Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,035
- 144,387
Habari hii ni kwa mujibu wa Martin Maranja Masese kupitia mtandao wa X.
-
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limempatia dhamama Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na viongozi wengine wa chama hicho waliokamatwa muda huu saa 2 usiku jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure amesema viongozi hao wametakiwa kesho saa tatu asubuhi kuripoti polisi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo iliyotolewa leo Jumapili Septemba 10, 2023 ilisema kuwa Lissu na wenzake watatu walishikiliwa kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia polisi kufanya kazi zao.
Mwandishi wa Habari kutoka Jambo TV, Oscar Kasubi aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo naye ameachiwa usiku huu.
-
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limempatia dhamama Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu na viongozi wengine wa chama hicho waliokamatwa muda huu saa 2 usiku jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure amesema viongozi hao wametakiwa kesho saa tatu asubuhi kuripoti polisi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo iliyotolewa leo Jumapili Septemba 10, 2023 ilisema kuwa Lissu na wenzake watatu walishikiliwa kwa tuhuma za kufanya mikusanyiko isiyo halali na kuzuia polisi kufanya kazi zao.
Mwandishi wa Habari kutoka Jambo TV, Oscar Kasubi aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo naye ameachiwa usiku huu.