Tujikumbushe enzi hizo: Je uliiandikaje Barua yako ya kwanza ya Mapenzi, na Je ilikubaliwa?

Sokoro waito

JF-Expert Member
Nov 21, 2014
2,201
2,587
Hamjambo wadau, Leo katika kufikiri hapa na pale nimekumbuka enzi hizo niko shule ya msingi darasa la sita huko karibu na Kenya, tulikuwa tukisoma na binti mmoja mrembo aliyeitwa Flora ila hakuwa mjanja kunizidi darasani maana nilikuwa vizuri kumzidi kimasomo. Sasa kama mnavyojua ikatokea nikaanza kumtamani tamani(maana kwa umri ule sikujua hata maana ya kupenda) nikawa nawaza jinsi gani nimwambie wakati huo naogopa kweli kumtamkia msichana kuwa namtaka, bhasi kama mnavyojua enzi hizo hata simu hazikuwepo kwa wingi hapa Bongo na aliyekuwa na simu alikuwa ni bepari tena anayeishi mjini. Sasa nikapanga plan A na B ili nimwambie kuwa nampenda japo sikumpenda bali tamaa tu! Plan A ilikuwa hivi: nimtumie best wangu wa karibu ambaye pia alikuwa rafiki yake ili kumfikishia ujumbe wangu lakini katika kutekeleza plani hii nikagundua yule best naye alimhitaji japo kwa sitaki nataka!. Baada ya kugundua hilo nikaamua kufanya plan B ambayo ni ya kuandika barua ya kumuomba kuwa mpenzi, teh teh! Bhasi wadau nikaandaa kalamu , karatasi na rula huku nikitafuta maneno mazuri ya kumchanganya changanya ili nimpate kiulaini! Nikaandika barua ile kwa mfumo wa barua ya maombi ya kazi japo nilikuwa namaliza kuandika nafuta na kurudia upya kwasababu ya hofu ya kukataliwa na yule mrembo. Baadae nikaificha kwenye mfuko wa daftari alionishonea dada yangu, nikaenda zangu shule ila nikaogopa kumpa, siku ya pili nikaopopa tena, oooh baada ya siku kadhaa, dada yangu akachukua ule mfuko ili akague daftari zangu, ndipo akaipata hiyo barua ooh wacha anibane ila hakunifinya mashavu wala kusema kwa mama maana ningechezea bakora za kutosha. Sasa wadau hadi hapo plan zangu zote zikawa zimefeli kiurahisi, nikaamua kuacha kumtafuta tena Flora. Tupe wewe uzoefu wako wa enzi hizo, je uliandika barua au ulitumia njia nyingine ikakubaliwa au ikakataliwa?
 
Kwa niaba yake.
1473682540649.jpg
 
Mimi enzi hizo nipo form three miaka hiyo ya 1993, kuna binti mmoja alikuwa anaitwa Bupe yeye alikuwa fomu one lakini tulikuwa tunasoma shule tofauti. Binti huyo nilimpenda sana, kumwambia nilikuwa naogopa. Ikabidi niandike barua ambayo nilizunguka nayo mfukoni kwa muda wa mwezi mmoja na kila tukikutana nilikuwa naogopa kumpa.

Kuna siku tukaonana naye,nikamwambia nna barua yako, akauliza imetoka wapi? Nikamwambia we ukiisoma utajua imetoka wapi! wakati huo kijasho chembamba kikinitoka, alipoifungua tu, ikabidi mimi nikimbie na kumwacha,

Jamani kutongoza enzi hizo ilikuwa ni taabu sana!
 
Mimi enzi hizo nipo form three miaka hiyo ya 1993, kuna binti mmoja alikuwa anaitwa Bupe yeye alikuwa fomu one lakini tulikuwa tunasoma shule tofauti. Binti huyo nilimpenda sana, kumwambia nilikuwa naogopa. Ikabidi niandike barua ambayo nilizunguka nayo mfukoni kwa muda wa mwezi mmoja na kila tukikutana nilikuwa naogopa kumpa.

