Tukio hili la Tanga litufumbue macho

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,147
10968469_752076654863108_1886840473355374991_n.jpg



Vyombo mbalimbali vya habari nchini, jana vilitanda kwa habari nzito na ya kustusha kwamba askari mmoja wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wa kikundi cha wahalifu kilichokuwa kimejichimbia katika mapango ya Amboni mkoani Tanga.

Mbali ya kuuawa kwa askari huyo, pia askari wenzake wawili na polisi watatu walijeruhiwa katika mapambano hayo yaliyoelezwa kuwa yalidumu kwa takriban saa 48 katika maeneo ya maporomoko ya Mikocheni, kijiji cha Amboni umbali wa kilomita 10 kutoka jijini Tanga.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Paul Chagonja, alithibitisha kujeruhiwa kwa askari polisi watatu, askari wa JWTZ wawili na mmoja aliyefariki; na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo.

Chagonja alisema askari wanaendelea na operesheni ya kuwatafuta watu hao wanaodaiwa kujichimbia kwenye mapango hayo ya Amboni.

Kwa mujibu wa Chagonja, hadi kufikia juzi walikuwa wamekamatwa watu watatu wakiwa na silaha za jadi zikiwamo mishale, pinde na mikuki.

Kwa hakika, hali hiyo siyo tu inaleta wasiwasi kwa wakazi wa eneo la Amboni, bali pia inaweza kuzua hofu kubwa kwa usalama wa maeneo mengine nchini. Ni imani yetu kuwa jitihada zinazoendelea sasa jijini Tanga kwa ushirikiano wa pamoja wa polisi na vyombo vingine vya usalama zitazaa matunda na mwishowe wahalifu wote watadhibitiwa na kufikishwa mbele ya mkono wa sheria.

Hata hivyuo, pamoja na imani yetu hiyo, sisi tunadhani kwamba ipo haja kwa jeshi letu la polisi na vyombo vingine vya usalama kuchukulia tukio hili kuwa ni sehemu ya kutuzindua ili tuongeze nguvu zetu maradufu katika kukabili uhalifu nchini.

Hii inatokana na ukweli kuwa katika siku za hivi karibuni, kumekuwapo na matukio kadhaa ya vituo vya polisi kuvamiwa na majambazi, askari kuuawa na silaha kadhaa kuporwa, zikiwamo za kivita kama Sub Machine Gun (SMG).

Tukio la hivi karibuni lilikuwa ni la polisi wawili waliokuwa doria jijini Tanga kuvamiwa na majambazi wenye visu na kisha kuporwa bunduki mbili aina ya SMG zinazodaiwa kuwa kwa pamoja zilikuwa na risasi takriban 60. Taarifa zilieleza kuwa mmoja wa polisi waliokumbwa na tukio hilo alilazwa hospitali baada ya kuchomwa kisu na majambazi hao.

Siku chache kabla ya taarifa za tikio la askari kuporwa bunduki wakiwa doria jijini Tanga, kulitokea uhalifu mwingine wa kutisha kwenye kituo cha polisi Ikwiriri, Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani. Majambazi wanaokadiriwa kufikia 10 wakiwa na silaha za aina mbalimbali za moto na jadi, waliwaua askari wawili pamoja na kupora silaha saba na kulipua bomu katika kituo hicho.

Askari polisi waliouawa katika tukio hilo ni PC Judith Timoth na Koplo Edgar Mlinga. Na hadi sasa, hakuna taarifa za kina juu ya kukamatwa kwa watu waliohusika na uhalifu huo licha ya jeshi la polisi kuahidi zawadi nono ya Sh. milioni 20 kwa yeyote atakeyewezesha kukamatwa kwa majambazi waliotenda unyama hao.

Tukio hilo lilikuwa ni mfululizo wa matukio mengine mawili yaliyohusisha uvamizi kwenye vituo vya polisi katika kipindi kifupi kisichozidi miezi saba. Awali, Juni 11, 2014, watu wasiojulikana walivamia Kituo kidogo cha Polisi Mkamba kilichoko katika Wilaya ya Mkuranga na kuua askari polisi mmoja pamoja na mgambo. Askari aliyeuawa katika tukio hilo ni D 9889 Koplo Joseph Ngonyani huku mgambo akiwa ni Venance Francis, aliyefariki wakati akitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) huku askari Mariamu Mkamba, akijeruhiwa lakini alitibiwa na kupona.

Katika tukio hilo, majambazi yalipora bunduki mbili aina ya SMG, tatu aina ya shotgun na magazini 30 zilizokuwa kwenye ghala la muda zikisubiri kupelekwa kwenye kituo kikubwa chenye ghala kuu la silaha.

Kwa mara nyingine, Septemba, 2014, majambazi yalivamia Kituo Kikuu cha Polisi kilichoko katika Wilaya ya Bukombe mkoani Geita na kuwaua askari wawili na kuwajeruhi wengine watatu.

Vilevile, majambazi hayo yalifanikiwa kupora bunduki 10 aina ya SMG, risasi ambazo idadi yake haikutambulika na pia mabomu ya kutupa kwa mkono.

Kutokana na mfululizo wa matukio haya, NIPASHE tuliwahi kuhoji katika tahariri yetu ya ........ kwamba je, kulikoni hivi sasa uvamizi huu umehamia kwenye vituo vya polisi? Kulikoni vituo hivyo vinavyotegemewa kuwa kimbilio la wananchi kwa ajili ya usalama wao na mali zao vigeuzwe kuwa dango la majamabzi kujitwalia silaha kwa ajili ya shughuli zao za kihalifu?

Tulieleza hofu yetu kwamba isije ikawa mfululizo wa matukio hayo ni ishara ya kuwapo kwa kikundi fulani cha watu, wenye malengo fulani ya kihalifu, wangali wakijipanga kwa kujikusanyia silaha hizo nzito za polisi kwa sababu wanazozijua wao.

Sisi tunaamini kwamba kwa muda wote wa kuibuka kwa vitendo hivi vya kihalifu, bado kuna mahala tutakuwa hatujapafanyia kazi vizuri. Ni dhahiri vile vile kuwa zipo dalili za kuwapo na mwanya kwa wahalifu kutenda watakayo huku sisi tukiendelea kutoa majawabu mepesi.

Tunafikiri kwamba jeshi la polisi na vyombo vingine vinavyohusika moja kwa moja na usalama wa raia na mali zao kujipanga zaidi ili kutuhakikishia usalama wetu.

Kwa mfano, sisi tunadhani kwamba Mkuu wa Jeshi la Polisi ana wajibu wa kuangalia ni kwa namna gani wanaweza kuongeza uwajibikaji wa askari wetu. Taarifa za majamabzi kuwapora askari silaha nzito za moto kwa kutumia visu haziashirii mwelekeo mzuri.

Tunaingiwa hofu kwamba pengine, silaha zile zile zilizoporwa kwa askari wetu zinaweza pia kuangukia mikononi mwa wahalifu kama hawa waliobukia Amboni Tanga na kutishia usalama wa raia na mali zao.

Ni kwa kuzingatia yote hayo, ndipo tunapoona kwamba sasa, tukio hili la Tanga lichukuliwe kama sababu ya kutufungua macho katika kuhakikisha kwamba usalama wetu uanendelea kuwa wa uhakika na kamwe hatubabaishwi na wahalifu wa aina yoyote ile.

Mathalan, tumeelezwa kwamba katika tukio la Amboni (Tanga), taarifa za kuwapo kwa silaha kwenye mapango hayo zilitolewa na raia wema kwa polisi na ndipo vyombo vya dola vilipofuatilia na kuanza kuchukua hatua.

Sisi tunajiuliza, silaha zote hizo zilipita vipi hadi kufikishwa katika mapango hayo ya Amboni pasipo vyombo vyetu vya usalama kuzibaini na kuwakamata wahusika kungali mapema? Ni baadhi ya maswali yanayopaswa kuwa chanzo cha kuongeza umakini.

Pamoja na yote yanayotokea, sisi tunaamini kwamba bado taifa letu lina vyombo imara vya kutuhakikishia ulinzi na usalama. Isipokuwa, ni wazi kwamba kuna mahala tumeteleza na hivyo ni wajibu wa Mkuu wa Jeshi la Polisi, kwa ushirikiano na vyombo vingine vya usalama na wadau wengine kuangalia kwa kina ni wapi pana tatizo na kutafuta majawabu ya kweli yatakayoondosha tishio lolote la usalama.

CHANZO: NIPASHE

 
Naona sisiemu kupitia hao magaidi feki watakuja kufanya masaka(masacre) yatakayoghalimu maisha ya watu kama ilivyotokea arusha.
 
hapa serikali ijipime na kutafakari sana kwa kina sana juu ya mafunzo ya [jkt] maana hawa vijana wanaopitia [jkt] wanaporudi mtaani baada ya kumaliza masomo hawapati hajira,

na tayari umesha wafundisha kupambana na kutumia silaa wengine wasio waadilifu moja kwa moja watajiingiza kwenye vitendo viovu,kama ujambazi na ugaidi, matokeo yake,[jkt] itakua inazalisha majambazi na magaidi,

ushauri wangu kwa serikali ifanye tafakuri kwa kina juu ya [jkt] kwa sasa kutokana na mazingira na kizazi tulicho nacho kwa sasa,isijikute inazalisha genge la majambazi na magaidi,

serikali itazame sera zake,kwa kufufua viwanda na kutengeneza fursa za elimu ya ujasiria mali kwa watu wake,waondoe urasimu na vikwazo lukuki juu ya sera za kujitegemea,

watoe elimu ya biashara tangu mashuleni watu wajengewe elimu ya kujitegemea tangu elimu ya msingi,badala ya kuwapeleka [jkt] wawa andae hawa watoto tangu wadogo waingiziwe elimu ya biashara na kujitegemea,

serikali ishirikiane na taasisi za watu wanaotoa elimu ya mafunzo ya ujasiria mali,na kuweka vipindi katika tv na radio vitakavyo wahamasisha watu kujiajiri wenyewe,na kikifanya chombo kama [tbs] kuwasaidia hawa wajasiria mali kwa kuondokana na urasimu,na vikwazo walivyo navyo sasa kwa kuwathibisha wajasiria mali wadogo wadogo,

haya yakifanyika nchi ihi itazidi kuwa kisiwa cha amani, kwa kuwa watu watakuwa huru kiuchumi na kimaendeleo MUNGU ibariki tanzania,
 
Tatizo la kuwa na rais mbovu.....hii yote ni kwa sababu majasusi wanajaribu kumpima akili, uvumilivu na uwezo wake. Kwa kweli kama ni rais tu, amatufelisha watanzania.
 
Tatizo la kuwa na rais mbovu.....hii yote ni kwa sababu majasusi wanajaribu kumpima akili, uvumilivu na uwezo wake. Kwa kweli kama ni rais tu, amatufelisha watanzania.

Inyelijensia ya nchi is at its weakest.
Dalili zilianza kutolewa na wananchi huko Tanga toka mwaka jana, jamaa anasafiri tu kufukuzie per diem.
 
.....nchini ina udini si mwl.Nyerere alishawaonya,hamkumsikia?.
 
naona sisiemu kupitia hao magaidi feki watakuja kufanya masaka(masacre) yatakayoghalimu maisha ya watu kama ilivyotokea arusha.

hivi kwa nin siasa chafu imetawala vichwa vya watu mpaka wanakuwa wavivu wa kufikiri kuhusu usalama wao wenyewe?
 
hapa serikali ijipime na kutafakari sana kwa kina sana juu ya mafunzo ya [jkt] maana hawa vijana wanaopitia [jkt] wanaporudi mtaani baada ya kumaliza masomo hawapati hajira,na tayari umesha wafundisha kupambana na kutumia silaa wengine wasio waadilifu moja kwa moja watajiingiza kwenye vitendo viovu,kama ujambazi na ugaidi, ushauri wangu kwa serikali ifanye tafakuri kwa kina juu ya [jkt] kwa sasa kutokana na mazingira na kizazi tulicho nacho kwa sasa,isijikute inazalisha genge la majambazi na magaidi,

serikali itazame sera zake,kwa kufufua viwanda na kutengeneza fursa za elimu ya ujasiriamali kwa watu wake,waondoe urasimu na vikwazo lukuki juu ya sera za kujitegemea, watu wajengewe elimu ya kujitegemea tangu elimu ya msingi,wawa andae hawa watoto tangu wadogo waingiziwe elimu ya biashara na kujitegemea.

....HAPO UMENENA MKUU HAYO NDIYO MAWAZO YAKUJENGA TAIFA LETU KWA MTINDO HUUTUTASONGAMBELE KIFIKRA. KEEP IT UP..!!
 
​kinachoniuma zaidi wananchi wanaambiwa warudi kwenye maeneo ya hali ni shwari, kuna ushwari gani wakati silaha hamjazikamata wala hata mtuhumiwa mmoja hajakamatwa, mnatuaminisha nni???
 
Wazee hio ni cinema ya kutungwa na
Wana siasa waliofeli wa ccm hakuna cha ugaidi
Wala uhalifu watanzania mtadanganyika
Hivi mpaka lini wenzenu wanatafuta kisingizio
Cha kuzuia mikusanyiko ya vyama vya upinzani
Wasizuie ile katiba inayolazimishwa :
 
Watu waliovaa yebo yebo ndio wawataabishe
Majeshi yetu yote na mizinga iliyoko huko
Leo siku ya 4 Sijui 5 hao watu wana silaha za jadi
Kwa mujibu wa chagonja : eti wametoroka
Sasa watanzania tulitakiwa tupeleke
Batalian ngapi za Jeshi kupigana na wavaa yebo yebo
Kweli ccm imekuwa mene mene tekel na Peres
 
Hawa watu wanatoka wapi? inakuwaje watu wanafanya vitendo kama hivyo halafu polisi hawawajui? Mimi nafikiri vyombo vyetu vya usalama vimelala! Mjumbe wa nyumba kumi hawajui? Siku hizi utakuta hujuma barabarani, mabango yamengolewa, matairi yanachomwa barabarani na kuharibu barabara n.k. watu hawa hawafahamiki katika vijiji hivyo? Inawezekana vipi? Wakenya wanakuja kujifunza kwetu jinsi tulivyokuwa na utawala mzuri hadi katika nyumba kumi, kwamba chochote kinachotokea pale kinafahamika. Sasa tumeacha jambo zuri na haya ndiyo matokeo! Watu wanaanzisha kambi za mafunzo ya kigaidi, hatujui kinachoendelea? Kwa mtindo huu, hayo yanayotokea Somalia, Kenya, Nigeria, Pakistani yalianza hivi hivi. Yanakuja, au tuseme yamefika!
TULITAKIWA TUWE TUMEAMKA JUZI. BADO TUMELALA, TUMELALA!
 
Back
Top Bottom