Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Katika utangulizi wake kuna maneno yanasema "Binadamu wanapofanya umoja wa aina yo yote huwa wanayo shabahaya kuunda umoja huo.Pengine ni umoja wa kujipatia elimu , au wa kufanya biashara,au wa kucheza ngoma,au kuimba nyimbo,au kwenda kumzika jirani ,n.k .Vitendo vyao vyote huwa vina shabaha ile moja ,yaani kusudi la kuunda umoja huo vitendo vyao vizuri ni vile vinavyosaidia kuitimiza shabaha yao na vibaya ni vile ambavyo vinapinga kutimizwa kwa shabaha yao havihusiani kabisa na kutimizwa kwa shabaha hiyo"
anaendelea kusema kuwa " sisi tulipounda TANU shabaha yetu kubwa ilikuwa kuondoa serikali ya kikoloni katika nchi yetu , vitendo vyetu vilikuwa vikisaidia kutimiza shabaha yetu ya UHURU........'
Nilipokuwa nasoma hapa nikajiuliza ,hivi shabaha ya CCM ni nini?
vitendo vyao vinalenga kuifikia shabaha hiyo?
Kuna mtu anaijua shabaha ya CCM leo?
Umoja wao upo?Umeunganika ama viungo vingine vimekufa ? Na kama viungo vimekufa wana haja ya kuwepo ? ama watazikwa lini? Nani wa kuwazika hawa?
Tutafakari pamoja ...
anaendelea kusema kuwa " sisi tulipounda TANU shabaha yetu kubwa ilikuwa kuondoa serikali ya kikoloni katika nchi yetu , vitendo vyetu vilikuwa vikisaidia kutimiza shabaha yetu ya UHURU........'
Nilipokuwa nasoma hapa nikajiuliza ,hivi shabaha ya CCM ni nini?
vitendo vyao vinalenga kuifikia shabaha hiyo?
Kuna mtu anaijua shabaha ya CCM leo?
Umoja wao upo?Umeunganika ama viungo vingine vimekufa ? Na kama viungo vimekufa wana haja ya kuwepo ? ama watazikwa lini? Nani wa kuwazika hawa?
Tutafakari pamoja ...