Kuna siku tukaonana naye,nikamwambia nna barua yako, akauliza imetoka wapi? Nikamwambia we ukiisoma utajua imetoka wapi! wakati huo kijasho chembamba kikinitoka, alipoifungua tu, ikabidi mimi nikimbie na kumwacha,

Jamani kutongoza enzi hizo ilikuwa ni taabu sana!
teh teh kwahyo ulifanyaje kuulizia jibu lako? Au ndio uliondoka moja kwa moja?
 
Haya mambo ya barua yanakumbusha mbali sana. Mara ya kwanza kupata kizaa cha barua nilikuwa nimeandikiwa barua kwenye kikaratasi na mrembo ikawekwa kwenye box la kiberiti. Yule binti kamtuma mdogo wake ailete home, dogo kufika home sikuwepo akamuachia mdogo wangu kuwa kaka yako akija mpe hichi kibox.

Mdogo wangu nae alikuwa anataka kwenda kucheza kamuaga mama kamuambia Kaka **** akija kuna kiberiti chake nimekiacha chumbani kwake. Mama alivyosikia tu kuna kiberiti akaenda room kucheki ndani kuna barua.

Nilivyorudi nilipewa counselling, sikuchapwa wala nini ila nilipewa lecture ya maneno na sikurudia tena kuandika barua.
 
Kiukweli njia iyo nlikua naitumia sna kipindi icho,sio km nlikua siwez kuongea la hasha,nkiona dem ananikwepakwepa kwny face 2 face. nlikua na uwezo wa kuandik barua hta 2 kwny zile karatac za kujibia mtihan zile ngefu za primary na zte zinajaa maandshi uku na uku.yaan kwa msichana mwenye akil ndg anaweza akashika anapomalizia na akasahau alipotokea.daah nkikumbuka huwa nacheka sna na kujiona nlikua kituko flan iv Mkuu..
 
teh teh kwahyo ulifanyaje kuulizia jibu lako? Au ndio uliondoka moja kwa moja?
Kwa kawaida kufuatilia majibu always siyo issue ngumu. Ngumu ni ku-break the ice.

Mimi wakati nikiwa darasa la pili niliandika barua yangu ya kwanza. Ilikuwa na vituko maana nilikuwa sina nyimbo nyingi na japo nilijaribu kutafuta neno la tafsida, ila ilikuwa ngumu kwa umri ule. Niliandika barua mbili, moja kwa ajili yangu na nyingine kwa ajili ya ndugu yangu ambaye alikuwa hawezi kuandika vizuri wakati huo na tulikuwa tuna-target wasichana ambao ni ndugu (kwa baba zao)...

Zile barua nilizunguka nazo mfukoni, shuleni nilikuwa naenda nazo (maana tulikuwa tunasoma shule moja), kuchunga mbuzi naenda nazo (maana tulikuwa tunachunga mbuzi jirani na mto ambako na wao walikuwa wanakuja kumwagilia bustani yao mchicha na maharage kila jumatatu, jumatano na jumamosi).

Pamoja na hayo yote, sikuwahi kupata ujasiri wa kuwakabidhi zile barua. Hofu kuu ilikuwa pale unapo-imagine itakuwaje akiisoma akachukia na kuamua kwenda kushtaki nyumbani kwenu (maana wasichana wa huko bush enzi hizo ilikuwa kawaida sana kukusemea kwa wzazi wako ukiongea mambo ambayo hawayapendi, kama hilo).

Baada ya kipindi kirefu kama miezi miwili zilichakaa, zikachanika na nikaamua kuzitupa na kuzika kabisa ndoto za kuwatokea.

Mwisho wa siku walikuja kuwa shemeji zangu maana kaka yetu mkubwa alimwoa dada yao mkubwa mwaka ule ule.

Hiyo ilikuwa 1986
 
Kwa kawaida kufuatilia majibu always siyo issue ngumu. Ngumu ni ku-break the ice.

Mimi wakati nikiwa darasa la pili niliandika barua yangu ya kwanza. Ilikuwa na vituko maana nilikuwa sina nyimbo nyingi na japo nilijaribu kutafuta neno la tafsida, ila ilikuwa ngumu kwa umri ule. Niliandika barua mbili, moja kwa ajili yangu na nyingine kwa ajili ya ndugu yangu ambaye alikuwa hawezi kuandika vizuri wakati huo na tulikuwa tuna-target wasichana ambao ni ndugu (kwa baba zao)...

Zile barua nilizunguka nazo mfukoni, shuleni nilikuwa naenda nazo (maana tulikuwa tunasoma shule moja), kuchunga mbuzi naenda nazo (maana tulikuwa tunachunga mbuzi jirani na mto ambako na wao walikuwa wanakuja kumwagilia bustani yao mchicha na maharage kila jumatatu, jumatano na jumamosi).

Pamoja na hayo yote, sikuwahi kupata ujasiri wa kuwakabidhi zile barua. Hofu kuu ilikuwa pale unapo-imagine itakuwaje akiisoma akachukia na kuamua kwenda kushtaki nyumbani kwenu (maana wasichana wa huko bush enzi hizo ilikuwa kawaida sana kukusemea kwa wzazi wako ukiongea mambo ambayo hawayapendi, kama hilo).

Baada ya kipindi kirefu kama miezi miwili zilichakaa, zikachanika na nikaamua kuzitupa na kuzika kabisa ndoto za kuwatokea.

Mwisho wa siku walikuja kuwa shemeji zangu maana kaka yetu mkubwa alimwoa dada yao mkubwa mwaka ule ule.

Hiyo ilikuwa 1986
ka hadith vle
 
Kwa kawaida kufuatilia majibu always siyo issue ngumu. Ngumu ni ku-break the ice.

Mimi wakati nikiwa darasa la pili niliandika barua yangu ya kwanza. Ilikuwa na vituko maana nilikuwa sina nyimbo nyingi na japo nilijaribu kutafuta neno la tafsida, ila ilikuwa ngumu kwa umri ule. Niliandika barua mbili, moja kwa ajili yangu na nyingine kwa ajili ya ndugu yangu ambaye alikuwa hawezi kuandika vizuri wakati huo na tulikuwa tuna-target wasichana ambao ni ndugu (kwa baba zao)...

Zile barua nilizunguka nazo mfukoni, shuleni nilikuwa naenda nazo (maana tulikuwa tunasoma shule moja), kuchunga mbuzi naenda nazo (maana tulikuwa tunachunga mbuzi jirani na mto ambako na wao walikuwa wanakuja kumwagilia bustani yao mchicha na maharage kila jumatatu, jumatano na jumamosi).

Pamoja na hayo yote, sikuwahi kupata ujasiri wa kuwakabidhi zile barua. Hofu kuu ilikuwa pale unapo-imagine itakuwaje akiisoma akachukia na kuamua kwenda kushtaki nyumbani kwenu (maana wasichana wa huko bush enzi hizo ilikuwa kawaida sana kukusemea kwa wzazi wako ukiongea mambo ambayo hawayapendi, kama hilo).

Baada ya kipindi kirefu kama miezi miwili zilichakaa, zikachanika na nikaamua kuzitupa na kuzika kabisa ndoto za kuwatokea.

Mwisho wa siku walikuja kuwa shemeji zangu maana kaka yetu mkubwa alimwoa dada yao mkubwa mwaka ule ule.

Hiyo ilikuwa 1986
Umenikumbusha mbali sana mkuu. Yaani nikikumbuka huwa najicheka sana. Katika kipindi kibaya kuliko vyote ni umri wa balehe na muda kidogo kabla ya balehe. Kuna vituko sana hapa.
 
Hahahhhhhhh, me mshikaji wangu niliompa ampelekee mlengwa alisoma na kuwapa wanafunzi wengine bila kumpa muusika aseee... ilikuwa bonge la aibu
teh teh sipati picha jinsi ulivyoaibika, huenda hata ulianza kukwepa kwenda parade au darasani.
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu. Yaani nikikumbuka huwa najicheka sana. Katika kipindi kibaya kuliko vyote ni umri wa balehe na muda kidogo kabla ya balehe. Kuna vituko sana hapa.
huo umri ni hatari japo pia utakuwa ulikuachia somo tosha la kujua jinsi ya kumlea mwanao mwenye umri wa balehe.
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu. Yaani nikikumbuka huwa najicheka sana. Katika kipindi kibaya kuliko vyote ni umri wa balehe na muda kidogo kabla ya balehe. Kuna vituko sana hapa.
huo umri ni hatari japo pia utakuwa ulikuachia somo tosha la kujua jinsi ya kumlea mwanao mwenye umri wa balehe.
 
Back
Top Bottom