Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #21
Masikini nchi yangu!!
Family friend wangu mmoja ambaye alikuwa waziri ktk awamu ya kwanza na ya pili amenisimulia visa vifuatavyo kuhusu Marehemu Sokoine;
Anasema Marehemu Mwalimu Nyerere alikuwa na tabia kuna siku akifanya kazi sana asubuhi mchana akienda lunch huwa analala kidogo kabla hajarudi Ikulu kuendelea na kazi. Kuna siku ilitokea dharura ya kikazi na Marehemu Sokoine akiwa ni PM alitaka maelekezo ya Mwalimu. Akapiga siku akaambiwa Mwalimu kapumzika kidogo, akasema muamsheni, Mwalimu akaamshwa tatizo likatatuliwa.
Anaendelea kusema huyu Bwana alikuwa mfuatiliaji SANA ktk utendaji wa kazi, alinipa mfano Sokoine alipokuwa PM alimwita waziri wa ulinzi ampe update ya silaha zilizopo katika makambi mbalimbali ya jeshi. Siku ya pili bila waziri kujua, Sokoine akawa anapiga simu kwa wakuu wa vikosi mwenyewe wampe data kazi ambayo imemchukua siku moja tu. Baada ya wiki 2 waziri anakuja na "update" yake na anakuta tayari mwenzie anayo na la kushangaza iliyo sahihi zaidi!
He was true leader, big loss to the nation.
Dar si Lamu.. believe me Sokoine was not Mrema....
Tunaye Sokoine aliye Hai- EL, kijana, mchapakazi, mmasai. Anajua kutoa maagizo na kufuatilia. Huchukia mambo yakienda vibaya. Si unaona anavyosimamia ujenzi wa madarasa?
Kutokana na wasifu na utendaji wake kazi nathubutu kusema kuwa shule si kipimo cha uteandaji, Moringe alikuwa na shule ndogo lakini aliwatingisha na kuwanyima usingizi watu waliokwenda shule.
daima tutamkumbuka sokoine
Wazee, heshima yenu kwanza,
Kama mtu ana sifa fulani, mvuto wa watu unakuwepo hata kama matangazo yanakoma. Ni vema kutofautisha kati ya mvuto wa matangazo na mvuto wa sifa ambapo vyote viwili vinajenga mvuto wa watu. Matangazo yaligunduliwa ili kujaribu kuchukuwa nafasi ya sifa ambacho ni kiini katika mvuto wa watu. Hivyo basi, mvuto wa watu halisi sio sifa ya msimu kama ilivyo Kiangazi na Kipupwe, bali ni sifa ambayo mtu anakufa nayo kama Sokoine. Lakini hiyo sifa ikiwa ni matokeo ya kilemba cha ukoka kama ilivyokuwa kwa Mrema, ndipo inakuwa na tabia za msimu. Ndio maana amedolola kwa sasa.
Wazee, heshima yenu kwanza,
Akaanzisha tabia mbaya ya kulala uvunguni mwa vitanda vya wanandoa. Hizi ni busara alizokopa kutoka kwa mabibi wa kijadi waliokuwa wanataka kuhakikisha kama mke aliyeolewa na mjukuu wao ana bikira au la!. Waziri unamwita mke wa mtu ofisini kwako, tena kupitia kwenye vyombo vya habari? Kwa nini Waziri anaingilia ndoa za watu? Kwa nini asiimalishe taasisi zinazoshughulika na mambo ya jamii? Nchi inaporwa, vyombo vya dola vimewekwa kibindoni, Waziri anayeongoza taasisi zote hizo yuko ofisini na mke wa mtu akisuluhisha ugomvi wa makonde yatokanayo na wanandoa kunyimana uroda, au kufumaniana. Hizi zote ni shughuli na sio kazi.
Kwa nini Mrema alipata umaarufu wakati ule na sio sasa hivi?
Kama huna sababu mhimu sana inayokuzuia kukusanya habari za marehemu Sokoine na kuziweka kwenye kitabu, basi inafaa ufikirie kuifanya kazi hiyo.
Sababu ya wewe kuwa mdogo wakati huo sio ya msingi. Si lazima uandike peke yako, lakini unaweza kuwa chachu na mshiriki imara kati ya kundi la watu kama akina Mawado mnaoweza kuendesha na kuifanikisha shughuli mhimu kama hiyo.
Baadhi ya matatizo yetu mara nyingi ni haya ya kutegeana. Kumsubiri mtu mwingine afanye.