Twaha Kiduku mpiganaji mtulivu, mchokozi wa ngumi zitakazo kuweka kwenye kumi na nane yake

Leslie Mbena

JF-Expert Member
Nov 24, 2019
207
677
TWAHA KIDUKU: MPIGANAJI BORA WA NDONDI KWA SASA TANZANIA.

Leo 21:30 hrs 29/08/2020

Twaha Kiduku mpiganaji mtulivu,mchokozi wa ngumi zitakazo kuweka kwenye kumi na nane yake ambayo itakukutanisha na jebu moja matata ya mkono wa kulia toka kwenye mwili uliojaa kwa mazoezi ya tofali na kusukuma tairi ya treka kupandisha Mlima Uluguru kupitia barabara ya Mji Mkuu,rock garden,Bahati Camp na kuteremka hadi Masuka Village kuelekea Masika kati kati ya Mji wa Morogoro.

Katika pambano lake na Dulla Mbabe, nyota nyingine katika ndondi za Tanzania, Twaha Kiduku alionyesha utulivu na kurusha makonde yake ya kulia na kushoto yaliyokuwa yakitua kwenye kichwa cha Dulla Mbabe, yakimsukuma Dulla Mbabe hadi kwenye kamba za ulingo katika sekunde za mwanzo hata dakika za mwisho za pambano,

Twaha Kiduku aliweza kuendeleza machachari yake ya awali hadi raundi ya 12 baina yake na Dulla Mbabe ambaye ni mrefu kiumbo na kuweza kupenyeza masumbwi ya kujibu mapigo pale shambulizi lilipoelekea kuvuruga utulivu wake,Ustadi wa Twaha Kiduku ulionekana pale alipovurumisha makonde 435 kulinganisha na 429 ya Dulla Mbabe na asilimia 35 ya makonde yake yalifika mahala pake kulinganisha na asilimia 19 ya mpinzani wake.

- Twaha Kiduku na staili ya Upiganaji wa Mjerumani.

Wajerumani ni watu wenye kutumia nguvu, kama umewahi kumuona mpiganaji "Brock lesnar" akiwaangamiza wapinzani wake kwenye wwe na ufc, Twaha Kiduku ndiye mwenye kutumia mfumo uleule wa Wajerumani katika kumchakaza mpinzani wake yeyote anayetokea mbele yake,

Kwa Tanzania, Twaha Kiduku ni mfano wa Rashid "Snake boy" Matumla ni muhimu kumtaja Rashid Matumla kama kipimo, standard au "measuring stick" katika ngumi za Tanzania,kwa mchambuzi wa ngumi,Yassin Ustadh atakubaliana nami kuwa rekodi ya Twaha Kiduku ya Ushindi wa mechi 13,kupoteza mechi 6 na draw 1 hii ni rekodi nzuri ya Ushindi na kupigwa ni sehemu ya changamoto ya mchezo.

Mada Maugo amewahi kupigwa na Francis Cheka,Francis Cheka amewahi kupigwa na Thomas Mashali,lakini bado Twaha Kiduku mwenye uwezo wa kutupa ngumi 221 akiwa ulingoni kunamfanya kuwa mpiganaji bora kabisa wa ngumi kwa sasa,

Katika ndondi ukipigwa idadi ya ngumi 221 zikatua bala bala katika paji lako la uso,hiyo ni idadi kubwa katika historia ya masumbwi, hali inayoweza kukufanya kujiuliza kila mara ni vipi Twaha Kiduku anaweza kupata nafasi ya kupiga idadi hiyo kubwa ya makonde katika paji lako la uso!?

Kwa takwimu ya jumla ya makonde 858 yanayoweza kutupwa ulingoni baina ya watu wawili,makonde 450 yakimkosa kila mtu na makonde 221 yakifika katika mwili wako,hiki ndicho kinachoweza kushangaza mpiganaji yeyote na kumpa salute yule aliyeweza kupenyeza makonde 221 katika paji lake la uso,

Nimalizie kwa kusema Twaha Kiduku si bondia tena wa kuachia kidevu chake kichakazwe na bondia yeyote na kwa sasa ni wakati sahihi wa kupambana na Bondia bora Hassan Mwakinyo,Twaha Kiduku anatisha, Moja ya sababu ya kwa nini Twaha Kiduku anatisha sana ni kwa sababu hadharau mpinzani na siku zote anataka kukabiliana na mabondia bora mfano wa Dulla Mbabe ambaye amepambana nae na baada ya pambano amekuwa bora na ndiyo maana Twaha Kiduku ni mahiri sana.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master's in Leadership and Management.

-Research; Assessing Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Nimemuangalia Yuko vizuri, akiwa ulingoni
Hachoki yeye humfuata mpinzani, huku ameweka gadi na kuinama halafu anapiga makonde ya kushtukiza anakuwa kama the "smokin' Joe Frazier, japo stailI akikutana na hard puncher anakalishwa mapema sana
 
Itakuwa bora zaidi Twaha Kiduku aende majuu akapigane huko kama mara mbili hivi akishinda zote ndio aje kupigana na Mwakinyo , mimi mwenyewe nitaenda kuangalia live . Sio sawa kumkutanisha Kiduku sasa hivi na Mwakinyo zaidi kumkutanisha sasa hivi itakuwa haya mambo yetu ya kibongo aliye juu mshushe chini .

