Tuwaeleweje wasiomuunga mkono Magufuli?

Msulunje

Member
Oct 6, 2015
67
35
Vyombo vingi vya habari vimekuwa vikipokea pongezi za wananchi kutoka kila pembe ya Tanzania wakiunga mkono hotuba ya Rais John Magufuli aliyoitoa wakati akizindua Bunge la 11 Ijumaa iliyopita.

Walio wengi wameguswa na hotuba hiyo, wakisema inatoa matumaini makubwa kwa Watanzania na inathibitisha kwamba Rais Magufuli, kama alivyosema mwenyewe, hakutoa ahadi zilizolenga kujipatia kura tu wakati wa kampeni, bali kuhakikisha anazitekeleza kwa vitendo kwa faida ya Watanzania.
Hata hivyo, tunaona katika mitandao ya kijamii na hata kwenye vyombo vya habari baadhi ya Watanzania wachache wakionekana kutomuunga mkono Rais, na wengine wakionekana wazi kuwaunga mkono wabunge waliofanya kitendo cha aibu Ijumaa iliyopita cha kupiga kelele, kuzomea na kususa hotuba ya Rais Magufuli.

Baadhi ya vitabu vya dini vinafundisha kwamba binadamu ana njia mbili; ama ile anayoitaka Mwenyezi Mungu ambaye ndiye aliyemuumba au ya shetani. Ni kwa muktadha huo, tunaungana na kauli ya Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliyekaririwa na vyombo vya habari likiwemo gazeti hili jana, akisema kwamba mtu yeyote anayempinga Rais Magufuli, maana yake ni kwamba atakuwa unaunga mkono mafisadi, wala rushwa na wabadhirifu.

Katika maoni yake, Zitto alisema mtu anayepinga ufisadi, uzembe, ubadhirifu, uvivu na rushwa hawezi kumzomea Rais Magufuli au kumpinga kwa namna moja au nyingine badala ya kumuunga mkono. Zitto alifafanua kwamba mtu wa aina hiyo kwa hali yoyote atakuwa ana maslahi binafsi na mafisadi na hataki mabadiliko chanya.

Zitto akaenda mbali kwa kusema kwamba huu ndio wakati ambao Watanzania watawajua watu ambao wapo upande wa mafisadi au upande wa wananchi. Hata sisi tunajiuliza kwamba wanaompinga Magufuli wanataka nini hasa?

Je, wanataka tuendelee kuwa taifa ambalo matajiri hawalipi kodi isipokuwa wanaokamuliwa zaidi ni watu masikini, wenye kipato cha chini na wafanyakazi? Je, wanataka watu waliouziwa viwanda na mashamba waendelee kuyahodhi hata kama wameshindwa kuyaendeleza kwa mujibu wa mikataba?

Yaani wanachukia dhana nzima ya kufufua viwanda vya zamani na kuanzisha vipaya? Je, wanataka tuendelee na watendaji serikalini wasiowajibika ipasavyo ambao wamegeuza sekta ya umma kuwa sehemu ya kuchuma badala ya kuitumikia kwa faida ya wananchi wote?

Wanakataa asipambane na wala rushwa, wanataka alee wazembe katika utumishi wa umma na pia wanataka asizibe mianya ya uchakachuaji wa fedha za umma? Zitto, licha ya kuwa kiongozi wa chama cha upinzani, alisema uzalendo unamtaka kumuunga mkono Rais katika vita dhidi ya ufisadi na kusimamia ustawi wa watanzania, hususan wanyonge. Na sisi swali letu kwa wanaoonekana kutokuwa upande wa rais ni hili. Je, uzalendo wao ni kuunga mkono kitu gani?

Baadhi ya watu hawa, kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakijinadi kwamba wanachukia ufisadi. Je, sasa wanaposhindwa kuunga mkono rais anayeahidi kupambana na ufisadi tuwaeleweje?

SOURCE: Habari leo online
 
Hotuba ya Magufuli ina nini kipya? Sethi Benjamini alikufa kwa kutembea kilometer kibao kuunga mkono hotuba ya JKN kuhusu Azimio la Arusha! Huyu ambaye ameingizwa madaraka kwa mtutu wa Bunduki na Wizi wa Kura wamuunge Mkono kwa lipi? Futuhi la Vitanda? Kutekeleza Sera za Africa Mashariki kuhusu Safari za Nje? Maisha ya Watanzania kuwa Mazuri ghafla? au Umeme wa power bank?
 
Ndugu watanzania wenzangu, kumekuwa na mijadala ambayo mingine ni kumkatisha tamaa rais wetu JPM, najiuliza hivi tunahitaji rais wa aina gani. Huyu ndugu ameonesha nia dhahiri ya kupambana na kuipeleka Tanzania katika hali bora zaidi, kinachotakiwa ni kumuunga mkono na kumpa moyo, nasikitika kuona baadhi yetu wakigeuka kuwa watabiri kuwa ooo huyu atakwama nk nk, tumwache afanye kazi na tumpe ushirikiano, bla bla hazitatusaidia
 
Tumuunge Mkono kwa Mauaji ya Kamanda Mawazo? au Katibu wa Madereva? Home shopping Centre watafungwa kwa kukwepa kodi?
 
Hatuhungi mkono porojo, kila mtu anaweza kuongea, na uhalali wa yeye kuwa hapio na kuongea unatoka wapi? angekuwa msafi asingekubali kukalia kiti kisicho chake
 
Vyombo vingi vya habari vimekuwa vikipokea pongezi za wananchi kutoka kila pembe ya Tanzania wakiunga mkono hotuba ya Rais John Magufuli aliyoitoa wakati akizindua Bunge la 11 Ijumaa iliyopita.
Walio wengi wameguswa na hotuba hiyo, wakisema inatoa matumaini makubwa kwa Watanzania na inathibitisha kwamba Rais Magufuli, kama alivyosema mwenyewe, hakutoa ahadi zilizolenga kujipatia kura tu wakati wa kampeni, bali kuhakikisha anazitekeleza kwa vitendo kwa faida ya Watanzania.
Hata hivyo, tunaona katika mitandao ya kijamii na hata kwenye vyombo vya habari baadhi ya Watanzania wachache wakionekana kutomuunga mkono Rais, na wengine wakionekana wazi kuwaunga mkono wabunge waliofanya kitendo cha aibu Ijumaa iliyopita cha kupiga kelele, kuzomea na kususa hotuba ya Rais Magufuli.
Baadhi ya vitabu vya dini vinafundisha kwamba binadamu ana njia mbili; ama ile anayoitaka Mwenyezi Mungu ambaye ndiye aliyemuumba au ya shetani. Ni kwa muktadha huo, tunaungana na kauli ya Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliyekaririwa na vyombo vya habari likiwemo gazeti hili jana, akisema kwamba mtu yeyote anayempinga Rais Magufuli, maana yake ni kwamba atakuwa unaunga mkono mafisadi, wala rushwa na wabadhirifu.
Katika maoni yake, Zitto alisema mtu anayepinga ufisadi, uzembe, ubadhirifu, uvivu na rushwa hawezi kumzomea Rais Magufuli au kumpinga kwa namna moja au nyingine badala ya kumuunga mkono. Zitto alifafanua kwamba mtu wa aina hiyo kwa hali yoyote atakuwa ana maslahi binafsi na mafisadi na hataki mabadiliko chanya.
Zitto akaenda mbali kwa kusema kwamba huu ndio wakati ambao Watanzania watawajua watu ambao wapo upande wa mafisadi au upande wa wananchi. Hata sisi tunajiuliza kwamba wanaompinga Magufuli wanataka nini hasa?
Je, wanataka tuendelee kuwa taifa ambalo matajiri hawalipi kodi isipokuwa wanaokamuliwa zaidi ni watu masikini, wenye kipato cha chini na wafanyakazi? Je, wanataka watu waliouziwa viwanda na mashamba waendelee kuyahodhi hata kama wameshindwa kuyaendeleza kwa mujibu wa mikataba?
Yaani wanachukia dhana nzima ya kufufua viwanda vya zamani na kuanzisha vipaya? Je, wanataka tuendelee na watendaji serikalini wasiowajibika ipasavyo ambao wamegeuza sekta ya umma kuwa sehemu ya kuchuma badala ya kuitumikia kwa faida ya wananchi wote?
Wanakataa asipambane na wala rushwa, wanataka alee wazembe katika utumishi wa umma na pia wanataka asizibe mianya ya uchakachuaji wa fedha za umma? Zitto, licha ya kuwa kiongozi wa chama cha upinzani, alisema uzalendo unamtaka kumuunga mkono Rais katika vita dhidi ya ufisadi na kusimamia ustawi wa watanzania, hususan wanyonge. Na sisi swali letu kwa wanaoonekana kutokuwa upande wa rais ni hili. Je, uzalendo wao ni kuunga mkono kitu gani?
Baadhi ya watu hawa, kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakijinadi kwamba wanachukia ufisadi. Je, sasa wanaposhindwa kuunga mkono rais anayeahidi kupambana na ufisadi tuwaeleweje?

SOURCE: Habari leo online
Ni nyumbu na mafisadi wao ndio pekee wanaompinga Magufuri kisa wamekosa kuongoza nchi na pia wanahofia mahakama ya majizi na mafisadi sasa yanawatumia nyumbu kama kinga yao ili wavuke mto Mara salama,lakini wameshachelewa kilichobaki ni kuisoma namba na kusaga meno.
 
