UAMSHO wanawatumia waislam kutimiza malengo yao

mngony

JF-Expert Member
Jul 27, 2012
5,193
6,381
mimi ni muislamu lakini nimeshtukia hichi kikundi cha UAMSHO kuwa ni kikundi cha kisiasa kinachowatumia waislamu bila wenyewe kujijua! Uamsho wanataka kujitenga na bara wakisingizia huku ni makafiri, je huku hakuna waislamu? Kwa nini wamuue askari ambaye ni Muislamu mwenzao? Katika uislam si haramu kumwaga damu ya muislamu mwenzako? hawa waislamu gani? kwa nini watoe taarifa za kuwa kiongozi wao ametekwa na hali ilikua haijulikani yuko wapi na kama ametekwa au la!? dereva anasema alishuka akapanda gari lingine na alikua akiwasiliana na watu, huko ndo kutekwa tena bila hata purukushani tena gari limekuja taratibu! na hilo gari lake mwanzo alikua akiendesha mwenyewe kwa nini alimua kumpisha dereva wake?Huo si uongo ambao ni haramu katika uislamu! Kwa nini zichomwe ofisi za CCM peke yake, mbona CUF nayo ni serikali pia? je CCM huko zanzibar viongozi wao makafiri? je hao CUF waumini? kama ni hivyo kwa nini unamuacha huyu CUF kwa sbb anaonekana mnafiki anashirikiana na makafiri CCM! Hawa ni wanasiasa wa mda mrefu ambao wamekua wakitaka Zanzibar ijitenge lakini wakashindwa katika hoja za kisiasa,ndo kipindi kile ikabidi rais achaguliwe ambaye sio mhafidhina akawekwa sheina agombee, na Rais kikwete akaahidi kusimimia muungano pamoja na shein hadi ikaundwa kamati ya kushughulikia kero ya muungano! kwa vile walishindwa wameamua kutumia mwamvuli wa dini! ni hatari sana, ni kama kipindi kile CUF ilivokuwa ikijinasibisha na uislam! Na kila mwenye akili atakubali kuwa hichi kikundi Kina mkono mkubwa kutoka mataifa ya nje, taifa fulani ambalo siku hizi limekua mstari wa mbele kusimamia mataifa kujitenga maadam wana maslahi ya kiuchumi pindi tu taifa hilo likishajitenga.
 
Siamini kabisa wewe ni muislam, naamini kabisa wewe nikikojozi kama vikojozi wenzako, hujawai fika kwenye mihadhara ya muamsho na kuwasikiliza zaidi unachoongea nikilekile wanachoongea vikojozi wenzio

 
kaka mimi ni mwislamu. kama unahoja toa tusitukanane wala mimi sitokutukana. kumbuka shujaa sio yule mwenye nguvu nyingi ila ni yule anaeweza kudhibiti ghadhabu zake.
 
kaka mimi ni mwislamu. kama unahoja toa tusitukanane wala mimi sitokutukana. kumbuka shujaa sio yule mwenye nguvu nyingi ila ni yule anaeweza kudhibiti ghadhabu zake.


Asante, Mkuu, kama nimuislam jaribu kufika kwenye mihadhara au sikiliza kasseti zao ili uelewe policy zao badala ya kuleta mada dhidi ya policy za uamsho, madai kama haya tunayasikia kwa vikojozi, kwahiyo ni vizuri uwasikilize mwenyewe uelewe ukweli

Respect
 
Hawa watu nikawaida yao kutumika ccm imekuwa pia ikiwatumia sana wakati wa kupiga kura, na Cuf nayo inawatumia sana na sasa UAMSHO mara Ponda, na bei yao ni ndogo sana yaani pilau, kofia, kanga, kitenge, Tshirt na ccm haifanyi juhudi ya kuwapa maarifa ya kufikiri ili ifikie malengo yake.
 
Siamini kabisa wewe ni muislam, naamini kabisa wewe nikikojozi kama vikojozi wenzako, hujawai fika kwenye mihadhara ya muamsho na kuwasikiliza zaidi unachoongea nikilekile wanachoongea vikojozi wenzio


mkuu mbona una itikadi kali na maneno yasiyokuwa na tija? Toa hoja sio kutukana.
 
