mngony
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 5,193
- 6,381
mimi ni muislamu lakini nimeshtukia hichi kikundi cha UAMSHO kuwa ni kikundi cha kisiasa kinachowatumia waislamu bila wenyewe kujijua! Uamsho wanataka kujitenga na bara wakisingizia huku ni makafiri, je huku hakuna waislamu? Kwa nini wamuue askari ambaye ni Muislamu mwenzao? Katika uislam si haramu kumwaga damu ya muislamu mwenzako? hawa waislamu gani? kwa nini watoe taarifa za kuwa kiongozi wao ametekwa na hali ilikua haijulikani yuko wapi na kama ametekwa au la!? dereva anasema alishuka akapanda gari lingine na alikua akiwasiliana na watu, huko ndo kutekwa tena bila hata purukushani tena gari limekuja taratibu! na hilo gari lake mwanzo alikua akiendesha mwenyewe kwa nini alimua kumpisha dereva wake?Huo si uongo ambao ni haramu katika uislamu! Kwa nini zichomwe ofisi za CCM peke yake, mbona CUF nayo ni serikali pia? je CCM huko zanzibar viongozi wao makafiri? je hao CUF waumini? kama ni hivyo kwa nini unamuacha huyu CUF kwa sbb anaonekana mnafiki anashirikiana na makafiri CCM! Hawa ni wanasiasa wa mda mrefu ambao wamekua wakitaka Zanzibar ijitenge lakini wakashindwa katika hoja za kisiasa,ndo kipindi kile ikabidi rais achaguliwe ambaye sio mhafidhina akawekwa sheina agombee, na Rais kikwete akaahidi kusimimia muungano pamoja na shein hadi ikaundwa kamati ya kushughulikia kero ya muungano! kwa vile walishindwa wameamua kutumia mwamvuli wa dini! ni hatari sana, ni kama kipindi kile CUF ilivokuwa ikijinasibisha na uislam! Na kila mwenye akili atakubali kuwa hichi kikundi Kina mkono mkubwa kutoka mataifa ya nje, taifa fulani ambalo siku hizi limekua mstari wa mbele kusimamia mataifa kujitenga maadam wana maslahi ya kiuchumi pindi tu taifa hilo likishajitenga.