Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

Mkumbusheni Lisu kuwa kuna mstari baina ya kuwa mgombea na kuwa Rais,

Sasa yeye anafikiri kuwa mgombea wa Urais ndio tayari ushakuwa Rais hivyo unakuwa juu ya vyombo vya dola.

Aende tu huko anakoitwa kwani jamaa wanauwezo wa kumfuata na kumchukua muda wowote wakitaka.
Huo huo mstari mkumbushe na jiwe kuwa wananchi wa tunduma hawastahili kufokewa wa kupangiwa mtu wa kumchagua hivyo achunge ndimi yake
 
Lissu anatafuta sababu ya kushindwa
kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu,maelezo utayakuta polisi,na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote
Kwa sheria za Lumumba kweli wanaweza,
 
Polisi wa Tanzania wanajua kuwa raia hasa wapinzani ndio wana jukumu la kutii sheria bila shuruti.

Sirro anatii sana amri kutoka juu kuliko kufuata weledi wa kazi, hii inanikumbusha yule aliyekuwa IGP wa Kenya Mohammed Yusuf walipopelekwa The Hague, Uholanzi kufuatia mauaji ya baada ya uchaguzi wa 2017 alivyokuwa akibubujikwa na machozi akidai yeye alikuwa akitii amri kutoka juu...!!!
 
Huyu jamaa ni jeuri haswaaa, ila mashabiki wake mnaona sasa hatua zikichukuliwa msilielie.

JPM ANATOSHA
CCM USHINDI NI JADI
 
Heheheee.... Ukweli ni kwamba, hiyo ni sawa sawa na barua ya harusi tu!

Wito au barua ya polisi LAZIMA ieleze KOSA ANALOITIWA KWALO ikiambatana na "statement of probable cause" kuhusu kosa hilo!

Huwezi tu kuita mtu kienyeji enyeji! Angalau sio kwenye nchi tunayoiita "Jamuhuri" (sijui hata kama unaelewa maana ya Jamuhuri wewe mataga?)

Vinginevyo hiyo itakuwa ni Jamuhuri ya kihuni tu kama mapolisi watakuwa wanajiendesha kama genge la walevi.

Polisi hawako juu ya sheria. Wafuate hizo procedures waache kujidekeza!
Umegusa eneo muhimu sana, MATAGA hawaelewi maama ya Jamhuri. Ndio tatizo linapoanzia
 
Lissu anatafuta sababu ya kushindwa
kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu,maelezo utayakuta polisi,na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote
Hayo ni mazoea , na ndio loophole watu wasiojulikana wanaitumia pia .
Magari ya polisi doria Yana plate namba zisizoelezeka Siku hizi na hata sidhani kama yana bima na yet tunqona sawa ,
 
Back
Top Bottom