masharti kuwa ukitaka nikusaidie niache nilale na mkeo....had it been you, ungekubali kwa vile tu una shida na sio huyo jamaa?

Defeatist mentality kama hizi ndio zinazorutubisha ufisadi, la laiti zingeshamiri during anti-colonial struggle basi wala uhuru usingepatikana.

And I completely disagree with you kwamba huwezi kuleta changes in society bila kijani na njano. Kwani kijani na njano ndio iliyoibua sakata la richmond? Kwani kijani na njano ndio ilipelekea Balali kutoroka ulaji wake? You cant be serious, man!
 
SIJAONA WATANZANIA WALIOPO NJE WAKAFANYA YA MAANA kwa WABONGO wenzao(wakiwepo basi tujulisheni)....watu wataishia ktk matumbo yao, Familia zao na wale mmhh....

Kwani mtu anapokuja nje anakuja kwa ajili ya kufanya "ya maana" kwa wenzie au kwa ajili ya tumbo lake na familia yake?Kila mtu amekuja kivyake,how then utegemee kufanyiwa ya maana na mwenzio,especially kama wewe mwenyewe hufanyi ya maana?By the way,sema hujasikia(na sio hujaona) Watanzania walio nje ambao wana msaada kwa wenzao.Nenda kwa Michuzi utaona kuna tangazo la shukrani za ndugu wa marehemu mmoja aliyefia UK ambaye anashukuru msaada wa Watanzania flani,au kama una mtu Houston,waulize kuhusu jamaa aliyerudi kutoka TZ akiwa na mkewe na watoto kisha kuzuiliwa airport kutokana na probs za makaratasi...and how watz wenzie helped him...or ask watu waliokumbwa na misiba na namna walivyosaidiwa.Pengine kabla ya kulaumu watu,fanya sensa ya kufahamu watanzania hao unawaowazungumzia wako wa ngapi,wako wapi na wanajimudu vipi.Kutoa ni moyo sio utajiri,na ndio maana JOHN MASHAKA hasifiwi kwa vile ni mtu wa Wall Street bali kwa moyo wake wa kutoa.Au huyo nae sio Mtanzania?

Ukiwa hujapatwa na tatizo (au kama you keep probs to yourself) utawezaje kujua namna watanzania wanavyosaidiana wakiwa nje?Na kumbuka,msaada kwa mwezio si jambo la lazima bali ni hiari na kudumisha social animality yetu.
 
Back
Top Bottom