Tatizo moja hawa wa2 sidhani kama wakiambiwa vitu na viongozi wao huwa wanafikiria kwa kina kabla ya kuchukua hatua. Mfano ishu ya mbagala nilitegemea hata yule mtoto wa kislam achukuliwe hatua na waislam. Hivi kwa mfano ukiwa umetoka kazini mara unakuta TV yako ya chumbani imevunjika. unamuuliza mwanao, anakwambia kuwa ameivunja mtoto wa jirani alipokuwa anajaribu kuibeba na kukimbia nayo. kwa kuwa nilimwambia hana nguvu za kuibeba hiyo TV. sasa yeye ndio akaidondosha. Hivi wewe kwa akili zako utaenda kugombana na mzazi wa mtoto wa jirani kweli?. je hautamchukulia mwanao hatua aliyetoa tv ndani?.
 
Tatizo moja hawa wa2 sidhani kama wakiambiwa vitu na viongozi wao huwa wanafikiria kwa kina kabla ya kuchukua hatua. Mfano ishu ya mbagala nilitegemea hata yule mtoto wa kislam achukuliwe hatua na waislam. Hivi kwa mfano ukiwa umetoka kazini mara unakuta TV yako ya chumbani imevunjika. unamuuliza mwanao, anakwambia kuwa ameivunja mtoto wa jirani alipokuwa anajaribu kuibeba na kukimbia nayo. kwa kuwa nilimwambia hana nguvu za kuibeba hiyo TV. sasa yeye ndio akaidondosha. Hivi wewe kwa akili zako utaenda kugombana na mzazi wa mtoto wa jirani kweli?. je hautamchukulia mwanao hatua aliyetoa tv ndani?.

Kama Mzazi wa mtoto anakawaida ya uchokozi, na mtoto wake anapokosea kutakuwa na vitu viwili;

1-Kafundishwa tabia mbaya na wazazi wake
2-Katumwa (kukojoa) au kuvunja tv kwa makusudi

Hii inategemea uhusiano wako na mzazi, hivi karibuni mzazi huyuhuyu, alimzika mtoto wake Bagamoyo kwenye makaburi ya waislam na kuweka misalaba, na pia alichoma qura'n kwa makusudi nk...nk..nk... Bila kuomba msamaha, je kutakuwa na uhusiano mzuri?


 
Kama Mzazi wa mtoto anakawaida ya uchokozi, na mtoto wake anapokosea kutakuwa na vitu viwili;

1-Kafundishwa tabia mbaya na wazazi wake
2-Katumwa (kukojoa) au kuvunja tv kwa makusudi

Hii inategemea uhusiano wako na mzazi, hivi karibuni mzazi huyuhuyu, alimzika mtoto wake Bagamoyo kwenye makaburi ya waislam na kuweka misalaba, na pia alichoma qura'n kwa makusudi nk...nk..nk... Bila kuomba msamaha, je kutakuwa na uhusiano mzuri?



kwa hiyo huyo mzazi kama anaishi nyumba ya jirani na ukute amepangisha. utachukua uamuzi wa kwenda kuharibu na kuchoma nyumba nzima pamoja na wapangaji wengine ikiwemo hata ya baba mwenye nyumba?. kisa una bifu na m2 mmoja?
 
Hawa watu nikawaida yao kutumika ccm imekuwa pia ikiwatumia sana wakati wa kupiga kura, na Cuf nayo inawatumia sana na sasa UAMSHO mara Ponda, na bei yao ni ndogo sana yaani pilau, kofia, kanga, kitenge, Tshirt na ccm haifanyi juhudi ya kuwapa maarifa ya kufikiri ili ifikie malengo yake.

