Tupeane mbinu za kuishi na mwanamke mgomvi kwenye ndoa

Huuh ushauri kiboko aisee amwandalie kimwiko hahaaaa amchape kiruuuuu umesahau kuwa upele humwota asiye na kucha. Huyu mkewe kamweka kwenye kipochi manyoya hafurukuti

hahahaa! Labda kama iko hvyo basi jamaa hana jinsi. Ila ningekuwa mm hyo ndio dawa yao. Ukianza kubishana na mwanamke hutamweza
 
hahahaa! Labda kama iko hvyo basi jamaa hana jinsi. Ila ningekuwa mm hyo ndio dawa yao. Ukianza kubishana na mwanamke hutamweza
Huyu kamwendekeza mkewe kabla ya kuanza kuishi pamoja na inaonyesha huyu mkewe ni kila kitu huamua alitakalo. Hata nyumba ukikosea msingi inabomoka na wanawake hujua kusoma weakness za wanaume akishajua udhaifu lazima uanaume unaisha kabisa kukuonea hakuishi,hakusikilizi.
Sasa we we siuna msimamo mkali unafikiri mwanamke akikujua atasumbua ni ananyooka mwenyewe
 
Huyu kamwendekeza mkewe kabla ya kuanza kuishi pamoja na inaonyesha huyu mkewe ni kila kitu huamua alitakalo. Hata nyumba ukikosea msingi inabomoka na wanawake hujua kusoma weakness za wanaume akishajua udhaifu lazima uanaume unaisha kabisa kukuonea hakuishi,hakusikilizi.
Sasa we we siuna msimamo mkali unafikiri mwanamke akikujua atasumbua ni ananyooka mwenyewe

kweli kabisa ni hatar kabisa mwanamke akiijua tabia yako lakn inaleta heshima sana mwanamke akiijua misimamo yako na principle.
 
Habari wanajamii,

Ni muda mrefu sijaingia humu sababu ya pilikapilika zilizokuwepo pamoja na kuwepo kwa magroup ya whatsupp kumepunguza concentration ya kuchangia mada humu.

Naomba tupeane mbinu za kuishi na mwanamke mgomvi kwenye ndoa ambae kila wakati anakuwa mtu wa ku complain kwamba ananyanyaswa ila ukamwambia akueleze unamnyanyasa na kitu gani hana jibu, ukijaribu kuangalia ama kujiuliza unamnyanyasa na nini huoni.

Kuna wanawake ambao hawaridhiki hivyo kila unachomfanyia anaona humtoshelezi. Akitaka kila siku wiki nzima mle nyama mtakula ila bado atalalamika sili vizuri.

Kama una tv ndani, labda anataka yeye aangalie chanel zake tu kwakuwa labda ana interest na movies, atashinda asubuhi hadi jioni na tv, ila wewe ukitaka uangalie taarifa ya habari ya saa 2 usiku ya dakika 20, atasema huo ni udikteta na unambagua.

Hazipiti siku 2 bila kupigiana simu na mama yake, ila baba mkwe atakaa hata mwaka hajamjulia hali. Ukimwonya kitu anasema huo ni uonevu, sipendi kukoromewa nitaenda kwetu.

Mwanamke kama huyu ambaye hawazi positively hata siku moja bali kuwaza negatively kila wakati na anakuwa mpinzani kwa kila kitu katika ndoa ni njia gani nzuri ya kuishi nae maana wengine tuna mioyo ya ubushoke ila siyo kwa kupenda bali kutokana na heshima mtu unakuwa nayo sasa ukiwaza kuchukua maamuzi magumu, jamii itakuangalia tofauti.

Najua huku kuna washauri wazuri na waliobobea bila kuwasahau wafurahishaji, wapondaji na watukanaji.

Nawasilisha.

Jishushe kila inapobidi lakini usijidhalilishe mtaishi kwa amani na ukiona anazidi sana muonyeshe kidogo kwamba wewe ni mwanaume na una mipaka na viwango vya uvumilivu
 
Kichapo,,,,,,tafuta kimada wa kukupunguzia stress pia mruhusu aende kwao kwa kua unampenda tafuta mtu lipa hela ya kutosha mwambie a m spy akiwa huko kwao jibu utalipata lkn unakiwa kua na kifua
 
Katika vitu nisivyopenda na vinaharibu wanawake ni maigizo ya TV ni janga la ndoa
 
Anzisha mfumo dume kidogo,humo ndani baba mko wangapi?
Solution unayo tatizo huna courage ya kuchukua hatua
 
Habari wanajamii,

Ni muda mrefu sijaingia humu sababu ya pilikapilika zilizokuwepo pamoja na kuwepo kwa magroup ya whatsupp kumepunguza concentration ya kuchangia mada humu.

Naomba tupeane mbinu za kuishi na mwanamke mgomvi kwenye ndoa ambae kila wakati anakuwa mtu wa ku complain kwamba ananyanyaswa ila ukamwambia akueleze unamnyanyasa na kitu gani hana jibu, ukijaribu kuangalia ama kujiuliza unamnyanyasa na nini huoni.

Kuna wanawake ambao hawaridhiki hivyo kila unachomfanyia anaona humtoshelezi. Akitaka kila siku wiki nzima mle nyama mtakula ila bado atalalamika sili vizuri.

Kama una tv ndani, labda anataka yeye aangalie chanel zake tu kwakuwa labda ana interest na movies, atashinda asubuhi hadi jioni na tv, ila wewe ukitaka uangalie taarifa ya habari ya saa 2 usiku ya dakika 20, atasema huo ni udikteta na unambagua.

Hazipiti siku 2 bila kupigiana simu na mama yake, ila baba mkwe atakaa hata mwaka hajamjulia hali. Ukimwonya kitu anasema huo ni uonevu, sipendi kukoromewa nitaenda kwetu.

Mwanamke kama huyu ambaye hawazi positively hata siku moja bali kuwaza negatively kila wakati na anakuwa mpinzani kwa kila kitu katika ndoa ni njia gani nzuri ya kuishi nae maana wengine tuna mioyo ya ubushoke ila siyo kwa kupenda bali kutokana na heshima mtu unakuwa nayo sasa ukiwaza kuchukua maamuzi magumu, jamii itakuangalia tofauti.

Najua huku kuna washauri wazuri na waliobobea bila kuwasahau wafurahishaji, wapondaji na watukanaji.

Nawasilisha.

Mithali 17 : 1
Afadhali mego kavu pamoja
na utulivu, Kuliko nyumba yenye karamu nyingi
pamoja na magomvi.
 
Lol ugomvi, mikelele ndani ya nyumba haifai hata kidogo. Cha muhimu timiza majukumu yako kama baba.
 
Habari wanajamii,

Ni muda mrefu sijaingia humu sababu ya pilikapilika zilizokuwepo pamoja na kuwepo kwa magroup ya whatsupp kumepunguza concentration ya kuchangia mada humu.

Naomba tupeane mbinu za kuishi na mwanamke mgomvi kwenye ndoa ambae kila wakati anakuwa mtu wa ku complain kwamba ananyanyaswa ila ukamwambia akueleze unamnyanyasa na kitu gani hana jibu, ukijaribu kuangalia ama kujiuliza unamnyanyasa na nini huoni.

Kuna wanawake ambao hawaridhiki hivyo kila unachomfanyia anaona humtoshelezi. Akitaka kila siku wiki nzima mle nyama mtakula ila bado atalalamika sili vizuri.

Kama una tv ndani, labda anataka yeye aangalie chanel zake tu kwakuwa labda ana interest na movies, atashinda asubuhi hadi jioni na tv, ila wewe ukitaka uangalie taarifa ya habari ya saa 2 usiku ya dakika 20, atasema huo ni udikteta na unambagua.

Hazipiti siku 2 bila kupigiana simu na mama yake, ila baba mkwe atakaa hata mwaka hajamjulia hali. Ukimwonya kitu anasema huo ni uonevu, sipendi kukoromewa nitaenda kwetu.

Mwanamke kama huyu ambaye hawazi positively hata siku moja bali kuwaza negatively kila wakati na anakuwa mpinzani kwa kila kitu katika ndoa ni njia gani nzuri ya kuishi nae maana wengine tuna mioyo ya ubushoke ila siyo kwa kupenda bali kutokana na heshima mtu unakuwa nayo sasa ukiwaza kuchukua maamuzi magumu, jamii itakuangalia tofauti.

Najua huku kuna washauri wazuri na waliobobea bila kuwasahau wafurahishaji, wapondaji na watukanaji.

Nawasilisha.

