Ubaguzi unavyoimaliza Zanzibar

Ntaramuka

Senior Member
May 2, 2008
169
27
Ukiongelea mpasuko uliopo hapa Zanzibar, waliowengi hasa walioko Tanzania bara huzaidi kuhusu CCM na CUF au UNGUJA na PEMBA. Ni kweli kuna mpasuko mkubwa sana na tofauti za waziwazi zinazoonekana kati ya wapemba na waunguja kiasi kwamba wapemba hukosa hata kuajiriwa kwa sababu tu ya upemba, hali ambayo hupelekea kwa waombaji wa ajira ambazoziko chini ya muungano kulazimika kuandika maombi maalum bara ili waweze kuajoriwa.

Sio siri hili la CCM VS CUF na UNGUJA VS PEMBA lipo, lakini katika hali ya kushangaza kuna ubaguzi mwingine mkali sana na mbaya zaidi unaoendelea hapa unguja, huu ni ubaguzi wa KUSINI na KASKAZINI.

Kama kiongozi mwenya mamlaka fulani akitoka mkoa wa KASKAZINI NGUJA, basi wale wa upande mwingine wa KUSINI UNGUJA, yaani MAKUNDUCHI, MUYUNI nk. wanaumia vibaya mno.

Ubaguzi huu ni mbaya zaidi na ambao bila kuangaliwa vizuri zaidi unaweza kuliangamiza taifa la zanzibar.
 
Speaking f mambo ya UBAGUZI...



Lakini mbali na hayo, ngoja niwachekeshe kwa kuwaeleza jinsi mtu huyu alivyokubuhu katika kujenga chuki na fitina kwa kujifanya mtetezi wa wale anaowaita "wazawa", huku akiwa na lengo la kujinufaisha binafsi kwa kutumia mgongo wa chuki na fitina hizo anazopandikiza. Mwaka 1994, alitoa kauli zake zenye sumu ya ubaguzi pale alipodai kwamba sehemu kubwa ya maeneo ya katikati ya Jiji la Dar es Salaam inakaliwa na Watanzania wenye asili ya Kiasia na kwamba "wazawa" hawapo katika maeneo hayo. Aliyekuwa Rais wakati huo, Mzee Ali Hassan Mwinyi, akamuagiza Waziri aliyekuwa akishughulikia masuala ya ardhi, Mheshimiwa Edward Lowassa, kumpatia Mengi eneo kubwa la ardhi katikati ya jiji karibu na ilipo International House. Lakini mara tu alipopewa eneo hilo akaliuza kwa Fida Hussein, mfanyabishara Mtanzania mwenye asili ya Kiasia.
-Rostam Aziz

yap...ubaguzi huo...

btw CUF na CCM zanzibar wote hawautaki muungano...nyie wabara ndio mnaoungangania
 
Nadhani tumetekwa na historia... kwamba ni lazima tuendelee na muungano kwa vile tukiuvunja tutakosa sifa ambazo tumekuwa tukipewa na kupigiwa mfano afrika!!!!! MATOKEO YAKE MUUNGANO UNALAZIMISHWA KIASI KWAMBA BARA INAONEKANA KAMA VILE INA AGENDA YA SIRI KATIKA MUUNGANO - KAMA COMORO WAMEWEZA, ZANZIBAR PIA WATAWEZA
 
Wandugu, nilikuwa Pemba last week. The place is dead, miundo mbinu imekufa na jamaa ameingia mitini hapiti hakanyagi Pemba. Zaidi ya hapo wana sera za "tutakula dongo meaning hata kama iweje hawachagui CCM, na wale wa Unguja wanasema kumbi kwa kumbi meaning akitoka mtoto wa Karume anakuja mtoto wa ....read btn the lines.
 
Wandugu, nilikuwa Pemba last week. The place is dead, miundo mbinu imekufa na jamaa ameingia mitini hapiti hakanyagi Pemba. Zaidi ya hapo wana sera za "tutakula dongo meaning hata kama iweje hawachagui CCM, na wale wa Unguja wanasema kumbi kwa kumbi meaning akitoka mtoto wa Karume anakuja mtoto wa ....read btn the lines.

kweli Pemba utafikiri uko wild wild west ya 18th century...ya kwenye sinema za cowboys

hakufai
 
Zanzibar Pemba zote zinatumia utaifa wa Tanzania, kama kuna utaifa mwengine hebu tutupie kwenye katiba gani? Juzi tu tumeona vipi ZFA kama wanataka uwakilishi wa FIFA basi Zanzibar ikubali kuwa koloni la Tanzania,
Yule anaeuliza ili kuwe na Taifa, lazima uwe na nchi, serikali ,jeshi uthibitisho wa utaifa kama kadi ya uraia au Passport, hapo utaona Zanzibar hawana jeshi hawana fedha hawana uraia na mwisho hata michezo wanasema hata si koloni sijui tuiiteje.
 
ukiongelea mpasuko uliopo hapa zanzibar, waliowengi hasa walioko tanzania bara huzaidi kuhusu ccm na cuf au unguja na pemba. Ni kweli kuna mpasuko mkubwa sana na tofauti za waziwazi zinazoonekana kati ya wapemba na waunguja kiasi kwamba wapemba hukosa hata kuajiriwa kwa sababu tu ya upemba, hali ambayo hupelekea kwa waombaji wa ajira ambazoziko chini ya muungano kulazimika kuandika maombi maalum bara ili waweze kuajoriwa.

Sio siri hili la ccm vs cuf na unguja vs pemba lipo, lakini katika hali ya kushangaza kuna ubaguzi mwingine mkali sana na mbaya zaidi unaoendelea hapa unguja, huu ni ubaguzi wa kusini na kaskazini.

Kama kiongozi mwenya mamlaka fulani akitoka mkoa wa kaskazini nguja, basi wale wa upande mwingine wa kusini unguja, yaani makunduchi, muyuni nk. Wanaumia vibaya mno.

Ubaguzi huu ni mbaya zaidi na ambao bila kuangaliwa vizuri zaidi unaweza kuliangamiza taifa la zanzibar.

hii inaonyesha umgeni kwenye visiwa hivyo na unataka kupotosha ukweli wa suala. Hayo unayoyaeleza yalikuwepo tangu baada ya mapinduzi lakini hayakuwa kigezo cha kuimaliza zanzibara. Wenyewe wakiishi kwa kustahamiliana lakini huu ukoloni mpya mliouleta na kuanza kutumia tofauti za wazanzibari kwa faida yenu ndio unaoimaliza zanzibar. Kama mnajali basi mgechukua hatuwa za kuondosha hali hiyo badala ya kuipalilia kwa vile mgawanyiko wa wazanzibari na urahisi wa kuimeza.
 
zanzibar pemba zote zinatumia utaifa wa tanzania, kama kuna utaifa mwengine hebu tutupie kwenye katiba gani? Juzi tu tumeona vipi zfa kama wanataka uwakilishi wa fifa basi zanzibar ikubali kuwa koloni la tanzania,
yule anaeuliza ili kuwe na taifa, lazima uwe na nchi, serikali ,jeshi uthibitisho wa utaifa kama kadi ya uraia au passport, hapo utaona zanzibar hawana jeshi hawana fedha hawana uraia na mwisho hata michezo wanasema hata si koloni sijui tuiiteje.
.

ili kuwa taifa lazima uwe na vitu vikuu vitatu. Chombo cha kutunga sheria ( yaani bunge), uwe na chombo cha kutafsiri sheria (yaani mahakama huru). Na chonbo cha kusimamia sheria (yaani serikali) na cha mwisho kisichokuwa rasmi ni vyombo vya habari (yaaani hawa kazi yao kupasha habari,kuelimisha na kuburudisha.)

hivyo ni vitu vya msingi. Lakini kuna national identity kama wimbo wa taifa, sarafu,bendera n.k.

Sasa jaribu kuangalia kama zanzibar sio taifa.

mimi ninavyojua kisheria zanzibar ni taifa lakini sio doula
 
Nakubaliana fika na wewe zanzibar kuna ubaguzi wa wapemba na waunguja hilo lipo dhahiri.

lakini lazima ukubali kuwa tanganyika kuna udini. Ambao nyerere alijaribu sana kuuficha lakini sasa unajitokeza waziwazi. Na huu ni hatari zaidi.

Mola atunusuru
 
halo Barubaru
naona unachanganya sasa hebu nipe chombo cha kutunga sheria kipi walichonacho Zanzibar? Baraza la Wawakilishi sio linalotunga sheria ni baraza la kupitisha sheria, nitakupa mfano labuda ulikuwa dogo enzi hizo, Seif Sharifu alikuwa Waziri Kiongozi na ilisomwa na kupitishwa Bajeti ya Serikali mpaka mwisho ndipo Bunge lilipokuja na kushusha THAMANI YA HELA YA MADAFU nini kilitokea kaulize kwenye chombo cha kutunga sheria mimi simo

Makamo wa Raisi wa Tanzania kwa hali ya Zanzibar ni awe Raisi wa Zanzibar wapi alipo sasa mbona chombo cha kutunga sheria hakikutunga sheria hiyo, mimi simo usiniulize
 
kweli Pemba utafikiri uko wild wild west ya 18th century...ya kwenye sinema za cowboys

hakufai
Vipi kwani? Magu. Kibondo, Biharamulo kunafaa? si kuko kwa karne ya 17 tu na enzi za Red Indians- Acha masimango yasiyo na msingi.
 
Kama kiongozi mwenya mamlaka fulani akitoka mkoa wa KASKAZINI NGUJA, basi wale wa upande mwingine wa KUSINI UNGUJA, yaani MAKUNDUCHI, MUYUNI nk. wanaumia vibaya mno.
Bwana mkubwa wewe ni Bwana Ntaramuka au Nta-lamka. Naona umeamka na mpya hii. Aste aste baba!!!!.
 
Huu mpasuko wa ubaguzi hata Bara tuko nao,nikweli nyani haoni takole!!
 
Kuhusu huu ubaguzi wa wazanzibar kwa misingi ya ya maeneo ya kutoka ni suala lililowazi. Mimi si mgeni wa visiwa hivi na isingekuwa huu muungano wa tulionao sasa hali ingekuwa mbaya zaidi.

Kuna wakati mzanzibar ananyimwa ajira kwa misingi hii hii ya kibaguzi na mtu huyu kuamua kuomba kwa kupitia Tanzania bara na akafanikiwa. Sasa kama si muungano huu watu hawa wanaonyimwa ajira hizi wangeweza kuchukua hatua zingine ambazo huenda zingekuwa mbaya wa wananchi wasio na hatua wa hapa zanzibar.
 
sentensi yako ya mwisho inasema italiangamiza taifa la Zanzibar

Kwani Zanzibar ni Taifa?
Sual la Zanzibar ni nchi au la linakuwa gumu hasa kutokana na misamiayi yetu ya kiswahili, ila kwa kingereza ni rahisi sana na hapo utagundua kuwa zanzibar ni nchi.

Katika kiingereza kuna NATION (TAIFA), STATE (DOLA), COUNTRY(NCHI).
 
Back
Top Bottom