MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Nimepitia karatasi za wapiga kura, ambazo zimetundikwa maeneo mbalimbali katika vituo vya kupigia kura tarehe 31/10/2010.
Katika orodha waliyoweka tume ya uchaguzi, kuna aina mbili za namba za wapiga kura.
Namba ya kwanza wamepewa wale wote waliojiandikisha katika vituo halali kwa kujaza fomu zao na kupigwa picha, kisha kupewa kadi ya mpiga kura.
Kwa mfano namba 47880568 ni namba halali na imeandikishwa kwenye daftari la wapiga kura.
Namba aina ya pili zipo kwenye orodha ya wapiga kura lakini hazina maelezo yoyote, na jambo la kushanga namba hii pia imo kwenye daftari la wapiga kura.
Mfano ni namba 19272311 na 19272348 hizi namba zipo kwenye daftari lakini hazieleweki ni za nani, na kwa nini zimewekwa kwenye daftari la wapiga kura. Kwa uchunguzi wangu hizi namba ziko nyingi kweli kweli kwenye kila kituo nilichopitia.
Tume ya uchanguzi imekuwa ikidai kuwa idadi ya wapiga kura ni zaidi ya 19,000,000 idadi ambayo watu wengi wamekuwa wakipinga, ukweli ni kuwa hizi namba hewa zitawekwa kwenye daftari la kupiga kura jumapili zikiwa na maelezo ya watu na picha zao na watapiga kura.
Mawakala wote wa vyama vya upinzani kuanzia sasa wapitie orodha zilizotundikwa ukutani. Waandike namba zote ambazo hazina majina na maelezo yoyote, siku ya jumapili wahakikiki namba hizi na namba zilizopo kwenye daftari la wapiga kura kwa kila kituo.
La sivyo namba hizi zitaliza wengi, baada ya uchaguzi.
Hakikisha mwenyewe uhalifu huu wa tume kwa kuweka namba hizo kwenye link yao hii hapa:-
http://www.nec.go.tz/?modules=reg_status⊂