Ukiunga mkono ndio inakuwaje na usipounga mkono ndio inakuwa vipi?
Kama hamtaki hata tumzike Mawazo aliyeuwawa kikatili mnatutaka tuunge mkono futuhi?
Pelekeni upuuzi huko
 
Ndugu watanzania wenzangu, kumekuwa na mijadala ambayo mingine ni kumkatisha tamaa rais wetu JPM, najiuliza hivi tunahitaji rais wa aina gani. Huyu ndugu ameonesha nia dhahiri ya kupambana na kuipeleka Tanzania katika hali bora zaidi, kinachotakiwa ni kumuunga mkono na kumpa moyo, nasikitika kuona baadhi yetu wakigeuka kuwa watabiri kuwa ooo huyu atakwama nk nk, tumwache afanye kazi na tumpe ushirikiano, bla bla hazitatusaidia

Kwa taarifa yako kumpinga ndio kumjenga kuliko kumsifia watu wote, mgema akisifiwa..... Halafu uzoefu unaonyesha kila kiongozi anayeingia madarakani anaingia kwa mbwembwe nyingi, unakumbuka fagio la chuma, ukweli na uwazi, maisha bora kwa kila mtanzania? Tanzania hatujawahi kuwa na mwanzo mbaya kwa kiongozi wetu shida ya viongozi wetu ni utekelezaji, ni mapema mno kumpa sifa hizo kulingana historia yetu. Kama ana nia ya dhati ahakikishe rasimu ya Warioba inarudishwa bungeni kurekebishwa na muundo wa hilo bunge ahakikishe wanasiasa wawe asilimia 40 tu wajumbe wote, kwani huku Africa tunahitaji taasisi imara na sio kiongozi imara. Na kwa taarifa yako wanaompinga huyo Magufuli ni wanaccm kwa wingi wao kwani wengi ndio walikuwa wavunja sheria.
 
Tumuombe Mwenyezi Mungu, yote aliyoahidi Mhe. Rais yatimie ili kila mmoja aile hiyo cake.
 
Kwa taarifa yako kumpinga ndio kumjenga kuliko kumsifia watu wote, mgema akisifiwa..... Halafu uzoefu unaonyesha kila kiongozi anayeingia madarakani anaingia kwa mbwembwe nyingi, unakumbuka fagio la chuma, ukweli na uwazi, maisha bora kwa kila mtanzania? Tanzania hatujawahi kuwa na mwanzo mbaya kwa kiongozi wetu shida ya viongozi wetu ni utekelezaji, ni mapema mno kumpa sifa hizo kulingana historia yetu. Kama ana nia ya dhati ahakikishe rasimu ya Warioba inarudishwa bungeni kurekebishwa na muundo wa hilo bunge ahakikishe wanasiasa wawe asilimia 40 tu wajumbe wote, kwani huku Africa tunahitaji taasisi imara na sio kiongozi imara. Na kwa taarifa yako wanaompinga huyo Magufuli ni wanaccm kwa wingi wao kwani wengi ndio walikuwa wavunja sheria.
HUU ndiyo ujinga kutoka kwa MJINGa kama wewe, kwa sababu tu unataka kumjenga unalazimika kumpinga? Hauna akili wewe. Kaungane na wajinga wenzako kule mwanza mkatumie mwili wa marehemu kama mtaji wa kujiimarisha kisiasa.
 
Hotuba ya Magufuli ina nini kipya? Sethi Benjamini alikufa kwa kutembea kilometer kibao kuunga mkono hotuba ya JKN kuhusu Azimio la Arusha! Huyu ambaye ameingizwa madaraka kwa mtutu wa Bunduki na Wizi wa Kura wamuunge Mkono kwa lipi? Futuhi la Vitanda? Kutekeleza Sera za Africa Mashariki kuhusu Safari za Nje? Maisha ya Watanzania kuwa Mazuri ghafla? au Umeme wa power bank?

wanajua yote ila ubabe tu wa kishetani
 
Hotuba ya Magufuli ina nini kipya? Sethi Benjamini alikufa kwa kutembea kilometer kibao kuunga mkono hotuba ya JKN kuhusu Azimio la Arusha! Huyu ambaye ameingizwa madaraka kwa mtutu wa Bunduki na Wizi wa Kura wamuunge Mkono kwa lipi? Futuhi la Vitanda? Kutekeleza Sera za Africa Mashariki kuhusu Safari za Nje? Maisha ya Watanzania kuwa Mazuri ghafla? au Umeme wa power bank?

Ukiambiwa uthibitishe ayo usemayo utaweza?
 
toa ushahid mzee...si najibu ya majimboyote mnayo!! tupe mfani jimbo moja tu zilipoibiwa kura....or else.....angalia sana kuna jela kaka

Ushahidi upo, mwanahalisi imeandika kila kitu, Si Makamba wala Kailima aliyebisha kwamba walichotangaza si kura halisi ni sham
 
toa ushahid mzee...si najibu ya majimboyote mnayo!! tupe mfani jimbo moja tu zilipoibiwa kura....or else.....angalia sana kuna jela kaka

mkuu hawa wengine wanaongea tu bila kuwa na ushahidi wowote wakueleweka.P
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom