Tujikumbushe kijarida cha TANU NA RAIA kilichoandikwa na Nyerere 1962

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Katika utangulizi wake kuna maneno yanasema "Binadamu wanapofanya umoja wa aina yo yote huwa wanayo shabahaya kuunda umoja huo.Pengine ni umoja wa kujipatia elimu , au wa kufanya biashara,au wa kucheza ngoma,au kuimba nyimbo,au kwenda kumzika jirani ,n.k .Vitendo vyao vyote huwa vina shabaha ile moja ,yaani kusudi la kuunda umoja huo vitendo vyao vizuri ni vile vinavyosaidia kuitimiza shabaha yao na vibaya ni vile ambavyo vinapinga kutimizwa kwa shabaha yao havihusiani kabisa na kutimizwa kwa shabaha hiyo"

anaendelea kusema kuwa " sisi tulipounda TANU shabaha yetu kubwa ilikuwa kuondoa serikali ya kikoloni katika nchi yetu , vitendo vyetu vilikuwa vikisaidia kutimiza shabaha yetu ya UHURU........'


Nilipokuwa nasoma hapa nikajiuliza ,hivi shabaha ya CCM ni nini?
vitendo vyao vinalenga kuifikia shabaha hiyo?
Kuna mtu anaijua shabaha ya CCM leo?
Umoja wao upo?Umeunganika ama viungo vingine vimekufa ? Na kama viungo vimekufa wana haja ya kuwepo ? ama watazikwa lini? Nani wa kuwazika hawa?

Tutafakari pamoja ...
 
baada ya shabaha ya kumwondo mkoloni kufanikiwa hawakuka chini kutengeneza shabaha nyingine ndio maana hawajielewi hadi kusababisha ufisadi n.k
 
prof shivji anakuambia kuwa ccm iliitwa chukua chako mapema toka ilipoundwa 1977.
maanqa yake ni kuwa ilionekana haina shabaha.
 
Katika utangulizi wake kuna maneno yanasema "Binadamu wanapofanya umoja wa aina yo yote huwa wanayo shabahaya kuunda umoja huo.Pengine ni umoja wa kujipatia elimu , au wa kufanya biashara,au wa kucheza ngoma,au kuimba nyimbo,au kwenda kumzika jirani ,n.k .Vitendo vyao vyote huwa vina shabaha ile moja ,yaani kusudi la kuunda umoja huo vitendo vyao vizuri ni vile vinavyosaidia kuitimiza shabaha yao na vibaya ni vile ambavyo vinapinga kutimizwa kwa shabaha yao havihusiani kabisa na kutimizwa kwa shabaha hiyo"

anaendelea kusema kuwa " sisi tulipounda TANU shabaha yetu kubwa ilikuwa kuondoa serikali ya kikoloni katika nchi yetu , vitendo vyetu vilikuwa vikisaidia kutimiza shabaha yetu ya UHURU........'


Nilipokuwa nasoma hapa nikajiuliza ,hivi shabaha ya CCM ni nini?
vitendo vyao vinalenga kuifikia shabaha hiyo?
Kuna mtu anaijua shabaha ya CCM leo?
Umoja wao upo?Umeunganika ama viungo vingine vimekufa ? Na kama viungo vimekufa wana haja ya kuwepo ? ama watazikwa lini? Nani wa kuwazika hawa?

Tutafakari pamoja ...
Aise wewe kweli umetafakari hawa jamaa hawana mbele wala nyuma
 
