Ozzie
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 3,217
- 1,259
Bahati mbaya sana, kwetu hakuna uwanja wa ndege; na hata kama ungekuwepo sijui kama ningeweza kumudu usafiri. Na ningemudu kusafiri naamini bado ningepata shida zilezile za Air Tanzania na Precision air.
Zamani zile nikipata nafasi ya kwenda kusalimu wazazi, nilikuwa naenda KAMATA kupanda Scandinavia. Hawa hawakuwa wababaishaji, ila walipokufa nafasi yao imejazwa na magari UCHWARA kama SUMRY, Mbeya Express, n.k; ambayo yanajinyumbulisha kuwa yenye kiwango cha kufanana na Scandinavia Express; wakati hawatakuja kufikia chembe ya huduma waliyokuwa wakiitoa.
Leo nilitakiwa niwe Safarini kwenda Mkoani. Nilikata ticket ya Mbeya Express Ijumaa hii. Lakini nimefika hapa Ubungo, jamaa wa Mbeya Express wanasema gari letu lina matatizo hivyo wanataka tupande SUMRY mbofumbofu. Wao wanaita 'kufaulisha'. Mimi nimekataa. Sasa 'naunda kamati' nifanye uamuzi wa kurudi nyumbani na begi zangu. Nashukuru wamerudisha nauli, ljapo haihusishi gharama za kunileta Ubungo Bus Terminal na kunirudisha nyumbani (ni kama elfu 40).
Hii ni mara yangu ya sita kubadirishiwa gari. Mara ya mwisho ilikuwa wiki tatu zilizopita. Nilikata ticket gari ya SUMRY siku moja kabla ya kusafiri, siku ya pili nafika Ubungo wakasema gari haikurudi toka mkoani, hivyo wakanipandisha kwenye gari iitwayo TAQWA. Shida nilizopata kwenye gari hiyo, zimenifanya leo nisikubali 'kufaulishwa'.
Hivi haya magari kwanini wana huduma mbovu kiasi hiki? Hakuna mshindani anayeweza kuja? Au waje wadhungu pia wawekeze wawafundishe waswahili adabu? Na kwanini wakatishe abiria ticket ilhali wakijua hawatakuwa na gari? Na wengine huwa wanadanganya, wanajifanya gari kama imeharibika kumbe itakuwa walikuandikia muda usio sahihi ili pindi utakapofika wakupakie kwenye gari lingine, na hivyo kutopoteza pesa yako.
INAUDHI SANA.
Zamani zile nikipata nafasi ya kwenda kusalimu wazazi, nilikuwa naenda KAMATA kupanda Scandinavia. Hawa hawakuwa wababaishaji, ila walipokufa nafasi yao imejazwa na magari UCHWARA kama SUMRY, Mbeya Express, n.k; ambayo yanajinyumbulisha kuwa yenye kiwango cha kufanana na Scandinavia Express; wakati hawatakuja kufikia chembe ya huduma waliyokuwa wakiitoa.
Leo nilitakiwa niwe Safarini kwenda Mkoani. Nilikata ticket ya Mbeya Express Ijumaa hii. Lakini nimefika hapa Ubungo, jamaa wa Mbeya Express wanasema gari letu lina matatizo hivyo wanataka tupande SUMRY mbofumbofu. Wao wanaita 'kufaulisha'. Mimi nimekataa. Sasa 'naunda kamati' nifanye uamuzi wa kurudi nyumbani na begi zangu. Nashukuru wamerudisha nauli, ljapo haihusishi gharama za kunileta Ubungo Bus Terminal na kunirudisha nyumbani (ni kama elfu 40).
Hii ni mara yangu ya sita kubadirishiwa gari. Mara ya mwisho ilikuwa wiki tatu zilizopita. Nilikata ticket gari ya SUMRY siku moja kabla ya kusafiri, siku ya pili nafika Ubungo wakasema gari haikurudi toka mkoani, hivyo wakanipandisha kwenye gari iitwayo TAQWA. Shida nilizopata kwenye gari hiyo, zimenifanya leo nisikubali 'kufaulishwa'.
Hivi haya magari kwanini wana huduma mbovu kiasi hiki? Hakuna mshindani anayeweza kuja? Au waje wadhungu pia wawekeze wawafundishe waswahili adabu? Na kwanini wakatishe abiria ticket ilhali wakijua hawatakuwa na gari? Na wengine huwa wanadanganya, wanajifanya gari kama imeharibika kumbe itakuwa walikuandikia muda usio sahihi ili pindi utakapofika wakupakie kwenye gari lingine, na hivyo kutopoteza pesa yako.
INAUDHI SANA.