Tumsaidie Huyu Dada Kisheria

ExpertBroker

JF-Expert Member
Jun 1, 2009
454
107
Kuna dada tuko naye ofisini, alizaa na jamaa yapata miaka mitano iliyopita! Wakati mtoto ana miezi 4 jamaa akaoa mwanamke mwingine bila kumwambia mzazi mwenzie wa awali! Huyu dada alipata fununu kwamba kuna vikao vinaendelea lakini jamaa akadai ni vikao vya ndugu yake! OK, hiyo si ishu kwani jamaa ana uhuru wa kuoa mwanamke anayemtaka.

Ishu kubwa hapa kwa huyu dada ni kwamba jamaa hataki kabisa kumsaidia mtoto wake kwa maana ya matumizi na school fees, toka mtoto yupo kindagarten na sasa yupo darasa la kwanza! Jamaa hataki kabisa kujihusisha na masuala ya huyu mtoto wake wa nje kwa kuhofia mke wa ndoa atajua! Kinachomuuma huyu dada ni kwamba yeye binafsi ana matatizo na hawezi kumudu kuendelea kumlea mtoto peke yake wakati baba yake yupo hapa jijini Dar na ana kipato, Kinachouma zaidi ni kwamba jamaa hajawahi kumwambia huyu dada kama kaoa? Je, achukue hatua gani?
 
Atafute kazi ili amlee mtoto wake! Jamaa inaonekana hampendi mtoto wala mama yake sasa unataka afanyeje?
 
Unafikiri hilo jibu ulilotoa la msaada kisheria ama labda hukusoma vizuri thread yenyewe! Mada imekuja katika jukwaa la sheria ili wadau watupe experience jinsi ya kufanya, na kama sikosei kuna Sheria ya kutetea haki za watoto! Unaposema jamaa hamtaki mtoto wala mama, unafikiri sheria haimbani mshikaji?
 
Kwa hapo aende ustawi wa Jamii ofisi zilizo karibu nae ambapo atapata msaada
naamini anajua jamaa anafanya kazi wapi au anapatikana vipi ili hata kama ni woto aweze kuupokea maana kama ameshindwa kuhandle matter kistaarabu ni bora jambo hilo liende mbele zaidi. Itakapothibitika kweli kuwa mtoto ni wa kwake na hataki kumtunza jambo hilo linaweza pelekwa mahakamani ambapo mahakama itaamu namna ya mtoto kuweza kulelewa ikiw ani pamoja na baba kukatwa mshahara ili kuweza kufidia malezi ya mtoto
 
Labda umpatie hii sheria aisome hasa kifungu cha 8 na 9. Akimaliza aende akatafute mwanasheria wa kumsaidia. Kama hana hela aende Tawla pale Ilala sharif shamba au WLAC pale kinondoni Lang'ata hall au LHRC pale Biafra au TLS pale Ada Estate.
 

Attachments

  • Law of the Child Act.pdf
    1.1 MB · Views: 33
Haya yanawakuta akina Dada wengi hapa Nchini, tatizo ni kutojua sheria na wakati mwingine kutopata msaada wa kutosha kutoka vyombo vinavyohusika. Kwa mfano Dada anapambana na mwenye fedha, hii inawakuta sana wafanyakazi wa ndani wanapopewa mimba na matajiri zao huwa wanaishia kwenda kujifungulia vijijini kwao. Kisha watoto hao hurudi mjini wamekwishapata umri kidogo na kuwa machokoraa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom