Tuwakemee sana kina dada wanaozaa na kutelekeza watoto kwa wazazi wao

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,486
Asalam Alekhu wanabodi,

Natambua uwepo wa wanaMMU wenye kutoa ushauri mzuri, kejeli, matusi, mzaha, madongo, like, bila kuwasahau wa mipasho. Itifaki imezingatiwa.

Kuna hili jambo limeshamiri kwa kiasi fulani kwenye jamii zetu ambalo kiukweli siyo zuri na ingependeza kina dada wenye tabia hizo kujitafakari, na wale ambao wana mpango wa kufanya hivyo pia wasifanye hivyo.

Unakuta mdada anazaa hata watoto 6 kila mtoto ana baba yake, na akishapata ujauzito fainali kuanzia kulea mimba hadi mtoto akue anaenda kumalizia nyumbani kwa wazazi, na mtoto akishaweza kucheza tu, anamwachia mama amtunze, yeye anaenda huko kutega tena, hadi anafikisha hata watoto 6 na unakuta bibi yao ndo anahangaika kila kitu na hao watoto hadi shule!

Hivi mdada kama huyo anafaa apewe jina gani maana siyo ustaarabu hata kidogo. Hata kama ni watoto wawili, hayo bado siyo maadili. Na sitakubaliana na anayesema baba zao wanakataa mimba, baba 6 wote wakatae mimba? Halafu kina baba hawakatai mimba bila sababu tena za msingi.

Halafu kuna mitoto mingine inaletwa kwa staili hiyo, unakuta ina mitabia ambayo unaweza ukatafuta kijiji kizima mwenye tabia hiyo asiwepo. Sote kwa pamoja tukemee kina dada wenye tabia za aina hizi. Wapo watoto sasahivi wanamaliza hata chuo kikuu na hawawajui baba zao, na sio kwamba hawapo hai, bali tatizo ni hawa dada zetu.

Nawatakia Jumapili njema wote.
 
mbona kuna mbaba humu JF anamiliki benki mbili sijui na vitu gani vingine, anataka kutelekeza mwanae kisa kamchoka mkewe...
labda huyo mwanamke alizaa na mume wa mtu kisa ana benk akapeleka dudu lake kutegesha mtoto ili apate mali
 
Kwa hiyo bora wapeleke watoto kwa mama zao wakalelewe au bora watoe mimba ili tuwaone wema? naomba nijibu mleta mada.

Mara nyingi baadhi ya wanawake wakishazalishwa na kuachwa, wanakuwa na hofu ya kuingia kwenye mahusiano mapya, na wanakuwa wanachagua chagua sana ili tu kupata atakayedumu nae, bahati mbaya ya wengi unakuta anaangukia kule kule anazalishwa na kuachwa tena.

Pia baadhi ya wanaume ni sababu, unajua kabisa huyu mwanamke ana mtoto na mnaanzisha mahusiano labda niseme unakuwa umemaanisha kuwa atakuwa mke, lakini kutokana na inavyochukuliwa kuwa mwanamke aliyezaa anaweza kurudiana na aliyezaa nae inapelekea kutokuwa na imani na mwanamke yule au kupewa ushauri unaopelekea kuahirisha malengo ya kuwa nae, mwanamke anajikuta anaachwa kwa mara nyingine.

Wanawake pia baadhi yetu, baada ya kuachwa na kuzalishwa kujiamini kunapotea kabisa, kutokana na hofu wanayokuwa nayo baadhi hujikuta anaona ni bora kumzalia huyu aliyempata ili kumfanya awe wake milele kumbe mwenzie hana hata future nae, anajikuta anaachwa na hana uwezo wa kulea huyo/hao watoto, ndo watoto wanapelekwa kwa bibi sasa.

Note: Haifurahishi kujaza watoto kwa mama ila ni bora kuliko kutoa mimba na kuua viumbe visivyo na hatia.

Wanawake wanaofanya wanatakiwa kuelemishwa sio kukemewa, waelimishwe jinsi ya kuithamini miili yao, pia elimu ya uzazi wa mpango wapewe, asilimia kubwa now tunajua kuhusu uzazi wa mpango ila si wote. Waache kujirahisi au kumaliza stress kwa kuingia kwenye mahusiano mapya yanayopelekea kuongeza mizigo zaidi kwenye familia
 
Kwa hiyo bora wapeleke watoto kwa mama zao wakalelewe au bora watoe mimba ili tuwaone wema? naomba nijibu mleta mada.

Mara nyingi baadhi ya wanawake wakishazalishwa na kuachwa, wanakuwa na hofu ya kuingia kwenye mahusiano mapya, na wanakuwa wanachagua chagua sana ili tu kupata atakayedumu nae, bahati mbaya ya wengi unakuta anaangukia kule kule anazalishwa na kuachwa tena.

