Tuna tatizo kubwa sana la elimu ndilo linafanya tuwe maskini na wapumbavu.

Cashman

JF-Expert Member
Jun 8, 2018
2,293
3,965
Napenda kuanza na nukuu ya mwanafalsafa simkumbuki jina aliyesema " Elimu humfanya mwerevu kuwa mwerevu zaidi na mpumbavu kuwa mpumbavu zaidi"

Kuna kitu hatujakigundua katika suala zima la elimu.Tuna watu wenye ma PhD na ma degree wengi zaidi ya asilimia 99.9 tumewaamini kama "think tanks" wa nchi kumbe hawawezi kufikiri kabisa.

Kipimo cha wao kupata hizo shahada ni uwezo wa kukumbuka vitu na sio uwezo wa kuchakata.Kukumbuka vitu ni kipaji kama alicho nacho ndege kasuku.Kipaji cha kukumbuka vitu hakiwezi kuwa kipimo cha akili.Bahati mbaya maprofesa wengi, na wasomi wengi walipatikana kwa kipimo hicho cha uwezo wa kukumbuka.Hawa ndio wanaitwa watu wenye akili sana.

Nasikitika kusema kuwa nchi yetu kama siyo nchi zetu za kiafrika,tutaendelea kuwa maskini wakubwa hadi pale tutakapochoma misingi ya elimu tuliyorithishwa na mzungu.Siamini kama wachina wanasoma upumbavu unaotupotezea muda shuleni na vyuoni.

Anatakiwa kiongozi anayeweza kuliona hili.
Kufuta vyeti vyote ambavyo havileti suluhisho kwa changamoto tulizo nazo.
Inatakiwa uthubutu mkubwa.

Binafsi ninaumia sana kwa hii hali kuendelea.Tutakuwa wateja wa simu ,teknolojia,silaha,sawa hadi toothpick na cotton buds?!!
Tutasoma kwa mtindo huu huu tuliodanganywa eti 7:4:2:3?!!Ni nani alifanya utafiti kuwa huu mfumo ndio unafaa?
Niko tayari kupokea matusi lakini siamini katika wasomi wetu ambao wengi wameifanya elimu kama nyenzo ya kuibia serikalini na kwa watu,cheti kama kitu cha kutambia mtaani na ikibidi kutukania watu wasio nacho,kama nyenzo ya kutunga sheria kandamizi ili ziwalinde mkiiba kwa kushirikiana na watu weupe.
 
BLOOM TAXONOMY ndio inayotumika kuandaa mitihani. Kwa hio hoja yako kuwa TZ inapima kumbukumbu tu sio kweli.
Hata hivyo kuna waliosoma huko China, Urusi nk ambako wanapima nyanja zote za elimu bado hawajaleta matokeo.
Labda upo sahihi kwenye suala la mtaala kuwajaza watu vitu visivyokuwa na tija ktk maisha.
Mfano huwezi kukuta swali likiuliza
"wewe kama mwanafunza wa TZ unawezaje kutatua tatizo la maji kijijini kwako ? "
Maswali yanachochea ufahamu wa nchi tusizoushi
Nakumbuka swali hili
"Egypt is Nile and Nile is Egypt, discuss"
Swali kama hili lingewafaa watoto wa Misri sio TZ.
Sisi tuulizane how can you start a mining company, fishing company, Timbre Industry.
How can we remove technological gape and dependency from imperialist.
Mpaka muda huu graduate wa physics engineering hajui mbinu za kuanzisha start up tech company.
Upande wa sayansi hakuna learn by doing. Kuna tuproject tuchache tu.
Wenzetu sasa hivi wana kozi mpya kama physics engineering ili kuweza kupata graduate wa kuendana na wakati sisi bado tunafundushwa physics kama natural science.
Mtaala ndio shida kubwa, unatakiwa kuendana na teknolojia.
Mtoto wa shule ya msingi mpaka leo hana computer wala matumizi ya internet na vio gozi wanaona poa tu.
Kuna mambo wanajua wakitafanya yataleta mapinduzi ila hawataki tu sio kwamba hawawezi kufikiri bali wanapuuzia tu.
Prof Shayo (al marhemu) aliwashauri viongozi waanzishe technological hub kila mkoa ila viongozi walimpuuza, marekani wameanzisha Silicon valley hub, China nao wana gwanzou. Shayo aliwahi kutoa wazo miaka ya 80 kabla ya china na USA hii ina maana kuna teknolojia zingezaliwa kwenye hizo habu.
Shida nyinigine ni kwamba mtu mweusi huwa haya amini mawazo ya mtu mwanzake mweusi, anaamini kushauriwa na mzungu au mchina, japo hata hayo mawazo ya mtu mweupe kiongozi wa kiafrika huyapindisha.
My dear jf member selfish is a faculty of our heart and mind, usitegemee kwamba sisi tutakuja unda ndege hilo futa.
 
Napenda kuanza na nukuu ya mwanafalsafa simkumbuki jina aliyesema " Elimu humfanya mwerevu kuwa mwerevu zaidi na mpumbavu kuwa mpumbavu zaidi"

Kuna kitu hatujakigundua katika suala zima la elimu.Tuna watu wenye ma PhD na ma degree wengi zaidi ya asilimia 99.9 tumewaamini kama "think tanks" wa nchi kumbe hawawezi kufikiri kabisa.

Kipimo cha wao kupata hizo shahada ni uwezo wa kukumbuka vitu na sio uwezo wa kuchakata.Kukumbuka vitu ni kipaji kama alicho nacho ndege kasuku.Kipaji cha kukumbuka vitu hakiwezi kuwa kipimo cha akili.Bahati mbaya maprofesa wengi, na wasomi wengi walipatikana kwa kipimo hicho cha uwezo wa kukumbuka.Hawa ndio wanaitwa watu wenye akili sana.

Nasikitika kusema kuwa nchi yetu kama siyo nchi zetu za kiafrika,tutaendelea kuwa maskini wakubwa hadi pale tutakapochoma misingi ya elimu tuliyorithishwa na mzungu.Siamini kama wachina wanasoma upumbavu unaotupotezea muda shuleni na vyuoni.

Anatakiwa kiongozi anayeweza kuliona hili.
Kufuta vyeti vyote ambavyo havileti suluhisho kwa changamoto tulizo nazo.
Inatakiwa uthubutu mkubwa.

Binafsi ninaumia sana kwa hii hali kuendelea.Tutakuwa wateja wa simu ,teknolojia,silaha,sawa hadi toothpick na cotton buds?!!
Tutasoma kwa mtindo huu huu tuliodanganywa eti 7:4:2:3?!!Ni nani alifanya utafiti kuwa huu mfumo ndio unafaa?
Niko tayari kupokea matusi lakini siamini katika wasomi wetu ambao wengi wameifanya elimu kama nyenzo ya kuibia serikalini na kwa watu,cheti kama kitu cha kutambia mtaani na ikibidi kutukania watu wasio nacho,kama nyenzo ya kutunga sheria kandamizi ili ziwalinde mkiiba kwa kushirikiana na watu weupe.
Point. Ila hutaona wachangiaji
 
Kosa Kubwa
Ni kuweka Mfumo wa kupambania Jibu lililo sahihi kwa miaka mingi na kuaminisha watu Kuna jibu moja tu.

Vita ikahamia kwenye kukariri jibu sahihi kuliko kujiuliza zaidi na kutafuta mengine yaliyo sahihi.

Shida Kubwa
Maswali Yale Yale ya juzi na jana ila leo yanataka majibu tofauti na wewe una moja uliloliita Sahih na huamini Wala kujishuguulisha kutafuta mengine.

Tuna wataalam wengi wa misamiati ambayo hawajawahi kuiishi

Tunaandaliwa kupita njia wanazochonga Wengine pinsi kila mtu alitakiwa awe mchonganji Kama sio kushiriki kikamlilifu katika uchongaji.

Wi misieduketed.
Dumbing us down.
 
Back
Top Bottom