Ninawasiwasi huenda huyo mkeo ni mzaliwa wa kwanza, au kalelewa na mama pekee, au ni binti pekee ktk familia.
 
siyo mzaliwa wa kwanza ila ni binti wa pekee kati ya watoto 7

OK.
Huenda amelelewa kwa kudekezwa sana na mama coz akina mama wengi wakipata mtoto mmoja tu wa like wanamtetea sana, kiasi kwamba kila anachotaka anatimiziwa, na kila anachotenda kinakubalika pasipo kuhojiwa. Hili ni tatizo baadaye tunapo ishi nao kama wanandoa. Binafsi nimepitia mazingira kama yako kwa miaka takribani mitatu. Ilifika muda nilitaka kumwacha, lakini.....ashukuriwe Mwenyezi Mungu kunipa ujasiri, nimeendelea kuvumilia.
Sasa mwezi uliopita, nikashangaa ananiambia "Mume wangu, naomba unisamehe, kwa muda mrefu nimekuwa nakujibu vibaya"....... Nilimwangalia.....nikavuta hisia weeeee........(moyoni nikajisemea bahati yako). Kisha nikamwuliza, Nani kakwambia umekuwa ukinijibu majibu mabaya? Akasema ametafakari yeye mwenyewe. Nikamwambia, "kama ni kweli unacho kisema, natarajia mabadiliko" Nilimweleza ukweli kwamba imefika mahali namwona kama MWANAMKE na siyo MKE. Nikamsihi aishi kama MKE.
Hata hivyo, kuna hatua kadhaa nilisha zichukua ndani ya ndoa,,
Kwa mfano:
1. Mara nyingi swala La tendo LA ndoa lilikuwa na ugovi sana. Wakati mwingine anaweza kukuambia hajisikii hadi wiki tatu. Ukimkomalia, vita yake hiyo looooo! Mara unanibaka.
NIKAONA ISIWE TABU. NIKAWA SIMGUSI TENA MPAKA AJISIKE YEYE. HAIJALISHI HATA KAMA MWEZI UPITE. Akaniuliza kwani mwenzangu vipi? Nikamwambia, nasubiri ujisikie.
2. Swala LA pesa limesumbua sana. Pesa yote nilikuwa naiweka wazi. Mwenzangu anapoona pesa sijui mikono inawasha,, yani anataka kununua kila anachokiona mpaka hela iishe kiasi kwamba tunaishiwa na kuingia kwenye madeni kila kukicha. Nikipingana naye, anasema namnyanyasa kwasababu yeye hana ajira rasmi. ISIWE TABU. NIKAAMUA.... MIMI NDIYE NITAJUA KUNA KIASI GANI CHA PESA, NA NITAPANGA BAJETI MWENYEWE. Akaniuliza mbona......
Nikamwambia,, ni kweli kwasababu naona unapojua pesa tuliyo nayo unapata tabu, kila kitu unataka kununua. nimekuondolea kishawishi mpaka UBADILIKE.

NAONA NETWORK IMEANZA KUSOMEKA KWA MBALI
 
dini hairuhusu kabisa aisee halafu anasema akiondoka kukimshinda atakuja kuomba msamaha, hivyo hata ukitimua kuna kurudi. Kikubwa labda kutimuliwa mbele ya mashahidi.

Pole, hii case inanikumbusha case ya rafiki yangu, nae mke wake alikuwa na tabia na mienendo kama hiyo. Na siku moja aliondoka na kuchukua kila kilicho chake. Huwezi kuamini baada tu ya wiki moja akampigia simu mshikaji eti anataka kurudi. Jamaa yangu akamwambia kaa huko huko ntakuja kukuchukua. Yule mwanamke hakusubiri akachukuliwe alirudi mwenyewe. Jamaa yangu akawa mpole wakaendelea kuishi pamoja. Japo huyu mwanamke tabia yake ya ugomvi na kuto kuridhika viliendelea.. walikuwa na maisha standard flani vile kwa maisha yetu ya hapa bongo....... Hatimayake jamaa yangu mziki wa huyu mwanamke ulimshinda akahama yeye akamwacha akaenda kuanza maisha mapya. Ila mali zote walizokuwanazo alimwachia huyo mwanamke. MWANAMKE MPUMBAF NI SHIDA UTAZEEKA KABLA YA SIKU ZAKO SIR LUTA. Jichunguze kwanza wewe mwenyewe kwanza na ikiwezekana badilika tabia, hapa na maanisha kubadilika positively. Kama ni mtu mwema nae atabadilika na mtafurahia maisha. If not.... we only live once.... tambaa.... move on.... chapa lapa... tembea....timue.... kitoe.
 
Back
Top Bottom