Pia baadhi ya wanaume ni sababu, unajua kabisa huyu mwanamke ana mtoto na mnaanzisha mahusiano labda niseme unakuwa umemaanisha kuwa atakuwa mke, lakini kutokana na inavyochukuliwa kuwa mwanamke aliyezaa anaweza kurudiana na aliyezaa nae inapelekea kutokuwa na imani na mwanamke yule au kupewa ushauri unaopelekea kuahirisha malengo ya kuwa nae, mwanamke anajikuta anaachwa kwa mara nyingine.

Wanawake pia baadhi yetu, baada ya kuachwa na kuzalishwa kujiamini kunapotea kabisa, kutokana na hofu wanayokuwa nayo baadhi hujikuta anaona ni bora kumzalia huyu aliyempata ili kumfanya awe wake milele kumbe mwenzie hana hata future nae, anajikuta anaachwa na hana uwezo wa kulea huyo/hao watoto, ndo watoto wanapelekwa kwa bibi sasa.

Note: Haifurahishi kujaza watoto kwa mama ila ni bora kuliko kutoa mimba na kuua viumbe visivyo na hatia.

Wanawake wanaofanya wanatakiwa kuelemishwa sio kukemewa, waelimishwe jinsi ya kuithamini miili yao, pia elimu ya uzazi wa mpango wapewe, asilimia kubwa now tunajua kuhusu uzazi wa mpango ila si wote. Waache kujirahisi au kumaliza stress kwa kuingia kwenye mahusiano mapya yanayopelekea kuongeza mizigo zaidi kwenye familia
Asanteeee
 
Kwa hiyo bora wapeleke watoto kwa mama zao wakalelewe au bora watoe mimba ili tuwaone wema? naomba nijibu mleta mada.

Mara nyingi baadhi ya wanawake wakishazalishwa na kuachwa, wanakuwa na hofu ya kuingia kwenye mahusiano mapya, na wanakuwa wanachagua chagua sana ili tu kupata atakayedumu nae, bahati mbaya ya wengi unakuta anaangukia kule kule anazalishwa na kuachwa tena.

Pia baadhi ya wanaume ni sababu, unajua kabisa huyu mwanamke ana mtoto na mnaanzisha mahusiano labda niseme unakuwa umemaanisha kuwa atakuwa mke, lakini kutokana na inavyochukuliwa kuwa mwanamke aliyezaa anaweza kurudiana na aliyezaa nae inapelekea kutokuwa na imani na mwanamke yule au kupewa ushauri unaopelekea kuahirisha malengo ya kuwa nae, mwanamke anajikuta anaachwa kwa mara nyingine.

Wanawake pia baadhi yetu, baada ya kuachwa na kuzalishwa kujiamini kunapotea kabisa, kutokana na hofu wanayokuwa nayo baadhi hujikuta anaona ni bora kumzalia huyu aliyempata ili kumfanya awe wake milele kumbe mwenzie hana hata future nae, anajikuta anaachwa na hana uwezo wa kulea huyo/hao watoto, ndo watoto wanapelekwa kwa bibi sasa.

Note: Haifurahishi kujaza watoto kwa mama ila ni bora kuliko kutoa mimba na kuua viumbe visivyo na hatia.

Wanawake wanaofanya wanatakiwa kuelemishwa sio kukemewa, waelimishwe jinsi ya kuithamini miili yao, pia elimu ya uzazi wa mpango wapewe, asilimia kubwa now tunajua kuhusu uzazi wa mpango ila si wote. Waache kujirahisi au kumaliza stress kwa kuingia kwenye mahusiano mapya yanayopelekea kuongeza mizigo zaidi kwenye familia
Well said. Kwani ufanye mapenzi hadi upachikwe mimba kabla ya ndoa? Note that mwanamke ndiye anapaswa kuwa makini zaidi maana mwanaume akishaharibu kwa kukusjtdia ama kutokusudia, anaweza akala kona. Kwanini uzini? Unafanya dhambi mara 6 usingizie kukataliwa? Kuwaelimisha ni kwamba waache kabisa kuzini na uzinzi.
 
Asalam Alekhu wanabodi, natambua uwepo wa wanaMMU wenye kutoa ushauri mzuri, kejeli, matusi, mzaha, madongo, like, bila kuwasahau wa mipasho. Itifaki imezingatiwa.

Kuna hili jambo limeshamiri kwa kiasi fulani kwenye jamii zetu ambalo kiukweli siyo zuri na ingependeza kina dada wenye tabia hizo kujitafakari, na wale ambao wana mpango wa kufanya hivyo pia wasifanye hivyo.

Unakuta mdada anazaa hata watoto 6 kila mtoto ana baba yake, na akishapata ujauzito fainali kuanzia kulea mimba hadi mtoto akue anaenda kumalizia nyumbani kwa wazazi, na mtoto akishaweza kucheza tu, anamwachia mama amtunze, yeye anaenda huko kutega tena, hadi anafikisha hata watoto 6 na unakuta bibi yao ndo anahangaika kila kitu na hao watoto hadi shule!

Hivi mdada kama huyo anafaa apewe jina gani maana siyo ustaarabu hata kidogo. Hata kama ni watoto wawili, hayo bado siyo maadili. Na sitakubaliana na anayesema baba zao wanakataa mimba, baba 6 wote wakatae mimba? Halafu kina baba hawakatai mimba bila sababu tena za msingi.

Halafu kuna mitoto mingine inaletwa kwa staili hiyo, unakuta ina mitabia ambayo unaweza ukatafuta kijiji kizima mwenye tabia hiyo asiwepo. Sote kwa pamoja tukemee kina dada wenye tabia za aina hizi. Wapo watoto sasahv wanamaliza hata chuo kikuu na hawawajui baba zao, na co kwamba hawapo hai, bali tatizo ni hawa dada zetu.

Nawatakia j2 njema wote.
''kumlaumu punda na kumsahau mpanda punda ni kutomjali punda'' kupata mimba na kuilea mimba ni kazi ya watu wawili, yaani mwanamke na mwanaume. Lakini kwanini kulea mtoto kwako wewe kuwe ni jukumu pekee kwa mama wa mtoto huyo? TUNAKATAA MIMBA, TUNATELEKEZA FAMILIA, [wengine wapo humu humu jf] Sasa na wao wafanye nini sasa na ikiwa upendo wa kweli na msaada mtakatifu upo kwa mama yake tu... haya acheni mabibi wawaleleeni watoto zenu sasa.
 
''kumlaumu punda na kumsahau mpanda punda ni kutomjali punda'' kupata mimba na kuilea mimba ni kazi ya watu wawili, yaani mwanamke na mwanaume. Lakini kwanini kulea mtoto kwako wewe kuwe ni jukumu pekee kwa mama wa mtoto huyo? TUNAKATAA MIMBA, TUNATELEKEZA FAMILIA, [wengine wapo humu humu jf] Sasa na wao wafanye nini sasa na ikiwa upendo wa kweli na msaada mtakatifu upo kwa mama yake tu... haya acheni mabibi wawaleleeni watoto zenu sasa.
kwanini wazini ama wafanye mapenzi kabla ya ndoa?
 
Wanaume nanyi msikimbie mimba zenu
yaani kubishana huku ni sawa na kutaka kukata chuma kwa meno mwisho wa siku meno yataumia. Stress 90% zinakuwa kwa mwanamke. Na wanawake wengine hupenda iwe hivyo maana kuna wengine hushindana kwenye tabia chafu.
 
''kumlaumu punda na kumsahau mpanda punda ni kutomjali punda'' kupata mimba na kuilea mimba ni kazi ya watu wawili, yaani mwanamke na mwanaume. Lakini kwanini kulea mtoto kwako wewe kuwe ni jukumu pekee kwa mama wa mtoto huyo? TUNAKATAA MIMBA, TUNATELEKEZA FAMILIA, [wengine wapo humu humu jf] Sasa na wao wafanye nini sasa na ikiwa upendo wa kweli na msaada mtakatifu upo kwa mama yake tu... haya acheni mabibi wawaleleeni watoto zenu sasa.


kweli kabisa.Wanaume bhanaaa
 
yaani kubishana huku ni sawa na kutaka kukata chuma kwa meno mwisho wa siku meno yataumia. Stress 90% zinakuwa kwa mwanamke. Na wanawake wengine hupenda iwe hivyo maana kuna wengine hushindana kwenye tabia chafu.
Duh haya mkuu
 
Mimi siwalaumi hata kidogo dada na shangazi zetu kwa kufanya hivyo. Hicho wanachofanya ni matokeo ya ujinga na umasikini.

Wengi wanaofanya hivyo ni wale wanaotokea katika jamii au maeneo duni (Mfano uswahilini, vijijini n.k). Pia watu ambao hawakupata fursa ya kuelimika. Siamini mtu mwenye elimu ya astashahada anaweza kufanya hivyo.

Tusiumizwe na matokeo ya mambo bali tujielekeze katika msingi wa Tatizo. Tuna maadui watatu ujinga, maradhi na umasikini. Tuwekeze Muda, nguvu, akili, weledi, ujuzi na maarifa ili kuwaondoa maadui hao.
 
Back
Top Bottom