Ndivyo wenzetu wakenya wanavyofanya wanabebana sana kwenda kimataifa ingawa Kenya hubebana sana kwenye riadha, kandanda , ndondi si sana siku hizi wamerudi nyuma so Tz kama wasanii wa bongi flavor wanavyopasau anga Africa na Dunia , ni muda wa wanamasumbwi tuwaone mkipanda majukwaa makubwa kule ambapo Tsh 200,000 wao wanaiona ni $ 100.
 
Sasa wapigane na hassan mwakinyo wakati uzito wao tofauti yaan umeeleza vizuri tu lkn ulichoongea mwishoni umeharibu
 
NILIFANYA UCHAMBUZI HUU KABLA YA PAMBANO...

Boxing analysis Kati ya DULLA vs TWAHA !

Kwa upande wangu ni kama ifuatavyo;

Dulla Mbabe : Ana advantage ya urefu..bondia mrefu anapopigana na mfupi automatically style inakua hii...Mrefu anakua "backpedal " na mfupi anacheza "first" au wanasema "be first ".. Kwa sababu mfupi hawezi kumpiga mrefu akiwa mbali lazima aingie ndani.
Kwa hiyo kimkakati wa kupambana bondia mrefu anatumia "jab" (ngumi ya utangulizi) kama ulinzi lkn pia kama silaha ya kuanzisha mashambulizi.

Twaha ni mfupi kidogo kuliko Dulla lkn ana kasi katika kutupa ngumi.. Ana speed ya miguu kuweza kuingia ,kushambulia na kutoka..huyu ni "swarmmer boxer " ...ngumi yake kuu ni upper cut( Ngumi inayotoka nyuma na kuingia uvunguni mwa mpinzani wake..lkn lazima amshushe kimo kwa kupiga cross punch kwenye mbavu.

Mwisho! Kwa kua wote ni "orthodox stance boxer" (wanatanguliza mguu na ngumi ya kushoto"...na pia Dulla ni mrefu lkn slow ina maana pomoja na urefu wake lkn uwezekano wa kupigwa ni mkubwa.

Urefu wa Dulla ungelimsaidia kama angekua "Southpaw stance boxer" (anaetanguliza mguu na ngumi ya kulia) Kwamba Hamidu asingeliweza kuingia ndani kirahisi na kupiga na kutoka.


NB; UCHAMBUZI NILIUFANYA KWENYE GROUP LA WhatsApp .
 
"Kiduku ya Ushindi wa mechi 13,kupoteza mechi 6 na draw 1 hii ni rekodi nzuri ya Ushindi na kupigwa ni sehemu ya changamoto ya mchezo."

Hamna Bondia hapo. Eti rekodi nzuri hapa mwandishi ameonesha mahaba ya kifala
Yaani 46% ndio ushindi halafu anasifiwa. Ni ujinga. Atauawa, mwambieni akaze tako
 
Joe frazier ni mmoja ya my best boxer. Kiduku hana hard chin kama smokin joe. Siyo hard puncher like him. Though ana speed na anajitahidi sana kukwepa.

Nimemuangalia Yuko vizuri ,,akiwa ulingoni
Hachoki yeye humfuata mpinzanI ,, huku ameweka gadi na kuinama halafu anapiga makonde ya kushtukiza anakuwa kama the "smokin' Joe Frazier ,,,japo stailI akikutana na hard puncher anakalishwa mapema sana
 
Wewe ndo utakuwa twaha kiduku mwenyewe si kwa sifa hizi na mapambio. Records za jamaa ni za hovyo wewe unasema ni best records? Kweli? Mbona unatufanya wote hatujui boxing?

Jamaa ana uzuri wa speed na pumzi lakini si hard puncher. Na pia hana hard chin. Hayo mapambano 6 amepigwaje ?tena angalau ingekuwa 6 katika 40+. But mapambano sita katika 20 na moja draw. He isnt that best.
 
NILIFANYA UCHAMBUZI HUU KABLA YA PAMBANO...

Boxing analysis Kati ya DULLA vs TWAHA !

Kwa upande wangu ni kama ifuatavyo;

Dulla Mbabe : Ana advantage ya urefu..bondia mrefu anapopigana na mfupi automatically style inakua hii...Mrefu anakua "backpedal " na mfupi anacheza "first" au wanasema "be first ".. Kwa sababu mfupi hawezi kumpiga mrefu akiwa mbali lazima aingie ndani.
Kwa hiyo kimkakati wa kupambana bondia mrefu anatumia "jab" (ngumi ya utangulizi) kama ulinzi lkn pia kama silaha ya kuanzisha mashambulizi.

Twaha ni mfupi kidogo kuliko Dulla lkn ana kasi katika kutupa ngumi.. Ana speed ya miguu kuweza kuingia ,kushambulia na kutoka..huyu ni "swarmmer boxer " ...ngumi yake kuu ni upper cut( Ngumi inayotoka nyuma na kuingia uvunguni mwa mpinzani wake..lkn lazima amshushe kimo kwa kupiga cross punch kwenye mbavu.

Mwisho! Kwa kua wote ni "orthodox stance boxer" (wanatanguliza mguu na ngumi ya kushoto"...na pia Dulla ni mrefu lkn slow ina maana pomoja na urefu wake lkn uwezekano wa kupigwa ni mkubwa.

Urefu wa Dulla ungelimsaidia kama angekua "Southpaw stance boxer" (anaetanguliza mguu na ngumi ya kulia) Kwamba Hamidu asingeliweza kuingia ndani kirahisi na kupiga na kutoka.


NB; UCHAMBUZI NILIUFANYA KWENYE GROUP LA WhatsApp .
Uchambuzi mzuri Sana mkuu
 
NILIFANYA UCHAMBUZI HUU KABLA YA PAMBANO...

Boxing analysis Kati ya DULLA vs TWAHA !

Kwa upande wangu ni kama ifuatavyo;

Dulla Mbabe : Ana advantage ya urefu..bondia mrefu anapopigana na mfupi automatically style inakua hii...Mrefu anakua "backpedal " na mfupi anacheza "first" au wanasema "be first ".. Kwa sababu mfupi hawezi kumpiga mrefu akiwa mbali lazima aingie ndani.
Kwa hiyo kimkakati wa kupambana bondia mrefu anatumia "jab" (ngumi ya utangulizi) kama ulinzi lkn pia kama silaha ya kuanzisha mashambulizi.

Twaha ni mfupi kidogo kuliko Dulla lkn ana kasi katika kutupa ngumi.. Ana speed ya miguu kuweza kuingia ,kushambulia na kutoka..huyu ni "swarmmer boxer " ...ngumi yake kuu ni upper cut( Ngumi inayotoka nyuma na kuingia uvunguni mwa mpinzani wake..lkn lazima amshushe kimo kwa kupiga cross punch kwenye mbavu.

Mwisho! Kwa kua wote ni "orthodox stance boxer" (wanatanguliza mguu na ngumi ya kushoto"...na pia Dulla ni mrefu lkn slow ina maana pomoja na urefu wake lkn uwezekano wa kupigwa ni mkubwa.

Urefu wa Dulla ungelimsaidia kama angekua "Southpaw stance boxer" (anaetanguliza mguu na ngumi ya kulia) Kwamba Hamidu asingeliweza kuingia ndani kirahisi na kupiga na kutoka.


NB; UCHAMBUZI NILIUFANYA KWENYE GROUP LA WhatsApp .
MKUU screpa Unazungumziaje Pambano La Leo La TK na DM??
 
NILIFANYA UCHAMBUZI HUU KABLA YA PAMBANO...

Boxing analysis Kati ya DULLA vs TWAHA !

Kwa upande wangu ni kama ifuatavyo;

Dulla Mbabe : Ana advantage ya urefu..bondia mrefu anapopigana na mfupi automatically style inakua hii...Mrefu anakua "backpedal " na mfupi anacheza "first" au wanasema "be first ".. Kwa sababu mfupi hawezi kumpiga mrefu akiwa mbali lazima aingie ndani.
Kwa hiyo kimkakati wa kupambana bondia mrefu anatumia "jab" (ngumi ya utangulizi) kama ulinzi lkn pia kama silaha ya kuanzisha mashambulizi.

Twaha ni mfupi kidogo kuliko Dulla lkn ana kasi katika kutupa ngumi.. Ana speed ya miguu kuweza kuingia ,kushambulia na kutoka..huyu ni "swarmmer boxer " ...ngumi yake kuu ni upper cut( Ngumi inayotoka nyuma na kuingia uvunguni mwa mpinzani wake..lkn lazima amshushe kimo kwa kupiga cross punch kwenye mbavu.

Mwisho! Kwa kua wote ni "orthodox stance boxer" (wanatanguliza mguu na ngumi ya kushoto"...na pia Dulla ni mrefu lkn slow ina maana pomoja na urefu wake lkn uwezekano wa kupigwa ni mkubwa.

Urefu wa Dulla ungelimsaidia kama angekua "Southpaw stance boxer" (anaetanguliza mguu na ngumi ya kulia) Kwamba Hamidu asingeliweza kuingia ndani kirahisi na kupiga na kutoka.


NB; UCHAMBUZI NILIUFANYA KWENYE GROUP LA WhatsApp .
Mabondia wengi wa Tanzania hawatumii techniques katika kupambana ndio maana mapambano yao mengi hayavutii!

Pambano lao litaamuliwa na uchovu na chin!

Twaha ana chin nzuri, ana nguvu na hachoki haraka ingawa hayupo vizuri technically, hana accuracy, hana movement, hana defence

Dullah ana nguvu lakini hana chin nzuri na anachoka haraka, technically hayupo vizuri, hana movement, defence pia hana accuracy!

Twaha ana nafasi zaidi kuliko Dullah!
 
Back
Top Bottom