Imani ya Tanu

SIASA YA TANU NI KUJENGA NCHI YA UJAMAA, MISINGI YA UJAMAA
IMETAJWA KATIKA KATIBA YA TANU, NAYO NI HII


Kwa kuwa TANU inaamini:-

(a) Kwamba binadamu wote ni sawa;
(b) Kwamba kila mtu anastahili heshima;
(c) Kwamba kila raia ni sehemu ya Taifa na anayo haki ya
kushiriki sawa na wengine katika Serikali tangu ya Mitaa, ya
Mikoa hadi Serikali Kuu;
(d) Kwamba kila raia anayo haki ya uhuru wa kutoa mawazo
yake, ya kwenda anakotaka, wa kuamini dini anayotaka na
wa kukutana na watu mradi havunji Sheria;
(e) Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika jamii
hifadhi ya maisha yake na ya mal i yake aliyonayo kwa
mujibu wa Sheria;2
(f) Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata malipo ya haki
kutokana na kazi yake
(g) Kwamba raia wote kwa pamoja wanamiliki utajiri wa asili
wanamiliki utajiri wa asili wa nchi hii ukiwa kama dhamana
kwa vizazi vyao;
(h) Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda
sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia
muhimu za kuukuza uchumi; na
(i) Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe,
kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili
kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya
mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine
na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani
na siasa ya watu wote kuwa sawa.
MADHUMUNI YA TANU
Kwa hiyo basi, makusudi na madhumuni ya TANU yatakuwa kama
hivi yafuatavyo:-
(a) Kuudumisha uhuru wa nchi yetu na raia wake;3
(b) Kuweka heshima ya mwanadamu kwa kufuata barabara
kanuni za Tangazo la Ulimwengu la Haki za Binadamu.
(c) Kuhakikisha kwamba nchi yetu inatawaliwa na Serikali ya
watu ya kidemokrasia na ya kisoshalist;
(d) Kushirikiana na vyama vyote vya siasa katika Afrika
vinavyopigania uhuru wa bara lote la Afrika;
(e) Kuona kwamba Serikali inatumia mali yote ya nchi yetu kwa
kuondoshea umaskini; ujinga na maradhi;
(f) Kuona kwamba Serikali inasaidia kwa vitendo kuunda na
kudumisha vyama vya ushirika;
(g) Kuona kwamba kila iwezekanapo Serikali inashiriki hasa
katika maendeleo ya uchumi wa nchi yetu;
(h) Kuona kwamba Serikali inatoa nafasi zilizo sawa kwa wote,
wake kwa waume, bila kujali rangi, kabila, dini au hali;
(i) Kuona kwamba Serikali inaondoa kila namna ya dhuluma,
vitisho, ubaguzi, rushwa na upotofu;4
(j) Kuona kwamba Serikali ya nchi yetu inasimamia barabara
njia kuu za kuzalisha mali na inafuata siasa ambayo
itarahisisha njia ya kumiliki kwa jumla mali za nchi yetu;
(k) Kuona kwamba Serikali inashirikiana na dola nyingine katika
Afrika katika kuleta Umoja wa Afrika.
(l) Kuona kwamba Serikali inajitahidi kuleta amani na salama
ulimwenguni kwa njia ya Chama cha Umoja wa Mataifa.5
 
Katika utangulizi wake kuna maneno yanasema "Binadamu wanapofanya umoja wa aina yo yote huwa wanayo shabahaya kuunda umoja huo.Pengine ni umoja wa kujipatia elimu , au wa kufanya biashara,au wa kucheza ngoma,au kuimba nyimbo,au kwenda kumzika jirani ,n.k .Vitendo vyao vyote huwa vina shabaha ile moja ,yaani kusudi la kuunda umoja huo vitendo vyao vizuri ni vile vinavyosaidia kuitimiza shabaha yao na vibaya ni vile ambavyo vinapinga kutimizwa kwa shabaha yao havihusiani kabisa na kutimizwa kwa shabaha hiyo"

anaendelea kusema kuwa " sisi tulipounda TANU shabaha yetu kubwa ilikuwa kuondoa serikali ya kikoloni katika nchi yetu , vitendo vyetu vilikuwa vikisaidia kutimiza shabaha yetu ya UHURU........'


Nilipokuwa nasoma hapa nikajiuliza ,hivi shabaha ya CCM ni nini?
vitendo vyao vinalenga kuifikia shabaha hiyo?
Kuna mtu anaijua shabaha ya CCM leo?
Umoja wao upo?Umeunganika ama viungo vingine vimekufa ? Na kama viungo vimekufa wana haja ya kuwepo ? ama watazikwa lini? Nani wa kuwazika hawa?

Tutafakari pamoja ...
Mpaka Kieleweke, unaweza kutuwekea hapa hicho kijarida? Shukran
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom