Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,658
- 46,322
Kumuachia Mungu matatizo yaliyo ndani ya uwezo wa kibinadamu, kumuomba upendeleo, suluhisho kwa kila jambo au kumsifia kwa baadhi ya mambo ni sawa? Au ni uchovu wa akili?
Huwa nikiwasikiliza baadhi ya watu wanaotoa kauli za kusubiria Mungu awaadhibu waonezi au wadhulumaji wao au awatatulie baadhi ya mambo naona kama watu waliojikatia tamaa kwa kila kitu na hawajui chochote cha kufanya.
Mfano umeibiwa, umedhulimiwa kitu au fedha, umedhalilishwa mbele ya hadhara, umefukuzwa kazi kwa figusu tu za boss n.k Unapomuachia Mungu unataka afanye nini hasa?
Huwa naona hata wapinzani wa kisiasa nao wanatoa kauli za kumsubiria Mungu atende jambo kwa wale wanaoona hawawatendei haki au wanashangilia jambo baya linapowapata wapinzani maadui wao kana kwamba ni malipo kutoka kwa Mungu!
Hata kama unaamini yuko Mungu anayejibu ni ujuha kumsubira au kutamani awape mikasa maadui au watesi wako, hasa kwa Wakristo ambao wameambiwa wasamehe kwa kila jambo. Ni ujuha kumuomba akusaidie upate upendeleo tofauti na binadamu wenzako katikati mambo mbalimbali, ni aina fulani ya "narcissism". Unaweza kukuta msomi fisadi wa TRA au mfanyabiashara mkubwa mkwepa kodi amevaa T-shirt "Sisi ni wale tunaosaidiwa na Bwana!" Kwamba wale masikini wanaotoseka kwa kukosa huduma nzuri kutokana na ufisadi hawasaidiwi na Bwana?
Mimi nafikiri dini zetu wakati mwingine zinatuondolea kabisa kuyaona maisha katika uhalisia wake. Kwamba mdhulumaji au Mtesi anaweza kuishia maisha yake tena yakiwa marefu sana kwa raha mustarehe kabisa hapa duniani, kwamba kuna mambo mengi yaliyo ndani ya uwezo binadamu na kwa uhakika ambayo tunapaswa kuyatatua kwa akili zetu badala ya kumuachilia na kumsubiria Mungu na kwamba sehemu kubwa ya maisha ya binadamu hata kwa wale wanaomuani Mungu yanaweza kuelezewa kwa bahati zaidi au randomness/chance/coincidence kuliko kitu kingine.
Huwa nikiwasikiliza baadhi ya watu wanaotoa kauli za kusubiria Mungu awaadhibu waonezi au wadhulumaji wao au awatatulie baadhi ya mambo naona kama watu waliojikatia tamaa kwa kila kitu na hawajui chochote cha kufanya.
Mfano umeibiwa, umedhulimiwa kitu au fedha, umedhalilishwa mbele ya hadhara, umefukuzwa kazi kwa figusu tu za boss n.k Unapomuachia Mungu unataka afanye nini hasa?
Huwa naona hata wapinzani wa kisiasa nao wanatoa kauli za kumsubiria Mungu atende jambo kwa wale wanaoona hawawatendei haki au wanashangilia jambo baya linapowapata wapinzani maadui wao kana kwamba ni malipo kutoka kwa Mungu!
Hata kama unaamini yuko Mungu anayejibu ni ujuha kumsubira au kutamani awape mikasa maadui au watesi wako, hasa kwa Wakristo ambao wameambiwa wasamehe kwa kila jambo. Ni ujuha kumuomba akusaidie upate upendeleo tofauti na binadamu wenzako katikati mambo mbalimbali, ni aina fulani ya "narcissism". Unaweza kukuta msomi fisadi wa TRA au mfanyabiashara mkubwa mkwepa kodi amevaa T-shirt "Sisi ni wale tunaosaidiwa na Bwana!" Kwamba wale masikini wanaotoseka kwa kukosa huduma nzuri kutokana na ufisadi hawasaidiwi na Bwana?
Mimi nafikiri dini zetu wakati mwingine zinatuondolea kabisa kuyaona maisha katika uhalisia wake. Kwamba mdhulumaji au Mtesi anaweza kuishia maisha yake tena yakiwa marefu sana kwa raha mustarehe kabisa hapa duniani, kwamba kuna mambo mengi yaliyo ndani ya uwezo binadamu na kwa uhakika ambayo tunapaswa kuyatatua kwa akili zetu badala ya kumuachilia na kumsubiria Mungu na kwamba sehemu kubwa ya maisha ya binadamu hata kwa wale wanaomuani Mungu yanaweza kuelezewa kwa bahati zaidi au randomness/chance/coincidence kuliko kitu kingine.