sorry sijazungumzia la Ponda,nazungumzia UAMSHO,yanaweza kuwa yanafanana kidogo kwa kuwa yanahusu kiongozi wa kiislamu lakini nazungumzia dhana nzima ya UAMSHO na harakati zao za kujitenga na Tanzania bara! na pia sio vizuri kutukejeli kuwa sio ndo tunapewa hizo kanga na kofia na CCM, kumbuka hawagawi misikitini au makanisani. tusiharibu mjadala tutoe hoja
 
naomba waislamu tuchangie! kwa wakristo siwakatazi ila najua wengi wenu mkichangia mtaleta kejeli au maneno makali mtawaamisha waislamu hawataweza kunijibu mimi watakua wanajibu kejeli na maneno yenu makali badala ya kujibu hoja zangu. otherwise mchangie vizuri na msitoke nje ya mada hope mumenielewa
 
Muislam anayemuua muislam mwenzake hugeuka kafiri rightaway. Sitashangaa kusikia watu wakiwakana uamsho kwa vile hawajafuata sharia ya Mwenyezi Mungu. Wanataka kujitenga na muungano ingawa wanatumia njia chafu na yenye madhara kwao kwani wataumizana wakati serikali ya muungano iko Dar ikitanua na bosi wake akijirusha ughaibuni na jamaa zake. Tumieni akili jamani mtamalizana na mnachotafuta hamtakipata kwa vile mtawapa jamaa sababu ya kuwavunja vunja viungo.
 
Muislam anayemuua muislam mwenzake hugeuka kafiri rightaway. Sitashangaa kusikia watu wakiwakana uamsho kwa vile hawajafuata sharia ya Mwenyezi Mungu. Wanataka kujitenga na muungano ingawa wanatumia njia chafu na yenye madhara kwao kwani wataumizana wakati serikali ya muungano iko Dar ikitanua na bosi wake akijirusha ughaibuni na jamaa zake. Tumieni akili jamani mtamalizana na mnachotafuta hamtakipata kwa vile mtawapa jamaa sababu ya kuwavunja vunja viungo.

really it is! Sasa sijiskia labda kusema askari kauwa bahati mbaya! hapana kapigwa mapanga kabisa alaf tunakuja kudai tunapigania haki za waislamu wakati tunawauwa wenzetu wenyewe! mwislamu anaefikiria hapa tu panatosha kujiuliza! UAMSHO NI SIASA KABISA WALA SIO ABOUT RELIGION
 
kwa hiyo huyo mzazi kama anaishi nyumba ya jirani na ukute amepangisha. utachukua uamuzi wa kwenda kuharibu na kuchoma nyumba nzima pamoja na wapangaji wengine ikiwemo hata ya baba mwenye nyumba?. kisa una bifu na m2 mmoja?


Kama Judicial System inampendelea jirani kuliko wewe, upouwezakano mkubwa kwa binadamu yoyote kuchukua sheria
mkonono n haya ndiyo yaliyotokea wakati jirani anachoma Qur'an, filamu ya matusi kwa Mtume (S.A.W), kuzika mkiristo makaburi ya waislam na kuweka misalaba hawakuchukuliwa hatua yoyote na hata kikojozi hasingechukuliwa hatuwa ya kisheria kama shinikizo la waislam lisingefanyika
 
really it is! Sasa sijiskia labda kusema askari kauwa bahati mbaya! hapana kapigwa mapanga kabisa alaf tunakuja kudai tunapigania haki za waislamu wakati tunawauwa wenzetu wenyewe! mwislamu anaefikiria hapa tu panatosha kujiuliza! UAMSHO NI SIASA KABISA WALA SIO ABOUT RELIGION

Kama askari alikuwa upande wa maadui nae ni adui hata kama ni raia wa nchi moja au dini yako, yeye amesha kusaliti nae nisawa na adui
 
Kama askari alikuwa upande wa maadui nae ni adui hata kama ni raia wa nchi moja au dini yako, yeye amesha kusaliti nae nisawa na adui

mtume hakuwajua wanafki? aliwauwa? sasa we hukmu ya kumuua mwislamu mwenzako inatoka wapi? alaf nenda kapitie kwenye vitabu vya dini hukmu ya kumuua mwislamu mwenzko kwa maksudi ni straight motoni! hiyo kwa bahati mbaya unaambiwa ufunge miezi miwili! uaskari wake ndo uadui kwa uislamu? ile si kazi tu. kwa hakika kila mmoja wetu atakuja kuulizwa yeye kama yeye kwani kila mtu amepewa akili na uwezo mkubwa wa kufikiria
 
