Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Chilambo...chilambo...unaniskia..?..nakuskia Charles..?hapa Uwanja wa Taifa kumekucha Zamoyon Mogela anawainua wapenzi wa Simba...Simba 1 Maji Maji toka Songea hawajapata kitu ....haya Chilambo endelea..!! asante sana Charles hapa Mwanza mambo bado si Pamba wala Ushirika toka moshi waliojipatia bao..lala laal laaa goooooo!!!wakati napokea toka kwako Charles mshambuliaji wa Pamba John Makelele alipata krosi safi sana toka kwa Hamza Mponda anaukwamisha mpira wavuni Pamba 1 Ushirika hawajapata kitu....Daaah ni mengi sana ya kukumbuka sijui kama zile enzi za RTD zitarudi.
 
Ndugu kama hukuwepo usiseme uongo hapa, mkoa kwa mkoa saa 7 mchana? Kipindi cha mkoa kwa mkoa kilikuwa kila siku ya alhamisi au ijumaa kama sikosei baada ya taarifa ya habari ya saa nne asubuhi


Nilipenda kipindi hiki,ilikuwa saa 7 mchana i think !
 
Eshe Muhidini enzi hizo alikuwa anaripoti kutoka Tanga

Mke mdogo wa Maulidi Kitenge wa ITV (msiniulize habari ya umri wao)


Pascal, hebu ongezea na hawa:

26. Tido Muhando (Mzee wa Mwananchi) - Pia nafuatilia sana simulizi zake za kila Jpili - Mwananchi Newspaper.
27. Deborah Mwenda
28. Sarah Dumba
29. Charles Hiral ( Mzee wa BBC)
30. Ishe Muhidin
31. Frolian Kaiza
32. Halima Kiemba
33. Betty Mkwasa ( Mwanasiasa kwa sasa)
34. January Constatine
35. Lando Mabula
36. Abubakar Lyongo
37. Sued Mwinyi
38. Nswima Elnest
39. Malima Ndelema
40. Richard Leo
41. Mohamed Kisengo
42. Christina Chokunogela
43. Shaban Kisu
44. Salim Bonde
45. Sekion Kitojo
46. Ahmed Kipozi
47. Fatma Kipozi
48. Ezekiel Malongo
49. Abdul Ngalawa
50. Hendrick Maiko Libuda
 
Duh mmenikumbusha mbali sana.nilikuwa nakipenda sana tena sana kipindi cha mama na mwana.sikumbuki jina la mtangazaji ebu nikumbusheni wajf.nilikuwa sikosi kipindi .yaani nakosa raha nisipokisikiliza .hivi yupo yule mtanganzaji?? Pia kile kipindi cha zilipendwa kila jumapili nilikipenda sana

Jaman namie namkumbuka sana sana sana..anaitwa Debora Mwenda. Sijui yupo wapi mama yetu nakumbuka hadithi za Adili na Nduguze, Binti Chura, nk!! Dah! kweli ya kale ni dhahabu..
 
Ndugu kama hukuwepo usiseme uongo hapa, mkoa kwa mkoa saa 7 mchana? Kipindi cha mkoa kwa mkoa kilikuwa kila siku ya alhamisi au ijumaa kama sikosei baada ya taarifa ya habari ya saa nne asubuhi

Punguza jasba ,hata kama hormones ziko juu,ndio maana sentence yangu inaishia i think!!!!
If so,nikumbushe kila kipindi cha ngoma za makabila,ilikuwa lunch time kama sio saa 7,au 8 hivi.

Nani alikuwa mtangazaji?
 
Wakati ule was so nice!Hakukuwa na udini wa kipumbavu kama sasa,Watangazaji walikuwa watangazaji,no body alimind eti ni dini gani huyu.Wasije wakasema hakukuwa na Mkuu wa radio RTD dini fulani tangu uhuru!!

Ila wakati wa kusikiliza mechi ya Yanga na Simba,kama uko mikoani ilikuwa presha kubwa sana.Ila watangazaji waliokuwa biased,utwajua siku hiyo!!!

Nakumbuka mechi ya Simba na Yanga,ambapo tulichapwa 6-0.Nilikuwa teenager,machozi yalinitoka.
Kipa alikuwa Bernard Madale,na baadae watu wakawa wanashona suruali zinaitwa Asante Madale!
 
Jazba JF???? Nilichkiona ni kuwa unadanganya watu kama hujui uliza uambiwe, kwani kuuliza si ujinga. Anza thread tangu mwanzo utamjua mtangazaji wa hicho kipindi cha ngoma za makabila but saa saba hakukuwa na hicho kipindi wala hiyo saa nane, saa nane baada ya muhtasari wa habari kulikuwa na kipindi cha chaguo la msikilizaji, upo hapo


Punguza jasba ,hata kama hormones ziko juu,ndio maana sentence yangu inaishia i think!!!!
If so,nikumbushe kila kipindi cha ngoma za makabila,ilikuwa lunch time kama sio saa 7,au 8 hivi.

Nani alikuwa mtangazaji?
 
  1. Namkumbuka Michael Katembo na kipindi chake cha ngoma za asili kikiitwa "Tumbuizo Asilia", jinsi alivyosababisha ngoma za jadi zipendwe kutokana na mbwembwe tu za mtangazaji wa kipindi.
  2. Namkumbuka David Wakati kwenye kipindi cha "Jibu Lako" ambako niliwahi kutuma swali langu akalijibu.
  3. Abisai Steven namkumbuka kwa kile kipindi cha "Mikingamo" (mambo ya kuchomeana enzi ile ya vuguvugu la wahujumu uchumi early to mid 1980's).
  4. Napenda kuamini kuwa Deborah Mwenda bado yupo, alikuwa na kipindi chake "Mama na Mwana" kilikuwa na hadithi tamtam sana.
  5. Nadhir Mayoka namkumbuka kwa sababu ya vipindi vyake vya maigizo na vichekesho vya akina "Pwagu na Pwaguzi", kulikuwa na igizo moja maarufu la "Mkataa Pema Pabaya Panamwita" ambalo mastaa wake walikuwa Mzee Jongo, Matuga, Bi Sauda, Majengo, Mzee Kipara, Mama Haambiliki na wengine.
  6. Hivi yule Abdu Ngarawa yuko wapi? "Tunawaletea mazungumzo baada ya habari"!
  7. Halafu wale wawakilishi wa mikoani: Barty Kombwa (Arusha), Ben Kiko (Dodoma), Tumbo Risasi (Songea) na wengine na mbwembwe zao
  8. Enock Ngombale yuko wapi?
  9. Watangazaji wa mpira Omar Jongo, Ahmed Jongo, Mikidadi Mahmoud, Chilambo Dominick
 
Hivi Pascal Mayalla kile kipindi chako cha "Tuimbe sote" unazo bado zile nyimbo? Nilikuwa napenda sana zile kwaya. Kama nakumbuka vizuri wewe ndiye uliyetambulisha magwiji wa enzi hizo "Muungano Cultural troupe" na kwaya yao ikiongozwa na Gaspar Tumaini, na ile ya TOT (Jogoo la Afrika) chini ya Captain John Komba. Nazikumbuka zile nyimbo za kumsifia Mzee Ruksa "Ali Mwinyi kiongozi wetu tumpambe maua, tumpambe pambe, tumweke mbele, tumempa jembe nyundo ang'oeng'oe, afyekefyeke, shamba linone, kisha tuvune..." hii ni mwanzoni mwa 1986 alipokuwa bado hajapata jina la "Ruksa".
 
Jazba JF???? Nilichkiona ni kuwa unadanganya watu kama hujui uliza uambiwe, kwani kuuliza si ujinga. Anza thread tangu mwanzo utamjua mtangazaji wa hicho kipindi cha ngoma za makabila but saa saba hakukuwa na hicho kipindi wala hiyo saa nane, saa nane baada ya muhtasari wa habari kulikuwa na kipindi cha chaguo la msikilizaji, upo hapo

Sio Chaguo la msikilizaji, bali kilikuwa kinaitwa Ombi lako, na pia hakikuwa siku zote, siku zingine tulikuwa tunatupiwa mashairi (Malenga wetu),

CC: jazba
 
Last edited by a moderator:
Watangazaji wazuri waliobaki TBC ni, Shaban Kissu, Sued Mwinyi, Agnes Mbapu na Kingalame. Walio wengi vimeo wanajifanya wajuaji sana wawapo hewani. Hakuna nidhamu kama iliyokuwepo enzi za akina Nyaisanga. Wananiuzi sana wanapotumia maneno kama Mwalyego 'ameweza' kufeli masomo.4 au Tino (aliweza) kukosa penati!!!
 
Noel Namaloe HAKUWA mtangazaji bali alikuwa fundi mitambo wa OB Van ya RTD; enzi hizo hilo OB Van ndiyo lilikuwa gari pekee TZ lenye mitambo ya kurusha matangazo!

...Ninalifahamu hilo Mkuu na hata Mkuu niliye m-quote hakusema huyo ni Mtangazaji. Alitaja mafundi Wawili nami ndio nikasahihisha jina la mmojawapo. labda ungerudi nyuma kidogo ungeona kwa nini niliweka hilo jina hivyo. Uwe na Amani
 
naongeza:
26. ALLY SALEHE - MBILI KASOROBO NA MIDUNDO SAUTI YAKE ILIKUWA KAMA YA MASOUD MASOUD NGULI WA MUZIKI
27. KWEGIER MUNTHALI
hawa walikufa kwa ajali ya gari la Kwegier Munthali likigongwa na treni hapo gerezani /shaurimoyo?? waliopona ni pamoja na HILDA MWAIPOPO - sijui yu wa wapi - nilisikia aliolewa Kenya??
28. KHADIJA SAID - MWANAMKE WA KWANZA MTANGAZAJI - SIJUI KAMA YU HAI - KIPINDI CHAKE CHA WATOTO - MAMA WA KIGOMA HUYU.

umenigusa sana juu ya Salama Mfamao - kuna siku alipiga wimbo do you remember wa phil collins na kamvua kalikuwa kananyunya mahala fulani hadi wa leo ukipigwa wimbo huo huikumbuka sauti yake iliyokuwa nzuri.

29. DEBORAH CHIHOTA badae MWENDA.
30. RAY CHIHOTA
hawa walikuwa mtu na dada yake na mzee wao Chihota alikuwa maarufu Temeke na Serikalini. Ray alikufa kwa ajali ya gari Zimbabwe alikoamua kufuata roots. Ray alikuwa kwenye idhaa ya Kiingereza akiendesha kikundi cha vijana wakiimba Pop. Vijana kama kina Hussein Shebe nk. Pia alikuwa anasoma Taarifa za habari kwa Kiingereza


Mkuu Makah, Asante. Hawa kina Chihota hawa, Je walikuwa na Undugu wowote na Yule Norman Chihota ambaye katika kipindi hicho alikuwa akitamba sana kwenye Riadha hasa kwenye mbio za Mita 400 akiiwakilisha TZ kwenye michuano mingi ya kimataifa ya riadha??

 
Suleiman Hega atakuwa anamkumbuka - kama una mawasiliano naye nina imani atakuwa anamkumbuka Khadija. hata kuna kipindi miaka 10 ya Uhuru watangazaji wastaafu walikaribishwa kutangaza nilimsikia huyu mama

...Khadija Said, Mwaka 1981 wakati Sikukuu ya Wakulima ilipofanyika Kitaifa mkoani Kigoma yeye ndio alipewa heshima ya kuja kuitangaza live redioni kutokana na kuwa kwao ni Ujiji Kigoma.
 
Watangazaji wazuri waliobaki TBC ni, Shaban Kissu, Sued Mwinyi, Agnes Mbapu na Kingalame. Walio wengi vimeo wanajifanya wajuaji sana wawapo hewani. Hakuna nidhamu kama iliyokuwepo enzi za akina Nyaisanga. Wananiuzi sana wanapotumia maneno kama Mwalyego 'ameweza' kufeli masomo.4 au Tino (aliweza) kukosa penati!!!

Asante! Wee kama Mimi Mkuu. Yaani huwa naudhika kweli mtu mzima aliyekwenda shule anatangaza eti "Fulani AMEWEZA kulazwa hospitali baada ya kupata ajali...'! Yaani Ujinga kwa kwenda Mbele!!
 
Ndugu kama hukuwepo usiseme uongo hapa, mkoa kwa mkoa saa 7 mchana? Kipindi cha mkoa kwa mkoa kilikuwa kila siku ya alhamisi au ijumaa kama sikosei baada ya taarifa ya habari ya saa nne asubuhi

...Ram, nawe Utaonekana ni wa Juzi Juzi tu! Kwa kipindi kirefu wakati Watangazaji hawa Nguli wakitamba hewani taarifa ya Habari ilikuwa ni Saa MOJA Asubuhi, Saa SABA Mchana, Saa MBILI Usiku, Saa NNE Usiku Sauti ya Mapinduzi ZBar na Saa TANO Usiku Taarifa ya Habari ya Masaa 24 kisha baada ya hapo kama ni Alhamisi kinafuata kipindi cha MISAKATOO! ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya nyimbo mpya za bendi iliyokuwa imeenda kurekodi nyimbo zake mpya RTD siku chache kabla!
 
...Ram, nawe Utaonekana ni wa Juzi Juzi tu! Kwa kipindi kirefu wakati Watangazaji hawa Nguli wakitamba hewani taarifa ya Habari ilikuwa ni Saa MOJA Asubuhi, Saa SABA Mchana, Saa MBILI Usiku, Saa NNE Usiku Sauti ya Mapinduzi ZBar na Saa TANO Usiku Taarifa ya Habari ya Masaa 24 kisha baada ya hapo kama ni Alhamisi kinafuata kipindi cha MISAKATOO! ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya nyimbo mpya za bendi iliyokuwa imeenda kurekodi nyimbo zake mpya RTD siku chache kabla!

Saa nne asubuhi ilikuwepo taarifa ya habari kama sikosei,saa kumi alasiri pia ilikuwepo<hata kifo cha sokoine kilitangazwa wakati huo,saa moja usiku habari kutoka sauti ya tz zanzibar
 
Back
Top Bottom