mtume hakuwajua wanafki? aliwauwa? sasa we hukmu ya kumuua mwislamu mwenzako inatoka wapi? alaf nenda kapitie kwenye vitabu vya dini hukmu ya kumuua mwislamu mwenzko kwa maksudi ni straight motoni! hiyo kwa bahati mbaya unaambiwa ufunge miezi miwili! uaskari wake ndo uadui kwa uislamu? ile si kazi tu. kwa hakika kila mmoja wetu atakuja kuulizwa yeye kama yeye kwani kila mtu amepewa akili na uwezo mkubwa wa kufikiria


Kama wewe kweli ni Muislam sio kibaraka, kasome Qur'an 66;9. nimefunga mchezo nakusubiri......
 
Kama wewe kweli ni Muislam sio kibaraka, kasome Qur'an 66;9. nimefunga mchezo nakusubiri......
nimeisoma, je huyo mwislamu mwenzetu mliyemuua mmejua yukoje au sababu yeye tu ni askari? Unakumbuka mkataba wa hudaybia ulisainiwa kati ya nani na nani? Tunaacha kufuata kiigizo chema kutoka kwa mtume tunakurupuka na matokeo yake ni vurugu! mtume angekua hvo huo uislam ungetufikia? we unajua kuwa kuna mtu kipindi cha mtume alikua akivizia nyumbani kwa mtume then akawa anajisaidia mlangoni then anaondoka, mtu alimjua na wala hakukurupuka kumhukumu kupigwa wala kuuwawa bali kila anapochafua anasafisha, je waislamu leo tunaiga mwenendo wa mtume! alaf hata mtume aliambiwa msiwapige wala kuwatoa watu katika majumba yao mpka watakapoanza wao kuwapiga,na ndo maana mtume aliweza kuishi na makafari kupitia mkataba wa hudaybia! na ikitokea kosa kafanya mmoja na sio makafiri kwa pamoja hakukurupuka na kuwahukumu makafiri wote! Aliyemlea mtume baada ya kufarika mama na babu yake alikua mwislamu? mbona waliishi bila tatizo wala mtume hakumhukum mpka anakufa anabaki kumkumbusha atamke shahada? hiyo aya ya 66:9 haikushuka? kwa nini mtume hakumhukumu mjomba wake huyo? ni kwa sbb hakuanzisha vita aliishi nae vizuri.
 
Mimi nijuavyo waislam hawahongwi kofia ama pilau
Ila najua kuna wagalatia wanahongwa gongo ulezi chibiku tu na kutoa kura zao kwa wagalatia mafisadi
Ama kuhusu malengo ya Uamsho hili darasa pana
Walianza na harakati nyingi za kijamii lakini sasa kuna hili Zanzibar kuondokana na ukoloni wa Tanganyika
Kwani ukoloni ? Kwa sababu nia ya Muungano haikua nzuri watanganyika walikua na nia ya kuimeza zenj
Wewe fikiria kitu kimoja tu kuna sababu gani za kufanya suala la mafuta kuingizwa kitapeli ndani ya mambo ya muungano?
Na wakati huo zanzibar hawafaidiki na gas ya songo songo ?
Hawafaidiki na madini ya dhahabu
Kwa nin tanganyika wasiwaachie zenji kuchimba mafuta yao ?
Jee inawezekana tuhamishe makao makuu ya serikali ya muungano yawepo zenji?
Mambi ni mengi na kazi ya uamsho ni hii kuwafahamisha waislam kuwa muungano sio
Mila na utamaduni wa nchi hizi ni tofauti
Mfumo wa maisha wa nchi hizi ni tofauti
Tabia za watu wake pia ni tofauti
Marafiki wa tanganyika pia ni tofauti na wale zenj
Hivyo muungano ulikua ni kasa la kulazimishwa kihistoria
UAMSHO WANAAMSHA. Na support yao ni kubwa kuliko unavodhani wapo wabunge police mawaziri majaji wakulima wafanyakazi bila ya kujali itikadi zao wote wanasema Zanzibar kwanza

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom